Huyu Dereva tax atanivunjia ndoa yangu, nifanyeje?

Huyu Dereva tax atanivunjia ndoa yangu, nifanyeje?

maamuzi uliyofanya ni ya pupa na umemwaibisha mumeo, kutembea na dereva tax wenu ni aibu kubwa!

huko ulipoenda kwenye suluhisho la pili nako muda si mrefu utakuja tena kuomba msaada wa ushauri...

mumeo nae ana shida kwani kutengeneza fumanizi la kushtukiza ni kukuaibisha na wewe pia, nadhani busara itumike hapo, ila ugumu uliopo ni kuwa wewe tayar uaminifu kwa mumeo haupo.
achana na huyo kidumu chako, kaa na mumeo muyamalize ya dereva tax msiaibishane

swala la mumeo kutofanya vizuri kitandani sio la kulisemea hadharani, jaribu nawe kutafuta suluhisho si la mwanaume nje ila kuhakikisha mumeo anakula vizuri vyakula vya kutia nguvu mwaili.
 
Heheeeeeiya wasafi classic...
Akati kuna wengine mnafirigisa wake za watu huko kwenye magroup Watsap mxiiieew.

Bibie usikubali kufumaniwa aibu itakuwa yako mwenyewe.
Pia unaweza tengeneza mwendelezo wa visasi
Ukaja ukapigwa mande.
 
Mengi sitaki hata kuuliza ila, Hivi wajua kuwa hakuna fumanizi bila wote wawili kukutwa uchi? Sasa weye waona vyema tu kuanika machuchubaa yako nje nje watu wakuangalie? Je, ikiwa huyo mlevi wako (mumeo) atacheleweshwa kumalizia glass ya mwisho akute taxi dreva yupo mzigoni. Unaonaje hao mabaunsa keshoye wakija kukuomba wachungulie tuu kwa macho walichokiona? Je wakiamua kukufuatilia nyendo zako za IBAADA KUU na huyo God fearing man wako, naye utaruhusu wamuoe??
Dada, utavuna unachotaka kupanda
 
Yaani mke wa ndoa unapigwa pu.mbu kwenye
gheto la kuazima kwa mshikaji...??
wewe ni zaid ya kahaba.

Mkuu mimi ndio maana siji kuoa!!!!
" ?hata nikitaka kuoa niambie ntamuoa nani?/
watu wana watu wao wengine toka zamani/
ukiambiwa we ni boyfriend haimaanishi uko
peke yako/
wadogo usoni wanahifadhi wazee wako/
sijui ni dhiki au tamaa tu??/
watoto wanaanika njaa tu/
hawafikirii mapenzi wanachoona wao ni
mkwanja tu/?"
 
Hilo suluhisho lilikuwa na kubomoa au kujenga??

Imeandikwa mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba yake mwenyewe.

Na mtoa mada bado anipenda ndoa yake hilo unaliona hata anavyoelezea. Kama kisa ni cha kweli mpeni mawazo ya kujenga.
na ndio maana kuna sehemu ya uzi wake nimehighlight nimeshindwa kuuliza namalizia zapper yangu nirudi
 
Mkuu mimi ndio maana siji kuoa!!!!
" ?hata nikitaka kuoa niambie ntamuoa nani?/
watu wana watu wao wengine toka zamani/
ukiambiwa we ni boyfriend haimaanishi uko
peke yako/
wadogo usoni wanahifadhi wazee wako/
sijui ni dhiki au tamaa tu??/
watoto wanaanika njaa tu/
hawafikirii mapenzi wanachoona wao ni
mkwanja tu/
?"
heshima pesa ndevu urembo
 
Daah...kweli wee umalaya ni tabia yako, umetafuta tu sababu ya kuchepuka. Huna ushahidi wa kutosha kuwa mumeo anachepuka ila umedai nawe unachepuka kupata kitulizo. Kwa taarifa yako hutafuti kitulizo, unatafuta kadhia ambayo umekaribia kuipata. Akifuminiwa tax driver unadhani wee utabaki na jina safi? Unadhani hakuna wanaojua kuwa kashakulala mara 6 kwenye mageto ya jamaa zake? Unadhani watakaa kimya? Umalaya ni kipaji chako usisingizie sababu zingine.
 
na ndio maana kuna sehemu ya uzi wake nimehighlight nimeshindwa kuuliza namalizia zapper yangu nirudi
Sweet16 ukimalizia upite hapa kwangu tumalizie hii J&B tuweze kuelewa hili jambo
 
Last edited by a moderator:
Halafu dada kama huyu ukimkuta anaomba kanisani anajifanya kajazwa na Roho Mtakatifu hadi kanisani wengine hawasikilizani!!!
Mungu aturehemu kweli!!!
 
~Mwili wako ni hekalu la Mungu hebu fikiri unavyolichafua.
~kila mke awe na mume wake mwenyewe, ona unachofanya.
~Sifa ya mtu ambaye ni "God fearing" ni kujiepusha na uovu na kutokukubaliana na matendo ya uovu.
~Wewe ni mwanamke uliyeamua kuibomoa nyumba yako kwa mikono yako mwenyewe.
~Heshima ya mumeo inashuka , na dharau kutoka kwa munaoabudu nao.
~Mbaya zaidi badala ya kumfanya arudi kwa Mungu mumeo unazidi kupoteza kwa matendo yako maovu.
~Umeonja nje na tayari umeanza kuexperience utamu tofautitofauti. Hii tabia itakutesa sana hautaridhika na mumeo, kila mwanaume utatamani uone yukoje. Na bahati mbaya sana watu hatufanani, kwa hiyo hautatosheka hata siku moja. ukisikia kuwa mtumwa wa shetani ndiyo huko sasa uliko wewe. Atakutumikisha apendavyo na mwisho wa utamu kuna uchungu, utaishi maisha ya hofu, utu wako unadharaulika, ndoa yako iko mashakani, watu watakujua kumbe ni malaya n.k
 
hii makala Ishawahi kuandikwa kwenye gazeti la Ijumaa Mwandishi Akiwa ni Bro Joseph Shaluwa ingawa umejaribu kuibadilisha sana lakini kuna Vitu bado umesahau kuviondoa...
 
ahaaaa!! ngoja nkamwambie dereva tax aache kukusumbua ili asije akaliwa
 
Kama wewe ni mke wa mtu, ungetafuta mume wa mtu.
 
Unasema kuwa mume wako ana kimada wakati hujawahi kumshika na huyo kimada wa kumkamata na kitu chochote ambacho kinaweza kuthibitisha kuwa ana kimada. Sasa kama hujawahi kumfumania wala kumshika na uthibitisho wowote kuwa ana kimada umejuaje kuwa mumeo ana kimada? Au wewe ndo aina ya wale wanawake ambao wakiambiwa kitu huamini moja kwa moja bila ya kufikiri na kufanya utafiti? Na kama hukuwahi kumfumania mumeo wala huna uthibtisho wowote kuwa mumeo ana kimada huoni kuwa utakuwa unasbabisha ugomvi usiokuwa na msingi na kumhukumu mwenzio kwa kitu ambacho usichokuwa na uhakika nacho?

Na kwa nini uliamua kumsaliti mwenzio? Wakati unafunga ndoa uliapa nini mbele Mungu na sasa hivi unafanya? Hata kama mumeo alikusaliti kweli haina maana na wewe ulipe kisasi kwa kumsaliti pia, eti kwa kuwa mwenzako amekanyaga mkojo basi wewe ndo unaamua kukanyaga mavi kabisa au kwa kuwa mwenzako amemwaga mboga basi wewe ndo unamwaga na ugali kabisa.

Haya niambie umepata faida gani baada ya wewe kuchepuka huko nje? Ama kweli akili ni nywele na kila mtu ana zake na ndio maana hata neno la Mungu linasema "Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe." Nakutakia kila la heri katika kuivunja ndoa yako and always remember every decision you make has its consequences.
 

Ndoa ulishaivunja toka siku amekugegeda...
.. Hayo mengine ni formalities tu
 
Back
Top Bottom