I am depressed. Naombeni ushauri

I am depressed. Naombeni ushauri

Take home ya mume 800k
Take home ya mke 2300k

Jumla ya pesa ya familia kwa ajili ya kula, mavazi, elimu na maendeleo 800k. Ikizidi hapo hiyo ni favor tu...

Mwanaume kama unataka uishi walau 70yrs lazima mambo mengine yakae kisogoni.
 
  • Thanks
Reactions: Ccc
Mwanamke unajiita ngangali utakua mbisha sana wewe

Au wewe ndo muhasisis wa ngangali na ngunguli
 
Yaan kwa mishahara yenu hiyo bado mnawaza kuomba mtaji sehemu?
Kwann mtoto umpeleke shule ya gharama kubwa wakati mtaji huna?Tatzo wanawake mnapenda show off sana.

Issue ndogo tu kama hyo inakupa depression kweli?Think twice

Anyway pole dada
Kaka kwenye ndoa kipato Cha mwanaume ndio kipato cha familia
 
Kuishi na Ke ni ngumu sana, inahitaji akili sana maana huenda hata hiyo shule(sijui gharama yake) mke ndio amesema mtoto aende, wakati gharama za shule ni kubwa na jamaa hana huo uwezo. Wanawake wana tabia ya kuigana, ameona watoto wa jirani wanasoma shule X anataka wa kwake nae aende huko bila kuangalia kipato cha mume.

Jamaa nae kuona hivyo anaangalia tu, anakuangalia aone utaenda nalo hadi wapi, si umeamua ku-take lead mwenyewe!! Mwisho lazima mkae kwenye drawing table mpange, ingekuwa hiyo 2300k+800k inawekwa mezani na kupangiwa majukumu, usingekuja ĥapa kutafuta ushauri, ndoa ya wawili wenye 40+ ilitakiwa kuvuka haya matatizo mda sana.
 
Amekaa bila kazi miaka minne unamlisha daa hapo ndio ungepeta stress
Kuhusu shule jikune unapofikia
Mtoto mdogo bado hata miaka miwili mitatu anaweza kusoma shule zetu na ukamsaidia pia

Mwanaume ndio wa kukusaidia sana ila kaeni myamalize na wewe jiwekee akiba kidogo kwani binadamu hatosheki
Nakumbuka nilipo kuwa na miaka 18, anko ali Nikuta nyumbani naangalia cartoon.

ali sema kijana naona ume amua kuwa mume wa pili nyumbani kwa dada yangu, haya we kimburu beba nguo tuondoke😂😃
 
Habari great thinkers.

Nimekuwa msomaji kwa muda mrefu sana humu, ila imenilazimu nijiunge ili nitoe nilichonacho maana ninahisi kuzidiwa moyoni sipati kulala usiku. Nahitaji ushauri.

Mimi ni mama wa mtoto mmoja wa miaka 6, nimeolewa miaka 8 iliyopita, nyumba tunayoishi tumepewa na mama mkwe kwa hiyo hatujajenga na wala hatulipi kodi. Najua unajiuliza hizi information za nini leta hoja, sawa nakuja na hoja.

Ni hivi mume wangu ana kipato cha kawaida tu kwa mwezi labda laki 8 take home. Binafsi nina kipato kwa mwezi kama 2.3m take home. baada tu ya kufunga ndo mume wangu alipoteza kazi kwahiyo alikaa nyumbani kuanzia 2017 akaja kupata kazi 2021 lakini tuliiishi bila shida.

Yeye kwao ni last born ana kaka na dada. Mimi kwetu ni wa pili kuzaliwa ila nahudumia wazazi pia. Kipindi yupo nyumbani ni kamwambia aongee na kaka yake amuazime mtaji wa kufanya biashara lakini mwenzangu alikuwa akikaa kimya, so miaka ikaenda mpaka alivyokuja kupata kazi.

Mwaka jana mwishoni nikagusia tena na kumpa idea ya biashara na alionekana kuipenda sana akasema sawa, na hiyo mwaka jana nilimwambia kwa kuwa mtoto anaingia darasa la kwanza hatuwezi kutegemea mshahara pekee. Ingawa mimi nimefungua biashara ila bado changa na pia ninafanyaga tender za kuprint, kufunga zawadi na kadhalika.

Mtoto tumemtafutia shule kwa pamoja na ada alikuwa anaijua tangu Novemba, nikamwmabia ngoja nikupunguzie mzigo nitalipia usafiri na uniform akasema sawa.

Nikawa namkumbusha kulipa ada anasema anakumbuka. juzi jumapili anasema hiyo ada kubwa sana hatoweza hiyo shule, imagine bado wiki shule zifunguliwe.

Baadae nikamuuliza kuhusu ile idea ya biashara vipi? mana haijalishi mtoto anasoma wapi jinsi anavyozidi kukua madarasa ndivyo gharama zinazidi, akasema mi mambo ya biashara siyawezi wala sijawahi kuyawaza, duuh nikabaki nimetoa macho, nikamuuliza mbona ile idea uliipenda na ukasema utaifanya utamuazima kaka yako mtaji akasema mi siwezi hayo mambo.

Haa, moyo wangu uliinama sana tangu hiyo siku nina mawazo sipati usingizi. Najiuliza niongee na kaka yake au dada yake wamshauri kama hawezi kutegemea kukua kimaendeleo kwa mshahara tu au nibaki nalo? na nikibaki nalo nifanyeje?

Hawazi kujenga, hawazi kununua kiwanja, 2024 january nilimwambia tuweke kiasi cha fedha kwa ajili ya kununua kiwanja akaweka mwezi wa kwanza nadhani kwa kuwa nilimkalia kooni.

Baada ya hapo akawa hawezi kuna siku nikamuuliza akasema mi niache tu na hayo mambo. Nikaacha nikaendelea mwenyewe, ila peke yangu nguvu ni ndogo.

Naombeni ushauri jamani mimi ni mtu mzima nina 40+ nashindwa kuomba ushauri wa rafiki zangu mana ndo yataenezwa.

Nadhani ninaweza pata depression kama ningebaki navyo moyoni kichwa kinauma kwa kuwaza.

Naombeni ushauri tafadhali.
Kwa hio akili yako pata tu depression.. kwanza huna tatizo lolote... Eshimu ndoa yako msikilize mmeo... 2.3 + 0.8 =3.1M
Na mnalipwa hio Hela kila mwezi mmeshindwaje kukaa kama familia mtatue changamoto za kawaida kama hizo
 
Kuishi na Ke ni ngumu sana, inahitaji akili sana maana huenda hata hiyo shule(sijui gharama yake) mke ndio amesema mtoto aende, wakati gharama za shule ni kubwa na jamaa hana huo uwezo. Wanawake wana tabia ya kuigana, ameona watoto wa jirani wanasoma shule X anataka wa kwake nae aende huko bila kuangalia kipato cha mume.

Jamaa nae kuona hivyo anaangalia tu, anakuangalia aone utaenda nalo hadi wapi, si umeamua ku-take lead mwenyewe!! Mwisho lazima mkae kwenye drawing table mpange, ingekuwa hiyo 2300k+800k inawekwa mezani na kupangiwa majukumu, usingekuja ĥapa kutafuta ushauri, ndoa ya wawili wenye 40+ ilitakiwa kuvuka haya matatizo mda sana.
unanikandamiza kwa kuwa nimesema kipato changu mkuu? nimejibu hapo juu shule ni ya kanisa na alishauri yeye mtoto aende shule ya kanisa. hapo tatizo ni mimi kivipi?
 
Hizi ndoa mnazoingia kichwa kichwa bila kujuana kiundani matokeo yake ndo haya.
 
Kwa hio akili yako pata tu depression.. kwanza huna tatizo lolote... Eshimu ndoa yako msikilize mmeo... 2.3 + 0.8 =3.1M
Na mnalipwa hio Hela kila mwezi mmeshindwaje kukaa kama familia mtatue changamoto za kawaida kama hizo
kwahiyo tatizo ni mimi? kwanini hujaona tatizo zaidi ya mimi kuwa tatizo? je nikikwambia hata hiyo laki 8 yake ameanza kuhudumia miezi kadhaa iliyopita baada ya kukuta wali maharage kila siku bado utasema tatizo ni mimi?
 
ndio ila kama umesoma kuna mtu nimemjibu kuwa mshahara wangu ninahudumia wazazi wangu pia ninakatwa bima ya wazazi na mkwe kinachobaki ndo kinawekwa mezani kama familia. Pili biashara nilichukua mkopo kazini ambapo pia nakatwa na nilimshirikisha. nimempa wazo la biashara ila mtaji akaazime kwa kuwa kinachobaki hakitoshi kufungua hiyo biashara kwahiyo ili kitoshe inabidi kuazima au kukopa ambapo yeye hataki kukopa.
Saidia nyumbani ila usimsahau mume wako.
ni kweli kiasili mwanamke anatakiwa ahudumiwe ila sio lazima kipato chako hakijitoshelezi.
bado unaweza pambania mtoto akasoma kwa ushauri tu tafuta thread za LIKUD kuhusu shule za English Medium kwa wale wenye vipato vidogo.
#ISHI NA MUME WAKO WEWE MWENYEWE HUJAKAMILIKA.
 
Wanawake pesa zao ni tamu kwelikweli!

Bora angeoa jobless tu akakaa home kulea kuliko huyu anayemkalia kooni mumewe awe ombaomba badala azungumzie hata kuweka akiba biashara ianze kama mradi wa familia na ukisimama vyema mkope.

A beggar at 40+!,hata mimi ningekataa.

Unayajua mahusiano ya ndugu wa kibongo? Akuanzime mtaji?
 
Duh pole
Kuhusu shule mwambie atafute anayoweza afford...
Kuhusu maendeleo fanya unayoyaweza mengine muachie afanye
Punguza kufanya majukumu yake
Atabweteka huyo
Nunua kiwanja andika jina lako na la mtoto
Anza kujenga mdogo mdogo
Akija kustuka umefika mbali
Wanawake wabinafsi utawajua tu na wala hawajifichi,maana chuki yao kwa Mwanaume asiyempenda huwa haijifichi!!
 
Miaka 40+, watu wazima wawili hamna hata kipande cha ardhi? Ikitokea mmefumba macho leo huyo mtoto wenu atarithi hiyo flatscreen?

Achana na maneno ya marafiki, achana na magroup ya wamama walioshindikana......watu wanafiki sana, huko kwenye magroup wanajifanya hawachangii chochote kwenye familia, ila kiuhalisia wao ndo wanaendesha familia.

Kaa chini na mumeo, pangeni kwa pamoja, wekeni mshahara mezani muupangie matumizi ya pamoja, kisha muamini, let him lead......mume haelekezwi, mume anashauriwa kwa upole, kisha unamuachia siku kadhaa za kutafakari ulichomshauri........using'ang'anize kila unachotaka au unachoshauri afanye hapo hapo......wenzetu hawapo hivyo.
 
Miaka 40+, watu wazima wawili hamna hata kipande cha ardhi? Ikitokea mmefumba macho leo huyo mtoto wenu atarithi hiyo flatscreen?

Achana na maneno ya marafiki, achana na magroup ya wamama walioshindikana......watu wanafiki sana, huko kwenye magroup wanajifanya hawachangii chochote kwenye familia, ila kiuhalisia wao ndo wanaendesha familia.

Kaa chini na mumeo, pangeni kwa pamoja, wekeni mshahara mezani muupangie matumizi ya pamoja, kisha muamini, let him lead......mume haelekezwi, mume anashauriwa kwa upole, kisha unamuachia siku kadhaa za kutafakari ulichomshauri........using'ang'anize kila unachotaka au unachoshauri afanye hapo hapo......wenzetu hawapo hivyo.
Siku moja nagusa simu nakuta mke wangu kamuhadithia mwenzie asitoe pesa Aache kila kitu afanye Mume wake , wakati kama juzi alitoka kunipa 3M ya issue fulani nilikwama , nikajua kumbe wanawake hua mnapotezana wenyewe maana , familia yoyote mkifanya umoja mnasonga mbele , mkianza ubinafsi na familia inasambaratika na Mnaishia kufa maskini , kama mwenzenu anapata pesa anataka Mume wake aombe kwao wakati wangekaa wakajadili wajichange waanze taratibu , kwanza wanakaa bure hawalipi Kodi ilitakiwa wasave wafanye mambo mengine, lakini pia 40+ kukaa bure kunadumaza akili Sana hawana bills ili akili ziwakae sawa
 
kwani hayo mambo ukiyafanya wewe kuna hasara gani?

wewe tafuta kiwanja na lipa ada then yeye muache kwenye chakula.

huwezi kumlazimisha mtu mzima,itakiwa anastarehe yake aipendayo.

build your future.
 
Back
Top Bottom