Huwezi Pinga Kuwa Dini (madhehebu yote) yamegeuka kuwa biashara zinangonya waumini. Kama una hoja utasikilizwa na kujibiwa

Huwezi Pinga Kuwa Dini (madhehebu yote) yamegeuka kuwa biashara zinangonya waumini. Kama una hoja utasikilizwa na kujibiwa

Siku moja wakati nipo kijijini nilikuwa natoka kanisani na jamaa mmoja akawa analalamika sana swala la michango kuzidi.....yule mwamba siku hizi nasikiia aliamua kuwa muislam
Shida yetu ukisema ukweli unaonekana eti unataka kuasi kanisa kimsingi unakuwa na hoja na unatakiwa usikilizwe na kujibiwa vyema. Mnashikana mashati halafu Hela zinaliwa ovyo tu. Ukweli michango Kwa Sasa inaogopesha sana.
 
Siku moja wakati nipo kijijini nilikuwa natoka kanisani na jamaa mmoja akawa analalamika sana swala la michango kuzidi.....yule mwamba siku hizi nasikiia aliamua kuwa muislam
Dizain yako kuandika uwongo jambo lionekane zuri ni chap tu,hakuna mtu labda awe mwendawazimu atauza roho yake kwa issue ndogo kama hiyo.

Muulize mleta mada akikaa kimya bila kutoa hiyo anayoiita michango kuna mtu anamfata kumuamsha akatoe?
 
Nipo tiyari kukosolewa lakini Kwa uthibitisho tu na sio mbwembwe zingine.

Kwanza hakuna kwenye biblia sehemu yoyote Ile watu walifanya harambee ya kumnunulia mtume ama nabii punda ama farasi Kwa Wakati huo maana hapakuwa na magari Wala pikipiki.

Hivyo usafiri wao ulikuwa Punda,Ngamia au farasi. Lakini bado sijawahi ona waumini/washiriki wa kipindi hicho wakifanya changizo Ili wanunue japo punda ya nabii/mtume wao.

Kwanini na sema haya? Saivi dini zimegeuka kuwa biashara kubwa sana na wengi wamekuwa wakitoboa ndani ya muda mfupi.

Sababu zake ziko wazi tu.

Hapa nitataja makanisa makubwa mawili tu kama mfano achana na miradi binafisi ya wakina Geodavie, Malisa, Mwamposa, Sunguye nk.

Tangu ni zaliwe na kukulia katika Ukristo bado sijawahi ona eti kanisa limejengwa na mtu mmoja ama hata wao wenyewe makao makuu.

Katika Kijiji chetu tulikuwa tunasalia darasani miaka ya 90 Na badae tukaanza michango tukanunua kiwanja wenyewe bila msaada wa paroko ama katekista baada ya kununua kiwanja tukafyatua matofali ya tope sisi wenyewe.

Hatimaye tukaezeka kwa nyasi. Ukumbuke mafundi ilikuwa Bure kufyatua nk Kila kitu tulifanya juu yetu wenyewe watu wakijitoa Hadi misosi Wakati wa ujenzi wa kanisa Hilo.

Baada ya kukamilisha watu walizidi kuongezeka mara dufu na hatimae tukafanya harambee na kuezeka Kwa bati na kujenga Kwa cement.

Katika kipindi hicho chote tulikuwa tunatoa sadaka na zaka tu michango ilikuwepo kama tu hapo kanisani Kuna muumini anahitaji msaada na tulikuwa tunatoa shilingi kumi ishrini na wenye uwezo watatoa shilingi200 hata 500 kabisa.

Sasa baada ya kuwa wengi na kuwa tumejenga michango ikaanza maradufu sijui ilitokea wapi hasa miaka ya 2006-2009 michango ilikuwa mingi mara imetoka jimboni au parokiani. Hapohapo tunaambiwa kumtegemeza katekista nk.

Ketekista huyu huyu mnaishi nae anakwakwe analima na kufanya Kila kazi lakini Cha ajabu anategemezwa(kuchangiwa)

Hadi Sasa michango imekuwa mingi sana na kutajirisha watu wengine tu.

Hapa ni makanisa yote hata Kwa wasabato mambo ni Yale Yale wanaweza wakaanza wao huita kundi Hilo kundi linakuwa la watu hata7 tu au chini/zaidi ya hapo.

Lakini punde wakiwa wengi tu michango na harambee kuuziwa vitabu vya roho ya unabii lesoni nk ukipiga hesabu unaona wazi kabisa hapa hizi ni biashara.

MFANO Kwa wasabato Kila baada ya miezi3 wanakuwa na lesoni mpya na wananunua na usiponunua Kuna mafungu kadhaa wakadhaa utasomewa ukitishwa kuwa hutakua kiroho utabaki Hivi Hivi miaka nenda Rudi.

Ukija kwenye vyombo vya mziki(choir) mtachangishwa kama kawaida kununua vyombo vya mziki vya kisasa. Yaani Kila kitu kinacho li husu kanisa mtachangishwa.

Lakini ikumbukwe kuwa Zaka na sadaka mnatoa Kila Leo na iwapo ikionekana matoleo yamekuwa kidogo atakuja kiongozi wa juu huko kuja kuhimiza watu wamtolee Mungu matoleo.


Kwa upande wa Roma wao wameenda mbali zaidi usipotoa michango na ikatokea ukapatwa na maswahibu basi tegemea hutapata msaada kutoka kanisani.

Ikumbukwe kule utauziwa Kila aina ya sanamu uitakayo japo sio lazima ila rozali ni muhimu utanunua Kuna kanga za bikira maria na batiki zenye picha ya yesu kabeba kondoo utauziwa. Sijui kanga za Wawata nk

Sasa Hivi tuna barua ya zawadi ya mtoto yesu ambayo tumepangiwa kiasi Cha kutoa Kwa waajiriwa!?

Ikifika kiangazi pia Huwa tunatoa shukuran ya mavuno (matomoro)
Pia Kuna matoleo maalumu Kila Misa hapa hutolewa Kila aina ya mazao inayopatikana maeneo hayo

MFANO wa matoleo hayo ni kama
Ndizi,tikiti mahindi,tambi,Mvinyo kama dompo,asali,mbuzi,kuku,mchele nk

Lakini michango Iko palepale na hawana huruma na maisha Yako.
Ukipata tatizo wewe utaombewa ila wao wakipata shida watahitaji Hela. Tuamke.

Kwa kifupi mambo ni mengi sana ambayo tunayafanya wenyewe tu bila kutegemea msaada wa wazungu (makao makuu) lakini punde tu tukikamilisha Hela zinaenda huko zote.

MFANO mkajichangisha mjenge shule ama hospital (jambo zuri ) Mtachangishana Kwa kushikana mashati Hadi shule/hospital mtamaliza lakini usitegemee eti Kwa sababu mlichangia Kwa kuuza kuku na mbuzi wako Ili ijengwe Ile shule utapata japo discount kidogo tofauti na yule hajachanga kabisa Bali ada utatoa kama kawaida na mtoto wako atarudishwa tu iwapo utachelewa kumlipia ada yake.

Cha ajabu ni kwamba Watoto wa wachungaji watasoma Bure Watoto wa maaskofu watasoma Bure kabisa licha kuwa hawo wachungaji wanalipwa mishahara minono kuwazidi Hadi waalimu.

Hapohapo wanaosomeshewa Watoto wao Bure usafiri wananunuliwa,nyumba anaishi Bure Tena nzuri chakula umeme na maji washiriki wanalipia.

Choo kikijaa kanisa litahusika kutoa Hela ya mzibuaji. Sasa unakaa unajiuliza inakuwaje hii na watu Bado hatuzinduki na kupinga haya mambo. Na hata itokee kanisani labda Kuna mtoto wa masikini asiye jiweza kusomesha na ana akili na hata kanisani ana mahudhurio mazuri namna Gani hawezi soma Bure otherwise washiriki washikane mashati kumchangia la sivyo hata soma abadani.

Nimesikia wasabato Hadi wamepelekana mahakamani Kwa kula rushwa mamilion ya kanisa. Hao wanaitwa watumishi wa Mungu wamemuibia Mungu Hela na suruhisho ni mahakamani Wala sio Kwa Mungu Tena.

Nimezungumzia makanisa mawili haya kama mifano achana na wajasiriamali wa hadharani kama nilivyo wataja hapo juu Hawa wameiga na kuja kiubunifu zaidi.

Ndio maana wanauza maji,vitambaa, mchanga na mafuta ya upako.Hawa wameiga tu.

Ifike mahala Sasa tutoke usingizini tupinge maana niliwahi kusikia mchungaji wa kisabato akisema michango itazidi kurindima Hadi yesu arudi. Kwa maana ya haraka yesu asiporudi mapema kazi tunayo na pona yetu yesu arudi mapema.

Nimeekeza Kwa uchache sana lakini yapo mengi zaidi yanafanyika.

Waafrica Vijana wenzangu wapo tiyari kuunda kwaya wakachangishana na kununua vyombo vya mziki vya mamilio ya shiringi. Lakini hao hao hawawezi kujichangisha walau wawe na kiwanda japo Cha kutengeneza sabuni kamwe hawawezi.

Tupingeni biashara hizi zilizo kuja Kwa mgongo wa dini.


Kwa maelezo haya yote naomba kujuzwa wapi kwenye biblia kumewahi kuwa na mshike mshike kama tulio nao Sasa?

NB: Usilete habari za Anania na safira hapa.View attachment 3178150
Dini ni Utapeli, dini ni.uzwazwa, dini ni chanzo cha ubaguzi
Kwenye dini na madhehebu ndio maficho ya majambazi, wauaji, watekaji. Waizi na wazinzi.

Dini ni chanzo cha vita, dhambi nyingi zimejificha humo.

Ewe Mtanzania epuka hu utapeli wa mchana kweupe.
Hiyo Mbingu wanayokuhubiria wao hawaitaki? Mbona wanazini na wake za watu, mbona wanaroga, wanazaa nje?
 
Kwenye uislamu hizi mambo hakuna nakumbuka kuna kioindi Nilipata ajali nukasalimika nilienda kutoa sadaka ya Shukrani kanisani 300k sijui ile sadaka ilifanyiwa nini ?

Hakika tuzinduke Vijana hizi dini hasa ukristo kwa sasa zinaonekana ni mawazo ya binadamu kutengeneza pesa tu.
Dini ni chanzo cha vita, dini zinakunyima amani ambayo Mungu alikuumba nayo. Angalia Somalia, Sudani, Gaza, Syria na Yemeni.

Dini usiziamini.
Ushoga na usagaji umejificha humo. Kimbia Braza acha kupoteza muda wako.
 
KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani Wana biashara za shule, vyuo vikuu, hospital, majengo ya biashara, nyumba za wageni na Bado Wana skendo za kutapeli watu mashamba Bagamoyo

Karibia taasisi zote za dini Zina hizi biashara na michango Iko palepale. Mnanyonywa Hadi basi
 
Christianity is a business, Jesus is the Product, Church members are the Customers, Church leaders are the Beneficiaries.

Ukristo ni biashara, Yesu ni Bidhaa, Waumini ni Wateja, Viongozi wa kanisa ni Wanufaika.

Amkeni nyie mtaibiwa hadi lini?

Wake up you people!

Jikomboeni kutoka kwenye utumwa wa hizi imani za kidini.
Nimeshawakomboa watu kama sita wanawake wawili na wanaume wanne, wamenishukuru sana.

Dini na mashehebu ni vyanzo vya kuzalisha hofu na uhasama kwenye jamii.
Mafundishi yao yako hivi

1. Wanakuroga ndio maana huolewi
2. Wanakuroga ndio maana biashara zako zinakufa
3. Wanakuwangia ndio maana unaumwa umwa.
4. Wanakuonea wivu majirani zako ndio maana watoto wamwkuwa wahuni.
5......yaani upuzi mwingi sana. Hata ndugu siku hizi hawakaribishani wala kutembelea kwa hofu ya kurogwa na mikosi
 
Dini zote ni biashara ya kumuuza Mungu asiyethibitishika kuwepo kutatua matatizo yaliyoshindikana kwa watu wasiojielewa.
Eti Mungu ambaye ni Mfalme wa Amani ameshindwa kuleta Amani Gaza, Syria, Congo, Sudani, Somalia, na Tanzania( wasiojulikana).

Huyo Mungu mbona anatia mashaka sana.
 
Eti Mungu ambaye ni Mfalme wa Amani ameshindwa kuleta Amani Gaza, Syria, Congo, Sudani, Somalia, na Tanzania( wasiojulikana).

Huyo Mungu mbona anatia mashaka sana.
Mungu ni chaka tulilolitengeneza wenyewe ili tupate sehemu ya kutupia matatizo yetu yote ambayo hatujaweza kuyatatua tuyafiche humo mpaka tutakapoweza kuyatatua.
 
Pastor Mgogo alishasema mbinguni hakuna account fedha inaliwa hapahapa
Christianity is a business, Jesus is the Product, Church members are the Customers, Church leaders are the Beneficiaries.

Ukristo ni biashara, Yesu ni Bidhaa, Waumini ni Wateja, Viongozi wa kanisa ni Wanufaika.

Amkeni nyie mtaibiwa hadi lini?

Wake up you people!

Jikomboeni kutoka kwenye utumwa wa hizi imani za kidini.
Sasahivi ni biashara kabisa kuliko kipindi chochote kile.
 
Nimeshawakomboa watu kama sita wanawake wawili na wanaume wanne, wamenishukuru sana.

Dini na mashehebu ni vyanzo vya kuzalisha hofu na uhasama kwenye jamii.
Mafundishi yao yako hivi

1. Wanakuroga ndio maana huolewi
2. Wanakuroga ndio maana biashara zako zinakufa
3. Wanakuwangia ndio maana unaumwa umwa.
4. Wanakuonea wivu majirani zako ndio maana watoto wamwkuwa wahuni.
5......yaani upuzi mwingi sana. Hata ndugu siku hizi hawakaribishani wala kutembelea kwa hofu ya kurogwa na mikosi
Alafu Mrogaji Kama Si Jirani Yako Basi Ndugu Yako Wa Karibu,,Rafiki n.k Kwanini Vita Visizuke?Wanachonganisha Watu Huku Mitaani,,Wajitahidi Kuhubiri Upendo Na Kuchapa Kazi Zaidi
 
Mkuu umeandika vingi sana kwa upande wako unaweza kuwa na hoja but kwangu hainiingii akilini,miaka ya nyuma Kanisa Katoliki lilikuwa linapata misaada kutoka nje ila toka 2000s misaada ikakatwa so waamini wenyewe sisi ndiyo tunapaswa kulisimamia,kutoa sadaka hakufilisi kama unatoa kwa akili ulizojaaliwa na Mungu,watu hela tunahonga,tunakula beers michango ya harusi tunachanga vitu vya hovyo kabisa lakini kuiheshimu imani tunashindwa.

Lengo siyo kujisifia,hapo chini nimeenda leo kununua column speakers kwa ajili ya Kanisa lililonilea kijijini kwetu baada ya kuhudhuria ibada mwezi august nikasikia moja ya mipango ya Paroko ni kubadilisha spika zilizokuwepo (za radio) hazifai zinunuliwe nyengine,nimewiwa tu kushiriki ktk hilo na siyo kwamba nina hela nyingi sana.picha nilizipiga kwa ajili ya kumbukumbu zangu ila bahati mbaya sana nazitumia hapa naweza kuonekana kama najivuna but sivyo lengo langu ni ili watu wajue hata kama imani zao zimelala wapo bado ambao zipo hai.
IMG_20241216_151006.jpg
IMG_20241216_145720.jpg
 

Attachments

  • IMG_20241216_151006.jpg
    IMG_20241216_151006.jpg
    432.6 KB · Views: 1
Back
Top Bottom