Huyu ndiye daktari aliyejichoma sindano ya UKIMWI ili kuthibitisha kuwa UKIMWI ni uongo!

Huyu ndiye daktari aliyejichoma sindano ya UKIMWI ili kuthibitisha kuwa UKIMWI ni uongo!

Status
Not open for further replies.
"Sasa jiandae vyema na umsikilize kwa makini kabisa neno baada ya neno(usiruke neno) huyu mgunduzi wa HIV anachosema hapa.Narudia,huyu anayesema hapa ndiye mgunduzi wa HIV.Yaani ni 'mungu' wa wale wanaoamini katika dini ya VVU/Ukimwi.Natarajia kwamba hakuna mtu yeyote duniani atakayepinga maneno yake;msikilize hapa chini;
"You can be exposed to HIV many times without being chronically infected,our immune system will get rid of the virus within few weeks if you have good immune system" Na hata ukimfuatilia Prof.Duesberg(virology machine) anayepinga kuhusu HIV naye alishasema hivihivi.Huyu mungu wao anathibitisha tu maneno ya Duesberg ambayo mwanzo aliyakataa,sasa hivi anaona aibu.

Halafu endelea kumsikiliza anazungumzia matatizo halisi yanayotusumbua hasa katika nchi za afrika.

1.Nutrition/misosi
2.Oxidative stress;Hii nitaizungumzia kwa undani baadaye
3.Clean water

Halafu anasema "their immune system doesn't work well already even if they are not infected with HIV",maana yake ni kwamba, watu wanakuwa na ukimwi hata kabla ya kuingiwa na VVU.

Anaendelea kushauri njia za kupunguza maambukizi ya HIV huyu feki ambazo ni;
1.Nutrition
2.Proper antioxidants
3.Hygiene measures
4.Fighting the specific infection(tusisingizie HIV,tutibu tatizo halisi)

Anaulizwa:"If you have good immune system then your body can get rid of HIV?"
Anajibu:Yes.
Ooooh very interesting!!! au mimi naota?Hebu sikiliza wewe mwenyewe.

Anaendelea kusema tena kwamba;"This is important knowledge which is completely neglected,people always think of drugs and vaccines"

Na mwisho yeye mwenyewe anakubali kwamba alichokisema ni tofauti na kile alichosema kipindi cha nyuma,yaani vinapingana.Huyu jamaa ameingizwa kwenye kundi la watu wenye roho mbaya bila kupenda,sasa roho yake inamsuta na anaamua kusema ukweli.Huyu ndiye mgunduzi wa HIV feki,Robert Gallo alimuibia tu data na yeye ndiye katangazwa kwanza.Walichokigundua hata wenyewe wanajua kwamba hakisababishi Ukimwi,ni njaa tu ndio inawasumbua.

Haya sikiliza sasa;

"

Pamoja na hayo yote,hakuna virus anayesababisha ukimwi.Watu wanashindwa tu kuunganisha dots za maelezo niliyotoa kwa kuwa labda ni mengi sana na hayako kimpangilio kutokana na mjadala ulivyo.Hata wenyewe waliogundua huyo HIV feki wanajua kwamba HIV hasababishi ukimwi na ndio maana kuna wakati wenyewe kwa wenyewe wanapingana.Nitakuleteeni video nyingine inayoonesha kwamba wanapingana halafu ninyi wenyewe muamue.
Na ndio maana huyu mgunduzi alikubali kusema tu hayo lolote na liwe maana ndio ukweli wenyewe.Wengine wanasema HIV peke yake hawezi kusababisha ukimwi,anahitaji co factors,ilihali wengine wanasema HIV peke yake anaweza kusababisha ukimwi bila co factors,nitawaleteeni hiyo video.Unaona sasa penye ukweli uongo hujitenga?

Watu wanaogopa ukimwi kwa sababu ya kasumba tu,neno hili limewaingia vichwani mwao kwa kurudiwa mara kwa mara huku wakioneshwa video za kutisha za wagonjwa bila kujali uhalisia kwamba mgonjwa alikuwa anaumwa nini hasa.Watu wanaogopa kitu ambacho kilikuwapo tangu kabla ya kutangazwa kwa HIV,eti kwa sababu wameambiwa HIV anasababisha ukimwi ndio wanaugopa sasa,kumbe ulikuwapo tangu zamani na hautishi na unatibika kirahisi na wakati mwingine unaondoka wenyewe bila ya wewe kujijua,ukibalisha lifestyle tu uko poa.

Sasa Je,

1.Kuna daktari hapa kwetu anaweza kukwambia kama unaweza kuwa na HIV(feki) lakini kinga ya mwili wako inaweza kumdhibiti na kumtoa kama alivyosema huyu mgunduzi?Vinginevyo wapinge kwamba huyu sio mgunduzi.

2.Huyu mgunduzi anakwambia "people always think of drugs and vaccines" anaposema drugs anamaanisha ARVs kwa maana ndizo zinazotumika kwenye AIDS.Na maana yake nyingine ni kwamba,huwezi kuwa na HIV kama kinga yako iko safi.

Sasa kama mnatakata kujithibitishia wenyewe,muulize daktari yoyote bongo kama anaweza kukubali hayo aliyosema mungu wake.Hapo ndipo utakapoona kwamba kasumba ni kitu kibaya sana.

Wenzetu wazungu sio wepesi kupinga kama sisi ngozi nyeusi.Ushauri huu wengi wanaujua toka kitambo,na ndio maana they don't take a shit kwenye ugonjwa huu feki,wanakula raha tu.

Sisi weusi ndio tumefanywa malimbukeni na shimo la kutupia madawa yao yenye sumu.Halafu eti wanatuambia tuyahifadhi vizuri yasije kuharibika.UNAHIFADHI SUMU YA MWILI WAKO?WE VIPI?

Ama kweli watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.Eti unatakiwa uhifadhi vizuri sumu ya mwili wako.Sasa kama kuna daktari yupo,aje kupinga maneno ya huyu mungu wao.


Ndio sisi tulivyo,tunakimbia HIV tunakimbilia ARVs ambazo ndizo mziki mnene wenyewe.Hivi vitu watu hawawezi kuvielewa mara moja mpaka kwanza wajue historia ya medicine na viwanda vya madawa ikoje.Hapo ndio watajua kwamba watu hawana masikhara kwenye biashara.



Likes a bunch. Spread the knowledge.

-Kaveli-
 
Ok naendelea kukuelewa..
Ila hujanijibu kuwa kama ukimwi haupo, je nn kinapelekea mtu kufa na njia gani inaambukiza
Ngoja nimsaidie: Mambo makuu mawili yanayopelekea mtu kuumwa mpaka kufa ni;

1. Stress: Hii inajumuisha tatizo la kisaikolojia lililosababishwa na kuaminishwa kuwa Ukimwi unaua na ukiwa na ukimwi utaumwa magonjwa meng bila kupona, hii hupelekea mtu kuyapata hayo magonjwa kweli na kufariki

2. Madawa makali ya ARV: Dawa hizi huwa ni kali sana na huwa na sumu ambazo baada ya muda huubadilikia mwili na kuufanya kudhoofu ghafla na kupelekea kifo

Maelezo ni mengi sana ila nimejitahidi kufupisha.
 
Kabla ya hizo ARVs unakumbuka ukimwi ulimaliza watu wangapi kagera wakati unaingia??Na kama haukua ukimwi ulikua ni ugonjwa gani?
 
Ni huu utaratibu wa kwenda hospitali unajisikia maralia au tumbo linauma wanakwambia tunakupima na ngoma sijui wameutoa wapi,wanadhan kupima ngoma ni kama unapima joto la mwili,nilishaenda pale palestina kadoctor ka kike kakaniletea hizo mambo nikakaangalia nikasema nakuja kuja kushtuka nilitokezea mtaani kwangu
 
HIV/AIDS au VVU/UKIMWI hauambukizwi kwa njia ya ngono/sex na HIV hasababishi ukimwi.Jitahidini kidogo ku stretch uwezo wenu,elimu ipo lakini mnairuka kwa makusudi.

HIV/AIDS is a mindset disease.Sijui kama nitaeleweka kwa kusema hivi.Yaani ugonjwa huu haupo kiuhalisia,kinachoua si HIV bali kinachoua ni ARVs kwa wale wanaozitumia.Hata kama mtu hatumii ARVs na amedhoofika wewe mpime tu utagundua kwamba lazima awe na ugonjwa fulani unaofahamika,aidha TB,Pneumonia,Cancer nk.

Watu wanadhani mimi nimekurupuka kwa siku moja tu na kuja kuandika yote haya,la hasha nimefuatilia na kufanya tafiti ya mambo haya kwa zaidi ya miaka 5.Watu wanachukulia kirahisi sana,hawagundui hata kwa nini mimi ninawaeleza haya,hawagundui hata kidogo upendo huu ninaouonesha kwao.
Kwa kiasi fulani nakubaliana na wewe japo mimi najihusisha na sekta ya afya ipo hivi mwaka 2011 nilienda na kaka yangu temeke alikua na hali mbaya sana kupima aligundulika na TB na HIV hatukuamink tukapima hospital kadhaa majibu yakwa vilevile.sasa wakasema wataanza kutibu TB then ndo waje HIV kuzuia asilete madhara zaidi.
Kweli alitumia dawa za TB baada ya mda fulani akaanza kuwa sawa mpaka kupona..baada ya kupona akatakiwa kupewa ARVs bro alikataa kata kata na hakawa hatumii,,Mwaka 2013 mkewe akapata ujauzito na akajifungua mtoto nilifatilia kadi yake ya clinic alikua salama na mtoto hadi leo yuko salama na yeye mwenyewe ana afya na mkewe pia na hadi leo nikimuuliza anakwambia yeye ana amini ukimwi ni stori na atakufa kwa kingine sio ukimwi.Baba yangu mara kadhaa alikua ana mwita kumlazimisha mwisho wa siku ameona na yeye stori tu.

2014 Shangazi yangu na yeye alipata TB na kuambiwa ana HIV sasa wakati yupo hospital kuna dada mmoja akamwambia kama ataambiwa ana HIV asitumie zile dawa maana hata yeye aliaambiwa hivyo na hakutumia dawa na yuko fresh.akarudi home akasema na Mzee akamwambia afuatishe mfano wa kaka,mpaka leo yupo mzima wa afya na hatumii.

2005 Baba yangu mdogo aligundulika na HIV yeye na wake zake wawili.wakaanza kutumia dawa ilipofika 2006 aliaanza kuugua kuaharisha nk 23 august 2006 akafariki.
Mwaka unaofuata akafuatia mwanawe wa mwisho.
2008 mkewe mkubwa na yeye akaanza kuugua hatimaye akafariki.lakini mke mdogo yupo mpaka leo na anatumia dawa na mzima wa afya.

Nb:nimetoa ushuhuda wangu ili kuangalia huu ugonjwa unavyochanganya lakini kila mmoja kwa nafasi yake inapaswa asipuuze aweke 50/50 kisha afanye uchunguzi ajiridhishe japo kwa upande wangu naamini ukimwi upo ila kuhusu HIV bado kuna mkanganyiko kwangu..maana wanasema kuna mtu mwingime ana kaa hadi miaka 10 ndo anauaguani kitu ambacho hakiingii akilini maana tunaambiwa HIV anaua kinga za mwili na ni hatari sana,sasa kipindi chote hicho mtu awe salama wakati Malaria tu ndani ya wiki unapata habari
 
Very true! But HIV/AIDS weakens your body immune and leave it free for even fungus to kill you!
It's true watu tumeshindwa tu kujua maana ya UKIMWI ndio maana tunausingizia kuwa unaua mi nadhani maana halisi ya neno UKIMWI upo katika kirefu chake 'UKOSEFU/UPUNGUFU WA KINGA MWILINI' ukifikiria hii maana utagundua kuwa UKIMWI hauui mtu
 
Tukienda upande wa pili kwamba 'HIV' hayupo na AIDS haisababishwi na HIV pia na mimi nitakuletea scientific papers nyingi sana,halafu mwisho wa siku tutakuwa tunashindana kutoa scientific papers.Wewe umetoa scientific papers za watu unaowaamini na mimi nitatoa zangu za wale ninaowaamini,mwisho wa siku hata wana JF hawatang'amua chochote.

Hao unaowaamini wewe wameshindwa na wale ninaowaamini mimi kwenye lab experiments(ambazo kwa hapa ni vigumu kuwathibitishia watu maana tutajaza scientific papers tu humu) na real life experince.Yaani kile kinachoonekana kiuhalisia.

Tukienda kwenye body chemistry, hilo mimi sina tatizo na ninyi kwa kuwa hata nikikwambia uniletee electronics photos za hizo cells najua utaniletea kwa kuwa zipo kiuhalisia.Tatizo linakuja kwenye electronics micrographs za purified HIV.Najua hata ufanye vipi huwezi kuniletea hizo na ukileta lazima zitakuwa feki kwa kuwa hata hao unaowaamini walishakubali kwamba wameshindwa ku purify HIV,wewe unajua umuhimu wa purification hivyo sina haja ya kueleza mengi hapa.

Kama wameshindwa ku purify HIV,sasa ile picha ya HIV kwenye vitabu vyenu wameipata wapi?Evidence nzuri hapa ni ile ya matukio tunayoyaona mtaani.Maana hata niki disqualify hizo paper zako bado watu hawataelewa nini kinaendelea.

Robert Gallo na Luc Montaigner hawajawahi ku purify HIV.Hawawezi pia kuthibitisha kwamba HIV anasababisha AIDS.Usifikiri Kary Mullis ameingia uchizi kukataa kwamba HIV hasababishi AIDS wakati kipimo alichogundua cha PCR ndio kinategemewa kwenye haya mambo yenu.

Usifikiri Prof.Peter Duesberg ameingia uchizi kusema kwamba HIV hasababishi AIDS.Robert Gallo na Luc Montaigner wameshindwa kujibu hoja za hawa wachache tu niliowataja hapa,wewe ukiweza kujibu nitakushangaa sana umepata wapi maelezo hayo.Cha msingi ni kujibu hoja za hawa jamaa.Fahamu kwamba na hawa ni madaktari pia tena wenye hadhi ya juu duniani.

Pia fahamu kwamba Peter Duesberg anaijua virology vizuri zaidi ya hao wanaojiita wagunduzi wa HIV kwa maana ndio field yake hasa na ndio maana wanamkimbia hata kwenye open debate,ninyi hamlijui hili na hamuwezi kuambiwa.

Robert Gallo na Luc Montaigner(wagunduzi wa 'HIV') wameshindwa kujibu (kwa usahihi) hoja zifuatazo za Peter Duesberg.Naomba wewe uzijibu kama hutajali.

Nimeongeza neno kwa usahihi kwa kuwa mtu yeyote anaweza kutunga kitu chochote ili watu wamwamini hata kama hakina ukweli wa kisayansi.Hawa kina R.Gallo na L.Montaigner ndio ma father wa kutunga,wanachokisema ukilinganisha na lab experiment viko tofauti kabisa.Sasa jibu hoja hizo hapo chini.

Nimecheka hapo Peter duesberg anaijuwa virology kuliko luc montagnier.
Hivi kati ya Peter duesberg na luc montagnier ni nani kabobea katika virology????.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom