Niliwahi kutazama na kusikiliza Documentary moja kumuhusu JFK na uongozi wake pamoja na maisha binafsi kiujumla kuanzia utoto, malezi au makuzi yake, ujana, elimu , mpaka maisha ya kisiasa na mpaka kufikia kuwa rais wa nchi. Mzee mmoja wa kizungu mtu mzima sana jina nimemsahau alikuwa akihojiwa (alikuwa mfanyakazi wa Ikulu, Chini ya ofisi ya Rais)... Hakusita kuweka wazi kwamba Hayati JFK alikuwa muhuni sana! (Womanizer) hata mkewe alijua na ndoa haikuwa na amani, furaha wala raha kwa upande wa mwanamke. Vyombo vya ulinzi na usalama walitumia nguvu kubwa kuendeleza mahusiano mazuri kati yao kwa kuzima mizozo na magomvi ya mara kwa mara.
Inawezekana chanzo cha kifo cha JFK kilisababishwa na Umalaya wake wa Kipumbavu mpaka kufikia kufunguka maswala nyeti ya nchi na uongozi wake kwa ujumla kwa kimada.
Kimada mwenyewe alikuwa anatifuliwa mpaka na wahuni wengine wenye pesa pale Marekani, ikawa ni aibu na usalama wa nchi kuwekwa rehani, wasiwasi ukaigubika Ofisi ya Rais, Makamu wake, wizara ya ulinzi na mambo ya ndani.
Consensus iliyofikiwa ndio yale yaliyomkuta mchana ule wa November, 22 mwaka 1963... Na kifo kilimkuta akiwa na mkewe. Hapa ndo utakumbuka ule msemo wa waswahili "Usiteme bigijii, kwa karanga za kuonjeshwa" au "mwenda tezi na omo, marejeo ngamani"
Risasi za kutosha zilitawanya fuvu la kichwa chake, huku msafara wake hayati JFK ukiwa unaendelea... Kazi ya ziada akabaki nayo mkewe kukishikilia kichwa kisitawanyike kutokana na risasi nyingi kulengwa kichwani mwake.
Jamaa alifia mapajani mwa mkewe, na vile vihawara vyake wala havikuwepo kumsaidia alipokuwa anapambana na mauti mchana ule.
Madaraka yasiwabadilishe, tulieni na wake zenu.