can you prove that ustaarabu ni 100% linatokana na kiarabu na maana ya kiarabu ndio sahihi kuliko maana ya kiswahili maana unabishana kikasuku
FaizaFoxy ustaarabu umepata maana yake? kinyume cha mstaarabu ni mshenzi kama mwarabu alivyosema.wafuata uarabu(wastaarabu) na asiyefuata ni mshenzi. waliofuata masuala ya waarabu waliitwa wastaarabu.
kwenye mada yako ya kuwa huwezi kuongea kiswahili bila kujua kiarabu...ikiwa umewahi kusoma lugha, pole kwa kupewa mwanga mbovu. ukisoma asili ya lugha ya kiingereza utaambiwa vingi kuhusu warumi na wajerumani... ambao kila mmoja kwa wakati tofauti alimtawala muingereza. hata mfaransa ana mchango kwenye lugha ya kiingereza. ukiisoma historia kidogo tu utaelewa hili.
kiswahili kimekopa baadhi ya maneno toka kwa waarabu as kilivyokopa toka kwa kiingereza. neno ugali halitamkwi as linavyotamkwa kwa kiswahili... si utamaduni wa muingereza kula uji mgumu ndio maana hawana neno mbadala wa ugali kwa lugha yao. je muingereza hatoweza kuongea kiingereza bila kujua kiswahili kisa kuna neno ugali na safari??
Umekuja na mambo mengi, ngoja niyapunguze ili nikujibu kwa vipande vipande na tunapoendelea mnakasha tuelewane:
Maana ya neno "ustaarabu" nnaijuwa vilivyo na hiyo uliyoisema wewe kuwa ni kinyume chake, hapana. Si sawa.
Neno "shenzi" ni neno linalotokana na Kijerumani "shaiza", unajuwa maana ya "shaiza" na kwanini Waherumani walilitumia kuwaita mababu zetu?
Tafuta maana ya neno "ustaarabu" kama haujuwi sema nikusaidie, hali kadhalika tafuta maana ya neno 'shaiza" lililoibuwa neno "mshenzi", utashangaa!
Hilo nimelitolea ufafanuzi wake juu huko kwenye hii mada, inaonesha umekurupuka na haukuipitia mada, laiti ungekuwa umeipitia mada bila kukurupuka usingelileta kwani limejadiliwa na somo limeeleweka.
neno shenzi limeanza kutumika lini? not as a mode of production slavery ili kuwepo kwa kiasi kidogo zanzibar katika karne ya 19 kulikuwa na harufu ya utumwa. ukisoma utakuta kulikuwa na wastaarabu na washenzi... mjerumani alitoka wapi hapo? yawezekana sijui. kamrudie mzee yusuph halimoja iwapo uliwahi kumsikia au kuona series ya vitabu vyake. ameeleza vizuri juu ya mstaarabu(mfuata uarabu) na mshenzi(waliopotoka, wasioamini katika mungu mmoja) ni kharam kwa muislamu kumfanya muislamu mtumwa? ikiwa ndio ambao hawakuufuata uislam waliitwaje,??
Unauliza ujinga mpaka unanifanya nicheke.
Nnakwambia neno shenzi linatokana na Kijerumani halafu unauliza limeanza kutumika lini? Hivi unashindwa hata kufanya jitihada kiduchu kujuwa Mjerumani kaja lini kwenu? Unasikitisha sana.
Halafu mara umesharukia kwa "Watumwa". Hilo la utumwa ni mada nyingine kabisa, na usirukie huko, hupawezi, maliza hili kwanza ukienda huko itakuwa rahisi kwako kuelewa hilo.
nikiri kuwa siwezi kufanya majadiliano na wewe.
ukweli ni kuwa hujibu hoja kwa hoja bali maneno ya kishabiki. sitaweza kuju(w) a wala kuandika kiarabu samahani kiswahili
Unauliza ujinga mpaka unanifanya nicheke.
Nnakwambia neno shenzi linatokana na Kijerumani halafu unauliza limeanza kutumika lini? Hivi unashindwa hata kufanya jitihada kiduchu kujuwa Mjerumani kaja lini kwenu? Unasikitisha sana.
Halafu mara umesharukia kwa "Watumwa". Hilo la utumwa ni mada nyingine kabisa, na usirukie huko, hupawezi, maliza hili kwanza ukienda huko itakuwa rahisi kwako kuelewa hilo.
tatizo unawaza kwa mapungufu. ikiwa akili yako ingekuwa kama mikono yako yenye kuweza kutanuka ukiinyoosha ingelikuwa afadhali.huwa huna hoja zaidi ya kujichekesha? nimekuambia kulikuwa na mstaarabu na mshenzi kabla ya mjerumani. kama fuvu lako la kichwa haliubani ubongo wako kubaliana nami kuwa wastaarabu walikuwa na wapinzani wao(wasio wastaarabu) waliitwaje? kuna nyeupe na nyeusi, jinga na janja,staarabu na?? nimekwambia mzee halimoja kanipa uongo niliousema unaishia kucheka
Mshenzi atakuwepo wakati neno "shenzi" limetokana na Kijerumani? kama alikuwepo hakuitwa "mshenzi".
Bado hujajibu haya:
Jee, umeshayapata haya:
Tafuta maana ya neno "ustaarabu" kama haujuwi sema nikusaidie, hali kadhalika tafuta maana ya neno 'shaiza" lililoibuwa neno "mshenzi", utashangaa!
maana ya neno mstaarabu nimekupa kwenye kila post ni wafuata uarabu... itakuwa ajabu kama kulikuwa na wastaarabu peke yao... neno shaiza kwa mujibu wa Google ni shit kwa Kijerumani. nasikitika unataka kuiliazimisha shenzi itoke kwenye shaiza
Hiyo ni singular na plural? au?
Kiswahili ni lugha ambayo imetokana na Kiarabu na Kibantu na maneno mengine machache yaliongezeka kidogo kidogo kutoka lugha zingine za Afrika, Uropa na Asia.
Kabla ya kuja wakoloni wa ki Uropa maandishi yote ya Kiswahili yalikuwa kwa herufi za Kiarabu na matamshi yalikuwa kwa lafdhi ya Kiarabu.
Nnadiriki kusema leo hii, ili uongee na kuandika Kiswahili fasaha inabidi ujuwe Kiarabu. Bila hivyo utaboronga tu.
Na kama huna ustaarabu basi Kiswahili chako hakitakuwa fasaha.
Jee, unajuwa maana ya "ustaarabu"?
hich kiajuza bn kimeach kumpa unyumba kizee mwenzake kinaleta uarab hapa;
hoja dhaifu ili uongee kiswahil fasaha lazm ujue kiarabu
onni sigala hajaxoma kiarab wala kwend madrasa bt mrumbi wa lugha
Hebu yaondowe maneno yote yaliyotokana na Kiarabu katika maandiko yako hayo tuone kama tutaelewana. Jaribu.
Naam, tukisema tukisema "kibantu" hatumaanishi kabila fulani tunamaanisha jamii ya wabantu. Na neno kubwa linaloleta muunganisho wa wabantu ni "ntu". Hiyo "ba" ya kabla ni Kiarabu. Kwa maana hiyo, hata neno "Bantu" pia lina ustaarabu.
Maana ya "ustaarabu" si "civilization" kama ulivyoaminishwa na kuamini. Tafuta maana halisi ya neno "ustaarabu" ili likuingie na uelewe. Huwezi kuwa na ustaarabu halafu ukawa "cannibal" kwa sababu Waarabu hawana historia ya u "cannibalism".
Historia ya u "cannibalism" kutokea Kaskazini tumeisoma (na ushahidi wa maandishi upo) kuwa imekuja na "crusaders" wa kutokea Uropa.
Ukiijuwa maana kamili ya "ustaarabu" utabadili maandiko yako. Kwa hiyo tafsiri yako ya kulitafsiri neno la Kiswahili kwa Kingereza, neno ambalo 100% linatokana na Kiarabu inazidi kuyakinisha maneno yangu "Nnadiriki kusema leo hii, ili uongee na kuandika Kiswahili fasaha inabidi ujuwe Kiarabu. Bila hivyo utaboronga tu."
Kwa nini neno hilo la linalotokana na Kiarabu ulitolee tafsiri isiyoendana nalo wala isiyoleta maana halisi, kwanini hutafiti kiduchu kujuwa maana yake halisi ni nini ili ulielewe na ulitumie kiufasaha?
Jee, nikusaidie kwa kukufundisha maana halisi ya neno "ustaarabu"?
Nimeuliza kwenye post namba mmoja mstari wa mwisho "Jee, unajuwa maana ya "ustaarabu"?" akheri ya wewe uliyekuwa na ujasiri wa kujaribu kulijibu swali hilo kivyako kuliko wale waliojifanya hawajaliona hilo swali wakaliogopa na kulikimbia.