Kozo Okamoto
JF-Expert Member
- Oct 14, 2013
- 3,391
- 1,545
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nasikia KICHEFUCHEFU Na Hamu Ya Haja Big!
hivi mtu na akili zake anaweza vipi kwenda kujisimamaisha sehemu ili apigwe picha na mtu fulani na kuitumia picha hiyo kutangaza uchu wake?
BREAKING NEWS KUHUSU URAIS 2015, Urais ndani ya CCM ni Mwigulu Nchemba. (siri za vuja.)
Lile fumbo la nani atakuwa mgombea wa Urais kupitia CCM imeteguliwa baada ya SIRI kuvuja kuwa anayeandaliwa ni Mwigulu Nchemba. Taarifa za ndani tulizozipata toka kwa mjumbe mzito kwenye mfumo zinasema kuwa Mwigulu Nchemba ndio chaguo ndani ya CCM nakwamba sasa amekuwa akiitwa kwenye mikutano inayowaweka pamoja Marais wa Afrika na wengine Duniani ili apate kutambulishwa na kupata uzoefu wa mikutano mikubwa. Pia Mwigulu amepelekwa mataifa yote makubwa kwa siri kutambulishwa. Mwaka jana tarehe 25 May 2014 alipelekwa China na kuonana na viongozi wa juu wa CPC chama kinachotawala china akiwepo I PING na Rais wa China Xi Jing Ping.
Tar 10 August 2014 Mwigulu Alipelekwa Uingereza kwa Siri na kutambulishwa kwa chama Labor na kuandaliwa mkutano wa Watanzania. Tar 25 Nov 2014 Mwigulu alipelekwa Marekani majimbo 25 na baadae kuonana na Obama kutambulishwa kwa magavana wa majimbo yenye nguvu.
Alipotoka kule Mwigulu alipelekwa Ufaransa na Ujerumani tar 3 Mwezi wa kwanza kutambulishwa. Ziara za maeneo yote hayo Mwigulu Nchemba alikwenda na Msaidizi wa Rais wa Maswala ya Siasa Ndugu Rajabu Luhwavi.
Taarifa zinasema kuwa ndg Luhwavi ndiye mtu anayesifika kwa mipango ya ushindi akiunganisha watumishi wote kumpigia Kikwete 2005. Taarifa za hivi karibuni zimesema Rais Kikwete amekuwa akiambatana na Mwigulu katika matukio mengi yanayowaleta marais wengi pamoja.
Mfano tar 18 feb Mwigulu aliambatana na Rais Kikwete kule Rwanda na kutambulishwa kwa Marais wote wa Afrika Mashariki. Pia kabla ya hiyo Rais kikwente alikwenda na Mwigulu Marekani na China kumtambulisha kuwa ni kijanqa mwenye uwezo wa kufanya mabadiliko kwenye uchumi wa nchi.
Hivyo hivyo Mwigulu alikwenda Msumbiji kupata uzoefu wa kuapishwa kwa Rais Nyusi wa Msumbiji. Jana Mwigulu Nchemba alipelekwa Namibia kwa ndege maalumu akiwa na ma Rais wastaafu ndg Ally Hassan Mwinyi wa Awamu ya Pili na ndg Benjamin Willium Mkapa wa Awamu ya Tatu.
Jicho la ndani la chombo chetu linasema, Marais hao wastaafu walikabidhiwa jukumubla kumtengeneza Mwigulu kuijua miiko ya nafasi hiyo kubwa. Kila mtu anaamini kuhusu uwezo wa Mwigulu wa kuongoza. Pia hakuna ubishi kuhusubu uthubutu wake. Vile vile hakuna ubishi kuhusu vision yake.
Jambo moja tu ni kumtengeneza kuwa na mkao wa nafasi hiyo jambo walilokabidhiwa wazee hao. Inasemekana wamekaa naye mara kadhaa kwa masaa kadhaa na wametoa taarifa kuwa Mwigulu ameiva kwa nafasi hiyo
Taarifa za Uchunguzi wa ndani zaidi zinasema Mwigulu alipelekwa kwa Mwalimu wa Siasa nayehusika na kufunda viongozi kuhusu hotuba na mwenendo wa kiuongozi na kwa kiwango kikubwa amefanikiwa kumbadilisha Mwigulu kwa uongeaji wake, mwenendo na mwonekano wake na kumfanya aonekane kiuongozi wake.
Kwa nguvu aloyonayo Mwigulu ndani ya chama na ndani ya Umma ni dhahiri sasa anakwenda kupokea kijiti. Dalili hizi zinasemekana ndizo zilizowafanya wasaka urais wengine wapige kambi kwa Katibu Mkuu Kinana amzuie Mwigulu Nchemba kufanya mikutano.
Unaudhalilisha ukoo wa Mnkondya kwa kuja kumsifia mafia aliyejaa damu zisizo na hatia mikononi mwake. Hivi umekosa kazi ya kufanya au?Jimbo tunampa , Kitila Mkumbo.
Unaudhalilisha ukoo wa Mnkondya kwa kuja kumsifia mafia aliyejaa damu zisizo na hatia mikononi mwake. Hivi umekosa kazi ya kufanya au?