Huwezi na Hutoweza Kuongea / Kuandika Kiswahili fasaha

Huwezi na Hutoweza Kuongea / Kuandika Kiswahili fasaha

Umekwepa maswali ya msingi kwani ni wewe uliyeanzisha somo la nani kaja na kakuta nani na si mimi, sasa nnakuuliza kuhusu hayo hayo uliyoyaleta unasema hiyo mada nyingine! Hivi unaelewa ulichokiandika awali, hebu rudi kajisome.

Au umeona hapo hapajibiki ni suicide?

Sasa nnakupa challenge ndogo sana, katika hizo post zako ulizoandika Kiswahili, yatowe maneno yanayotokana na Kiarabu halafu tuone kama tutakuelewa ulichokiandika.


Duh! mpaka sasa naishiwa nguvu nafikiri labda hatuelewani! Kwani kuna mahali nimebisha au nimekataa kwamba Kiswahili hakina maneno ya Kiarabu?
Ngoja nirudie tena kwa mara ya mwisho labda!
Kiswahili ni Lugha ya kibantu kwa 100% ambacho kimeazima maneno kutoka lugha mbalimbali hapa Duniani kikiwemo Kiarabu
sasa kama nikitoa maneno ya kuazima siyo tu kutoka Kiarabu bali hata Kiingereza, kireno, Kijerumani n.k sitaweza kuandika nilivyoandika na hii siyo kwa Kiswahili tu, kwa mfano nimesema shule, neno shule ni la Kijerumani sasa nikitoa Shule nitakosa neno la kuweka lkn haimaanishi kwamba Kiswahili kimetokana na Kijerumani!

Leo hii Kiarabu chenyewe pia kinaazima maneno mengi kama Computer, Atom, Quantum, Software, Satellite,Chip, Technology, the Universe n.k sasa ukimwambia Muongeaji wa Kiarabu atoe neno Computer pia atakwama lkn haimaanishi kwamba Kiarabu ni Kiingereza au Kigiriki kwa kuwa tu wanatumia hayo maneno niliyoyataja!

 
Hivi ni kwa nini neno "shule" tumekopa ujerumani badala ya arabuni? Wazanzibari nao wanaita "skuli" wakilikopa kwa waingereza.
 
FaizaFoxy;

Wewe Mama wewe!! Nafurahi unajaribu kurudisha mpira uwanjani na dakika 90 zimeshaisha na umeshafungwa tayari goli za kutosha tayari. Nimegundua hoja zako hazijanyooka kokote zaidi ya kuzijaza majivuno.

Unang'ang'ana eti "unajua maana ya Isimu!" Mara Swahili ni lugha ya kiarabu! Mara Pwani ipi ninayoizungumzia, na eti ooh nakulisha maneno!! Khaaa!! Ndo umeweka Uzi kwa ajili hii!!? Yaani unazuga hujaziona proof nilizokuwekea zinazoonesha kiswahili kina asili ya ubantu!? Mbona unazuga hujaona maswali niliyoyauliza ndani ya post yangu na hujajaribu kujibu hata moja!? Eti sijasoma vizuri Uzi wako! Wewe, post yangu umeisoma vizuri?? Kama umeisoma ,mbona umeshindwa kuwa mwelewa!!
 
Last edited by a moderator:
Hivi ni kwa nini neno "shule" tumekopa ujerumani badala ya arabuni? Wazanzibari nao wanaita "skuli" wakilikopa kwa waingereza.

Hayo maneno hatujakopa, tumeyajuwa kutokana na Wajerumani na Waingereza, tukubaliane hilo kwanza.

Ni kama vile darasa, elimu, kitabu, maabara, yanatokana na Kiarabu.

Kinachokopwa hurudishwa. Labda ungesema tumeiba ningekuelewa.

Soma post namba moja mstari wa kwanza.
 
Barbarosa;

Hapana, hilo la kuazima nnakataa, cha kuazima hurudishwa, mimi nnasema hivi:

Kiswahili ni lugha ambayo imetokana na Kiarabu na Kibantu na maneno mengine machache yaliongezeka kidogo kidogo kutoka lugha zingine za Afrika, Uropa na Asia.


Challenge imekushinda, unajuwa wazi kuwa ukitowa maneno yenye asili ya Kiarabu kwenye Kiswahili, hauna tena Kiswahili na hatutaelewana kabisa.

Sasa rudi tena , katowe maneno hayo ya lugha zingine ulizozitaja nje ya Kiarabu.

Halafu hayo maneno uliyosema Kiarabu imeazima kwa lugha nyingine, inawekana hapo uko sahihi kuwa "wameazima" na ndiyo kwanza umetumia maana sahihi ya kuazima maneno, kwanini? kwa kuwa Waarabu wana maneno yao ya hivyo vitu lakini na hayo ya lugha nyingine wanayatumia ikibidi, kwa hiyo huko ndiko kuazima na kuazima si kule unakotaka wewe, kuwa Kiswahili tumeazima maneno ya Kiarabu, hapana, hatuna mbadala, kwa hiyo hatukuazima, hayo maneno ya Kiarabu tunayoyatumia kwenye Kiswahili ndiyo yanakifanya Kiswahili kiwe Kiswahili. (soma post namba moja mstari wa kwanza).

Kuna maneno ya Kiarabu ambayo yametokana na lugha nyingine lakini si hayo yote uliyoyaandika, katika uliyoyaandika ni moja tu (utaliona chini hapo). Ingawa leo hii hakuna Mwaarabu asiyeyejuwa hayo lakini haimaanishi hawana maneno yao (huko ndiko kuazima) Pata darsa dogo ya hayo maneno yako yanaitwaje Kiarabu:

Computer = Alhusb"a"
Atom = dhara"t"
Quantum = Kammiya "t"
Software = Al bar majiya"t"
Satellite = Al qamar asinaei
Chip = Raqaqa
Technology = Teknolojia (kama tunavyolitumia Kiswahili).
Universe = Al koun


Kitu kama haukijuwi usijaribu ku force. Unajuwa Kiarabu?
 
Last edited by a moderator:
Hiyo inayakinisha "point" yangu kuwa Huwezi na Hutoweza Kuongea / Kuandika Kiswahili fasaha, laiti tungekuwa wote tunayaandika maneno ya Kiswahili kwa Kiarabu wala kusingekuwa na utata, maneno hayo wala yasingeleta ubishi kabisa. Kwa sababu Kiarabu ni lugha yenye alama za matamshi kwenye "irabu" zake na haitegemei "vowels" za herufi pekee.

Tusingeweza kabisa kuandika "ntu" badala ya "mtu" au kinyume chake kama wengi watakamkavyo. Ingawa neno "ntu" ndiyo moyo wa Ubantu.

Kama maneno yote yakiandikwa kwa kiaarabu basi hakitakuwa Kiswahili tena bali ni Arabic.
 
Kama maneno yote yakiandikwa kwa kiaarabu basi hakitakuwa Kiswahili tena bali ni Arabic.

Hapana, hujaelewa. Nisome tena post namba moja. Kiswahili kwa kutumia herufi za Kiarabu, mbona lugha nyingi zinafanya hivyo? na hata hiki Kiswahili kabla ya kuja wazungu ndivyo kilivyokuwa kinaandikwa, na kuna wengi leo hii bado wanaandika Kiswahili kwa herufi za Kiarabu, tena wanakuwa wanakijuwa kweli kweli Kiswahili, si hiki chetu cha kubabia-babia..
 
Nilitegemea sana hilo kutoka kwenu mnaposhindwa kujibu hoja, nimelizowea sana hilo wala halinipi shida, katafute jingine. Hoja bado imesimama na haina upinzani.

Madam FF hapa umemaliza maneno, hata mimi nilitegemea kutokea hiki kitu. Tokea mwanzo wa mjadala huu. Unajua Madam, hawa wenzetu wakisikia neno Uarabu au Kiarabu basi akili zao zote zipo katika Uislam tuu. Anyway yote haya ni matokeo ya ule mfumo..........................
 
Tatizo lako kubwa umefundishwa na wazazi wako kuuliza maswali tu na walisahau kukufundisha kujibu maswali unayoulizwa!!!Bahati mbaya sitakujibu swali zako wala kufuata maelekezo yako yanayompeleka mtu upotevuni, kwakuwa umeshindwa kujibu maswali yangu na badala yake unatafuta dosari tu ili ligi isiishe. Chakufurahisha ni kwamba somo lako jipya litaishia hapahapa jf na kamwe haliwezi kuingizwa kwenye syllabus zetu kwa namna unavyotaka wewe. Endelea kujitutumua mama!!

Kwa sababu huna majibu.

Barbarosa na wengine wengi wanaodhani kuwa Mwarabu "alikuja" tu Afrika, hususan pwani ya Afrika Mashariki wanakisia tu, hawana ushahidi wowote kwa hilo.

Na anaposema "walikuja" wakawakuta Wabantu hapo ndiyo kishamaliza mjadala, kwani ukiisoma historia, utakuta Mbantu ndiyo kaja Pwani ya Afrika Mashariki juzi juzi tu, na alikuta tayari Pwani ya Afrika Mashariki wana lugha yao na utamaduni wao. Jee, Wabantu waliwakuta hapa akina nani?

Halafu linapokuja suala la "kuazima" maneno ya lugha nyingie, nimelitolea ufafanuzi ambao labda ni hayawani tu hawezi kuulewa, neno huazimwa wakati wewe tayari una neno lako lako la hicho ulichokiazima, nimetolea mfano wa hilo alipoleta maneno ambayo alidhani hayana Kiarabu chake, kuwa hayo ndiyo yameazimwa kwa kuwa Waarabu wanayo lakini pia hapa na pale hutumia hayo ya kigeni, lakini leo neno mbadala huna, unatumia la lugha nyingine halafu useme umekopa au umeazima? hapana, hujakopa wala kuazima, unalitumia kama lako na limetokana na lugha fulani, ukope ukilirudisha utatumia lipi? fikiri.

Leo hii hakuna mjadala kuwa bila Kiarabu Kiswahili hakuna, ikiwa ni hivyo basi, hakuna ubishi kabisa kuwa ili uongee na kuandika Kiswahili fasaha inabidi ujuwe Kiswahili kwa kutumia herufi za Kiarabu kupata ufasaha na kina cha maneno. Bila hivyo utaboronga tu.

Na hilo halina ubishi, msikilize Ali Hassan Mwinyi, mzaramo wa Mkuranga akiongea Kiswahili utapenda. Kwanini?

Hilo la haya yangu kuwa "syllabus" wala lisikupe shida, ila kumbuka tu, nimeweka kwenye post namba 33 habari inayoonesha mpaka Waliokuwa Waalim wa Kiswahili wa awali huko chuo kikuu cha Berlin, Ujerumani waliliona hili nnaloliandika hapa, walijifunza Kiswahili kwa herufi na matamshi ya Kiarabu ili kiwaingie na wakiingie barabar, na hawakuishia hapo, ilibidi wakajifunza na Kiarabu ili waende ndani zaidi katika uelewa wa Kiswahili. Kwanini?

Ni sahali sana swali hilo, huwezi kuwa fasaha wa Kiswahili cha amma kuandika amma kuongea kumshinda yule ajuae kukiandika Kiswahili kwa herufi za Kiarabu.
 
Wewe mama unajaribu kujipendekeza kwa waarabu ili iweje?......

1.Kiswahili sio Kiarabu na haitotokea kua kiarabu kamwe ..pia kiarabu sio kiswahili.

2. Sisi ni waafrika sio waarabu tafadhali tuondolee ushuzi wako humu

3. Ikiwa wataka kuwageuza waafrika wabantu wawe waarabu ...pole zako....hizo ni siku za utumwa...kajaribu Sudani wale ndio wenzako waarabu bandia....wanaojikweza kusiko.

4.Ikiwa una mahaba na waarabu na uarabu basi katoke hapo Uropa/Marekani ulipo ..funganya virago na uelekee Arabia....kule utakutana na uarabu kwa kila hali.

5.PWANI YA AFRIKA NI AFRIKA NA KULIISHI WAAFRIKA HATA KABLA YA MAANDISHI KUGUNDULIWA.......SEMA TU WAARABU WALIKUJA WAKAKUTA HAKUNA MAANDISHI KAMILI(RECORDS)NA KULETA MAANDISHI YAO(Thats why there presence was recorded).
pia walikuta wakaazi wa kiafrika wachache sana....pwani ya Kenya waliwakuta Mijikenda,Bajuni n.k.....wakawatawala.

6.AFRIKA YA MASHARIKI NDIKO BINADAMU WA KWANZA ALIKO ONEKANA KWENYE USO WA ARDHI /DUNIA.(Cradle of mankind).
HII INAMAANISHA WATU WOTE ....WAZUNGU KWA WAARABU ....WA ASIA N.K WALITOKEA AFRIKA(MIGRATED).....SO THEY CAN NEVER BE THE FIRST PEOPLE ON ANY AFRICAN COAST.....THERE WERE PEOPLE THEY LEFT THERE WHEN THEY FIRST MIGRATED OUT.


7. NARUDIA........KISWAHILI NI KIBANTU/KIAFRIKA...SISI NI WAAFRIKA WEUSI...PERIOD....UPENDE HUSIPENDE NA HAUTA TULAZIMISHA TUWE WAARABU...KAPELEKE PROPAGANDA ZAKO ZA KIARABU NA DINI ZAO KULE ARABIA.
 
Ninachopinga ni hilo neno imetokana, ukisema Kiswahili kimetokana na Lugha za Kiarabu na Kibantu maana yake ni kwamba Kiswahili ni sehemu ya lugha Kiarabu na hapo ndipo ninapopinga kwani siyo kweli bali Kiswahili kimetokana na Lugha za kibantu na kuazima baadhi ya maneno yake kutoka lugha nyingine zisizo za kibantu kikiwemo Kiarabu, Kijerumani, kiingereza, Kireno n.k! Kwa kifupi Kiswahili siyo sehemu ya lugha ya Kiarabu bali ni sehemu ya Lugha za Kibantu kwa 100%

Kaka nadhani wewe ni mgeni na huyo bibi FaizaFoxy
huwa hashindwi kitu na kazi kuongea ujinga na kubadirisha maneno tu, atakuzungusha mpaka uchoke huku hakuna cha maana anachoongea

DRC ndio nchi inayoongoza Africa kuwa na wazungumzaji wengi wa Kiswahili, provinces nne kubwa za Congo (Katanga, Maniema/Manyema, South Kivu na North Kivu) huko kote kunaongelewa Swahili, na Swahili ya huko ina less than 10% ya maneno ya Kiarabu, kwa mara ya kwanza ukiingia huko na Kishwahili chako cha Tanzania ni wachache sana watakuelewa, lakini wao wakizungumza utawaelewa vizuri mno kwa sababu wanaongea swahili yenye % kubwa ya kibantu

Kishwahili cha Congo hakina neno Alhamisi wala Ijumaa, kina siku ya nne na siku ya tano
kiswahili cha Congo hakina Ishirini wala Arobaini, kina makumi mawili na makumi manne
 
Last edited by a moderator:
Kama Kishwahili kilikuwa kinaandikwa kwa herufi za Kiarabu ndio kuna kifanya kuwa Kiarabu, basi sasa Kiswahili kimebadirika na kuwa kilatini kwa sababu kinaandikwa na herufi za Kilatini
 
Kwangu mimi lugha ni kwaajili ya mawasiliano ili kuelewana. Kama nakuelewa na unanielewa basi huo ufasaha utabaki kwa wanaofundisha tu.
Ukitaka kuamini ufasaha hauna tija angalia bubu anavyowasiliana na bubu mwenzie au asiye bubu, pia angalia kiziwi anavyo wasiliana na watu wa aina mbalimbali. Hapo ndio utajua umuhimu wa lugha ni kuwasiliana na masuala ya ufasaha yapo kwaajili ya kuongeza ajira tu.
 
hapana, hujaelewa. Nisome tena post namba moja. Kiswahili kwa kutumia herufi za kiarabu, mbona lugha nyingi zinafanya hivyo? Na hata hiki kiswahili kabla ya kuja wazungu ndivyo kilivyokuwa kinaandikwa, na kuna wengi leo hii bado wanaandika kiswahili kwa herufi za kiarabu, tena wanakuwa wanakijuwa kweli kweli kiswahili, si hiki chetu cha kubabia-babia..

nani anayeandika kiswahili kwa herufi za kiarabu?
Anayeandika kiswahili kwa herufi za kiarabu na ninavyoandika mm kuna tofauti gani? Maana wote twaandika neno moja
 
Hapana, hujaelewa. Nisome tena post namba moja. Kiswahili kwa kutumia herufi za Kiarabu, mbona lugha nyingi zinafanya hivyo? na hata hiki Kiswahili kabla ya kuja wazungu ndivyo kilivyokuwa kinaandikwa, na kuna wengi leo hii bado wanaandika Kiswahili kwa herufi za Kiarabu, tena wanakuwa wanakijuwa kweli kweli Kiswahili, si hiki chetu cha kubabia-babia..

Faida gani tutapata tukitumia hizo herufi za kiarabu?
 
nani anayeandika kiswahili kwa herufi za kiarabu?
Anayeandika kiswahili kwa herufi za kiarabu na ninavyoandika mm kuna tofauti gani? Maana wote twaandika neno moja

Wengi tu wanaotumia herufi za Kiarabu katika kuandika Kiswahili, kuna watu ambao mpaka leo hii mimi binafsi nnawaslliana nao kwa barua za Kiswahili kwa maandishi ya Kiarabu.

Pia huku kwetu pwani (nnadhani hata kwengine) bado kuna ustaarabu wa kupeleka barua za posa kwa Kiswahili kilichoandikwa kwa herufi za Kiarabu. Wengi hunifata niwaandikie barua za posa kwa sababu tu ntawaandikia kwa Kiswahili lakini kwa herufi za Kiarabu. Imekuwa kama ni desturi walioikuta na wanaiendeleza, utashangaa kuwa mpaka leo hii kuna wazee ambao wakipokea barua za posa ambazo hazijaandikwa Kiswahili kwa herufi za Kiarabu wanazirudisha, sijuwi kama unayafahamu hayo?

Kuhusu swali la "tofauti gani?", tofauti ni kubwa sana na hiyo huwezi kuielewa mpaka uwe unajuwa herufi na irabu za Kiarabu. Mfano mdogo sana ni matamshi ya maneno kama "lugha", wengi wetu leo wanatamka "luga", ni kosa. Neno lingine ambalo hata humu JF nimeona mara kwa mara likiandikwa visivyo ni "kuthibitisha" wengi huandika "kudhibitisha"wakati hayo ni maneno mawili tofauti. Ukijuwa herufi za Kiarabu kuzitamka na kuziandika hutoweza kufanya makosa hayo amma kwa kuandika amma kwa kutamka.
 
Kwangu mimi lugha ni kwaajili ya mawasiliano ili kuelewana. Kama nakuelewa na unanielewa basi huo ufasaha utabaki kwa wanaofundisha tu.
Ukitaka kuamini ufasaha hauna tija angalia bubu anavyowasiliana na bubu mwenzie au asiye bubu, pia angalia kiziwi anavyo wasiliana na watu wa aina mbalimbali. Hapo ndio utajua umuhimu wa lugha ni kuwasiliana na masuala ya ufasaha yapo kwaajili ya kuongeza ajira tu.

Hata hao ndugu zetu uliowataja wamebuni lugha yao na kama huitumii kiufasaha unaipatapata kutoka kwao, unakumbuka msiba wa Madiba kilitokea nini?
 
Back
Top Bottom