Huyu ndio mwanaume ninayemtaka, sitaki kuumiza moyo wangu una thamani

Hivi vigezo vingine mnavyovitaka mtakuja kuolewa na mapepo nyinyi wadada wa siku hizi za mwisho! Angalia usije ukataka mwanaume unaye mtaka aje na machozi ya samaki au sharubu za simba jike! Hivyo sio vigezo ila ni "Masharti ya kiuganga wa kienyeji" na kwa Masharti hayo, trust me utasubiri sana! Wapo walioweka Masharti ya ajabu kama hayo wakaishia kuolewa na waendesha guta tu (Ushahidi ninao). Sisi wakristo tuna amini mke /mume mwema anayetoa ni Mungu, sasa kampangie Mungu hayo Masharti ya kipepo uone kama hujawa Ajuza na hata wa kukutania tu kukuita mchumba usipate!!!! Kwanza unatoa vigezo vyote hivyo kwamba wewe ni malaika? Au ni BIKIRA? Any ways, najua nitakuwa nimekukwaza lakini utakuja yakumbuka haya maneno yangu
 
Aisee

- Itakuwa wewe ni mpenzi mkubwa sana wa tamthilia za Wakorea/Philippines/US
- Maana naona umeathirika sana na maisha ya tamthilia
 
Usisahau tuu kuwa alipo bwana na bibi yuko pembeni
 
Safi kabisa mkuu. Agiza soda nakuja kulipia [emoji23]
 
Mungu hawezi kusikiliza masharti ya kipuuzi kama haya mkuu
 
Sifa zote ninazo ila nataka Kitu kimoja tu toka kwako “BIKRA”
Kama ipo njoo PM tuyajenge.
 
Ukipapata panaweza geuzwa machimbo ya wanaume walio na sifa nyiiiiingi mnoo[emoji23] [emoji23] [emoji23]


Watz ni pasua kichwa asee
 
namjua mungu kuzidi wewe. wewe una hasira zako nenda kaangalie mpira Barcelona wanacheza
 
Daaaa!!!!nataman kuja ila vigezo vingine sina kama elimu uliyotaja pia mm siyo mrefu sana niko saizi yakati na tayari nina mtoto mmoja ila uzoefu wakuka inje ya inchi ninao maana nimekaa Africa kusini miaka mitano, kuhusu ajira sina ila nimeajiri maana nina mgodi wa dhahabu mkoani sgda hivyo nimetoa ajira pia nina duka la simu dodoma upande wa upendo nimefundishwa tangu utotoni nitakupenda haadi mwenyewe utataman ungenijua mapema wazazi wapo wote nashukuru mungu pia mm nimkweli na najiamin punguza vigezo tuyajenge
 
Elimu yangu lasaba sasa apoo ntakuwa nime kosa papuch!!!
 
namjua mungu kuzidi wewe. wewe una hasira zako nenda kaangalie mpira Barcelona wanacheza
Anaye mjua Mungu hawezi kuandika masharti ya kichawi kama haya. Pili mimi sipo interested na mpira hasa wa Ulaya. Tatu siwezi kukuoneshea hasira zangu wakati hujanikosea. Tunachosema hapa ni ushauri, unaweza ukachukua au ukaacha ila usije ukasema hatukukuambia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…