Uchaguzi 2020 Huyu mtu anaweza kuchukua hii nchi au anaweza kusababisha mambo yatakayosababisha mageuzi kutokea katika hii nchi

Uchaguzi 2020 Huyu mtu anaweza kuchukua hii nchi au anaweza kusababisha mambo yatakayosababisha mageuzi kutokea katika hii nchi

una mawazo yaliyokongoroka sana ! una umri gani mkuu ? Lissu hafanani kabisa na hao uliowataja

Nina umri wa kutosha wakati huo tayari nimemaliza degree yangu ya pili na nikiwa na akili timamu japo bado kijana sana. (ukipenda nitakwambia CV yangu utaipata wapi publicly)

Umri alio nao Lissu leo ndio umri aliokuwa nao Mrema, wakati huo akiwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani (1995) na anaeheshimika sana.

Upinzani nchi hii ni mpaka CCM ipasuke vipande. Kila ilipo pasuka uchaguzi kwao ulikuwa mgumu. Vinginevyo ni vichekesho tuu.
 
Ukipata majimbo zaidi ya manne (4), utakuta kichwa vhangu kimening'ia Mnazi mmoja baada ya kutangazwa, Uzi huu uhifadhi.
Hasara kubwa sana ! Chadema haitegemei kupewa ubunge ama Urais bali itapigania na hakuna tena uoga .
 
Salary Slip,

Naona sasa umeanza kupima kima Cha maji na kuona kirefu.. hapa umeanza kuchambua kiutu uzima tofauti na zamani uliamini Lissu tu ndie atashida Urais.

Lissu Sanasana ataendelea kuumia tu kuona JPM akishinda kwa asimilia 70%.
 
Nina umri wa kutosha wakati huo tayari nimemaliza degree yangu ya pili na nikiwa na akili timamu japo bado kijana sana. (ukipenda nitakwambia CV yangu utaipata wapi publicly)
Umri alio nao Lissu leo ndio umri aliokuwa nao Mrema, wakati huo akiwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani (1995) na anaeheshimika sana.

Upinzani nchi hii ni mpaka CCM ipasuke vipande. Kila ilipo pasuka uchaguzi kwao ulikuwa mgumu. Vinginevyo ni vichekesho tuu.
Wazee wa degree 4!
 
Naona sasa umeanza kupima kima Cha maji na kuona kirefu.. hapa umeanza kuchambua kiutu uzima tofauti na zamani uliamini Lissu tu ndie atashida Urais.

Lissu Sanasana ataendelea kuumia tu kuona JPM akishinda kwa asimilia 70%.
Magu hawezi kushinda katika uchaguzi ilio huru na wa haki hata kidogo.Lissu safari hatakuwa kama Lowassa aliomuachia Mungu, bali itakuwa tofauti kabisa.
 
Hivi wee jamaa hata una Wazazi kweli? Na kama unao huwa hata una muda wa kuwajulia angalau hali? Slow down man, hii Dunia haijaanza leo, utakuja kuishia kujiua siku moja kama ukiendelea hivyo kuabudu takataka, ...
Wewe hapo ulipo ni kuweweseka tu. Unakumbuka ulimjibu nini Nyani Ngabu alivyotabiri kurejea kwa Lissu? Sasa imetimia. Ulisema hataweza hata kunyanyuka kama atapona: sasa amepona na amenyanyuka. Ukasema, akiweza akinyanyuka hataweza kutembea. Sasa ni wewe au ma.ma yako anambeba mgongoni kwasababu hawezi kutembea? Wewe kwa yale maneno yako miaka 3 iliyopita, ulikuwa na uhakika na uliyoyaongea kwasababu lazima ulikuwa sehemu ya wale waoga ambao walishindwa kulenga shabaha.

Sasa muujiza umetendeka unaanza kuweweseka. Karma is real.
 
Wewe hapo ulipo ni kuweweseka tu. Unakumbuka ulimjibu nini Nyani Ngabu alivyotabiri kurejea kwa Lissu? Sasa imetimia. Ulisema hataweza hata kunyanyuka kama atapona: sasa amepona na amenyanyuka. Ukasema, akiweza akinyanyuka hataweza kutembea. Sasa ni wewe au ma.ma yako anambeba mgongoni kwasababu hawezi kutembea? Wewe kwa yale maneno yako miaka 3 iliyopita, ulikuwa na uhakika na uliyoyaongea kwasababu lazima ulikuwa sehemu ya wale waoga ambao walishindwa kulenga shabaha.

Sasa muujiza umetendeka unaanza kuweweseka. Karma is real....
Ile comment yake inamgharimu sana leo hii.
 
Lowassa na Mrema ndio walio wahi kuitikisa CCM, na haito tokea tena. CCM iko very dynamics inabadilika sana kufuatana na hali halisi na mapenzi ya wananchi kwa wakati huo.

2020 Utaona asilimia 80% ya wabunge CCM ni chini ya miaka orobaini. Upinzani kujivunia vijana haipo tena, wazee ndio wamesheheni upinzani.
Huwa una mawazo mfu wewe!
Unaandika usichokijua au hukijui unacho andika. Hiyo ndiyo hali halisi mtu akiambiwa aku describe
 
Hivi wee jamaa hata una Wazazi kweli? Na kama unao huwa hata una muda wa kuwajulia angalau hali? Slow down man, hii Dunia haijaanza leo, utakuja kuishia kujiua siku moja kama ukiendelea hivyo kuabudu takataka, ...

Yeye mbona ni mfuasi (wewe unaita kuabudu) wa Chadema na sio CCM?
Maana kitu kijulikanacho kuwa ni TAKATAKA ni CCM!
Chama kinachopata viongozi wake kwa rushwa ya waziwazi na kubarikiwa na viongozi wake wa juu utakiitaje kama sio takataka?
Tena jina hilo ni la staha kabisa, ingekuwa kule US tungekiita lile jina atumialo Trump, Shit hole party.
 
Hivi wee jamaa hata una Wazazi kweli? Na kama unao huwa hata una muda wa kuwajulia angalau hali? Slow down man, hii Dunia haijaanza leo, utakuja kuishia kujiua siku moja kama ukiendelea hivyo kuabudu takataka, ...

the most wise comment
 
Watumishi wa umma mateso ya miaka 5 ya hakuna increments, kupanda vyeo (walimu),ongezeko la mshahara,kutolipwa malimbikizo yenu n.k iwe ni fundisho na akili zenu kuikataa ccm kwa nguvu zote.Familia zenu ziikatae ccm.

Msiwapigie kura ya urais,wabunge wala madiwani.Ndiyo wadhalilishaji wenu

pole sana, mlishachelewa
 
TUNDU LISU SIYO MZEE LOWASA, ASIPUUZWE.

Na, Robert Heriel.

Moja ya sifa ya Mpumbavu ni kuishi kwa Dharau na mazoea. Tabia ya mazoea imeangusha watu wengi mashuhuri. Maisha hayana mazoea, maisha yanabadilika. Hivyo hata siasa haina mazoea, siasa zinabadilika, dakika moja inatosha kabisa kubadili mwelekeo wa siasa.

Hata katika michezo, timu zinazocheza kwa mazoea, ati mwaka fulani nilikufunga hivyo mwaka huu nitakufunga pia, bila kufanya jitihada huko ni kujidanganya.

Kuna watu wanafikiri kama watu wajinga, mtu mjinga huishi ulimwengu wa zamani, mtu mjinga anadhani dunia ya zamani niyasasa. Mtu mjinga hafikiri dunia inaenda mbele. Yeye anafikiri jana ni leo, na leo itakuwa kesho. Jambo ambalo sio kweli.

Hata katika Siasa, hasa katika bara letu la Afrika. Wanasiasa wengi wanatabia ya kufikiri kijinga jinga tuu. Yaani kama alishinda zamani basi anadhani kila siku atashinda, kama ni mbunge wa jimbo fulani anafikiri atabaki kuwa mbunge, kama chama chake ni chama tawala anafikiri kitaendelea kuwa tawala milele. Hivyo wengi huishi kwa mazoea na dharau, hali inayopelekea kutofanya jitihada za kusaidia wananchi.

Hili nimeliona katika siku chache tangu Lisu aanze harakati zake za kutafuta wadhamini.

Wapo watu wanaakili za kijinga, wanatumia jana katika siku ya leo.

Utasikia mjinga mmoja akisema; Hata Lowasa alikuwa anajaza watu hivyo hivyo, tena lowasa alikuwa ananguvu. Mwingine utasikia, Mbona huyu hajamfikia Dr. Slaa, mwingine atakuambia mbona hajafika hata nusu ya nyomi za Mzee Mrema. Mtu yeyote awazaye hivi huwaza kama mtu mjinga. Nimeshatoa sababu kuwa, moja ya mtu mjinga ni kudhani kila siku ni jumapili, pia ni kudhani kuwa kama alimshinda fulani basi hata huyu atamshinda. Wazo hili aliliwaza Mtu aitwaye Goliath, ati kwa vile yeye ni jemadari na ananguvu basi alivyomuona Daudi kakijana kadogo akakadharau, akatumia mazoea, wote tunajua, Goliath alikatwa kichwa na Daudi.

Tunafahamu hata kule Marekani, hakuna ambaye alijua Donald Trump angemshinda Hillary Clinton. Lakini Dharau za wapiga kura wa Hillary zilimpa ushindi Trump kwani hawakwenda kupiga kura .

Mzee Kinana aliongea jambo lenye hekima kubwa kuwa, hakuna uchaguzi rahisi. Hivyo watu wasichukulie mambo ni kama kawaida. Hata Mhe Rais ambaye anatetea kiti chake. Mhe. Magufuli mara kadhaa nimemsikia akiwaambia wanachama wake kuwa, wasichukulie rahisi, wasidhani wameshinda, ushindi bado, hivyo siku ya kura waende kupiga kura.

Hao ni watu wazima wenye akili. Watu wasioishi siku ya jana.

CCM kumshinda Lowasa sio kusmhinda Tundu Lisu
CCM kumshinda Dr Slaa sio kumshinda Lisu
CMM kumshinda Lipumba sio kumshinda Lisu
CCM kumshinda Mrema Sio kumshinda Lisu.

Kwanza ni watu tofauti kabisa, kitabia, kihaiba, kitaaluma, kinyakati.

MAMBO YANAYOMTOFAUTISHA Lisu na Lowasa

1. ASILI YA ITIKADI ZAO
Lisu hakuwahi kuwa CCM. Lakini hao wengine wote walishawahi kuwa Ccm. Hii ni moja ya Sababu kuu ya kwa nini Lisu asipuuzwe. Lisu ni Mpinzani OG.
Kubadili Itikadi ni sawa na kubadili jinsia, yaani ni sawa na mwanamke ajibadili awe mwanaume Bado atabaki kuwa mwanamke tuu. halikadhalika na kwa mwanaume. Mtu kama Mrema, Lipumba, Dr. Slaa, Lowasa hao ni CCM na watabaki kuwa hivyo.

2. UJASIRI
Lisu ni jasiri, haogopi kusema kile anachokiamini bila kujali matokeo, Lisu hamung'unyi maneno.Lakini Lowasa ni mtu wa kumung'unya maneno, Ujasiri wake ni mdogo ukilinganisha na wa Lisu. Kidogo Dr Slaaa anaweza kumkaribia Lisu lakini sio kumfikia Lisu.

Lowasa hakuwa na ujasiri wowote, pengine nikijaribu kumtetea, nitatoa sababu labda umri unachangia. Inasemekana umri unavyozidi kuwa mkubwa ndivyo ujasiri unavyozidi kupungua.

3. USHAWISHI
Lisu anaushawishi Mkubwa kuliko Lowasa. Kuna watu wanadhani Lowasa alikuwa na ushawishi, lakini sio kweli, Lowasa hakuwa na ushawishi wowote. Lowasa ni mtu wa mitego. Lowasa alikuwa anachambo ambacho ni pesa, waliokuwa wanamshabikia ni kutokana na kuvizia pesa zake. Yaani mtego wake ni kuwa Rais lakini chambo alichokitumia ni pesa. Watu walikuwa wanavizia pesa zake.

Lowasa ni sawa na mwanaume mwenye pesa anayeenda kuposa mwanamke. Kitakachomshawishi huyo mwanamke ni pesa zake na wala sio Lowasa.Hii ni tofauti na Lisu. Lisu ni kama mwanaume masikini anapoenda kumchumbia mwanamke. Hana pesa lakini anakubaliwa kutokana na maneno yake.

Lisu anajua kujenga hoja zenye ushawishi, na hii ni watu wachache wanayo. Lisu kamuacha mbali sana Lowasa kwenye kujenga hoja.

Kama Lowasa angekuwa anajua kuongea vizuri basi mwaka 2015 angeukwaa Urais. Lakini alizidiwa vilivyo na Magufuli. Wote tunajua kuwa Magufuli naye hajambo kwa mdomo, anajua kujenga hoja, Magufuli hata umpe masaa matatu hapo azungumze ataongea na hutatamani aache kuzungumza. Hiko ndicho kilimfanya Magufuli amshinde Lowasa mbali na sababu zingine.

Lisu asipuuzwe kwa maana mdomo anao, anajua kuongea, hashindwi kuongea siku nzima na ukatamani aendelee kuongea. Sifa ya watu wanaojua kushawishi pia wanachanganya na chumvi nyingi. Hilo lizingatiwe, wanautani, wanadata nyingi, wana mikwala, wanaswaga.

Lisu siku zinavyozidi kwenda anazidi kupata nguvu ya ushawishi kwa watu.Siku 60 ni nyingi sana kwa Mtu kama Lisu.

4. NYAKATI
Wakati wa Lowasa na Lisu ni tofauti kabisa. Japo tofauti ni miaka mitano lakini ni miaka mingi sana kisiasa, kiuchumi na kimtazamo.

Lowasa alikuwa kipindi ambacho changamoto za ajira zilikuwa ni ndogo. Vijana wasomi walikuwa wanaajiriwa kwa sehemu kubwa na serikali. Lakini Lisu kipindi hiki Vijana wengi wamesota kwa miaka mitano bila ajira za kueleweka. Sidhani kama kuna kijana msomi ambaye hatamuelewa Lisu wakati amesota miaka mitano, wengine mitatu kwa kadiri ya mwaka aliomaliza. Ni kijana mjinga tuu ambaye amesoma alafu hana muelekeo wa maisha ambaye hatamuelewa Lisu.

Kipindi cha Lowasa Watumishi wa Umma walikuwa wanaongezwa mishahara pia na kupandishwa madaraja. Lakini kipindi hiki cha Lisu, wafanyakazi wengi wanalia na kusaga meno kwa mishahara yao kudumaa huku gharama za maisha zikiendelea kupanda. Ni wafanyakazi wachache ambao hawatamuelewa Lisu, kwa maana wameguswa moja kwa moja.

Ongezeko la Kundi kubwa la vijana wenye umri kuanzia 18 Kuendelea linaweza likawa sababu pia ya kuwatofautisha Lisu na Lowasa.

5. HALI YA UTEGEMEZI IMEBADILIKA
Siku hizi hali ya utegemezi inazidi kubadilika.

Kura nyingi wanazo wanawake, CCM inavuna kura nyingi kwa wanawake hasa wategemezi ambao wanasubiri mume alete pesa nyumbani. Wanawake hawa ni moja ya mitaji ya CCM kwani wao hawajui pesa inatafutwaje. Wao ni Goalkeeper. Wanawake tegemezi wao lawama huwapa waume zao pale mume anaposhindwa kutoa matumizi. Mume yeye ndiye anajua anakutana na changamoto gani huko mtaani.

Hali ya sasa imebadilika kidogo, wanawake nao wanatoka kwenda kutafuta riziki. Sio kwamba 2015 kurudi nyuma hapakuwa na wanawake waliokuwa watafutaji, hasha! Ila zama hizi kumekuwa na ongezeko kubwa la wanawake wanaotafuta pesa. Hivyo nao wanajua ugumu wa kuipata pesa, wanaona vikwazo.

Nachelea kusema, mikoa yenye wanawake watafutaji wengi wao hawaichagui CCM, angalia Mkoa wa Mbeya, njoo Iringa, Twende Kigoma, Nenda Mkoa wa Mara, Shuka Arusha, kisha Kilimanjaro, fika Dar es Salaam. Mikoa hiyo wanawake wengi nao wanajishugulisha, hivyo wanaona ni kwa namna gani serikali iliyokuwa chini ya CCM inavyowapa wakati mgumu katika utafutaji wa Riziki.

Utegemezi kwa vijana, vijana wa siku hizi wengi wameamka. Wanajishughulisha wengine kwenye kilimo, bodaboda, saluni, ujasiriamali n.k. Mikoa yenye vijana wachapakazi, watafutaji wengi ni rahisi kusombwa na upepo wa Lisu.

Mbinu kubwa ambayo itawafanya wanawake kuelewa hoja za Lisu, ni kuwaambia nao waingie mtaani watafute hela. Sio asubiri chakula ndani ya nyumba yeye kazi yake kula na kunenepa. Mwambie mkeo toka nawe tusaidiane kutafuta, hapo hata siku akimsikia Lisu anaweza kuelewa.

Lisu na Lowasa ni mbingu na Ardhi.

6. KUKUA KWA MITANDAO YA KIJAMII NA TEKNOLOJIA YA MAWASILIANO.
Idadi ya vijana wanaomiliki simu janja wakati wa Lowasa na sasa ni mbali mno. Kumekuwa na ongezeko kubwa la vijana wanaotumia simu janja ambapo wengi wanajiunga na mitandao ya kijamii. Wewe mwenyewe unaweza kufanya utafiti mdogo kuwa ndugu zako wangapi au hapo mtaani kwenu ni watu wnagapi mwaka 2015 hawakuwa na simu janja na sasa hivi wanazo. Ni watu wangapi unawafahamu ambao 2015 hawakuwa wamejiunga na mitandao ya kijamii kama Facebook, Instagram, Twitter, Jamiiforum n.k na sasa wamejiunga. Utakuta ni wengi.

Ongezeko la watumiaji wa simu janja na wanamitandao ya kijamii linaathari kubwa katika siasa. Kwani siku hizi sio rahisi kudanganya, ukimsingizia mtu, muda huo huo hata bila vyombo vikuu vya habari kama ITV, TBC, StarTv n.k mtu anakanusa, na anatoa ushahidi.

Watu siku hizi hawasubiri habari za magazetini au kwenye Televisheni

Kumfananisha Lisu na Lowasa ni kutotumia akili vizuri. Lisu ananafasi kubwa ya kushinda ukilinganisha na Lowasa ambaye hata kuongea dakika kumi zilikuwa ni shida kabisa.

Mimi ningekuwa ndio CCM, ningehakikisha Tundu Lisu hapitishwi na NEC, pengine hiyo ndio ingekuwa Figisu figisu ya kumuondoa Mchezoni, najua sio haki lakini ni bora ningepambana naye kwenye masuala ya NEC, Kuliko kukimbizana naye kwenye kampeni.

Hii ni kutokana na upande wa Pili wa Zanzibar ambapo nako hapatoshi.

Ningekuwa mimi, mgombea mmoja kati ya Lisu au Maalimu Seif ningemuengua NEC ili abaki mmoja. Lakini kuwa na wote wawili kwa wakati mmoja, hakika sijui.

CCM wasipuuzie, siku 60 kwa mtu anayejua kushawishi ni siku nyingi mno. Msimfananishe Lisu na Mzee Lowasa. Hamtaamini,

Narudia, siku 60 ni siku nyingi sana. Siku 60 zinamtosha Lisu kugeuza akili za Watanzania.

Tuipende nchi yetu.
Tupendane
Tulinde amani kwa kutenda haki.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
 
Watumishi wa umma mateso ya miaka 5 ya hakuna increments, kupanda vyeo (walimu),ongezeko la mshahara,kutolipwa malimbikizo yenu n.k iwe ni fundisho na akili zenu kuikataa ccm kwa nguvu zote.Familia zenu ziikatae ccm.

Msiwapigie kura ya urais,wabunge wala madiwani.Ndiyo wadhalilishaji wenu
Tutawapigia kura kama kawaida. Kwasababu, tunajua fedha za kuongeza mishahara ndo zimejenga zahanati na vituo vya afya ambavyo wazee wetu, wake zetu na watoto wetu ndo wanapokwenda kupewa huduma kila wanapougua.

Tunajua pia fedha za kuongezea mishahara ndo zinatumika kugharamia Elimu Bure ili watoto wetu waweze kupata elimu bila vikwazo.

Tunajua pia fedha za kuongeza mishahara ndo zimejenga Miundombinu ya barabara katika kila kona ya nchi hii ambazo hata Tundu Lissu anazitumia sasa hivi kwenda kuomba wadhamini na kufanya mikutano ya hadhara.

Tunajua pia fedha za kuongeza mishahara ndo zimenunua ndege, kujenga SGR, Bwawa la Umeme, Flyover ambavyo hivi vyote vitakuza uchumi na kutuwezesha kuongezewa mishahara mara dufu huko baadae kuliko tungeongezewa sasa hivi.

Kwa maana hiyo, tumekubali nyongeza ya mishahara yetu itumike kuwanufaisha watanzania wote na siyo sisi kundi la watu wachache. Tunakataa UBINAFSI tunatukuza UZALENDO kwa nchi yetu.
 
Back
Top Bottom