Huyu kiongozi mzalendo, mwana wa Afrika hakujua kuwa walio karibu naye hawakumpenda na walimtakia mabaya kama ilivyokuwa kwa Thom Sankara?

Kipindi cha dhalimu hakukuwa na tofauti kati ya wazalendo na wajinga. Wakati huo wajinga waliitwa wanyonge ili walale vizuri.
Mie naona kwa sasa wajinga ni wengi na kila kukicha idadi inaongezeka. Kila kitu kinasifiwa pasipo hata kuhoji! Kwasababu tu walimchukia aliyetangulia.
Na ndio maana dhulma na urasimu vimerudi kwa kasi, rushwa inazidi kukita mizizi, ufisadi nk.

Hebu fikiria watu wanafanya kazi kwa makubaliano halafu mwisho wa siku hakuna malipo. Na hakuna anayeonesha kujali.
Vijana wanapewa mafunzo ya kazi maalum ya serikali, anwani za makazi,ndani ya saa chache ili kukwepa gharama, hakuna anayehoji! Wengine wanakaa kutwa nzima bila maji wala chakula, wanapewa elfu tano!

Report zisizo na uhalisia zinatolewa hadharani, watu wanapiga makofi!
Fedha za mkopo, msaada, kodi na tozo zinaelekezwa kwenye miradi inayofanana na kwa takwimu hizohizo, watu wanashangilia.
Bila shaka huu ni ujinga uliopitiliza!!
 
Alipendea na kina Sabaya, Polepole, Bashite n.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…