Huyu ndio Dr. Emmanuel Nchimbi ninayemfahamu

Huyu ndio Dr. Emmanuel Nchimbi ninayemfahamu

Promo....magufuli ana kazi kweli kweli najua vimemo kibao na vinaendelea kumiminika
 
Mimi ukiniambia anasimamia anachokiamini sikuelewi maana tumeshuhudia hapa majuzi katoka nje ya kikao cha kamati kuu akisema CCM hawajatenda haki, halafu baada ya mwezi mmoja anapanda jukwaani kumnadi huyo mtu aliyesema hakupitishwa kwa haki, huu msimamo wa kinafiki umenifanya nimshushe vyeo

Basi umewashusha vyeo wengi nakumbuka ukumbi mzima ulimwimbia lowassa
 
Jamani Sita hafai kabisa.Tungekuwa na katiba mpya sasa hivi na hii matatizo ingekuwa hakuna.afadhali ya polepole kuliko sita.huku Jusa haingii...Polex2 ajaribu.

Sorry cdhan kama mtu anatakiwa apewe uspika sababu ya uafadhali wake that slowslow guy is ccm-maslah to his bones!!! HAFAI USPIKA labda awe msaidiz wa cheo cha Nape or Mrithi
 
* AKICHAGULIWA, NCHI KUPATA SPIKA BORA KAMA "JOHN BERCOW" WA UINGEREZA

Uongozi ni mchakato wa ushawishi ndani ya jamii, kwamba mtu moja anapopata madaraka uwasaidia wengine kukamilisha malengo ya pamoja.

Uongozi ni kuvuka mipaka ya mazoea na kuanzisha mchakato wa mabadiliko inayowasaidia watu kufikiri, kushiriki na kufikia malengo kwa tija na ufanisi mkubwa. Katika mbio hizi za kumtafuta Spika wa bunge la JMT lazima tukiri wengi waliojitokeza wana sifa ila ni vyema pia tukakiri ya kwamba Dr. E. Nchimbi ana sifa za ziada dhidi ya wengine...

1. Anawaza Mafanikio Makubwa
Kiongozi bora lazima awe na maono juu ya kuhakikisha kuwa nchi yake, kampuni yake au eneo lolote alilofanyia/analofanyia kazi inapata mafanikio makubwa. Tumeshuhudia hilo kwa Dr. Nchimbi alipokuwa UVCCM, serikalini katika wizara mbalimbali na idara mbalimbali..

2. Ana Nia
Haitoshi tu kwa kiongozi kuwa na mawazo bali kiongozi mzuri lazima awe na nia ya kutimiza. Kiongozi mzuri na bora atafaa kuchaguliwa kuwa kiongozi endapo atakuwa na uwezo wa kuratibu na kutekeleza alichowaza, ajue njia anayopita na kuwatangulia anaowaongoza kwa vitendo. Dr. Nchimbi ana sifa hii

3. Kujitambua
Lazima kiongozi ajitambue mwenyewe ni mtu wa namna gani, ajue uwezo wake na mapungufu yake na awe tayari kujiongeza maarifa kila siku, ili aweze kupokea changamoto na mabadiliko. Dr. Emmanuel Nchimbi ana sifa hii

4. Msimamizi wa Maamuzi
Katika maisha ya siasa, mara nyingi malengo hukumbana na vikwazo. Hivyo ni wajibu kwa kiongozi kusimamia maamuzi sahihi na kwa wakati. Dr. Emmanuel Nchimbi ana sifa hii

5. Kukubali Kukosolewa
Viongozi wengi wasiokuwa na sifa za uongozi huwa hawakubali kukosolewa, wakidhani kuwa hivyo ndio njia ya kuthibitisha usahihi wao. Kiongozi makini ni yule ambaye atakuwa tayari kukosolewa na kuwapongeza wanaomkosoa. Dr. Nchimbi ni kiongozi anayekubali kukosolewa...

6. Kuwa Msikilizaji
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kuwasikiliza walio chini yake, wakubwa, apokee maoni yao na ikiwezekana ayafanyie kazi. Dr. Nchimbi kalionyesha hili alipokuwa UVCCM, wizara mbalimbali alizopita, ndani ya NEC na CC. Huyu ndio tunamhitaji katika nafasi ya spika wa bunge la JMT

7. Kufata Haki
Kiongozi imara anatakiwa kufata haki. Asijione au kuona kundi fulani ina haki zaidi ya wengine katika sheria. Ni muhimu kwake kuonyesha jamii wako huru katika mawazo na matendo. Dr. Nchimbi marazote amekuwa mfano wa kuubiri HAKI na Amekuwa muumini wa haki.

8. Kuwa Egemeo la Watu
Kiongozi lazima awe egemeo la watu katika shida na raha. Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kusikitika, kuomboleza au kufurahi pamoja na watu anaowaongoza bila kujitenga nao. Na kubwa zaidi ajitolee kuwatumikia watu kwa hali na mali. Dr. Nchimbi katika hili ni mfano wa kuigwa. Amefanya hayo UVCCM, serikalini na wizara mbalimbali..

9. Kukubali Lawama
Kiongozi mzuri ni yule anayediriki kukubali lawama, awe amefanya au la. Anachotakiwa kufanya ni kukubali kulaumiwa. Dr. Nchimbi ni mfano wa kuigwa katika hili, amewahi kubeba lawaza zisizo zake kwa sababu anaelewa dhana ya dhamana na ni kiongozi aliyeiva.

10. Utatuzi wa Matatizo
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuzuia migogoro na kuitatua kwa haraka. Muongozo bora katika hili ni kusimama katika mawasiliano bora na watu unaofanya nao kazi. Hakuna shaka kwamba Dr. Nchimbi ni wa kuigwa katika hili. Amefanya hili akiwa ndani ya UVCCM, wizara mbalimbali na katika vikao vikubwa vya kimaamuzi..

11. Uaminifu/Ukweli
Kiongozi mzuri na bora ni yule aliyemwaminifu na mkweli. Ni yule atakayekuwa tayari kuonyesha ubora wa matendo na kauli zake. Dr. Nchimbi amekuwa mfano katika hili..

12. Mbunifu
Kiongozi mzuri ni yule anayejua au kubashiri nini kitatokea kesho kulingana na mienendo ya jamii. Baada ya kugundua hilo ni wajibu wake kuwa mbunifu na kuzuia madhara kutokea. Dr. Nchimbi ni kiongozi aliyembunifu, ndio maana katika kipindi chake UVCCM tulishuhudia jumuiya iliyoimara na kulinganishwa na jumuiya zenye nguvu kama ANC Youth League au iliyokuwa KANU Youth 1992...

13. Mfuatiliaji wa Katiba, Taratibu, Sheria na Kanuni za kiutendaji na kiuongozi...
Lazima tukubaliane kuwa uongozi ni utaratibu na sio maamuzi ya watu fulani. Ni taratibu, sheria na kanuni zinazowekwa kufikia malengo. Dr. Nchimbi marazote amekuwa muumini wa kufanya kazi zake kwa kufata utaratibu, sheria, na kanuni husika..

NB: Ni jambo la wazi kwamba kumchagua Dr. Nchimbi kuwa spika wa bunge la 11 la JMT nchi itakuwa imepata spika bora, mahiri na shupavu kama "John Bercow" wa House of Commons. Dr. Nchimbi ana uwezo, ana sifa, na kubwa zaidi anatosha..

Note: Haya ni mawazo huru, hayana muingiliano na kundi lolote!.....
 
Nchimbi hawezi shika cheo chochote na kudumu, laana za wazee bado zinamtafuna, hawezi fika kokote, ndio mwisho wake pale alipo, huyu alimfanyia mabaya sana mzee Gama,

Yaaan kamsaidia gama afu unaleta umbea wako kanye hiyo mavi ndio uje hapa
 
Gama katika nchi hii ni mmoja tu, Dr lawrence Gama, huyu alimfanyia fitina nyingi, na wazee waliondoka na vinyongo, nchimbi hawezifika mbali,
 
Mtoa mada unamjua uyu jamaa kweli?
Tuliosoma nae nae Mzumbe twamjua ile nafasi hauwezi.
Na pia ukaribu wake na EL ndo kabisa unafanya awe mbali na iyo nafasi
 
mnaomsifia nchimbi mje mtuambie jimbo lake kalisaidia nini? kaingia umeme wa jenereta songea kaondoka kashindwa kuleta umeme wa maji.barabara ya songea mjini kwenda mateka anakofikiaga hapa songea vumbi tupu kifuku tope halisemeki. sifa ya nchimbi nikupandisha daraja majimaji na kuishusha tu.
 
* AKICHAGULIWA, NCHI KUPATA SPIKA BORA KAMA "JOHN BERCOW" WA UINGEREZA

Uongozi ni mchakato wa ushawishi ndani ya jamii, kwamba mtu moja anapopata madaraka uwasaidia wengine kukamilisha malengo ya pamoja.

Uongozi ni kuvuka mipaka ya mazoea na kuanzisha mchakato wa mabadiliko inayowasaidia watu kufikiri, kushiriki na kufikia malengo kwa tija na ufanisi mkubwa. Katika mbio hizi za kumtafuta Spika wa bunge la JMT lazima tukiri wengi waliojitokeza wana sifa ila ni vyema pia tukakiri ya kwamba Dr. E. Nchimbi ana sifa za ziada dhidi ya wengine...

1. Anawaza Mafanikio Makubwa
Kiongozi bora lazima awe na maono juu ya kuhakikisha kuwa nchi yake, kampuni yake au eneo lolote alilofanyia/analofanyia kazi inapata mafanikio makubwa. Tumeshuhudia hilo kwa Dr. Nchimbi alipokuwa UVCCM, serikalini katika wizara mbalimbali na idara mbalimbali..

2. Ana Nia
Haitoshi tu kwa kiongozi kuwa na mawazo bali kiongozi mzuri lazima awe na nia ya kutimiza. Kiongozi mzuri na bora atafaa kuchaguliwa kuwa kiongozi endapo atakuwa na uwezo wa kuratibu na kutekeleza alichowaza, ajue njia anayopita na kuwatangulia anaowaongoza kwa vitendo. Dr. Nchimbi ana sifa hii

3. Kujitambua
Lazima kiongozi ajitambue mwenyewe ni mtu wa namna gani, ajue uwezo wake na mapungufu yake na awe tayari kujiongeza maarifa kila siku, ili aweze kupokea changamoto na mabadiliko. Dr. Emmanuel Nchimbi ana sifa hii

4. Msimamizi wa Maamuzi
Katika maisha ya siasa, mara nyingi malengo hukumbana na vikwazo. Hivyo ni wajibu kwa kiongozi kusimamia maamuzi sahihi na kwa wakati. Dr. Emmanuel Nchimbi ana sifa hii

5. Kukubali Kukosolewa
Viongozi wengi wasiokuwa na sifa za uongozi huwa hawakubali kukosolewa, wakidhani kuwa hivyo ndio njia ya kuthibitisha usahihi wao. Kiongozi makini ni yule ambaye atakuwa tayari kukosolewa na kuwapongeza wanaomkosoa. Dr. Nchimbi ni kiongozi anayekubali kukosolewa...

6. Kuwa Msikilizaji
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kuwasikiliza walio chini yake, wakubwa, apokee maoni yao na ikiwezekana ayafanyie kazi. Dr. Nchimbi kalionyesha hili alipokuwa UVCCM, wizara mbalimbali alizopita, ndani ya NEC na CC. Huyu ndio tunamhitaji katika nafasi ya spika wa bunge la JMT

7. Kufata Haki
Kiongozi imara anatakiwa kufata haki. Asijione au kuona kundi fulani ina haki zaidi ya wengine katika sheria. Ni muhimu kwake kuonyesha jamii wako huru katika mawazo na matendo. Dr. Nchimbi marazote amekuwa mfano wa kuubiri HAKI na Amekuwa muumini wa haki.

8. Kuwa Egemeo la Watu
Kiongozi lazima awe egemeo la watu katika shida na raha. Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kusikitika, kuomboleza au kufurahi pamoja na watu anaowaongoza bila kujitenga nao. Na kubwa zaidi ajitolee kuwatumikia watu kwa hali na mali. Dr. Nchimbi katika hili ni mfano wa kuigwa. Amefanya hayo UVCCM, serikalini na wizara mbalimbali..

9. Kukubali Lawama
Kiongozi mzuri ni yule anayediriki kukubali lawama, awe amefanya au la. Anachotakiwa kufanya ni kukubali kulaumiwa. Dr. Nchimbi ni mfano wa kuigwa katika hili, amewahi kubeba lawaza zisizo zake kwa sababu anaelewa dhana ya dhamana na ni kiongozi aliyeiva.

10. Utatuzi wa Matatizo
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuzuia migogoro na kuitatua kwa haraka. Muongozo bora katika hili ni kusimama katika mawasiliano bora na watu unaofanya nao kazi. Hakuna shaka kwamba Dr. Nchimbi ni wa kuigwa katika hili. Amefanya hili akiwa ndani ya UVCCM, wizara mbalimbali na katika vikao vikubwa vya kimaamuzi..

11. Uaminifu/Ukweli
Kiongozi mzuri na bora ni yule aliyemwaminifu na mkweli. Ni yule atakayekuwa tayari kuonyesha ubora wa matendo na kauli zake. Dr. Nchimbi amekuwa mfano katika hili..

12. Mbunifu
Kiongozi mzuri ni yule anayejua au kubashiri nini kitatokea kesho kulingana na mienendo ya jamii. Baada ya kugundua hilo ni wajibu wake kuwa mbunifu na kuzuia madhara kutokea. Dr. Nchimbi ni kiongozi aliyembunifu, ndio maana katika kipindi chake UVCCM tulishuhudia jumuiya iliyoimara na kulinganishwa na jumuiya zenye nguvu kama ANC Youth League au iliyokuwa KANU Youth 1992...

13. Mfuatiliaji wa Katiba, Taratibu, Sheria na Kanuni za kiutendaji na kiuongozi...
Lazima tukubaliane kuwa uongozi ni utaratibu na sio maamuzi ya watu fulani. Ni taratibu, sheria na kanuni zinazowekwa kufikia malengo. Dr. Nchimbi marazote amekuwa muumini wa kufanya kazi zake kwa kufata utaratibu, sheria, na kanuni husika..

NB: Ni jambo la wazi kwamba kumchagua Dr. Nchimbi kuwa spika wa bunge la 11 la JMT nchi itakuwa imepata spika bora, mahiri na shupavu kama "John Bercow" wa House of Commons. Dr. Nchimbi ana uwezo, ana sifa, na kubwa zaidi anatosha..

Note: Haya ni mawazo huru, hayana muingiliano na kundi lolote!.....

Magamba wanamfumo kulindana wanaogopa mtu mwenye maamuzi magumu
 
Nchimbi hawezi fika mbali, nchimbi sio kiongozi, ule wakati wa uhuni uhuni umeshapita, namfahamu vizuri, hawezi fika kokote kisiasa na hata akifika atatolewa, namshauri arudi vyuon kufundisha, team magufuli haimtaki huyu, sorry nimejulishwa kuwa phd yake pia magumashi
 
DR EMMANUEL NCHIMBI - MFANO WA KUIGWA NA VIJANA.

Naomba leo hii nimzungumzie Dr Emmanuel Nchimbi kwa kipindi kifupi nilicho kuwa nae kama M/kiti wangu wa kamati ya kampeni ya vijana taifa kwenye uchaguzi mkuu 2015.

Nimeskia mengi yakisemwa kuhusu Dr Nchimbi, yapo ninayo yajua na yapo nisiyo yajua. Leo nimeamua kuzungumza kama Makamu M/kiti wa Kamati ya Kampeni ya Vijana Taifa juu ya Dr Emmanuel Nchimbi. Nitakuwa simtendei haki Dr Nchimbi wala siwatendei haki vijana wenzangu kama ninayo fahamu nitaacha yapite. Waswahili husema, mwenye sifa mpe sifa zake.

Nafahamu Dr Nchimbi ni mmoja ya viongozi walio jitolea kuchukua form ya kugombea nafasi ya uspika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Natambua mchakato huu ndani ya chama utaanza rasmi kesho katika kuchuja na kuleta majina matatu ambayo yatapelekwa kwa wabunge wa CCM lichaguliwe jina moja ambalo litawasilishwa bungeni kwa ajili ya kupigiwa kura.

Nayazungumza haya bila ya kujali kama jina la Dr Emmanuel Nchimbi litarudi ama halitarudi. Nazungumza haya nikiwa sio mpiga kura wa mchakato wote unao tarajiwa kumpata Spika wa bunge. Nazungumza haya yakiwa hayahusiani na nafasi yangu yoyote ndani ya chama, haya ni mawazo yangu mimi binafsi kama kada mtiifu wa Chama Cha Mapinduzi.

Naamini wengi tulio fanya kazi na Dr Nchimbi kwa kipindi cha takribani siku 60 za kampeni tutakuwa tumejifunza mambo mengi sana. Nitakuwa muwazi, kipimo alicho pimiwa Dr Emmanuel Nchimbi juu ya ile kauli, "Chama kwanza mtu baadae." niliishuhudia katika mchakato mzima wa kumtafutia kura Dr John Pombe Magufuli, wabunge na madiwani wa CCM.

Nakubaliana na wengi kuwa Dr Emmanuel Nchimbi ni mmoja ya watu ambao waliotoka nje ya kamati kuu na kutoridhika na namna uchujwaji wa wagombea wa urais walivyo patikana akiwa na Mh Sophia Simba na Mh Adam Kimbisa ndani ya kamati kuu. Niliwahi kumuuliza kwa nn uliamua kutofautiana na walio wengi? Alinijbu, unajua kwenye vikao kuna kukubaliana na kutokubaliana, ni mambo ya kawaida ktk vikao vyovyote hasa ndani ya chama. Na kwa bahati nzuri niliziweka sababu zangu wazi za kuto kukubaliana na maamuzi yaliyotolewa na wenzangu wa kamati kuu. Lakini mwisho wa siku demokrasia inatoa maamuzi yaliyo kubalika na wengi, na kwa kuwa halmashauri kuu pamoja na mkutano mkuu ulikubaliana na maamuzi yaliyo tolewa na walio wengi, Mimi kama Dr Emmanuel Nchimbi sina budi kuwaunga mkono na kuheshimu maamuzi ya chama changu. Na kweli alifanya hivyo na hata kwenye mikutano ya hadhara mbalimbali alionyesha msimamo wake juu ya kuwaunga mkono wagombea wa CCM.

Dr Nchimbi ni mmoja ya vijana wachache walio fuzu kipimo cha kukipigania chama chetu na kujionyesha hadharani kuwa ni kada mtiifu wa CCM; licha ya Ndugu Edward Lowassa kuamua kukihama chama.

Niliwahi kumuuliza, kwa nn wewe umeamua kubaki CCM? Akaniambia, ktk jambo ambalo naweza kwenda hata mahakamani kupinga maamuzi yake ni kunyang'anywa kadi yangu ya CCM. Nimekulia ndani ya chama hiki toka chipukizi, siwezi kung'atuka na niko tayari kukupigania chama hiki kwa nguvu zangu zote.

Dr Nchimbi nimemshuhudia mara kadhaa kwa vitendo juu ya uhalali wa kauli zake. Ktk kipindi chote tulicho fanya nae kazi kwenye kampeni, alijitoa usiku na mchana; kwa nguvu zake zote, kwa mikakati yake yote, kwa mapenzi yake yote, kwa hali na mali kuhakikisha Dr John Pombe Magufuli wa CCM ndiye anakuwa Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Sikuwahi kuona wala kushuhudia siri za vikao vyetu zikitoka nje. Dr Nchimbi ni mvumilivu kweli kweli. Mara zote aliunganisha UVCCM na Shirikisho na kujitahidi kumfanya kila mmoja wetu asijione yuko chini ya mwenzake. Alituunganisha, alitutia moyo na hata wakati mwingine tulipo ona mambo hayawezekani kwake yeye Dr Nchimbi halikushindikana jambo.

Dr Nchimbi ni muungwana sana, licha ya kuwa ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM lkn hatukuwahi kuona utofauti wa cheo chake kwenye kazi. Alijishusha na kufanya kazi na sisi kama vile ni watoto wa baba mmoja wa rika moja.

Dr Nchimbi sio mtu wa kukata tamaa hata kama jambo linaashiria kushindikana. Mara zote hasa pale tulipo rudishwa kurekebisha budget ya kampeni alitutia moyo tusikate tamaa na kutupa nguvu ya kusonga mbele.


Kwa kipindi chote tulicho wahi kufanya nae kazi, amekuwa msikivu sana. Hakujali wala hakubagua mtu. Alijitoa kwa moyo wake wote.

Nitasema wazi, mapenzi ya Dr Nchimbi na CCM ni kama chanda na pete. Anaipenda CCM bila ya unafiki, kwa dhati ya moyo wake. Sisi vijana tunajiona ni wenye bahati ya kipekee kufanya kazi na yeye.

Nje ya hapo, nakumbuka maandalizi ya miaka 38 ya CCM yaliyo fanyika Ruvuma. Yalifana na yalipendeza kwenye macho ya watu wengi. Ni kazi kubwa iliyo simamiwa na Dr Emmanuel Nchimbi. Nakumbuka bado siku moja tu maadhimisho yafanyike, kofia za vijana wa chipukizi zilikuwa hazijapatikana. Nilimuona alivyotokwa jasho kuhangaika huku na kule kuhakikisha jambo linafikiwa.

Dr Nchimbi ni mtu wa misimamo. Hata watu walipomkataa Dr Jakaya Kikwete yeye alisimama nae mpaka wakati wa JK ulipofika na kupata ridhaa ya watanzania kuwa Rais wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Dr Nchimbi amewahi kushikilia nafasi nyingi ndani ya chama na ndani ya serikali. Na ktk kipindi chote cha utendaji kazi wake aneonyesha ni mtumishi wa kweli, anayejali na kujali matatizo ya wananchi wake.

Hata pale watu wengi walipokuwa wanategemea kumuona Dr Nchimbi anachukua form ya kugombea uraisi hakufanya hivyo. Hata pale watu wengi walipokuwa wanategemea kumuona Dr Nchimbi anachukua form ya ubunge hakufanya hivyo. Leo amechukua form ya uspika, sina mashaka naamini alikuwa anajua anacho kifanya. Alikuwa anajua wapi anaweza kuwatumikia watanzania na kufanya vizuri zaidi, alikuwa anajua kwa kipindi kama hiki, sehem kama hii ndio sehem sahihi ya yeye kuwatumikia watanzania.

Naamini vijana wengi hasa wale aliyo bahatika kuwaongoza, watakuwa mashuhuda wazuri sana wa kumsemea mengi mazuri zaidi kuliko ninayo yafahamu. Naamini viongozi wenzake ndani ya chama, serikali na taasisi mbalimbali wanao uwezo wa kumuelezea mbali zaidi kuliko nilipo fikia mimi.


Wazungu husema, "if you don't appreciate what others have, you will never be blessed with what you have."

Nimemzungumzia Dr Emmanuel Nchimbi kama mwana taaluma niliye bahatika kufanya nae kazi, kijana mwenzangu niliye bahatika kushirikiana nae kwenye mambo mbalimbali. Nimeona uwezo, nguvu, spidi, hekima na busara zake. Na leo nimevutiwa kumzungumzia bila ya kujali kama jina lake litarudi ama la. Nelson Mandela aliwahi kusema, "do small things in a great way." Kwa hivi vichache tulivyo bahatika kufanya kazi na wewe na kwa ubora na viwango vyako. Sina mashaka hata kwenye bunge lijalo ambalo lina vugugu la vijana wengi wenye hulka na misimamo tofauti, unaweza kuwavusha salama.

Niendelee kukutia moyo, yatasemwa mengi yataletwa mengi ila siku zote mti wenye matunda ndio hupigwa mawe. Nina uhakika unaendana na kasi na nguvu ya Dr John Pombe Magufuli.

Asante kwa kuwa msaada kwa vijana wengi. Asante kwa kuwa msaada kwa watanzania wengi. Mungu akubariki sana. Tunakutakia kila la heri.

Nawatakia wagombea wote pia kila la heri. Namkubali Dr Emmauel Nchimbi, ila nitaheshimu maamuzi yatakayo fanywa na viongozi wetu wa chama. Spika atakaye pitishwa na bunge kwa mujibu wa sheria, ndiye tumaini langu na tumaini la watanzania.

Mungu ibariki Tanzania.

Imetolewa na:
Zainab Abdallah,
Makamu M/kiti wa Kamati ya kampeni ya Vijana & Shirikisho Taifa,
Kada Mtiifu wa CCM.
 
Twende na Nchimbi
Ni msomi
Ni kijana
Ana uwezo
Ana uzoefu mkubwa
Anaweza kuunganisha watu wa mitizamo tofauti
Ni mwanadiplomasia
Ana kipaji cha uongozi
Ni rika la wabunge waliowengi ktk kipindi hiki
Anaijua ccm ndani nje
Anaijua nchi yetu
Anaweza tumsaidie atalisaidia bunge.
Hafai kuwa spika. Bado ana u-uvccm sana. Bado ni kada sana wa ccm kiasi kwamba hawezi kuwa fair kwenye uspika. Hiyo nafasi inamfaa aidha Ndugai au Zungu
 
Back
Top Bottom