Huwezi na Hutoweza Kuongea / Kuandika Kiswahili fasaha

Huwezi na Hutoweza Kuongea / Kuandika Kiswahili fasaha

Kiswahili kabla ya kuja maandiko ya Kilatini kikiandikwa kwa herufi zipi?

Kiliandikwa kwa Kiarabu lakini kuandikwa kwa kiarabu hakukifanyi Kiswahili kuwa Kiarabu! Maandishi hayana uhusiano wowote ule na asili ya Lugha!

Kwa Mfano Kiirani/Kipersia/Kiafghanistani pia vinaandikwa kwa kutumia maandishi ya Kiarabu na Je Kipersia/Kiirani/Kiafghanistani ni Kiarabu? Au unahitaji kujua Kiarabu ili uweze kuongea Kipersia/kiafghanistani?
Hapana Kiirani/Kipersia siyo kiarabu na havina uhusiano wowote ule ingawaje Kiirani/Kipersia kina maneno zaidi ya 50% ya Kiarabu hivyo Kiswahili kuandikwa kwa harufi za Kiarabu au Kilatini hakukifanyi kuwa kiarabu au Kizungu (kilatini) leo hii pia tunaweza tukaandika Kiswahili kutumia alama za Kichina je utasema kwamba Kiswahili ni Kichina?
 
Kiliandikwa kwa Kiarabu lakini kuandikwa kwa kiarabu hakukifanyi Kiswahili kuwa Kiarabu! Maandishi hayana uhusiano wowote ule na asili ya Lugha!

Kwa Mfano Kiirani/Kipersia/Kiafghanistani pia vinaandikwa kwa kutumia maandishi ya Kiarabu na Je Kipersia/Kiirani/Kiafghanistani ni Kiarabu? Au unahitaji kujua Kiarabu ili uweze kuongea Kipersia/kiafghanistani?
Hapana Kiirani/Kipersia siyo kiarabu na havina uhusiano wowote ule ingawaje Kiirani/Kipersia kina maneno zaidi ya 50% ya Kiarabu hivyo Kiswahili kuandikwa kwa harufi za Kiarabu au Kilatini hakukifanyi kuwa kiarabu au Kizungu (kilatini) leo hii pia tunaweza tukaandika Kiswahili kutumia alama za Kichina je utasema kwamba Kiswahili ni Kichina?

Sasa nisome tena post namba moja kwa utuvu. Ngoja nikusaidie:

Kiswahili ni lugha ambayo imetokana na Kiarabu na Kibantu na maneno mengine machache yaliongezeka kidogo kidogo kutoka lugha zingine za Afrika, Uropa na Asia.

Umeelewa nini hapo?
 
Sasa nisome tena post namba moja kwa utuvu. Ngoja nikusaidie:

Kiswahili ni lugha ambayo imetokana na Kiarabu na Kibantu na maneno mengine machache yaliongezeka kidogo kidogo kutoka lugha zingine za Afrika, Uropa na Asia.

Umeelewa nini hapo?

Bado SIYO kweli Kiswahili hakijatokana na Kiarabu na kibantu! HAPANA, bali Kiswahili ni lugha ya Kibantu kwa asilimia Mia Moja (100%) iliyoazima maneno (tena mengi tu) ya Kiarabu na lugha nyingine zisizo familia ya Kibantu! Kuna tofauti kubwa sana Hapo!
Na huu ndiyo Upotoshaji mkubwa sana unaofanywa na kwa makusudi kabisa na lengo lake ni moja tu divide and rule!
 
Bado SIYO kweli Kiswahili hakijatokana na Kiarabu na kibantu! HAPANA, bali Kiswahili ni lugha ya Kibantu kwa asilimia Mia Moja (100%) iliyoazima maneno (tena mengi tu) ya Kiarabu na lugha nyingine zisizo familia ya Kibantu! Kuna tofauti kubwa sana Hapo!
Na huu ndiyo Upotoshaji mkubwa sana unaofanywa na kwa makusudi kabisa na lengo lake ni moja tu divide and rule!

Hayo maneno "iliyoazima" itayarudisha lini?
 
Hayo maneno "iliyoazima" itayarudisha lini?

Nimeshaandika hapo juu HAKUNA lugha inayojitosheleza kwa 100% Dunia hii, na kila Lugha inaazima maneno kikiwemo Kiarabu chenyewe, hivyo kutaka Kiswahili peke yake ndiyo kirudishe maneno kilichoazima na kuacha lugha nyingine zote ziendelee kuazima na kutumia maneno ya lugha nyingine huko siyo kukitendea haki Kiswahili chetu! Halafu isitoshe lugha huwa zinaazima maneno na kuyaasili kuyabadilisha na kuna uwezekano mkubwa (mimi sijui kiarabu) kwamba maneno ya kiarabu tuliyoyaazima yana maana nyingine kwa waongeaji wa kiarabu yaani sisi tunayatumia vingine kwa mfano nafikiri madrasa (sina uhakika) uarabuni labda wana maanisha shule yoyote ile lakini kwetu sisi ukisema madrasa ina maana shule inayaofundisha dini na siyo shule kwa ujumla!
 
Nimeshaandika hapo juu HAKUNA lugha inayojitosheleza kwa 100% Dunia hii, na kila Lugha inaazima maneno kikiwemo Kiarabu chenyewe, hivyo kutaka Kiswahili peke yake ndiyo kirudishe maneno kilichoazima na kuacha lugha nyingine zote ziendelee kuazima na kutumia maneno ya lugha nyingine huko siyo kukitendea haki Kiswahili chetu! Halafu isitoshe lugha huwa zinaazima maneno na kuyaasili kuyabadilisha na kuna uwezekano mkubwa (mimi sijui kiarabu) kwamba maneno ya kiarabu tuliyoyaazima yana maana nyingine kwa waongeaji wa kiarabu yaani sisi tunayatumia vingine kwa mfano nafikiri madrasa (sina uhakika) uarabuni labda wana maanisha shule yoyote ile lakini kwetu sisi ukisema madrasa ina maana shule inayaofundisha dini na siyo shule kwa ujumla!

Kama unaamini Kiswahili kimeazima maneno, jee neno swahili ambalo ni kiashiria cha kwanza cha lugha ya Kiswahili nalo limeazimwa pia? limeazimwa kutoka wapi? na kabla ya hili neno Kiswahili kulikuwa kuna neno lipi?

Unajuwa kitu kimoja, wewe unataka kulazimisha kuwa Kiswahili hakikutokana na Kiarabu lakini wakati huohuo unajisahau kuwa hata neno Kiswahili ni la Kiarabu.

Matatizo uliyonayo ni madogo sana, yanayokufanya usifikirie kwa mapana na marefu zaidi ya hapo ulipofikia. Tatizo la kwanza ni unataka kuongelea lugha wakati historia hauijuwi. Kwanza anza kuchambuwa historia ndipo utapoielewa vizuri lugha ya Kiswahili imetokana na nini, kwa kuanzia:

Nifahamishe, nini maana ya neno Swahili? na Waswahili ni akina nani? ili twende vyema, kwani Kiswahili ni lugha ya Waswahili. Kumbuka, kama hauwajuwi Waswahili ni akina nani na historia yao ni ipi hutoweza kujuwa Kiswahili kimetokea wapi.

Kujitosheleza kwa lugha au kutojitosheleza kwa lugha hakumaanishi kuwa "imeazima" maneno ya lugha nyingine. Mimi nnaona ni vyema tukasema "imechukuwa" maneno ya lugha nyingine kwa maana cha kuazima hurudishwa, wewe umeshindwa kueleza Kiswahili kitarudisha lini maneno "iliyoazima". Mimi nnasema; Nisome post namba moja sentensi ya kwanza.
 
Kwanza hapa sina nnacho "kihubiri", hapa nnaandika kuwapa watu faida ya kuwa na mawazo mapana zaidi. Si wale ambao wamefikia upeo wao usiozidi urefu wa pua zao, wasioelewa wanachokipinga ni nini, wewe ni mmojawao.

Kama hukielewi umejuwaje kama ni "urongo"?

Na huo "urongo" uko wapi?

Kusema vitu vya kipropaganda, ambavyo havina ithibati ya kisayansi ni kuhubiri. Umeendelea kuhubiri bila mafanikio, kwa ushahidi wa umavi umavi na kuunga unga...

Hoja yako kwa ujumla wake ni urongo!
 
Bado SIYO kweli Kiswahili hakijatokana na Kiarabu na kibantu! HAPANA, bali Kiswahili ni lugha ya Kibantu kwa asilimia Mia Moja (100%) iliyoazima maneno (tena mengi tu) ya Kiarabu na lugha nyingine zisizo familia ya Kibantu! Kuna tofauti kubwa sana Hapo!
Na huu ndiyo Upotoshaji mkubwa sana unaofanywa na kwa makusudi kabisa na lengo lake ni moja tu divide and rule!

Ana maana kuwa Kiingereza ni Kilatini, na Kireno ni Kihispania na Kibena ni Kihehe... Kiwango cha msamiati wa kuazima kinabadilika kila siku. Mfano, maneno kutoka katika lugha ya Kiingereza yameongezeka miaka ya karibuni kutokana na kuingiliana kwa mambo ya kiteknolojia.

Siamini kama hali ikiendelea hivi Kiswahili kitakuwa Kiingereza.

Kuhusu jina, FaizaFoxy amesahau kuwa Kiswahili kina majina mengi yanayobebwa na lahaja zake, kuna Kimvita, Kimakunduchi, Kiunguja na kadhalika ila waliosanifisha miaka ile wakatumia jina walilolikuta.

Msingi wa lugha ni mawasiliano, ni upumbavu kudhani kuwa watu hawajui lugha huku wanawasiliana pasi na shaka.
 
Last edited by a moderator:
Ana maana kuwa Kiingereza ni Kilatini, na Kireno ni Kihispania na Kibena ni Kihehe... Kiwango cha msamiati wa kuazima kinabadilika kila siku. Mfano, maneno kutoka katika lugha ya Kiingereza yameongezeka miaka ya karibuni kutokana na kuingiliana kwa mambo ya kiteknolojia.

Siamini kama hali ikiendelea hivi Kiswahili kitakuwa Kiingereza.

Kuhusu jina, FaizaFoxy amesahau kuwa Kiswahili kina majina mengi yanayobebwa na lahaja zake, kuna Kimvita, Kimakunduchi, Kiunguja na kadhalika ila waliosanifisha miaka ile wakatumia jina walilolikuta.

Msingi wa lugha ni mawasiliano, ni upumbavu kudhani kuwa watu hawajui lugha huku wanawasiliana pasi na shaka.

Upumbavu ni pale unaposoma lakini huelewi unachokisoma na unatoa maana za kufikirika bila hata ya kujaribu kujibu swali uliloulizwa.

Soma post namba moja halafu kwanza jibu swali lililopo, halafu uelezee katika uliyoyasoma kutoka kwenye post yangu namba moja unachokipinga ni nini? mpaka sasa unabwabwaja na kuhororoja lakini hujaaandika unachokipinga katika maandishi yangu ni kipi?
 
Gustav Neuhaus, Mwalimu wa Kiswahili, Mhariri na Mtumishi wa Serikali ya Kikoloni, ukisoma habari zake, wakati anajifundisha Kiswahili aliona ni bora akijuwe kwa kukiandika na kukisoma kwa Kiarabu kwanini?

Mwalimu wake wa Kiswahili wakati huo 1888, Chuo Kikuu Cha Berlin alikuwa akiitwa Carl Gothiff Burtner alimfundisha Kiswahili kutumia hati za Kiarabu. Jee kwanini? Fikiri.

Chanzo: http://www.qucosa.de/fileadmin/data/qucosa/documents/9470/6_13_bromber.pdf
 
FaizaFoxy;

Nafikiri wewe ndiyo unachanganya mambo na hili jambo ni rahisi sana!
Kiswahili SIYO Kiarabu (linguistically) na hakikutokana na Kiarabu na sababu ni hii, Kiarabu kiko kwenye Familia ya semetic/Afro languages na Kiswahili siyo Semitic languages na hakina uhusiano wowote ule na Semitic languages bali kiko kwenye familia ya lugha zijulikanazo kama bantu languages ambazo asili yake ni Afrika Magharibi Niger-Kongo!
Sasa kama ungesema Kisomali au Amharic (kiithiopia) ni Kiarabu hapo ningekuelewa kwa maana zote ni familia moja ya Hemitic langauages!

Sasa kama Kiswahili siyo sehemu ya semitic languages sijui hata hoja yako imebase wapi labda kama tunabishana kienyeji tu lkn siyo kitaalamu! Kwa maana Lugha zote Duniani zimepangwa kwenye makundi, na lugha zenye uhusiano mmoja ziko kundi moja sasa kama Kiswahili kingetokana na Kiarabu basi aidha Kiswahili kingekuwa ni semitic au kiarabu kingekuwa Kibantu ni rahisi kihivyo tu!
 
Last edited by a moderator:
Barbarosa;

Bado unarudi pale pale ambapo nilikueleza kuwa unaandika bila kuijuwa historia.

Swali langu moja tu, sijuwi kama unalikumbuka, soma post namba moja mstari wa mwisho, nijibu hilo kwanza ili tuendelee vyema.

Ukishajibu hilo, sasa jibu na hili kwa kuwa umelianzisha pazuri kabisa, kwenye historia, Ubantu ulikuja lini pwani ya Afrika ya Mashariki ambako ndiyo chimbuko la Kiswahili?

Naona "argument" yako ya "kuazima" sasa haipo tena na umekubaliana nami kuwa ni kuchukuwa na si kuazima.

Kwa hiyo hapo ukumbuke, ni kuchukuwa na si kuazima kama ulivyofikiria awali.
 
Last edited by a moderator:
Kiswahili ni lugha ambayo imetokana na Kiarabu na Kibantu na maneno mengine machache yaliongezeka kidogo kidogo kutoka lugha zingine za Afrika, Uropa na Asia.

Kabla ya kuja wakoloni wa ki Uropa maandishi yote ya Kiswahili yalikuwa kwa herufi za Kiarabu na matamshi yalikuwa kwa lafdhi ya Kiarabu.

Nnadiriki kusema leo hii, ili uongee na kuandika Kiswahili fasaha inabidi ujuwe Kiarabu. Bila hivyo utaboronga tu.

Na kama huna ustaarabu basi Kiswahili chako hakitakuwa fasaha.

Jee, unajuwa maana ya "ustaarabu"?

Kwamba lazima ujue Kiarabu.
Ebu ni nipe like. DR.wangu !
 
Kama haujuwi maana ya fasaha na haujuwi maana ya lugha, siwezi kukusaidia kwa hayo, naomba rudi kwa Mwalimu wako akusaidie, hapa si kima chako.
Si kwamba sijui/sijuwi, lakini nahisi inaweza kuwa tafsiri yako na yangu zikawa tofauti na hivyo tunaweza kubishana kwa tunalinganisha chungwa na parachichi.

Kwako wewe pengine lugha sio 'nasibu' na haibadiliki (static), na hivyo 'kiswahili fasaha' ni kile kilichozungumzwa kabla ya wakoloni kutoka Uropa na kinachotumia lafudhi/lafidhi ya kiarabu.
 
Mtoa Hoja..kwa maelezo yako inamaana kiswahili ni kiarabu...na kwako kiswahili fasaha ni kiarabu ndio maana unazihusiahanisha hizi lugha kwa ukaribu hivyo...hivyo hakuna kiswahili bila kiarabu ndivyo unavyotaka kutuaminisha..labda kwa maana rahisi tuambie kiswahili fasaha ni kipi?..kiarabu ni lugha iliyo athiri kiswahili tu kama lugha zingine zilivyo kiathiri kiswahili hivyo mantiki yako kuwa uweze kiswahili fasaha ni hadi ukijue kiarabu me nakataaa kwa miguu yote na mikono
 
Back
Top Bottom