Huyu mtu alikuwa jini au? Nilisoma na mwanafunzi kipanga ambaye ni mtoro, mtundu, anavuta bangi, kila kesi yumo, n.K

Huyu mtu alikuwa jini au? Nilisoma na mwanafunzi kipanga ambaye ni mtoro, mtundu, anavuta bangi, kila kesi yumo, n.K

primary 1997,kuna kijamaa kilikuwa kitori shule sio kawaida.
yaani kanachapwa leo na adhabu za kushika masikio,siku mbili baadae hakaji shule.

mtihani wa muhula kanashika nafasi ya pili au yq kwanza.necta kakapata wastani wa vipaji kakapelekwa songea boys.
 
Umbwe Sec alikuwepo jamaa moja naona ni kama unamzungumzia yeye
 
Huyo jamaa story yake na mm 99% tunafanana kasoro tu me nikipiga chini ajira now na biashara zangu
Ila enzi zangu akili ndo ilisababisha niwe naachwa
Ila kuanzia la sita mpk formsix nilikuwa kila mwaka na soma shule nyingine
Nimesoma shule 8 na zote nilikuwa naongoza class
Now nishaacha ujinga

Na Mungu nae alivyo ananipatia matoti madume tupu sjui huko mbele yataiga tabia ya baba[emoji24]
 
Wapo wengi tu, kama umewahi soma shule za vipaji unaweza kuwa na mifano mingi...

Mfano mmojawapo ni Wakili msomi wa the Don...kichwa sana yule mwamba na kafanya mambo mengi mengi tu akiwa skonga hahaha
Sure thing aisee, Msando alisoma Ilboru hivi right?

A-level nilisoma Mzumbe sekondari, ingawa nilikua vizuri lakini nilikutana na watu wapo gifted vibaya mnoo.

Nakumbuka kuna dogo wa form two tulikua tunasolve naye paper za A-level physics fresh tuu.

Imagine!!
 
MUNGU SIO MCHOYO

Watu……..endelea sasa kusoma chini

1.Waopata daraja la kwanza kwenye masomo au tunasema distinction ndio wanaokuwa ma-engineer.madaktari na wanasheria

2.Wanaopata daraja la pili kwenye masomo ndio wanaokuwa viongozi wa mashirika mameneja,maofisi waajiri,walimu wakuu,wakuu wa taasisi AJABU SASA WATU WA GROUP HILI ndio wanaowaongoza watu wa daraja la kwanza wanakuwa ni wakuu wao wa kazi au ma manager wao.

3.Wanaopata daraka la tatu kwenye masomo ndio wanaokuwa wanasiasa,wabungu,DED, AJABU SASA WATU WA GROUP HILI ndio wanaongoza magroup yote mawili hapo juu yaani la kwanza na la pili

4.Wanaopata daraja la nne kwenye masomo ndio wanaokuwa wafanya biashara wakubwa matajiri wenye mitaji hasa baada ya kugundua mambo ya darasani hawayawezi sana wanatumia uwezo wao wote mungu aliowajalia bila kuogopa na aibu kufanya biashara hata kama ni biashara uchwara au petty business lakini kiukweli wanafanikiwa na ndio wenye mitaji na hela nyingi.AJABU SASA WATU WA GROUP HILI kutokana na wao kuwa na nguvu ya pesa ndio wanaotawala na kuwaongoza watu wa ma group yote juu yaana la kwanza,la pili na la tatu.

5.Wanaopata daraja la tano kwenye masomo ndio wanaokuwa wanajeshi,polisi AJABU SASA WATU WA GROUP HILI wanapoona watu wa ma group yote juu manne yaani la kwanza,la pili,la tatu na la nne wanapeleka mambo hovyo ya nchi ambayo hayaeleweki wanachukua nchi ili kuyaweka mambo sawa hivyo watu wa magroup yote la kwanza hadi la nne wanafyata mkia wakiamua kuchukua nchi ndio wanaweza kuamua kuwarudishia watu wa ma group ya juu waweke mambo sawa la sivyo watachukua nchi tena na ndio maana watu wa ma group haya wanaogopwa na kuheshimika sana duniani hata raisi anayekuwa madarakani anajua wana uwezo wa kumtoa kwa nguvu.

6.Wanaopata daraja la sifuri au hawakusoma kabisa wanakuwa waganga wa kienyeji.AJABU SASA WATU WA GROUP HILI watu ma magroup yote niliyotaja kuanzia la kwanza hadi la tano wanapoona mambo yao hayawaendei vizuri wakiona ubunge unakaribia kukoma,kwenye ajira cheo hakipandi, biashara zao zinayumba mambo ya mapenzi hayako sawa hii hasa ni kwa wanawake wanakwenda kujisalimisha kwa watu wa group hili kuomba msaada

MUNGU SIO MCHOYO AMEGAWA VIPAJI NA RIZIKI KILA MMOJA AMEMPA STAHIKI YAKE

View attachment 1753783

View attachment 1753784

View attachment 1753786
Nilijua tu witch doctor lazima atakuwa mwafrika
 
Nilijua tu witch doctor lazima atakuwa mwafrika
uko sawa mkuu hata mimi wakati natafuta picha kwenye google kuweka vikolezo nimetafuta withdoctor mzungu nikakosa nikakutana na huyu mwenzetu.Ajabu sasa wewe google andika photo of angel utaona mzungu andika photo of satan utaona muafrica dunia haina usawa
 
Si huyu hapa! Unamficha wa nn?
20210415_191441.jpg


Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Huyu Bwana alikuwa anatukimbiza vibaya mno darasani, form 4 alipiga division 1 ya 11 ya enzi hizo kabla ya 2010, (zilikuwa adimu mno), shule ilikuwa haijawahi kupata mtu aliefaulu kwa ufaulu huu, shule ilikuwa ya kawaida sana

Siffa za huyu mtu

1. Alikuwa mtoro sana
2. Alikuwa mhuni huyu bwana, Form 2 alianza kuvuta bangi na form 3 alianza kuuza kabisa shuleni
3. Yeye na wenzake waliwahi kupewa suspension kwa kumpiga Mwalimu (jamaa alikuwa anapiga chuma), pia kutuhumiwa kufoji risiti ya ada
4. Kwenye Mapenzi huku kavunja mioyo ya mabinti wengi, alikuwa playboy.
5. Alikuwa kiongozi wa kundi bovu, wengi walitimuliwa ila yeye akili zilimlinda kuendelea kubaki
5. Waliojaribu kumwiga walifeli
6. Alipenda sana kusoma vitabu, hata aumwe huyu bwana kwake kusoma vitabu ilikuwa kama chakula, sizungumzii vitabu hivi vya darasani, ni vitabu vya elim binafsi

Leo hii atika pita pita zangu nilkutana na rafiki yangu flani wa sekondari, sasa katika mazungumzo ya nani yupo wapi anafanya nini, nilipigwa na butwaa ambalo hadi sasa ivi naona ni kama mujiza, Huyo bwana mtundu hapo juu saizi ana kazi nzuri tu katika moja ya taasisi kubwa ya serikali.

Tulipomaliza form 4 huyo bwana, huko form 6 alizidi utundu wake kufikia steji ya kuhama shule 3, biashara yake hio alianza kufata mzigo Arusha na akawa anauza mtaani na shuleni, ila akafaulu na divishen 1 ya 5 na kuongozea shule aliyosoma, na hioo shule walidhani alinunu mtihani, Nakumbusga tena enzi hizo hii divisiin 1 ya 5 ilikuwa nadra hasa kwenye shule aliyosoma ya kawaida

Akachaguliwa chuo safi tu kwa huo ufaulu wake, Na huko kwa uhuru aliopata nadhani unaweza kujenga picha, ila alihitimu kwa G.P.A ya 4.7 (first class), alipata kazi kiulaini sana, alipoenda kuendelea na masters alipomaliza matokeo yake yalimbeba zaidi saizi ana kazi nzuri tu, Mbali na hapo pia ana miradi halali.

Kwa sasa ni mtu aliebadilika sana kuwa miongoni mwa watu ambao ni mifano ya kuigwa, hana makuu wala vurugu, kawa mcha Mungu, watu wake wa karibu wanasema kaacha kuvuta bangi ila hunywa pombe mara chache sana, ni baba wa familia inayoishi vizuri kimaadili, n.k

Siku hizi kaacha ishu zake hizi nadhani yalikuwa mambo ya ujana ila bado najiuliza huyu ni mtu kweli?
Nilisoma na mwana kama huyo
Hapo ndo msemo wa msafara wa mamba kenge pia wapo uliponiingia zaidi akilini na kuniumiza mtima 😓😓
 
Huyu Bwana alikuwa anatukimbiza vibaya mno darasani, form 4 alipiga division 1 ya 11 ya enzi hizo kabla ya 2010, (zilikuwa adimu mno), shule ilikuwa haijawahi kupata mtu aliefaulu kwa ufaulu huu, shule ilikuwa ya kawaida sana

Siffa za huyu mtu

1. Alikuwa mtoro sana
2. Alikuwa mhuni huyu bwana, Form 2 alianza kuvuta bangi na form 3 alianza kuuza kabisa shuleni
3. Yeye na wenzake waliwahi kupewa suspension kwa kumpiga Mwalimu (jamaa alikuwa anapiga chuma), pia kutuhumiwa kufoji risiti ya ada
4. Kwenye Mapenzi huku kavunja mioyo ya mabinti wengi, alikuwa playboy.
5. Alikuwa kiongozi wa kundi bovu, wengi walitimuliwa ila yeye akili zilimlinda kuendelea kubaki
5. Waliojaribu kumwiga walifeli
6. Alipenda sana kusoma vitabu, hata aumwe huyu bwana kwake kusoma vitabu ilikuwa kama chakula, sizungumzii vitabu hivi vya darasani, ni vitabu vya elim binafsi

Leo hii atika pita pita zangu nilkutana na rafiki yangu flani wa sekondari, sasa katika mazungumzo ya nani yupo wapi anafanya nini, nilipigwa na butwaa ambalo hadi sasa ivi naona ni kama mujiza, Huyo bwana mtundu hapo juu saizi ana kazi nzuri tu katika moja ya taasisi kubwa ya serikali.

Tulipomaliza form 4 huyo bwana, huko form 6 alizidi utundu wake kufikia steji ya kuhama shule 3, biashara yake hio alianza kufata mzigo Arusha na akawa anauza mtaani na shuleni, ila akafaulu na divishen 1 ya 5 na kuongozea shule aliyosoma, na hioo shule walidhani alinunu mtihani, Nakumbusga tena enzi hizo hii divisiin 1 ya 5 ilikuwa nadra hasa kwenye shule aliyosoma ya kawaida

Akachaguliwa chuo safi tu kwa huo ufaulu wake, Na huko kwa uhuru aliopata nadhani unaweza kujenga picha, ila alihitimu kwa G.P.A ya 4.7 (first class), alipata kazi kiulaini sana, alipoenda kuendelea na masters alipomaliza matokeo yake yalimbeba zaidi saizi ana kazi nzuri tu, Mbali na hapo pia ana miradi halali.

Kwa sasa ni mtu aliebadilika sana kuwa miongoni mwa watu ambao ni mifano ya kuigwa, hana makuu wala vurugu, kawa mcha Mungu, watu wake wa karibu wanasema kaacha kuvuta bangi ila hunywa pombe mara chache sana, ni baba wa familia inayoishi vizuri kimaadili, n.k

Siku hizi kaacha ishu zake hizi nadhani yalikuwa mambo ya ujana ila bado najiuliza huyu ni mtu kweli?


"Bahati ya mwenzio usiilalie mlango wazi, kila mtu anakotoka anakujua yeye mwenyewe".
 
Huyu Bwana alikuwa anatukimbiza vibaya mno darasani, form 4 alipiga division 1 ya 11 ya enzi hizo kabla ya 2010, (zilikuwa adimu mno), shule ilikuwa haijawahi kupata mtu aliefaulu kwa ufaulu huu, shule ilikuwa ya kawaida sana

Siffa za huyu mtu

1. Alikuwa mtoro sana
2. Alikuwa mhuni huyu bwana, Form 2 alianza kuvuta bangi na form 3 alianza kuuza kabisa shuleni
3. Yeye na wenzake waliwahi kupewa suspension kwa kumpiga Mwalimu (jamaa alikuwa anapiga chuma), pia kutuhumiwa kufoji risiti ya ada
4. Kwenye Mapenzi huku kavunja mioyo ya mabinti wengi, alikuwa playboy.
5. Alikuwa kiongozi wa kundi bovu, wengi walitimuliwa ila yeye akili zilimlinda kuendelea kubaki
5. Waliojaribu kumwiga walifeli
6. Alipenda sana kusoma vitabu, hata aumwe huyu bwana kwake kusoma vitabu ilikuwa kama chakula, sizungumzii vitabu hivi vya darasani, ni vitabu vya elim binafsi

Leo hii atika pita pita zangu nilkutana na rafiki yangu flani wa sekondari, sasa katika mazungumzo ya nani yupo wapi anafanya nini, nilipigwa na butwaa ambalo hadi sasa ivi naona ni kama mujiza, Huyo bwana mtundu hapo juu saizi ana kazi nzuri tu katika moja ya taasisi kubwa ya serikali.

Tulipomaliza form 4 huyo bwana, huko form 6 alizidi utundu wake kufikia steji ya kuhama shule 3, biashara yake hio alianza kufata mzigo Arusha na akawa anauza mtaani na shuleni, ila akafaulu na divishen 1 ya 5 na kuongozea shule aliyosoma, na hioo shule walidhani alinunu mtihani, Nakumbusga tena enzi hizo hii divisiin 1 ya 5 ilikuwa nadra hasa kwenye shule aliyosoma ya kawaida

Akachaguliwa chuo safi tu kwa huo ufaulu wake, Na huko kwa uhuru aliopata nadhani unaweza kujenga picha, ila alihitimu kwa G.P.A ya 4.7 (first class), alipata kazi kiulaini sana, alipoenda kuendelea na masters alipomaliza matokeo yake yalimbeba zaidi saizi ana kazi nzuri tu, Mbali na hapo pia ana miradi halali.

Kwa sasa ni mtu aliebadilika sana kuwa miongoni mwa watu ambao ni mifano ya kuigwa, hana makuu wala vurugu, kawa mcha Mungu, watu wake wa karibu wanasema kaacha kuvuta bangi ila hunywa pombe mara chache sana, ni baba wa familia inayoishi vizuri kimaadili, n.k

Siku hizi kaacha ishu zake hizi nadhani yalikuwa mambo ya ujana ila bado najiuliza huyu ni mtu kweli?
Tanzania tumebarikiwa kuwa na ma genius kadhaa, mfano TUNDU LISSU, ni genius wa sheria, ila serikali haithamin uwezo wake!
 
Kuna mmoja nilisoma nae sekondari tatizo la yule jamaa ni mtoro hatari siku mwalimu akandaa siku ya kuchapa watoro Tena baada ya kumaliza mitihani ikafika zamu ya yule jamaa mwalim akaanza kucheka mwenyewe jaamaaa Masomo yote ana A alaf mtoro wenzangu na Mimi hatukuwa kutega hata kwenye thelathini Bora hatupo alimuacha.
 
Back
Top Bottom