I love my wife but...

Asha Dii, Smile na Rocky,

Nimewapata sana lakini mimi sifikirii kucheat coz hamna kitu nakosa kwa shemeji yenu. Na la pili ambalo kubwa ni kwamba shemeji yenu ana mbinu nyingi za kijasusi kuliko Scoland Yard hata nikijifanya james Bond najua nitadakwa.

Hehehe
 

Salito ,

Ushauri huu umekaa poa, nitaufanyia kazi
 
kwanini uishi kijasusi ndani ya ndoa? kwani hao marafiki unaotembea nao kwa kujihami wanakusaidia nini
 

Acha hizo biashara zako cha kuchat na ladies wakati ukiwa na wife
Hata kama ni kazi jipangie muda ambao utasema sasa ni mwisho w akupokea simu na kuchat kuhusu masuala ya ofc na darasani
Nilikuw ana tatizo hilo la watu wa ofcn kupiga simu hata usiku wa manane nikaja kuweka msimamo kuwa mwisho wa simu za ofcn ni saa mbili za usiku na weekend yote sipokei simu inayohusu kazi may be nikiwa niko ofcn naweza kupokea simu hizo
 



Wanao cheat hawaendi tu kusema sasa naenda cheat! Kuna vigezo na vishawishi vya mtu kucheat.... Na hata kama hufikirii kufanya hivo take note basi hao wanawake wawe na heshima kwa wife.... Na kaa upande wa wife sio kuwatetea kua "I love my wife but....." BUT nini? Kua you can not stand stop flirting with the gals hata kama you love your wife na she does not like it? Come on man open up nikuelewe......
 
Kama kuna kitu nachukia duniani ni hicho mkuu wewe ni mume wa mtu kujifanya eti ana urafiki na maledies na kusema eti ni friends tu
kuwa natural
kuwa mwanaumme

Kha! we Smiles.....Kuwa mwanaume ni pamoja na kuwa na friends na huwezi kuchuja wa kike ubaki na wa kiume tu...utakuwa sio wa 'kawaida'

Huyo mke mbona kama 'hajiamini' hivi?
 

Nadhani akifuata ushauri wako mambo yatamnyokea. Kuna muda wa kazini na kuna muda wa kuwa na familia.
 
Kha! we Smiles.....Kuwa mwanaume ni pamoja na kuwa na friends na huwezi kuchuja wa kike ubaki na wa kiume tu...utakuwa sio wa 'kawaida'

Huyo mke mbona kama 'hajiamini' hivi?



Sweetie acha kumdanganya na kumchangaya Maundumula.... Wewe kuna mwanamke anachat na wewe nikiwepo karibu yako ama tukiwa faragha usiku?
 
Kha! we Smiles.....Kuwa mwanaume ni pamoja na kuwa na friends na huwezi kuchuja wa kike ubaki na wa kiume tu...utakuwa sio wa 'kawaida'

Huyo mke mbona kama 'hajiamini' hivi?


Mkuu sidhani kama kuna sehem tumesema kuwa mtu asiwe na marafiki wa jinsia tofauti
tatizo linakuja pale unaposhindwa kuwathibiti hao marafiki wanajikuta wanachukua tena mpaka ule muda wako wa kuwa na familia yako
Yaani unajikuta badala ya kuwa na mkeo umpe na yeye nafasi ya kukusikiliz ana muongee mambo ya maisha wanauchukua tena so unabaki mpaka nyumbani nako unachat na kupigiwa simu za ofisini na the so called marafiki wa kike
 
kwanini uishi kijasusi ndani ya ndoa? kwani hao marafiki unaotembea nao kwa kujihami wanakusaidia nini

Smile ,

Naona hujanielewa buddy, nilikuwa namaanisha kwamba mama ana mbinu nyingi siwezi hata kumdanganya coz akiniuliza swali akiniambia niangalie usoni straight bila kupepesa nipe jibu anakuwa ameshani daka. Coz anajua nikiongopa nakuwaje
 

Umeona ee ..thats ma gal.....mwaaah
 
Sweetie acha kumdanganya na kumchangaya Maundumula.... Wewe kuna mwanamke anachat na wewe nikiwepo karibu yako ama tukiwa faragha usiku?

Sweetie, Maundumula anajua kabisa mi naongelea ukweli.....afu mbona watu wamebase sana kwenye kuchat sijui usiku? yeye anasema kuwa na 'urafiki wa karibu' na colleagues wa kike...sasa inavoonekana mke wake hataki kabisa kusikia icho kitu....itakuwa maisha gani? LOL Hilo la simu usiku kwen faragha, linaeleweka kuwa halitakiwi, ila usiku unaanzia saa ngapi? akipiga saa moja usiku nayo itakuwa usiku? inatakiwa ajieleze kila simu anayopigiwa sweetie? hahaa

Mi nashukuru unaniruhusu kupokea simu bila kulzimika kusema zinatoka wapi,..ili mradi hazituvurugii privacy yetu...and eventually our romance lol
 
Alichosema Maundumula ni hiki hapa Rocky,



Sasa hebu nambie manake na wewe una mke kama mimi, do you have such a situation at home? lol
 

Mimi naomba tu nikusalimu rafiki....maana tangu mwaka umeanza hatujaonana bana...! WISH YOU A BLESSED NEW YEAR!
 
Alichosema Maundumula ni hiki hapa Rocky,





Sasa hebu nambie manake na wewe una mke kama mimi, do you have such a situation at home? lol

Mkuu kwa huyu jamaa naona kuna more than communication. Hiyo ya mke kusema hataki jamaa awe na mawasiliano na wadada kuna kitu mke kashakiona kwa jamaa ambacho ni zaidi ya mawasiliano
Na ndo maana kila simu ikipigwa anatakiwa ajieleze aliyempigia ni nani na anataka nini
Marafiki wapo na wafanyakazi wenzetu ikiwepo pia tuliosoma nao ila respect kwa privacy yangu na mke wanaijua
Na wanajua wanatakiwa wafanyeje wanapotakiwa kuwasiliana na mimi na ni kwa wakati gani
 

Kaizer,

Wewe nadhani ndio umenielewa vizuri kuliko wote.

Hizi simu haziji usiku wajameni hii simu inaweza kuwa mchana kweupee lakini inaleta noma.

Swala kama la kumsaidia friend sidhani kama inajalisha awe ni male/female coz kila mtu anapata matatizo sasa kwa system ya madame a lady friend doesnt deserve no help when in need kama anakufa ni bora akufe tu.

Sasa Smile, Asha Dii et all imagine u were my friend and in need...
 


Sweetie tatizo wewe you have a doctorate ya ku manipulate maneno as a result ya reading between the lines... (that makes me so proud...lol). Kwa the way umeweka haya maneno uko sahihi kabisa!

Na Love take note hapa tumesikia upande mmoja wa shillingi, kwamba mkewe ni mjinga to the extent asijue na realise kua haiepkiki mume awe na colleague wa kike ambae waweza kua close? Siamini (na kama ni kweli namuonea huruma Maundu); Mie naona mpaka wife kalalama lazima hizo chatting zimevuka mpaka.... Mbona wee una wengi tu wawasiliana nao but ukisha ingia ndani I have your attention hata kulalama haiwezekani maana usha prioritise kipi/nani ni mhimu na wakati gani.... Na that is the way it is supposed to be.... About the calls I don't have to ask Sweetie.... I trust you....lol


Umemuona Happuch? mwambie namsalimu... (with Love)
 



Jamani si washinda kazini ..... Mkeo anakua anaona hizo simu inakua vipi? Au ndo mambo ya weekends? Hapa Sweetie a.k.a Kaizer kuna kitu anatetea akijua mwenyewe! lol (@ Kaizer...Sori Lov')
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…