Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata Yesu alipotaka kumponya yule kipofu alitema mate kwenye mchanga akamwambia ajipakeKumbe na mafuta aligawa🙄🙄🙄, alafu uko hapa unampigia debe... Sie tunaishi na neno bwana... Mafuta ya kina Liv sijui mwamposa bin suguye yenu msiejua neno la Kristo!
Yesu pia alisema " mkifuata neno langu mtafanya mambo makubwa zaidi yangu" kwa maana mtakuwa na nyota Kali zaidi yangu.Nyota Kali ni Ile iliyoonekana na mamajusi wa Mashariki.
Nyota ya Yesu Kristo, Mungu aliyekuja katika mwili wa mwanadamu.
Amen
Mafuta ni kilainishiKumbe na mafuta aligawa🙄🙄🙄, alafu uko hapa unampigia debe... Sie tunaishi na neno bwana... Mafuta ya kina Liv sijui mwamposa bin suguye yenu msiejua neno la Kristo!
Mafundisho potofu yasiyofaa kwa wanaofuata Nuru ya Yesu Kristo.
Hakuna mahala ambapo Mungu aliagiza uliamini NENO hata lukitoka kwa mwovu. Hata shetani alitumia Neno kumjaribu Eva na baadaye Yesu
Ni mganga kama waganga wengine
Ni tapeli kama matapeli wengine
Ni gambler kama gamblers wengine
Kwa ufupi ni mfanyabiashara
Anavuna ambacho hakupanda
Na serikali ipo kimya
Wajinga ndio waliwao
Kwa nini hawaendi kuwahubiria wagonjwa mahospitalini wapate kupona
Ujinga Umaskini na maradhi - shida inaanzia hapa.
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa…,
… mtaambiwa Yesu yuko huku nanyi mtaamini….
Ni mganga kama waganga wengine
Ni tapeli kama matapeli wengine
Ni gambler kama gamblers wengine
Kwa ufupi ni mfanyabiashara
Anavuna ambacho hakupanda
Na serikali ipo kimya
Wajinga ndio waliwao
Kwa nini hawaendi kuwahubiria wagonjwa mahospitalini wapate kupona
Ujinga Umaskini na maradhi - shida inaanzia hapa.
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa…,
… mtaambiwa Yesu yuko huku nanyi mtaamini….
Kama upo ndani yako kwanini unaenda kwa huyo Lovy?? Au Lovy ndo ndani yako iliyoandikwa kwenye biblia??Ufalme wa Mungu upo ndani yako. So kwenye biblia yako hakuna hilo andiko?
Low and indeed unqualified explanations.Nuru ni nuru mkuu haijalishi nani kabibeba.
Ukiwa kwenye chumba chenye giza.Akajakabaha/mzinzi/muuaji akawasha mshumaa, utaona kama ambavyo mshumaa huo angeuwasha mtenda mema asiye na dhambi kama wewe.
Low and indeed unqualified explanations.
Tunamuongelea Mungu ambaye amesema walio wake tutawatambua kwa matendo yao.
Huwezi kusema unatenda kazi za Mungu wakati unaishi kwenye dhambi. Lazima tuone Mungu alivyokibadilisha na tuone taswira yake katika maisha yako.
2 Wakorintho 11:14
Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
2 Wakorintho 11:15
Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.
Huyo ni Nabii wa uongo!!Yesu pia alisema " mkifuata neno langu mtafanya mambo makubwa zaidi yangu" kwa maana mtakuwa na nyota Kali zaidi yangu.
Wengine hatumjui, ungetupia picha yake na location piaMitaani huwaga kuna kamsemo maarufu sana :
" Dada angu wewe:
1. Huna tako ( shape)
2. Huna sura
3. Huna kazi.
4. Hujasoma.
5.Huna biashara.
6.Huna danga.
7. Hupati psi psi mtaani.
Halafu tangazo la mganga linapita unajifanya hutaki kuchukua namba za simu..
Nimeiona hali hii kwenye comments za baadhi ya watanzania kuhusu Prophet Lovy.
Sasa ndugu yangu. Wewe 👇
1. Huna kazi.
2. Huna biashara.
3. Mauzo kwenye biashara yako yana matege.
4. Huna nyota.
5. Huna mali yoyote ya maana.
6. Huna network
7. Huna connection.
8. Alama pekee uliyo ileta duniani ni chale.
9. Utambulisho pekee unao weza kutambulishwa nao ni ule anaopewaga mtu mpaka afiwe " huyu ndio yule jamaa aliefiwa" .
10. Au utambulisho wa ugonjwa " yule jamaa mwenye pumu"
11. Au kipara " yule jamaa mwenye upara"
Kibaya zaidi huna " utakatifu" yani wewe ni mtenda dhambi kama watenda dhambi wengine.
Halafu anatokea mtu anatangazwa kwamba ana uwezo wa kukufungua kutoka kwenye vifungo ulivyo fungwa, badala ya kwenda usaidiwe, wewe unaanza tena kumponda. Alie waroga Tanzania ndo yule yule alie waroga wagalatia.
Ngoja nikufundishe kitu kimoja ndugu yangu. Ukitaka kufanikiwa kwenye mambo yako hasahasa mambo ya kiroho kumbuka kanuni hii hapa chini 👇
" FOLLOW THE LIGHT AND NOT WHO CARRY THE LIGHT".
FUATA MWANGA USIMFUATE ALIEBEBA MWANGA.
Nimekuwa Muumini wa kanuni hii kwa muda mrefu sana. Mpaka baadhi ya ndugu zangu wananishangaa kwa sababu Mimi pamoja na kutoka katika familia na ukoo wa kiislamu lakini sijajifunga kwenye kufuata tu mafunzo ya Prophet Muhammad Peace Be Upon Him. Ninasoma pia na kufuata mafundisho ya Yesu.
Pia ninajifunza habari za ,Budha, Talmud,mafundisho ya wahindu, mafundisho ya imani za kiafrika etc na kote huko ninafuata MWANGA.
Back to the Prophet Lovy.
Jamaa ana nyota Kali sana.
Kwa habari ya upako jamaa yupo vizuri sana pia wakuu.
Msiyachukulie powa Yale mafuta aliyo kuwa anayatoa jana kwenye kongamano.
Yapo very very powerful. Kwa wewe ambae una jijua una vifungo vya kichawi etc mafuta yake yangekufaa sana.
Halafu wachungaji wa kicongo msiwachukulie powa wapo vizuri sana kiroho.
Nenda South Africa pale fanya research kuhusu .makanisa yanayo hudumiwa na wachungaji wa kicongo waulize watu wanao sali kwenye makanisa hayo wakupe tathmini ya kinacho watokea kwenye maisha yao.
Ukiwa una sali kwenye kanisa la mchungaji wa kicongo wala uhitaji kwenda kwa mganga wa kienyeji. Upako wa mchungaji pekee unatosha. ( wengi wenu humu wakristu kwa waislamu huwaga mnaenda kwa waganga pia . Sasa ukienda kwenye kanisa la mchungaji mcongo huhitaji kwenda kwa mganga)
Prophet Lovy ana nyota Kali sana. Prophet Lovy ana upako mkali sana.
Ambao hamkwenda jana kwenye kongamano lake mmejipiga gani wenyewe. Mmekosa kitu kikubwa sana kwenye maisha yenu...
Usimnenee vibaya Mtumishi wa Mungu
Hukumu huandikwa na kutolewa na Mungu pekee.MR. Deputy Jesus!! Usihukumu ili nawewe usije kuhukumiwa..