Huyu abiria wa Mwendokasi kanikera sana, Wabongo tutaacha lini hizi tabia za kueleza mambo binafsi kwenye "public"?

Huyu abiria wa Mwendokasi kanikera sana, Wabongo tutaacha lini hizi tabia za kueleza mambo binafsi kwenye "public"?

Mwache mwamba atumie Uhuru wa kuzungumza
Tanzania wote ni ndugu naamini abiria wenzake walitamani jamaa aendelee kuongea tu, Tanzania nchi nzuri unaongea kwa uhuru ata kama mtu humjui
 
Leo asubuhi wakati nimepanda mwendokasi kuna mwamba mmoja nimekutana naye siyo mara ya kwanza mimi kumkuta kwenye gari, nadhani kama sijakosa itakuwa mara ya pili au tatu.

Sasa huyu mwamba alikuwa akipiga stori na mtu aliyekuwa amesimama naye karibu, nadhani wanafahamiana, sasa huyo jamaa ninayemzungumzia hapa akawa ndio msemaji mkuu, yule mshkaji mwingine akawa anaitikia tu au kuchombeza kidogo kidogo.

Kwa kuwa asubuhi kulikuwa na utulivu na asilimia kubwa ya abiria tukawa tunawaza mishe zetu tunazoenda kuzifanya kwenye purukusani zetu, jamaa akawa anazungumza kwa sauti kubwa, siyo kubwa kiasi cha kukera, Hapana ila ilikuwa kubwa kiasia ambacho wote waliomzunguka ni kama wanamsikiliza yeye.

Jamaa akaanza kuwa anazungumza kuhusu maisha yake binafsi, mara yeye na mkewe mara majirani zake, mara fulani kafanya hivi na ningekuwa mimi ningefanya hivi…

Yaani kwa ufupi ni kama alikuwa anawasimulia watu ambao hata hawamjui kuhusu mambo yake binafsi, kibaya zaidi stori nyingine zikawa unaona kabisa hii ni uwongo ila anaongeza chumvi ili aonekane mwamba, ni ushamba tu.

Hii michongo ya kuzungumza mambo yetu binafsi Watanzania sijui tumeitoa wapi, yaani likitokea tukio kidogo tu mtu anadakia na kuanza kuelezea “Mimi ni hivi…” mara utasikia “Achana na hiyo, mimi yalinikuta…”

Wabongo tuache ushamba, kwani mtu hauwezi kuzungumza kwa sauti ya chini tu na ukasikika na huyo uliyenaye karibu yako, unaongeza sauti ili watu wakusikilize wewe ili iweje, tena wengine wanaenda mbali na kuzungumza kuhusu maisha yao binafsi kabisa na kuhisi ni sifa.
Ki saikolojia ni jambo zuri anatema nyongo
 
Mleta mada utakuwa mshamba na Dar

Dar unatakiwa ku mind your own business.
Usipende kutega tega misikio yako kama bwege kusikiliza wengine wanaongea nini.

Kifupi wewe una masikio ya umbeya na midomo ya umbeya. kaa mbali na umbeya uwe wa mwendokasi au popote.

Watu wa kuja washamba wa vijijini huko mnatia aibu
 
Mmh kwani ilikuwa lazima kumsikiliza sema na wewe ulitega sikio sanaaa ukanogewa na story za jamaa
 
Afya ya akili ni muhimu sanaa (punguza kubeba yasiyokuhusu na kupeleka kwingine)
 
Jf members wote tunamiliki magari yetu binafsi wewe ulitakiwa uwe mwanachama wa fb cause hauna gari
Te te te te nimesoma comments zote nimeona za kawaida tu kwa kuwa imenionesha levo zao za ufikiri, ila hii imenifanya nicheke, asante sana kwa kunipa tabasamu. Nami nitapambana ninunue gari langu.
 
Mleta mada utakuwa mshamba na Dar

Dar unatakiwa ku mind your own business.
Usipende kutega tega misikio yako kama bwege kusikiliza wengine wanaongea nini.

Kifupi wewe una masikio ya umbeya na midomo ya umbeya. kaa mbali na umbeya uwe wa mwendokasi au popote.

Watu wa kuja washamba wa vijijini huko mnatia aibu
Ndio nimeingia Dar wiki iliyopita bwana mkubwa.
 
Wacha kulalamika ,tafuta pesa ununue usafiri wako binafsi. Kama unaona mwendokasi jau ,ita uber ikupeleke unapokwenda uache kupangia watu maisha.
 
Kama unakereke nunua lako tu mbona kule kwenye madaladala wanagonga singeli kwa kwenda front tena full blast hamsemi? uhuru umerejea baada ya jiwe kufa, ukute alikua jela sasa ameamua kutumia uhuru wake vyema kabisa katika nchi ya mama yenu
 
Nipo nasoma spana ninazopigwa, nasoma kwa umakini sana sana sana
Achana na wahuni wa jamiiforums hawa wanaojifanya wote wanamiliki magari.

Wengine makapuku tu wanaoshindia mihogo.

Lakini ndio hivyo tena kwenye mitandao tunavumilia every tom and jerry.
 
Wacha kulalamika ,tafuta pesa ununue usafiri wako binafsi. Kama unaona mwendokasi jau ,ita uber ikupeleke unapokwenda uache kupangia watu maisha.
Uko sahihi mtu anakerwa kwenye basi badala ya kutoka kwenye basi na hasira za kutafuta pesa anunue gari yake binafsi anatoka na hasira ya kilichomkera kwenye basi

Mimi kuna siku basi limejaa tumesimama wima tumejazana kibao abiria mmoja akanikanyaga mguuni nikamwambia mbona unanikanyaga.Akanijibu kama hutaki kukanyagwa kwa mjazono huu shuka kakodi taxi .Nilinyamaza kimya nilishuka na hasira kuwa lazima nitafute gari yangu binafsi niepukane na hiyo adha.Na ndoto alitumia

Ukikerwa nyumba ya kupanga usiwe na hasira na wapangaji au wenye nyumba katafute yako.Hasira zipeleke kwenye kutafuta yako
 
Back
Top Bottom