Huyu ndiye aliyemtukana Rais Kikwete na sasa anatukana Marais wenzake

Hio inahusu Poverty ila GNI sio asilimia, unaweza ukai convert kwenda Asilimia ila yenyewe sio ni no tu index.
Tumia ubongo vizuri, heading imewekwa juu kuwakilisha data zote za chini ndio maana hata kwenye period(year) umeona hapo kwenye GNI imejazwa mwaka 2018.

Uwe unaacha Uongo uongo
 
 
Pinga hoja ya mwandishi, ambacho ni chombo cha habari Rwanda. Usianze kunishambulia mimi.
Mkuu kuna mambo mengine yanahitaji common sense tu, kuna hoja hata kuzisema mbele ya watu unatakiwa ujifikirie kwanza kama watu hawatakuona hazikutoshi.
 
Bado unaendelea na Ujinga wako wa kuweka screenshot?

Kina kushinda nini kuweka link? Tusome artcile yote na sio unachotaka wewe?
 
Mkuu kuna mambo mengine yanahitaji common sense tu, kuna hoja hata kuzisema mbele ya watu unatakiwa ujifikirie kwanza kama watu hawatakuona hazikutoshi.
Asante, kama huna data nichunie tu sio lazima ku quote comment zangu, sina muda na mipasho.
 
Definishon yako ni sawa na ya mu presida Trump.

utabisha.
#bigot
 
Bado unaendelea na Ujinga wako wa kuweka screenshot?

Kina kushinda nini kuweka link? Tusome artcile yote na sio unachotaka wewe?
Link si ndio zinakushinda kusoma?
Hiyo article ni ya 2013
Soma
 
Umemuelewa lakini?
Mbona anaeleweka.

Umasikini anaoutaja yy ni ule wa kukaririshwa.

Umasikini ni nn?? Ukimuuliza hili swali hatokujibu kabisa.

Hivi kuna nchi inauzidi Umasikini wa Ulaya per capita? Africa?
 
Ila zinatofautiana huo umasikini, we unafikiri kwanini nchi jirani kama Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Congo etc wengi wapo Tanzania wa natafuta maisha? Tanzania tuna u afadhali sana huu ukanda wetu,
Watanzania walivyojaa Mozambique, Malawi, Zambia, Uganda, Kenya, Botswana, Namibia na South Africa ni balaa na ukitoa labda wa Zambia na Malawi ambao wengi ni wafanyabiashara kwingineko majority ni machafuchafu wanaoaibisha Utanzania, do you know the reason? Ugumu wa maisha. Nchi zote hizo mtu akisema ni Mtanzania cha kwanza wanamuhisi ni mwizi mpaka atakapo-prove otherwise lakini wakisikia Mkenya hata kama ni mwizi watamfurahia kwa bashasha hoping he/she is a professional in a certain field.
Kama umewahi kusafiri around Africa definitely you know this.
Kwa South Africa bora hata useme wewe ni Mrundi kuliko Mbongo, Durban kumejaa machafuchafu wa Kibongo (ma street hobo, mateja) utadhani uko Kensington-Phills.
 
2008, article ya 2013 ila data za 2008.
 
Ukitoa South Africa na nchi za Kusini Tajiri kama Botswana hakuna Nchi jirani yetu ambayo ina Watanzania wengi kuliko Raia wa hio Nchi waliopo Tanzania.
 
Hizo data unazozikataa za AI ndizo hizo hizo data unataka tuamini haziko sawa. Iwe ni AI au World Bank etc, data zake ziko biased.
Na ukiwauliza kwanini data zenu ziko biased kiasi hiki, wanakwambia kwa sababu hakuna data za uhakika Afrika. Unabaki unashangaa tyu


Hiyo inatueleza
  • Wanapika hizo data, na kwa msingi huo
  • Data zao sio za Uhakika
In short hata hizo data za World Bank sio sahihi. Na itoshe kusema, sio data za kutumiwa mitaani mwetu. Utaharibikiwa na kuvurugwa kabisa.
 
Anaandikaga vitu hovyo akiamini Hakuna wajuaji. Kaweka data za Rwanda kuhusu slums za 2013 wakati world bank wana data ambazo ni recently Ila kwa kuwa zipo vizuri kaziacha, kwingine anatia za world bank. Huyu mshikaji hayupo sawasawa
 
Anaandikaga vitu hovyo akiamini Hakuna wajuaji. Kaweka data za Rwanda kuhusu slums za 2013 wakati world bank wana data ambazo ni recently Ila kwa kuwa zipo vizuri kaziacha, kwingine anatia za world bank. Huyu mshikaji hayupo sawasawa
Naamini yupo sawasawa mukichwa na anajua analolifanya.

Watu kama hao huwa wanajitoa akili kufikisha jumbe zao .😁😇
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…