Huyu kiumbe ananitesa sana usiku

Huyu kiumbe ananitesa sana usiku

Nyuki Mdogo

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2021
Posts
4,134
Reaction score
10,644
Yani anakuja anatua karibu na dirishani ninakolala anaanza kulia hovyo.

Hapo ni usiku wa manane, anakuja karibu mara 3 kwa wiki. Cha ajabu majirani zangu hawasikii akilia. Namna gani naweza mdhibiti?

Maana kiasili huyu si kiumbe mwema

FB_IMG_1681968578165.jpg
 
Chukua torch usiku ukisikia Analia,traatibu nyata!akiwa huko juu ya paa Fanya kama unamlenga na torch ,Kisha washa mara tatu Ile Zima,washa,Zima washa x3 ,atakimbia na hatorudi tena
 
Yani anakuja anatua karibu na Dirishani ninakolala anaanza kulia Hovyo..

Hapo ni usiku wa manane, anakuja karibu mara 3 kwa wiki. Cha ajabu majirani zangu hawasikii akilia.

namna gani naweza mdhibiti?

maana kiasili huyu si kiumbe mwema

View attachment 2593735
Kama ni muislam piga zile sura 3 usiku kabla ya kulala
(tunaziita Kul 3)
 
Tanya maombi ya Nguvu Mkuu, ukitaka kuthibitisha nguvu ya Maombi, siku akija usiku, amka anza kufanya Maombi, ataondoka na utakuja kutoa ushuhuda hapa!
 
Toa location ili tuhudhurie msiba siku yenyewe ikifika

Au mrudie Mungu wewe na familia yako kwa roho na kweli kama nimauza uza yatakwisha


Tenga usiku mmoja ili umuwinde na kumuua

Mpaka hapo problem solved 100%
 
Tanya maombi ya Nguvu Mkuu, ukitaka kuthibitisha nguvu ya Maombi, siku akija usiku, amka anza kufanya Maombi, ataondoka na utakuja kutoa ushuhuda hapa!
Thank you ubarikiwe sana
 
Yani anakuja anatua karibu na dirishani ninakolala anaanza kulia hovyo.

Hapo ni usiku wa manane, anakuja karibu mara 3 kwa wiki. Cha ajabu majirani zangu hawasikii akilia. Namna gani naweza mdhibiti?

Maana kiasili huyu si kiumbe mwema

Mafuta na Maji ya Mwamposa yanamhusu
 
Huyo ndege moja ya sifa yake ni kuweza kunusa mizoga iliyoko mbali.Na huweza hata kunusa kiumbe kinachokaribia kufa(Huwa anauwezo wa kunusa kugundua kiumbe ambacho cell zake za mwili zimekufa nyingi kwamba anae karibia kufa.)

Ndo maana mara nyingi huonekana mahali na baada ya muda kama mgonjwa eneo hilo yupo mtaona siku mbili tatu kafa (japo si mara zote) kwani anauwezo wa kunusa kiwango cha cell zilizikufa hata kwa mtu.


Kwa ushauri wangu Jitahidi chunguza hapo ndani unakitu gani chenye mfumo wa kuumwa sana kama Paka, mbwa au binadam mgonjwa.

Pia kutokana na mazingira yaezekana ame papenda hapo kwako

kama ambavyo ndege wengine hutengeneza Viota vyao kwenye baadhi ya nyumba.


Hivyo ifanye sehemu unayoishu kuwa safi kote ambako kutaondoa mazingira ya yeye kupenda hapo kwako
 
Back
Top Bottom