Huyu Jenista Mhagama kuondoka Utumishi ilikuwa suala la muda tu!

Huyu Jenista Mhagama kuondoka Utumishi ilikuwa suala la muda tu!

Ni kweli kabisa tatizo la watawala wanadhani kila mtanzania ana njaa na kwamba anatamani uteuzi ili agange njaa. Lakini tatizo hilo wa kulaumiwa sio Jenister bali wa kulaumiwa wa kwanza ni mamlaka ya uteuzi.
Mamlaka ya uteuzi in lawama kubwa, lakini washauri wanaohusika wizarani, hususan waziri, naye ana sehemu yake ya lawama.

Alitakiwa kushauri kinachotakiwa kufanywa, kwamba vetting ihusike na kuarifu watu kabla ya teuzi kutangazwa.

Ushauri wake ukikubalika, amechangia kufanya mchakato uwe bora.

Ushauri wake usipokubalika, anapima jambo, kama ni kubwa au dogo.

Kama jambo ni kubwa, anawajibika kujiuzulu, ili asiwe katika serikali ambayo katofautiana nayo katika jambo kubwa.

Kama jambo si kubwa, aanawajibika kukubaliana na ukweli kwamba ushauri wake haujakubalika, na kuendelea kuwa katika serikali kwa kujua kwamba lawama zozote zitakazokuja zitawakumba wote serikalini.

Hiyo ndiyo "collective responsibility".
 
Huyu mama amakuwa katika Cabinet muda sasa. Lakini wizara ambazo ameziongoza ni zile ambazo haziko mainstream, yaani hazitajwi siku hadi siku.

Lakini nilipoona uteuzi wa ma DC unakataliwa na wateule, na hivyo kumuaibisha sana mheshimiwa Rais Samia, nikajua kuna tatizo na mchakato na mamlaka za uteuzi.

Ilikuwa aibu tosha kwa Rais, anapomteua mtu, halafu mteule anasema "No Thanks"

Mchakato wa teuzi za viongozi waandamizi nchini inahusisha vyombo vingi vya uchunguzi, pamoja na kumhusisha mteule kama ataiweza kazi anayopewa.

Kwa wenzetu nchi zilizoendelea wanaenda hatua zaidi kwa wateule kuhojiwa na bunge au kamati zake.

Sasa lile sakata la wateule kukataa teuzi nikajiuliza huyu mama Jenista Mhagama , anaiweza kweli kazi aliyopewa?
Daah alituahidi ajira 1700+ akiwa bungeni kutoka database kasepa bila mkeka kuachiwa.

sijui simba chawene anaweza utoa huo mkeka ,maana majobless njaa inatuua huku mtaani, elfu 4 za wahindi viwandani tabu tupu.
 
Ukuu wa wilaya kama hupendi makando kando ya ofisin haufai.mshahara wa mkuu wa na maposho kwa mwezi haizidi 7mil .ila inqvirushwa vingi
 
kwa huyu, inawezekana siyo jinsia tu...hata uchawi unaweza ukawemo!
Bwana Madelu alisha thibitishia umma wa watanzania ndani ya bunge kwamba wabunge wanaelewa zaidi mambo ya uchawi kuliko hoja za kuijenga nchi
 
Huyo Jenister hana uwezo wote wa kuongoza wizara. Kavuruga huko utumishi na Sasa hata madaraja tu ya watumishi yemekwama hawapandi tena kwa wakati
 
Mamlaka ya uteuzi in lawama kubwa, lakini washauri wanaohusika wizarani, hususan waziri, naye ana sehemu yake ya lawama.

Alitakiwa kushauri kinachotakiwa kufanywa, kwamba vetting ihusike na kuarifu watu kabla ya teuzi kutangazwa.

Ushauri wake ukikubalika, amechangia kufanya mchakato uwe bora.

Ushauri wake usipokubalika, anapima jambo, kama ni kubwa au dogo.

Kama jambo ni kubwa, anawajibika kujiuzulu, ili asiwe katika serikali ambayo katofautiana nayo katika jambo kubwa.

Kama jambo si kubwa, aanawajibika kukubaliana na ukweli kwamba ushauri wake haujakubalika, na kuendelea kuwa katika serikali kwa kujua kwamba lawama zozote zitakazokuja zitawakumba wote serikalini.

Hiyo ndiyo "collective responsibility".
Hapa waziri anabebeshwa lawama zisizo za kwake, kwa sasa marais badala ya kushauriwa na mawaziri wao wanawashauri mawaziri πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ mawaziri wengi nao kwa sasa mambo mengi wanakutana nayo mitandaoni kama sisi. Lakini hata hivyo waziri wa maDC ni waziri wa TAMISEMI ambaye kimsingi kabisa kama hoja ingekuwa wale maDC kugomea teuzi alitakiwa awe wa kwanza kuwajibishwa. Kwa hiyo nahitimisha tu kwamba uhamisho wa Jenister have nothing to do with alichokisema mtoa hoja bali ni mapenzi ya rais tu na kuamua kuwahamisha au ana sababu nyingine tusiyo ifahamu ila sio iyo mtoa hoja anayoifikiria
 
Mkuu mamlaka ya uteuzi unatayarishiwa wateule na kuwa vet, yaani kuwachunguza kupitia vyombo vya dola.
Hapo ndio Jenistaer anahusika na kulaumiwa vile vile.
Nadhani ungeiweka kama ni hisia zako wala sio uhakika asilimia mia kwamba hiyo ndo sababu iliyomuondoa.
Pili, hao wakuu wa wilaya wako chini ya TAMISEMI hivyo wa kwanza kuchukuliwa hatua alitakiwa kuwa Kairuki.
Tatu, kwa teuzi zinazofanyika sasa inaonekana veting haifanyiki totally maana kwa matendo ya wateuliwa wangefanyiwa veting wasingefikiriwa hata kupewa ukuu wa familia.
Nne anayefanya veting sio waziri ni wataalamu hasa wa usalama maana waziri hana utaalamu zaidi ya kupewa ripoti hivyo kumuhukumu kwa kosa hilo inakuwa siyo sahihi.
 
Hapa waziri anabebeshwa lawama zisizo za kwake, kwa sasa marais badala ya kushauriwa na mawaziri wao wanawashauri mawaziri πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ mawaziri wengi nao kwa sasa mambo mengi wanakutana nayo mitandaoni kama sisi. Lakini hata hivyo waziri wa maDC ni waziri wa TAMISEMI ambaye kimsingi kabisa kama hoja ingekuwa wale maDC kugomea teuzi alitakiwa awe wa kwanza kuwajibishwa. Kwa hiyo nahitimisha tu kwamba uhamisho wa Jenister have nothing to do with alichokisema mtoa hoja bali ni mapenzi ya rais tu na kuamua kuwahamisha au ana sababu nyingine tusiyo ifahamu ila sio iyo mtoa hoja anayoifikiria
Ukishakubali kuwa katika serikali inayoteua watu kabla ya kuwaarifu, umeshakubali lawama zitakazotokana na hatua hiyo.

Inawezekana waziri huyu asihusike moja kwa moja, lakini hili suala linafanya baraza zima la mawaziri liwe lime fail.

Hili si suala la minute ministry policy, hili ni suala la overall good governance.

Kwa hivyo, inawezekana una point kwamba huwezi kumsema Mhagama kwa hili kwa kuwa ni la TAMISEMI.

Lakini, huwezi kumuondoa waziri yeyote kwenye lawama za serikali inayoteua watu kabla ya kuwataarifu.

Inaonekana baraza zima la mawaziri linacheza.
 
Siyo vyema kumlaumu Jenista kwa kuteuliwa katika nafasi alizowahi kuwepo. Wanaomshauri Rais kwa mfumo uliyopo ndiyo wenye lawama.

Uwezo wake ni mdogo kiuelewa na elimu yake ya kuunga. Ila mzuri katika fitina na maneuvering of things.

Wazee wa vetting wafanye kazi zao vizuri na utaratibu wa performance evaluation ufanye kazi. Kinyume cha hivyo wateuliwa hawawezi kulaumiwa.
 
Huyo Jenister hana uwezo wote wa kuongoza wizara. Kavuruga huko utumishi na Sasa hata madaraja tu ya watumishi yemekwama hawapandi tena kwa wakati
Hata taasisi na mashirika ya umma aliingilia utendaji wao na kupelekea malalamiko na utendaji mbovu,
Taasisi inataka kuajiri kibali kinakaa miaka miwili, jenista anajizungusha tu kwenye kiti yeye na ndumbaro kakake
 
Kawaida wateuliwa huulizwa kama wanaitaka kazi kabla ya kutangazwa.

Tanzania inaonekana watu wanabambikwa kazi bila hata kuulizwa kama wanaitaka, wakitegemewa wafurahi tu kwa sababu ni uteuzi wa rais. Hili ni jambo la kijinga sana na moja ya sababu utendaji unakuwa na matatizo, mtu anapewa kazi ambayo hata hakuiomba na pengine haijui.

Na katika zama hizi ambapo wengine wana taaluma zao na biashara zao, ukimbambika mtu kazi ambayo iko nje ya malengo yake matokeo yake ndiyo unapata hayo majibu ya "No, thanks".

Rais anaaibika.
Tatizo tunaishi kwa kukariri. Jinsi wanavyoitafuna nchi basi wanaamini kila mtu atakuwa na shauku ya kuwa sehemu ya utafunaji. Ndio maana ilikuwa jambo la ajabu sana kwa mtu kukataa teuzi.
 
Tatizo tunaishi kwa kukariri. Jinsi wanavyoitafuna nchi basi wanaamini kila mtu atakuwa na shauku ya kuwa sehemu ya utafunaji. Ndio maana ilikuwa jambo la ajabu sana kwa mtu kukataa teuzi.
Actually aliyekataa uteuzi anajielewa vizuri zaidi.
Na fedheha kubwa zaidi ni pale aliyekataa uteuzi kuambiwa atachukuliwa hatua za kinidhamu!

Kazi imesha kosa mvuto- maana sasa imekuwa adhabu.
 
Back
Top Bottom