Huyu ndiye Kiongozi na Mwanadamu anayependwa, kukubalika na mwenye ushawishi zaidi kwa sasa hapa nchini

Huyu ndiye Kiongozi na Mwanadamu anayependwa, kukubalika na mwenye ushawishi zaidi kwa sasa hapa nchini

Ndugu zangu Watanzania,

Kuna mwanadamu mmoja na Raia mmoja ambaye kwa sasa ndiye anayependwa , kukubalika,kuungwa mkono na mwenye ushawishi wa hali ya juu sana hapa Nchini.Ndiye Binadamu ambaye asipoonekana hata kwa siku moja tu hadharani watu wanaanza kumtafuta kama Pesa.Ni kiongozi ambaye anapendwa na watu wa makundi yote na mwenye kuheshimika sana hapa Nchini.

Huyu ndiye kiongozi na Mtu ambaye maneno yake tu huwafanya wagonjwa waliolazwa wodini na mahospitalini kupata tabasamu na nafuu na kujihisi wamepona wamuonapo mbele ya nyuso zao .ndiye kiongozi mwenye uwezo wa kuwapa faraja watu wenye majeraha mioyoni mwao.ndiye kiongozi ambaye kwa sasa ameteka mioyo ya mamilioni ya watanzania. Ndiye kiongozi pekee mwenye uwezo wa kuzungumza na kusikilizwa na kuaminika na kuaminiwa kwa jambo lolote lile.

Ndiye kiongozi ambaye amebeba matumaini na hatima ya maisha ya mamilioni ya watanzania mikononi mwake,ndiye kiongozi ambaye watu wote humtizama yeye kama nyota ya asubuhi kwa wavuvi.ndiye mtu ambaye watu wana imani ya kutimiza ndoto zao kupitia yeye.ndiye kiongozi ambaye amefanya mioyo na vifua vya watanzania kujawa na furaha ,amani, utulivu, matumaini na matarajio makubwa sana.

Anapendwa , kukubalika,kuungwa mkono ,kuaminika na kuwa na ushawishi Hapa Nchini kwa sababu Maisha yake hapa Duniani yamefanyika kuwa baraka kwa mamilioni ya watu .kwa sababu amegusa mioyo na Maisha ya mamilioni ya watanzania,kwa sababu ameleta tabasamu na matumaini kwa watu,kwa sababu ameleta nuru katikati ya Giza ya maisha ya watu,kwa sababu ameonyesha njia ya matumaini kwa watu waliokuwa wapo njia panda.kwa sababu amewezesha wengi kutimiza ndoto zao,kwa sababu kila uchao umekuwa bora kuliko jana kwa watanzania.

Huyu ni Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan Mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge.huyu ndiye mboni ya Taifa letu .ndiye aliyebeba na kushikilia furaha ya mamilioni ya watanzania.kwahakika Mama huyu jasiri , shupavu, imara, hodari na madhubuti ataendelea kuwa nguzo ya Amani ya Taifa letu kwa ulimi wake,matendo yake na uchapakazi wake utakuwa msingi wa ustawi wa Taifa letu na watanzania wote kwa ujumla wake.

Huyu Mama ni kama Maji tu usipoyanywa utayaoga tuuu utake usitake. Huwezi kumkwepa wala kumchafua wala kumpaka matope.Maana kibali alichopewa na Mungu kuongoza Taifa hili hakiwezi kunyang'anywa na Mwanadamu wala kuharibiwa na mtu mbele za watanzaniaView attachment 3160299View attachment 3160300

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kila Rais alikuwa na ushawishi kwa awamu yake ya Uongozi.
 
Rais wetu Mpendwa ni mcha Mungu na mwenye hofu ya Mungu.ndio maana amekuwa mtu mwenye kutenda haki kwa watu wote.
"Mtume (S.A.W) alisema: 'Hakika, kila mmoja wenu ni kiongozi, na kila kiongozi atawajibika kwa alicho kiongoza. Mfalme ni kiongozi wa watu wake, na atawajibika kwa watu wake; na mwanaume ni kiongozi wa familia yake, na atawajibika kwa familia yake; na mwanamke ni kiongozi katika nyumba ya mumewe, na atawajibika kwa nyumba ya mumewe; na mja ni kiongozi wa mali ya mwekezaji wake, na atawajibika kwa mali ya mwekezaji wake.' (Bukhari na Muslim)
 
PhD holder kutoka mzumbe 😀😀😀
Siyo tu Mzumbe bali ni kutoka vyuo mbalimbali.Na ikumbukwe vyuo vingi sana vina mpango wa kumpatia heshima hiyo kutokana na uchapakazi wake uliogusa Maisha ya mamilioni ya watanzania pamoja na kuleta mageuzi makubwa sana hapa Nchini kisiasa,kijamii , kiuchumi n.k.
 
Siyo kila Rais .Ndio Maana unaona wengine huondoshwa madarakani na wananchi kwa maandamano kabla hata ya wakati wao kufika.
Huyu wa kwetu ana miaka michache sana madarakani. Wakimuondoa kwa maandamano watakuwa wamemuonea kwa kweli.
 
Back
Top Bottom