Huyu Kamanda wa Jeshi anatukera sana wakazi wa Mbezi

Huyu Kamanda wa Jeshi anatukera sana wakazi wa Mbezi

Niliwahi kukutana na davis mwamunyange kwenye foleni tena akiwa hana ata gari yenye 4 stars plate number nilimgundua alivyofungua kioo ndio nkampungia mkono CDF huyu makini kabisa kupata kutokea ktk nchi hii
kweli mkuu jamaa ni mtu sana yule..,,..roho safi sana alafu hana makuu
 
Alafu Sio Kweli boss. Huyu upitaji wake ni tofauti na wengine.
Yeye wala hatugandishi kwenye Foleni.
Yeye anaumba njia tu mnampisha kidogo akipita mnaendelea.
Sema kwa njia hii kwa Mida hiyo uliyotaja boss unategemea utiririke?
Hakikisha kila siku u ayoenda town saa 06:30 upo Mwenge. Uone utakavyoifurahia njia hii.
Kama mimi tu yaan burudaaan kabisa.
Aman iwe nawe.
Habari wana jamvi,

Kwa wale wakazi wenzangu wa Mbezi Beach, Kunduchi, Goba na watumiaji wa barabara ya Bagamoyo kwa ujumla
bila shaka Mtakuwa mmekutana na huyu Kamanda wa Jeshi (Chief of Staff) ambaye kuanzia majira ya kila siku Asubuhi 12:30- 1:00 hutugandisha kwenye foleni kwa muda mrefu kila siku akisubiriwa kupita yeye na ma MPs wake wanaoning'inia kwenye milango bila sababu ya Msingi na wakati mwingine waki ning'inia na Bunduki na mavazi kama tuko Afghanistan...wakifokea watu barabarani kukaa pembeni tena wakiwa kwenye wrong Lane!

Binafsi ananikera sana, kama anahitajika kufika ofisini mapema si atoke mapema kama wengine...😡 au ndio Madaraka ya Kulevya?
Kuna siku niliwahi kuongozana na gari ya Waziri wa Ulinzi toka Uwanja wa ndege wa Dsm hadi hadi nilipofika Mwenge nao wakiwa kwenye foleni bila hamaki wala papara.

Hebu mfikishieni salamu huyu Kamanda, awaambie walinzi wake kuwa wastaarabu na kutotukera wananchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ndio tatizo LA viongozi wengi wa Africa,hao walinzi wake huwa kama majambazi,kufokea watu,kama vile walichokibeba,ni kitu nyeeeti sana,
Mimi huwa najiuliza,kama wao ni wanajeshi waliobobea kwenye medani za kivita,kwanini wanakuwa na papara wanapokuwa wanamsindikiza kiongozi wao?kwanini wasikae kwenye foleni,kimya kimya,bila mbwembwe,wamlinde boss wao vzr,bila papala,maana wanachokifanya,huwa ni "Ku atract attention" kiasi kwamba kama kuna watu wabaya wanaweza kumdhuru boss wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyu mtoa Mada kamuonea tu jamaa.
Ni kweli ana Ving'ora lakini sio vya kutugandisha.
Jamaa king'ora chake ni upishe apite dhen unaendelea.
Kama mjanja unaunga naye na unatobia. (Nishafanya hivyo mara4)
Sema kwa mida hii kwa njia hii hata kama hapiti mtu, folen inakuwa imeshakamata.
Akitaka awahi aone kama atakutana na kikwazo.
Anamsingizia kamanda wa watu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cheo chake ni Chief of Staff, ni cheo cha pili kutoka brigedia general...kama ukifuatilia zaidi unaweza kulipata jina lake mahali fulani naamini
kuna madaraka na cheo... CHIEF OF STAFF ni madaraka cheo chake huyo jamaa ni LIEUTENANT GENERAL mind you hicho cheo anaweza kupewa hata MAJOR GENERAL so sio lazima kiwe ni chapili kutoka jenerali

turudi kwenye shida yako nakumbuka mwaka 2017 nilikuwa mtumiaji mkubwa wa hiyo barabara mida ya jioni shughuli ilikuwa ni hiyohyo kwa former tpdf chief of staff LIEUTENANT GENERAL JAMES MWAKIBOLWA akastaafu nikajua shughuli itaisha

ila huyu mpya tena kaja LIEUTENANT GENERAL YAKUBU HASSAN MOHAMEDI pia shughuli ni hyohyo so usitegemee kama hii shida itaisha

hata upige kelele vipi shida yako haitaisha labda tu jamaa ahame kule kambini anapokaa ila asipohama na ninahisi kwa protakali za jeshi lazma akae kule...

nakuomba ubadilishe njia au ww uwe unawahi kabla yeye hajaanza kwenda kazini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niliwahi kukutana na davis mwamunyange kwenye foleni tena akiwa hana ata gari yenye 4 stars plate number nilimgundua alivyofungua kioo ndio nkampungia mkono CDF huyu makini kabisa kupata kutokea ktk nchi hii
Naunga mkono hoja mkuu,
Jirani yangu huyu mtu safi sana,akipita hata nafsi inakwambia mpungie mkono au hata salute mpgie.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
JF pana saivi ujumbe kaupata hata asipoupata yeye kwa kuona hiki ulichoandika atafikishiwa taarifa na House Boy wake au hata Rfk ake kua leo Kafunguliwa Thread na lazima abadilike.

Nakupa siku 3 tu mkuu utaona Changes.
 
Mbona Mwamnyange alikuwa jirani yetu na akitoka yeye ni gari yake tu na sana sana ni honi ila hakusimamisha mtu barabarani???? Mabeyo mbona wewe ni mtu wa amani kwa nini uwe hivi? I know you very well toka tupo Rwanda.
Kwenu jirani na kwa Mzee Matiko Mbezi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwamunyange alikuwa anapita kistaarab kabisa. Hana kwere baba wa watu
Alikuwa jirani yangu, hata kwenye msiba huwezi kumjua kwa haraka na kaunda suti yake au tisheti. Kuna wakati flani anakaa baa moja hivi hapo Afrikana (haina makelele kama pale kwa demu wako Khadija Facebook pub)!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuwa mvumilivu mkuu, huyo chief of staff anachukua masaa mangapi kupita huko barabarani. Hao watu wana taratibu zao, ndo maana gari lao likizima barabarani hutasikia mtu akiwapigia honi
 
Chief of staff ni mnazimu Mkuu wa JWTZ ni kiongozi wa ngazi za juu Kabisa katika usalama wa Nchi hii, ndio mtu wa kwanza kujua idadi ya dhana za kivita. Ninachokuona ww unachokereka zaidi ni namna MPs wanavyomlinda, ndugu utaumia roho yako bure, na ww kama unajua Kabisa kuwa muda furani lazima mkuu apite Kwa nini usiwe unawahi mapema? Ili huo msafara usiwe unakukuta
sasa mkuu mbona una mu address aonekane mtu mkubwa mnooo,,of course ana nafasi yake lakini sio kama hivyo unavyotaka kumkuza,,...anajua zana zote za kivita za nchi je chain yake ya command hawajui juu yake yupo cdf yupo waziri was ulinzi kuna waziri mkuu nao vp..anaofanya nao kazi kwa karibu hawafahamu..huko tiss wanaojua wangapi,,...tudiscuss the issue achana na mambo ya uzito..wazito wapo wengi sana ..na wanajua mengi ya nchi
 
Mkuu mimi ni mzoefu Wa hiyo barabara tangu enzi za mkwere kila asubuhi na jioni lazima kunakuwa na ving'ora vya hawa wajomba na tulishazoea huo utaratibu, mkuu all in all heshimu mamlaka husika hasa hawa mabaka mabaka ukileta ujuaji mwingi hawakawii kukufundisha adabu mpaka uhame mji na kuwachukia milele, mbona misafara ya rais mnapigishwa foleni mpaka Masaa mawili hulalamiki?
Kimsingi ni ulevi wa madaraka na ubushororo mwingi, maana kikatiba siyo mtu anayestahihi ving`ora na escort kama hiyo. Ni sawa na mkuu wa mkoa fulani katika nchi jirani alivyokowa amejitengenezea escort ya kufa mtu. Yaani hata akienda harusini ilibidi mji wote ujue kuwa leo katoka si ving`ora hiyo!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Usiishi kwa kukalili
sio uongo
mimi binafsi wakati nasoma Tambaza high school 2003 tulikuwa tunamuona CDF General george waitara na gari yake 4 star akiingia ngome kila siku hakuwa ma vingora wala mbwembe kama za siku hizi, tuliwahi kumpungia mkono na yeye akarudisha salamu.
mwaka huu nilikutanana chief of staff YH Mohamed dodoma anamsafara kama wa magari 5 na MP wa kutosha,tena barabarani kila kona ya dodoma Millitary police wanafanya kazi za trafiki polisi, nilibaki na duwaa ni kajisemea zama zimebadilika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom