I want to die a judge

I want to die a judge

STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

TULIPO ISHIA SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO........
“Ni siku ambayo siwezi kuisahau kwenye yaisha yangu, ni siku iliyo nifanya nikakosa kuwa na familia, ni siku ambayo haikunifanya nikawa na uhakika wa kusimama mbele ya wanawake nikajisifia urijali wangu, wanadamu ni wabaya sana yule mtu alizikata sehemu zangu za siri. Nililia sana ile siku, sehemu za siri kwa mwanaume ni zaidi ya utajiri wowote ule unao ujua wewe hapa duniani, hakuna mwanaume aliyekikosa hicho kiungo akasimama kwa ujasiri na kujisifia mbele za watu kwa sababu anaweza kuishia kwenye michezo mibaya sana, sikuamini nikiwa kwenye kilio kikali niliona amezishika sehemu zangu hizo za siri akazitupa mbali na hapo sikuweza kuelewa kilicho endelea tena” stori ya mzee huyu akiwa anatoa machozi ilimsisimua sana Jamal alikuwa amefumba macho kwa hisia mpaka nayeye chozi lilimtoka, alimfikiria mwanaume huyo amewezaje kuishi akiwa kwenye hali hiyo, kwenye hii dunia yenye masimango makubwa sana ukiwa na matatizo kama haya, alimuonea huruma sana huyo mbele yake kwake alikuwa ni kama baba lakini pia kwa nchi alikuwa ni jasusi hatari mno ila hakuna ambaye alikuwa anajua kwamba huyo mtu hana hicho kitu.

ENDELEA...........................

“Niko wapi hapa” lilikuwa ni swali langu la kwanza tu baada ya kushtuka kutoka kwenye usingizi wa kifo, macho yangu yalikuwa bado yana ukungu kiasi chake kwa mbali nilikuwa namuona mtu mmoja ambaye alikuwa amenipa mgongo, suti kubwa mwilini mwake ndicho nilicho fanikiwa kukiona kwa wakati ule. Mkono wangu mmoja na sehemu ya bega ulikuwa imejaa bandeji kiasi kwamba hata nyama za mkono zilikuwa hazionekani kabisa, sikuwa nakumbuka chochote nilishangaa nikiwa kwenye hiyo hali, macho yangu niliyageuza pembeni ndipo nilipo ziona mashine kubwa zikiwa zinaonyesha mapigo ya moyo yalikuwa yanaenda kwa utaratibu mzuri kama ilivyokuwa inatakiwa, mikononi kulikuwa na drip mbili ambazo zilinifanya kugundua kwamba nilikuwa mgonjwa na hapo huenda ilikuwa ni hospitalini. Nilitaka kuinuka niliuma meno kwa maumivu makali ya tumbo hiyo sehemu kilikuwa kimezamishwa kisu nadhani bado palihitaji muda wa kutosha ili kuweza kupona na kuwa kwenye hali ya usawa kabisa kama ilivyokuwa mwanzo.

Mguu ulikuwa umepigwa plasta maeneo ya paja ulikuwa hauna nguvu kabisa, nilitulia kidogo ndipo nilipoanza kuvuta kumbu kumbu ya nyuma juu ya matukio yaliyokuwa yamepita ili nielewe kivipi nimeweza kufika ile sehemu nikiwa hata sijitambui kabisa. Nilitoa machozi mengi sana baada ya kukumbuka mpaka muda huo sikuwa na sehemu zangu za siri, nilitamani sana ningeachwa nife pale pale na sio kusaidiwa nikiwa kwenye hali kama hii iliniuma mno, nilikuwa bado hata familia sina kabisa ila ndio hivyo maisha yangu mapema sana yalikuwa yamesha haribika kwa siku moja tu nikiwa kijana mdogo wa miaka ishirini pekee.

“Kwanini umenisaidia kuja kuteseka kwenye huu ulimwengu” mpaka muda huo bado mtu huyo alikuwa amenipa mgongo hivyo sikuweza kujua kabisa kama alikuwa ni nani yupo humo ndani japokuwa nilihisi tu kwamba ni lazima yeye ndiye aliyeweza kunisaidia kwani hakukuwa na mtu mwingine yeyote.

“Hongera sana kwa kuweza kurudi kwenye maisha mengine mr Timotheo Jordan” nilishtuka baada ya kuona mtu huyo alikuwa akinijua kwa usahihi sana, aligeuka kutazama nilipokuwa nilitamani sana ningesimama lakini sikuwa na huo uwezo kabisa, mwanaume huyo ndiye mtu aliyekuwa amesababisha mimi kuwa kwenye hiyo hali Jonson Malisaba ndiye mwanaume aliyekuwa mbele ya macho yangu nilikuwa kwenye ndoto na nilipaswa niamke sasa ndivyo akili yangu ilivyoweza kunidanganya kabisa kwa mara ya kwanza lakini hii haikuwa ndoto kila nilichokuwa nakiona mbele yangu kilikuwa cha kweli kabisa huyo ni mtu ambaye nilihitaji sana kukutana naye tuweze kuongea kwa mapana na marefu leo alikuwa yupo mbele yangu nikiwa kwenye hali ya majuto makubwa sana kwenye maisha yangu.

“Huyu mtu aliye nitendea haya yuko wapi kwa sasa?” niliuliza kwa hasira ni dhahiri nilitamani sana kumuona huyo mwanaume ila hata angekuja kiuhalisia kwa hali niliyokuwa nayo nisingeweza kusimama naye hata kidogo hasira hasara ndicho kilichokuwa kikiniendesha kwa wakati ule.

“Mshukuru sana MUNGU wako umeweza kuamka na kuiona siku nyingine, ni siku saba sasa tangu umelala kwenye hicho kitanda, ukipona utachukua vitambulisho vyako kwenye kabati lililopo pembeni yako hapo na usije ukarudi tena kufanya hicho ulichokuwa unajaribu kukifanya ni hatari sana kwako” alinishangaza maneno yake machache alitaka kuondoka baada ya kumaliza maelezo yake alianza kuondoka mle ndani.

“Ina maana umesha nijua mimi ni nani?”

“Hiyo ndiyo sababu iliyonifanya nikusaidie baada ya kukujua kwamba wewe ni mtu wa serikali”

“Wewe ni nani hasa mpaka uweze kunisaidia mimi mtu wa serikali ambaye ulikuwa na mpango wa kuniua na umenifanyia ukatili mkubwa kama huu kwenye maisha yangu?” aligeuka na kutabasamu baada ya kulisikia swali langu

“Dunia imebadilika sana, wanadamu siku hizi ni wajuaji kupitiliza yaani wanaweza kutengeneza stori kukuhusu wewe na watu wa huko nje wakaamini kwamba ni kweli wewe kweli ndivyo ulivyo, mimi nawewe ni watu sawa ila tumepishana tu namna ya ufanyaji wa kazi ndiyo maana wewe uliamua kuhisi unanijua sana ndiyo sababu ukapata mpaka ujasiri wa kunifuata majira yale ya usiku pale kichwani mwako ukiwa tayari una jibu lako kuhusu mimi kitu ambacho sio cha kweli kabisa” maelezo yake kiukweli yaliniacha njiapanda nilidhani labda ni kwa sababu sikuwa na elimu lakini alikuwa mtu wa kutumia akili kubwa sana kwenye kila neno lake ambalo alikuwa analitoa mdomoni mwake.

“Wewe ni nani hasa mpaka useme mimi nawewe ni watu sawa?” nilikuwa na hamu sana ya kuweza kumjua huyu mtu, alijongea taratibu akatoa kitu mfano wa mashine ndogo sana ambayo ni mojawapo ya mashine ambazo huwa zinatumika kukagulia watu kwenye mageti ya sehemu maalumu hasa Ikulu au sehemu kubwa sana za serikali, kwanza nilishangaa kitu kama hicho kakitoa watu, mle ndani ghafla kiza kilitawala zilibaki tu mashine ambazo ndizo zilikuwa zipo pale kuhakikisha maisha yangu yanasalimika kutoka kwenye kifo.

“Mehesh Prakash ndilo jina langu, sijazaliwa India ila maisha yangu nikiwa mdogo nimelelewa na mhindi mmoja ambaye alikuwa mfanya biashara mkubwa sana hapa nchini na ndiye aliyeweza kunipatia hilo jina, Jonson Malisaba ndilo jina langu la kuzaliwa, kwa sababu yule mhindi alinilea kama mwanae baada ya kunichukua kwenye kituo kimoja cha watoto yatima aliweza kunipenda kama mwanae wa kumzaa hivyo alinipa kila kitu nilicho kihitaji kwake nilikuwa mwanae kabisa hivyo namimi nilimzoea kama baba yangu, nilisoma kwenye shule nzuri sana na kufanikiwa kumaliza masomo yangu, nilikuwa nimekuwa kijana wa kujielewa ndipo yule mzee alipoweza kutoweka duniani, kwa sababu kila kitu alinirithisha mimi utajiri wake wote ulikuwa upo mikononi mwangu. Nilikuwa mtu mwenye pesa nyingi nikiwa bado kijana mdogo tu hivyo kuna mtu mmoja kutoka kwenye idara nyeti ya serikali alinifuata na kuniomba nitumie baadhi ya mali zilizopo kuisaidia serikali, kwa sababu ilikuwa ni nia ya kuisaidia nchi yangu mwenyewe nilikubali kuufuata ushauri wake kwa asilimia zote miamoja.

Ilifika siku akawa amenikalisha chini ndipo aliponipa hadithi kamili ya umoja ambao unaitwa M96 OWNER’Z, aliniomba niingie kwenye huo umoja kama moja ya wawekezaji ili nikajue unahusiana na nini hasa kwa sababu walikuwa wamesha utilia shaka mapema. Lilikuwa suala ambalo halikuhitaji mimi kukurupuka sana kulianza lakini nilitolewa wasi wasi baada ya kuweza kukutanishwa na mheshimiwa raisi ambapo yeye kwa mdomo wake aliniomba nifanye hivyo. sikuzubaa tena nilikubali moja kwa moja ilikuwa ni heshima kubwa sana kuweza kuombwa na mheshimiwa raisi. Huo ndio ulikuwa mwanzo wangu wa kuingia kwenye huo umoja nikiwa bado kijana, watu wale pesa zangu ziliwashawishi sana kuweza kunikubalia haraka kwa mara ya kwanza nilitamani sana kuweza kujua kilichokuwa kinaendelea kwenye kampuni ile iliyokuwa ikijihusisha na usindikaji wa nyama. Pesa nyingi nilizowekeza pale zilinifanya kuwa na nafasi kubwa, kuna siku nikiwa nipo nyumbani baada ya kutoka kwenye kazi zangu walikuja wanaume kumi na mtu mmoja ambaye mpaka leo sijawahi kufanikiwa kumuona sura yake wala kumjua baada ya yeye kufika tu umeme ulizima kila sehemu kwenye ule mtaa hivyo tuliongelea gizani nadhani huyo ndiye kiongozi mkuu wa huu umoja, ni mtu makini, hatari, analindwa kuliko hata ikulu panavyo lindwa, ana watu makini sana kiasi kwamba hata nzi hawezi kuigusa hata kola ya shati lake.

Jadesh Mikasa ndilo jina ambalo aliweza kunitajia kama ni la kwake japo kwenye kufuatilia kote hatukuwahi kulikuta hilo jina kwenye data zozote zile hapa duniani hivyo nilijua huenda ni mtu ambaye utambulisho wake haujulikani kabisa. Kwa mara ya kwanza alinipa mambo machache sana ambayo yanafanyika mle ndani kwa sababu tayari nilikuwa miongoni mwa wawekezeji wakubwa kwenye ile kampuni, mambo niliyokuwa nasimuliwa yalikuwa yanatisha mno ila nilipewa onyo kali sana licha ya kuificha familia yangu mbali watu wale walikuwa na taarifa zangu zote mpaka familia yangu ilipo, ni watu makini kupita kiasi hawafanyi kosa lolote lile kwenye mambo yao ambayo wanayafanya, sikuwa na namna ilinibidi nikubaliane na matakwa yao na kuwaaminisha hilo walianza kunipa mitihani ambayo kuna muda ilinilazimu kumwaga damu zisizokuwa na hatia yoyote ile, ni kazi ambayo nilikuwa nimekabidhiwa na nchi hivyo ilitakiwa niifanye kwa asilimia miamoja. Imani ndicho kitu pekee ambacho kitafanya wanadamu waweze kukupatia kila kitu kwenye maisha yako kama mtu hawezi kukuamini basi hakuna kitu utaweza kuambulia ndio maana waanadamu tunakumbushwa sana kuwa waaminifu kwenye kila jambo tunalo lifanya hasa pale unapokuwa mbele ya watu wanao kuamini sana. ndicho kitu nilichoweza kukifanya ilinibidi kwanza nifanye waniamini ndio maana nilikuwa tayari kufanya kila kitu ambacho wao walihitaji nikifanye ili waniamini” maelezo yake yalinifanya jasho linitoke sikuwahi kufikiria kama huyo mtu alikuwa ni mtu wa serikali na alikuwa pale kutekeleza majukumu ya kitaifa ila nilitatizwa na kitu kimoja ambacho mpaka muda huo sikukielewa kwa mtu huyo. Nilihema kwa nguvu mpaka hasira zangu zote zilikuwa zimeisha kabisa kwa mwanadamu aliyekuwa yupo mbele yangu kitu alichokuwa anakifanya ndicho ambacho hata mimi nilikuwa nakihangaikia kila siku kwa muda huo na ndicho kilinifanya kuwa kitandani kwa wakati huo.

“Sasa kama wewe ni mtu wa serikali kwanini watu wa usalama wakutafute sana namna hiyo na jina lako kule linaonyesha wazi wewe ndiye mtu unaye tafutwa zaidi?” nadhani swali langu lilikuwa mhimu sana kwa wakati ule hata kama ungekuwa ni wewe lazima ungemuuliza iweje mtu wa serikali atafutwe na serikali? Ilikuwa lazima anipe maelekezo ya kutosha kuhusu hilo.

“Serikalini najulikana kwa watu wachache sana hata mkurugenzi wa usalama wa taifa hanijui na ndiyo sababu unaona watu wa usalama wa taifa wananiandama, hata wewe nimekusaidia baada ya kujua unatoka ndani ya idara ya usalama wa taifa” alinieleza kwa kifupi bila wasi wasi

“Kama haupo chini ya idara ya usalama wa taifa sasa unafanya kazi chini ya nani?” swali langu lilimfanya atabasamu sana

“Inakubidi uwe na mdomo mfupi sana kwa maana ukijaribu kuurefusha unaweza kuwa miongoni mwa vijana watakao ingia kwenye historia mbaya ya kuweza kufa mapema wakiwa bado hawajatimiza kabisa malengo yao” aliweka kituo kidogo baada ya kuona siongei chochote aliendelea tena.

“Nafanya kazi na watu wawili, mkuu wa majeshi pamoja na mheshimiwa raisi” maelezo yake yalinishtua sana watu alio wataja walikuwa watu wakubwa mno hapa nchini, nilijikuta naanza kumuogopa mtu huyo baada ya kugundua inawezekana kuna mambo mengi sana ambayo siyajui bado kuhusu yeye

“Kwenye hiyo kazi wewe unasimama kama nani?” nilimuuliza nikiwa natokwa na jasho pale kitandani

“Mimi ni mtoa taarifa za mhimu zaidi ambazo zitaweza kuisaidia nchi kuhusu huu umoja ambao unaonekana ni hatari sana kwa maisha ya baadae”

“Kama walisha ujua kwanini wasiwakamate tu mambo yote yaishe?” niliuliza swali ambalo mimi mwenyewe baadae nililiona kuwa la kijinga sana kwani kama wangekuwa na huo uwezo wa kuwakamata kirahisi wangekuwa wameshafanya hivyo.

“Kwanini wewe umeshindwa kunikamata?” aliniuliza swali ambalo lilinipa mwanga juu ya uhatari wa hilo kundi kama huyu analindwa hivi huyo kiongozi wao itakuaje.

“Na huyo kiongozi wenu uliye mwita Jadesh alikwambia siri gani alipokuja kwako ambayo umesema ilikufanya mpaka uogope sana?” alibadilisha kidogo sura baada ya kumuuliza hilo swali.

“Ukiwa kama mwanaume jifunze namna ya kukitumia kifua chako kwa usahihi vinginevyo kitakuponza, upana wa kifua chako ndio usalama wa maisha yako ukihisi unayajua sana mambo hautafika hata kesho ukiwa bado unahema, ukitoka hapa nitafute kwa hiyo namba 911, hiyo ni namba ya polisi ukipiga we ongea nao kwa kuzuga zuga mpaka mmalize kuongea usitoke hewani hata ikikatwa baada ya dakika tano simu itaita kupitia namba hiyo hiyo ipokee utaongea namimi, tumia simu ya mezani na hakikisha hakuna anaye lijua hili” baada ya kumaliza maelezo yake kwa usahihi aliiweka kola ya shati yake vizuri iliyokuwa ndani ya suti, kiza kilichokuwa humo ndani kilinifanya nisimuone ila hatua za viatu zilinipa taarifa mwanaume huyo alikuwa anatoka humo ndani, dakika mbili baadae umeme uliwaka kama kawaida mle ndani.

Mimi mwenyewe sielewi elewi kinacho endelea kwenye hii hadithi akili yako ndiyo mafanikio yako ya haraka kuielewa.

Niseme tu 26 sina nyongeza tena nadondosha kalamu chini

Bux the story teller
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA

TULIPO ISHIA SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA.......

Baada ya kumaliza maelezo yake kwa usahihi aliiweka kola ya shati yake vizuri iliyokuwa ndani ya suti, kiza kilichokuwa humo ndani kilinifanya nisimuone ila hatua za viatu zilinipa taarifa mwanaume huyo alikuwa anatoka humo ndani, dakika mbili baadae umeme uliwaka kama kawaida mle ndani.

ENDELEA..................

“Kitu gani kinakufanya mpaka umekuwa mtu wa kuishi kwa kujificha sana namna hii kijana kama wewe” swali la kwanza kabisa kutoka kwa Alexander lilimfanya Ashrafu atabasamu akiwa na glassi yake mkononi anasafisha koo wasi wasi haikuwa sehemu ya maisha yake kijana huyu.

“Dunia hii wanaishi watu mbali mbali na wenye sifa tofauti tofauti, kuishi kwenye huu ulimwengu unatakiwa uwe kama kivuli mbele za nyuso za watu ili upate vitu unavyo vihitaji wewe ila ukiruhusu kila mtu akakujua kwa undani basi sahau kuhusu kila kitu kwenye maisha yako hakuna nafasi utaipata mbele ya dunia ukaweza kutekeleza yale ambayo ulikuwa unataka kuyatimiza kiurahisi. Ninaishi nitakavyo, ninaweza kupata kitu chochote kwa muda wowote ule bila usumbufu wowote ule, sina uhakika sana ila ni miongoni mwa watu wenye usalama mkubwa sana ndani ya mipaka ya nchi hii, maliza maswali yako yote kuniuliza ili nikianza yakwangu usije ukaujutia ulimi wako” kijana mstaarabu kwa mwonekano ila mambo yake yalikuwa ya kutisha mno ndiye aliyekuwa anamwambia Alexander maneno ya kijasiri haya, alijiamini mno Ashrafu Hamad

“Hahahaahahahaahhaahahahah vijana wa siku hizi mnakua vibaya sana labda huenda mmezaliwa nje ya ndoa au kwa sababu mmelelewa na ulimwengu badala ya wazazi wenu ndio maana mnajihisi mnaweza kuropoka chochote kile ambacho kinakuja kwenye vichwa vyenu, yaani kijana kama wewe ndo unaniambia mimi nitaujutia ulimi wangu, hahahahaahahahhahhhhahh……….” Alexander aliona kama kijana huyo hakuwa siriasi kwa alichokuwa anakiongea kwenye mdomo wake haikuwa sawa mtu kama yeye kuweza kutishwa na kijana kama huyo kwake kilikuwa kama kichekesho nadhani hawakuwahi kumfahamu kiundani sana mwanaume huyo lakini alikatishwa kwa ukali na Ashrafu.

“Umemaliza maswali yako” sauti ya ukali wakati huo glasi ilivunjwa kwa mkono ndiyo iliyo mshtua Alexander kwenye kicheko ambacho hakikuwa cha furaha muda wote alikuwa anazipiga hesabu zake kwa usahihi anaweza kutoka vipi kwenye kundi kubwa la watu walio mzunguka mahali hapo wakiwa na silaha.

“ok, nambie wewe ni nani hasa na huyo baba yako ni nani serikalini?” swali la Alexander lilimshtua sana Ashrafu, maisha yake yaliwekwa ya siri kubwa mno hakuna mtu wa nje aliyekuwa anajua kwamba huyo kijana ni mtoto wa mtu kutoka upande wa serikali, hiyo taarifa haikuwa njema kwake hata kidogo japo hakuonyesha mshtuko wa moja kwa moja.

“Hili jambo mnalijua wangapi?” hakuwa na namna ya kupepesa macho kwa namna yoyote ile alijua anajulikana vilivyo na huyo mtu japo kuhusu baba yake ndiye mwanaume huyo alihitaji kumjua kwa usahihi.

“Unapo amua kucheza michezo ya hatari namna hii unatakiwa kuelewa kwamba kuna watu ambao walisha icheza michezo kama hiyo wamekaa pembeni wanakuangalia tu unacho kifanya sasa nao wanapo amua kurudi tena mchezoni inaweza kuwa hatari kubwa sana upande wako,ni vyema ukaitumia nafasi yako kukaa nje na haya mambo ukayaishi maisha yako tu japo umesha chelewa kwani mpaka sasa mafaili yako yapo kwenye mikono ya watu hatari sana na hauwezi kuikwepa hiyo mikono ikiwepo mkono wangu mimi mwenyewe iliniuma sana siku ile napigwa na risasi na kijana wa kawaida kama wewe, nimekutafuta mno kwa miaka kadhaa iliyoweza kupita mpaka nilipo kuja kujua kwamba siku ile ulikuwa kwenye ile hoteli, umekaa na kuwatoa sadaka vijana wa watu wasiokuwa na hatia yoyote ile ili wewe uwe salama nadhani leo utanipa majibu sahihi” Alexander alikuwa akijiamini mno kiasi kwamba aliwashangaza mpaka wao waliokuwa humo ndani ya nyumba hiyo, alijongea bila wasi wasi kabisa akasogea mahali lilipokuwa friji aliitoa moja ya wine iliyokuwepo humo ndani akachukua glass mbili na kwenda nazo mezani, watu wote walikuwa wakimshangaa tu licha ya wanaume wote kuwa na silaha kali haikuwa sababu ya kumfanya awe na wasi wasi. Hayo ni maisha ya viumbe vya kutisha duniani, wanaweza kukifanya chochote kile mahali popote pale na kuondoka bila kuwa na wasi wasi wowote ule, Alexander alimpa ishara Ashrafu akae chini ndipo waongee alionekana kuwa na mazungumzo ya muda mrefu kidogo.

“Tangu nianze kuyaishi haya maisha yangu ya hivi nimekuwa binadamu wa kutisha sana kwenye maisha ya wanadamu wa kawaida, naogopwa mno mtaani, kuna watu hawatamani hata kidogo kukutana namimi kwenye maisha yao lakini wewe unakuja hapa kwenye himaya yangu licha ya kuona aina ya umakini wa watu waliopo hapa ambapo kwa akili ya kawaida tu huna uhakika kama utatoka na nafsi yako ikiwa salama umekuwa mtu wa kujiamini kupita kiasi ni mbaya sana kwa maisha ya mtu kama wewe ambaye kwa sasa ulitakiwa uwe umeoa na una mkeo mnalea watoto wenu na sio kuwafuatilia watu kama mimi japokuwa kwa wewe ilikuwa ni lazima tu kwamba ningekutafuta hata usingekuja siku ya leo” Ashrafu alikuwa amekaa kwenye sofa hapo chini kila mtu akiwa na glasi yake mkononi ya wine wanashushia taratibu, kama ingekuwa ndio mara yako ya kwanza kuwaona watu hawa lazima ungedhani kwamba walikuwa ni watu wenye ukaribu wa hali ya juu kama sio marafiki wakubwa ila hilo halikuwa na ukweli wowote, hao wote wawili walikuwa ni watu ambao walikuwa wanatafutana isivyo kawaida, imani juu ya uwezo wao ndivyo vilivyofanya wakae chini kwanza weweze kuulizana maswali ambayo yangewafaa kwa alfajiri hiyo.

“Mhhhhhhhhhh ni mwanadamu wa aina gani wewe ambaye unaweza kumtisha mwanaume aliyeweza kuingia ndani ya ikulu ambayo ndiyo sehemu inayo lindwa zaidi ndani ya nchi, kuna kila aina ya watu hatari kule, kunalindwa mpaka na mitambo maalumu ya mionzi hata hivyo nilifanikiwa kumuua raisi na kutoweka bila kukamatwa wala kugundulika na binadamu yeyote mpaka leo, vipi naweza nikakuogopa kijana kama wewe ambaye hata uhakika wa maisha yako huna unaishi kwa kujificha ficha tu ukiogopa kwamba huenda maisha yako yakachukuliwa muda wowote ule. Hapa nitaondoka ila sio kwa wewe kuniambia niondoke, nitaondoka kwa kujisikia mwenyewe nitakapo ona nimekipata nilicho kifuata” Tabasanu hafifu ndiyo ilikuwa sehemu ya kuhitimisha maelezo ya Alexander,ni kitu ambacho kilikuwa ni cha kutisha sana, leo Ashrafu alikuwa anaambiwa kwamba mtu ambaye alikuwa naye mbele yake ndiye aliyekuwa amemuua mheshimiwa raisi aliyeweza kupita kwenye madaraka, kumbu kumbu zake zilienda miaka kadhaa nyuma ilikuwa ni kweli kuna raisi alifia madarakani ghafla sana kifo chake kikiwa ni siri kubwa ambayo haikuruhusiwa kutoka nje ya ikulu kwamba chanzo chake ni nini, hakujiuliza mara mbili alihisi huyo mtu anaweza kuondoka na maisha yake humo ndani kizembe sana kama asipo jihami.

Kuingia na kutoka ikulu ukiwa salama tena umefanya mauaji ya mheshimiwa raisi hakikuwa kitu chepesi, kilihitaji binadamu mwenye roho ngumu sana kuweza kufanya hivyo, mguu wake mmoja uliipiga chupa ya wine ambayo ilikuwa mezani, chupa hiyo ilikuwa inaelekea upande wa pili mwa meza hiyo haikuleta madhara yoyote ile baada ya kupokelewa kwa ngumi nzito na kupasukia hewani wine ikasambaa mithili ya maji, risasi mbili zilikuwa zimefyatuliwa kwa spidi kutoka kwenye bastola ambayo ilikuwa ipo kwenye mikono ya Ashrafu, meza ya kioo ilipigwa na teke ambayo ndiyo iliyotumika kuzuia risasi hizo mbili, ni umbali mdogo sana walikuwa wamekaa hao watu ila tukio lililokuwa linatendekea hapo lilikuwa linaleta burudani sana machoni mwa walinzi waliokuwa wako pembeni. Alexander alikuwa amejirushia nyuma ya sofa moja na kuligeuza kwa wepesi, risasi zaidi ya sita ziliishia kunyofoa nyofoa nyama ya sofa hilo kutoka kwenye bastola ya Ashrafu.

Zilipigwa hapo zaidi risasi hamsini kutoka kwa walinzi waliokuwa na silaha za kutisha kwenye mikono yao ikiwa ni kama hatua ya kuweza kumuweka bosi wao kuwa salama, hakutakiwa kuwa hata na kidonda huyo mtu hakuna mlinzi angeweza kutoka salama akiwa hai, sofa lilikuwa limenyofoka nyofoka halikutamanika tena.

“Noooooo stop, he is mine(huyu ni wa kwangu) nahitaji afie kwenye mikono yangu kama hataweza kunijibu maswali yangu”, kitu cha kushangaza Alexander alitokea nyuma ya kabati akiwa hana hata wasi wasi baada ya kusikia kelele za Ashrafu kumhitaji waonyeshane uwezo wao hiyo ndiyo ilikuwa robo tatu ya maisha yake aliipenda michezo ya ngumi kuliko hata alivyo yapenda maisha yake, hawakuelewa kutoka kwenye lile sofa ni muda gani ameutumia kufika kwenye hilo kabati hiyo ndiyo sababu alisema yeye sio mtu wa kawaida walijisumbua tu kupiga risasi zao hapo alikuwa ameondoka muda mrefu sana.

Ashrafu hakuhitaji mtu yeyote aweze kuingilia hilo alihitaji kwa mkono wake kumfanya mwanaume huyo amjibu maswali yake kwa lazima kama sio kumuua, walinzi walisogea nyuma uwanja mkubwa ulikuwa umeachwa kwa sababu ya wanaume hawa wawili. Nguo ya kulalia aliyokuwa ameivaa Ashrafu ilikuwa inakuja usawa wa macho ya Alexander aliipangua kwa nguvu alikutanishwa na teke maeneo ya shingoni alikuwa anaenda kujibamiza ukutani miguu ilitumika kudunda kwenye huo ukuta akatua chini akiwa safi, traki safi ilikuwa mwilini mwa Ashrafu kifua kilichokuwa kimegawanyika kilikuwa kipo wazi kabisa.

Spidi ambazo zilikuwa zinakuja kwa nguvu ya upepo zilitumika ndani ya sekunde chache sana Alexander kuweza kufika sehemu ambayo alikuwepo ashrafu, mwili wa Alexander ulizungushwa kama tairi lililokuwa kwenye mwendo mkali alijigeuzia kwenye mbavu za Ashrafu ambaye alirudi nyuma baada ya mikono iliyo komaa kuzigusa mbavu zake kwa nguvu alikuwa anadondokea kwenye moja ya sofa, mkono wake mmoja aliegamia kwenye pembe ya sofa hilo akajigeuza ila kabla hajakamilisha hilo goti lilikuwa limefika kwenye tumbo lake, Alexander alikuwa anakuja kwa nguvu sana, goti hilo lilimpeleka ukutani sehemu ambapo palikuwa na ala ya upanga ulio onekana kuwa wa muda mrefu kidogo ukiwa upo hapo, mguu uligusa sehemu kilipokuwa kitufe cha kuutolea upanga huo ulidakwa kwa usahihi kwenye mkono wa kulia wa Ashrafu, Alexander alikuwa amefika lakini alirudi nyuma kidogo baada kuzigusa alama za damu kwenye tumbo lake. Alikuwa amekatwa na kijana huyo Ashrafu Hamad ambaye alikuwa mbele yake, alitabasamu uzembe wa sekunde kadhaa tu ulikuwa umefanya ajisahau sana mpaka mpinzani wake akapata sehemu ya kuzigusa sehemu za mwili wake.

“Sasa nahitaji unijibu vizuri, kile mlicho kifuata siku ile ndani ya jiji la mwanza mlikipeleka wapi na kichwa cha yule mzee kipo wapi mpaka sasa?” upanga wake ukiwa na alama za damu alimuuliza mwanaume ambaye alisemekana kuingia ikulu na kumuua mheshimiwa raisi kisha akafanikiwa kutoroka bila kukamatwa na mtu yeyote yule, huyo ndiye Alexander mwenyewe.

“Leo kama utapona siku nyingine unatakiwa ukiniona unikimbie nadhani kwa hiki kinacho enda kutokea hapa leo hata baba yako atajitokeza hadharani akiwalilia watu kwa kitu unacho enda kufanyiwa ni bora ungeendelea kujificha tu, dakika tano ukifanikiwa kuzimaliza sitakuwa na swali la kukuuliza kuhusu maisha yako nitakuacha uende ila kama zitakushinda basi taarifa ya habari ya leo inaenda kuzitangaza habari za kifo chako mtu ambaye kile mtu anajua ulishakufa” kauli ya Alexander ilifuatiwa na uchomolewaji wa visu viwili kwenye kiuno chake.


Atapona nani ataishi nani? tukutane wakati ujao 27 sina la ziada tena

Bux the story teller
 
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA

TULIPO ISHIA SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA.......

Baada ya kumaliza maelezo yake kwa usahihi aliiweka kola ya shati yake vizuri iliyokuwa ndani ya suti, kiza kilichokuwa humo ndani kilinifanya nisimuone ila hatua za viatu zilinipa taarifa mwanaume huyo alikuwa anatoka humo ndani, dakika mbili baadae umeme uliwaka kama kawaida mle ndani.

ENDELEA..................

“Kitu gani kinakufanya mpaka umekuwa mtu wa kuishi kwa kujificha sana namna hii kijana kama wewe” swali la kwanza kabisa kutoka kwa Alexander lilimfanya Ashrafu atabasamu akiwa na glassi yake mkononi anasafisha koo wasi wasi haikuwa sehemu ya maisha yake kijana huyu.

“Dunia hii wanaishi watu mbali mbali na wenye sifa tofauti tofauti, kuishi kwenye huu ulimwengu unatakiwa uwe kama kivuli mbele za nyuso za watu ili upate vitu unavyo vihitaji wewe ila ukiruhusu kila mtu akakujua kwa undani basi sahau kuhusu kila kitu kwenye maisha yako hakuna nafasi utaipata mbele ya dunia ukaweza kutekeleza yale ambayo ulikuwa unataka kuyatimiza kiurahisi. Ninaishi nitakavyo, ninaweza kupata kitu chochote kwa muda wowote ule bila usumbufu wowote ule, sina uhakika sana ila ni miongoni mwa watu wenye usalama mkubwa sana ndani ya mipaka ya nchi hii, maliza maswali yako yote kuniuliza ili nikianza yakwangu usije ukaujutia ulimi wako” kijana mstaarabu kwa mwonekano ila mambo yake yalikuwa ya kutisha mno ndiye aliyekuwa anamwambia Alexander maneno ya kijasiri haya, alijiamini mno Ashrafu Hamad

“Hahahaahahahaahhaahahahah vijana wa siku hizi mnakua vibaya sana labda huenda mmezaliwa nje ya ndoa au kwa sababu mmelelewa na ulimwengu badala ya wazazi wenu ndio maana mnajihisi mnaweza kuropoka chochote kile ambacho kinakuja kwenye vichwa vyenu, yaani kijana kama wewe ndo unaniambia mimi nitaujutia ulimi wangu, hahahahaahahahhahhhhahh……….” Alexander aliona kama kijana huyo hakuwa siriasi kwa alichokuwa anakiongea kwenye mdomo wake haikuwa sawa mtu kama yeye kuweza kutishwa na kijana kama huyo kwake kilikuwa kama kichekesho nadhani hawakuwahi kumfahamu kiundani sana mwanaume huyo lakini alikatishwa kwa ukali na Ashrafu.

“Umemaliza maswali yako” sauti ya ukali wakati huo glasi ilivunjwa kwa mkono ndiyo iliyo mshtua Alexander kwenye kicheko ambacho hakikuwa cha furaha muda wote alikuwa anazipiga hesabu zake kwa usahihi anaweza kutoka vipi kwenye kundi kubwa la watu walio mzunguka mahali hapo wakiwa na silaha.

“ok, nambie wewe ni nani hasa na huyo baba yako ni nani serikalini?” swali la Alexander lilimshtua sana Ashrafu, maisha yake yaliwekwa ya siri kubwa mno hakuna mtu wa nje aliyekuwa anajua kwamba huyo kijana ni mtoto wa mtu kutoka upande wa serikali, hiyo taarifa haikuwa njema kwake hata kidogo japo hakuonyesha mshtuko wa moja kwa moja.

“Hili jambo mnalijua wangapi?” hakuwa na namna ya kupepesa macho kwa namna yoyote ile alijua anajulikana vilivyo na huyo mtu japo kuhusu baba yake ndiye mwanaume huyo alihitaji kumjua kwa usahihi.

“Unapo amua kucheza michezo ya hatari namna hii unatakiwa kuelewa kwamba kuna watu ambao walisha icheza michezo kama hiyo wamekaa pembeni wanakuangalia tu unacho kifanya sasa nao wanapo amua kurudi tena mchezoni inaweza kuwa hatari kubwa sana upande wako,ni vyema ukaitumia nafasi yako kukaa nje na haya mambo ukayaishi maisha yako tu japo umesha chelewa kwani mpaka sasa mafaili yako yapo kwenye mikono ya watu hatari sana na hauwezi kuikwepa hiyo mikono ikiwepo mkono wangu mimi mwenyewe iliniuma sana siku ile napigwa na risasi na kijana wa kawaida kama wewe, nimekutafuta mno kwa miaka kadhaa iliyoweza kupita mpaka nilipo kuja kujua kwamba siku ile ulikuwa kwenye ile hoteli, umekaa na kuwatoa sadaka vijana wa watu wasiokuwa na hatia yoyote ile ili wewe uwe salama nadhani leo utanipa majibu sahihi” Alexander alikuwa akijiamini mno kiasi kwamba aliwashangaza mpaka wao waliokuwa humo ndani ya nyumba hiyo, alijongea bila wasi wasi kabisa akasogea mahali lilipokuwa friji aliitoa moja ya wine iliyokuwepo humo ndani akachukua glass mbili na kwenda nazo mezani, watu wote walikuwa wakimshangaa tu licha ya wanaume wote kuwa na silaha kali haikuwa sababu ya kumfanya awe na wasi wasi. Hayo ni maisha ya viumbe vya kutisha duniani, wanaweza kukifanya chochote kile mahali popote pale na kuondoka bila kuwa na wasi wasi wowote ule, Alexander alimpa ishara Ashrafu akae chini ndipo waongee alionekana kuwa na mazungumzo ya muda mrefu kidogo.

“Tangu nianze kuyaishi haya maisha yangu ya hivi nimekuwa binadamu wa kutisha sana kwenye maisha ya wanadamu wa kawaida, naogopwa mno mtaani, kuna watu hawatamani hata kidogo kukutana namimi kwenye maisha yao lakini wewe unakuja hapa kwenye himaya yangu licha ya kuona aina ya umakini wa watu waliopo hapa ambapo kwa akili ya kawaida tu huna uhakika kama utatoka na nafsi yako ikiwa salama umekuwa mtu wa kujiamini kupita kiasi ni mbaya sana kwa maisha ya mtu kama wewe ambaye kwa sasa ulitakiwa uwe umeoa na una mkeo mnalea watoto wenu na sio kuwafuatilia watu kama mimi japokuwa kwa wewe ilikuwa ni lazima tu kwamba ningekutafuta hata usingekuja siku ya leo” Ashrafu alikuwa amekaa kwenye sofa hapo chini kila mtu akiwa na glasi yake mkononi ya wine wanashushia taratibu, kama ingekuwa ndio mara yako ya kwanza kuwaona watu hawa lazima ungedhani kwamba walikuwa ni watu wenye ukaribu wa hali ya juu kama sio marafiki wakubwa ila hilo halikuwa na ukweli wowote, hao wote wawili walikuwa ni watu ambao walikuwa wanatafutana isivyo kawaida, imani juu ya uwezo wao ndivyo vilivyofanya wakae chini kwanza weweze kuulizana maswali ambayo yangewafaa kwa alfajiri hiyo.

“Mhhhhhhhhhh ni mwanadamu wa aina gani wewe ambaye unaweza kumtisha mwanaume aliyeweza kuingia ndani ya ikulu ambayo ndiyo sehemu inayo lindwa zaidi ndani ya nchi, kuna kila aina ya watu hatari kule, kunalindwa mpaka na mitambo maalumu ya mionzi hata hivyo nilifanikiwa kumuua raisi na kutoweka bila kukamatwa wala kugundulika na binadamu yeyote mpaka leo, vipi naweza nikakuogopa kijana kama wewe ambaye hata uhakika wa maisha yako huna unaishi kwa kujificha ficha tu ukiogopa kwamba huenda maisha yako yakachukuliwa muda wowote ule. Hapa nitaondoka ila sio kwa wewe kuniambia niondoke, nitaondoka kwa kujisikia mwenyewe nitakapo ona nimekipata nilicho kifuata” Tabasanu hafifu ndiyo ilikuwa sehemu ya kuhitimisha maelezo ya Alexander,ni kitu ambacho kilikuwa ni cha kutisha sana, leo Ashrafu alikuwa anaambiwa kwamba mtu ambaye alikuwa naye mbele yake ndiye aliyekuwa amemuua mheshimiwa raisi aliyeweza kupita kwenye madaraka, kumbu kumbu zake zilienda miaka kadhaa nyuma ilikuwa ni kweli kuna raisi alifia madarakani ghafla sana kifo chake kikiwa ni siri kubwa ambayo haikuruhusiwa kutoka nje ya ikulu kwamba chanzo chake ni nini, hakujiuliza mara mbili alihisi huyo mtu anaweza kuondoka na maisha yake humo ndani kizembe sana kama asipo jihami.

Kuingia na kutoka ikulu ukiwa salama tena umefanya mauaji ya mheshimiwa raisi hakikuwa kitu chepesi, kilihitaji binadamu mwenye roho ngumu sana kuweza kufanya hivyo, mguu wake mmoja uliipiga chupa ya wine ambayo ilikuwa mezani, chupa hiyo ilikuwa inaelekea upande wa pili mwa meza hiyo haikuleta madhara yoyote ile baada ya kupokelewa kwa ngumi nzito na kupasukia hewani wine ikasambaa mithili ya maji, risasi mbili zilikuwa zimefyatuliwa kwa spidi kutoka kwenye bastola ambayo ilikuwa ipo kwenye mikono ya Ashrafu, meza ya kioo ilipigwa na teke ambayo ndiyo iliyotumika kuzuia risasi hizo mbili, ni umbali mdogo sana walikuwa wamekaa hao watu ila tukio lililokuwa linatendekea hapo lilikuwa linaleta burudani sana machoni mwa walinzi waliokuwa wako pembeni. Alexander alikuwa amejirushia nyuma ya sofa moja na kuligeuza kwa wepesi, risasi zaidi ya sita ziliishia kunyofoa nyofoa nyama ya sofa hilo kutoka kwenye bastola ya Ashrafu.

Zilipigwa hapo zaidi risasi hamsini kutoka kwa walinzi waliokuwa na silaha za kutisha kwenye mikono yao ikiwa ni kama hatua ya kuweza kumuweka bosi wao kuwa salama, hakutakiwa kuwa hata na kidonda huyo mtu hakuna mlinzi angeweza kutoka salama akiwa hai, sofa lilikuwa limenyofoka nyofoka halikutamanika tena.

“Noooooo stop, he is mine(huyu ni wa kwangu) nahitaji afie kwenye mikono yangu kama hataweza kunijibu maswali yangu”, kitu cha kushangaza Alexander alitokea nyuma ya kabati akiwa hana hata wasi wasi baada ya kusikia kelele za Ashrafu kumhitaji waonyeshane uwezo wao hiyo ndiyo ilikuwa robo tatu ya maisha yake aliipenda michezo ya ngumi kuliko hata alivyo yapenda maisha yake, hawakuelewa kutoka kwenye lile sofa ni muda gani ameutumia kufika kwenye hilo kabati hiyo ndiyo sababu alisema yeye sio mtu wa kawaida walijisumbua tu kupiga risasi zao hapo alikuwa ameondoka muda mrefu sana.

Ashrafu hakuhitaji mtu yeyote aweze kuingilia hilo alihitaji kwa mkono wake kumfanya mwanaume huyo amjibu maswali yake kwa lazima kama sio kumuua, walinzi walisogea nyuma uwanja mkubwa ulikuwa umeachwa kwa sababu ya wanaume hawa wawili. Nguo ya kulalia aliyokuwa ameivaa Ashrafu ilikuwa inakuja usawa wa macho ya Alexander aliipangua kwa nguvu alikutanishwa na teke maeneo ya shingoni alikuwa anaenda kujibamiza ukutani miguu ilitumika kudunda kwenye huo ukuta akatua chini akiwa safi, traki safi ilikuwa mwilini mwa Ashrafu kifua kilichokuwa kimegawanyika kilikuwa kipo wazi kabisa.

Spidi ambazo zilikuwa zinakuja kwa nguvu ya upepo zilitumika ndani ya sekunde chache sana Alexander kuweza kufika sehemu ambayo alikuwepo ashrafu, mwili wa Alexander ulizungushwa kama tairi lililokuwa kwenye mwendo mkali alijigeuzia kwenye mbavu za Ashrafu ambaye alirudi nyuma baada ya mikono iliyo komaa kuzigusa mbavu zake kwa nguvu alikuwa anadondokea kwenye moja ya sofa, mkono wake mmoja aliegamia kwenye pembe ya sofa hilo akajigeuza ila kabla hajakamilisha hilo goti lilikuwa limefika kwenye tumbo lake, Alexander alikuwa anakuja kwa nguvu sana, goti hilo lilimpeleka ukutani sehemu ambapo palikuwa na ala ya upanga ulio onekana kuwa wa muda mrefu kidogo ukiwa upo hapo, mguu uligusa sehemu kilipokuwa kitufe cha kuutolea upanga huo ulidakwa kwa usahihi kwenye mkono wa kulia wa Ashrafu, Alexander alikuwa amefika lakini alirudi nyuma kidogo baada kuzigusa alama za damu kwenye tumbo lake. Alikuwa amekatwa na kijana huyo Ashrafu Hamad ambaye alikuwa mbele yake, alitabasamu uzembe wa sekunde kadhaa tu ulikuwa umefanya ajisahau sana mpaka mpinzani wake akapata sehemu ya kuzigusa sehemu za mwili wake.

“Sasa nahitaji unijibu vizuri, kile mlicho kifuata siku ile ndani ya jiji la mwanza mlikipeleka wapi na kichwa cha yule mzee kipo wapi mpaka sasa?” upanga wake ukiwa na alama za damu alimuuliza mwanaume ambaye alisemekana kuingia ikulu na kumuua mheshimiwa raisi kisha akafanikiwa kutoroka bila kukamatwa na mtu yeyote yule, huyo ndiye Alexander mwenyewe.

“Leo kama utapona siku nyingine unatakiwa ukiniona unikimbie nadhani kwa hiki kinacho enda kutokea hapa leo hata baba yako atajitokeza hadharani akiwalilia watu kwa kitu unacho enda kufanyiwa ni bora ungeendelea kujificha tu, dakika tano ukifanikiwa kuzimaliza sitakuwa na swali la kukuuliza kuhusu maisha yako nitakuacha uende ila kama zitakushinda basi taarifa ya habari ya leo inaenda kuzitangaza habari za kifo chako mtu ambaye kile mtu anajua ulishakufa” kauli ya Alexander ilifuatiwa na uchomolewaji wa visu viwili kwenye kiuno chake.


Atapona nani ataishi nani? tukutane wakati ujao 27 sina la ziada tena

Bux the story teller
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE

TULIPO ISHIA SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA.......

“Leo kama utapona siku nyingine unatakiwa ukiniona unikimbie nadhani kwa hiki kinacho enda kutokea hapa leo hata baba yako atajitokeza hadharani akiwalilia watu kwa kitu unacho enda kufanyiwa ni bora ungeendelea kujificha tu, dakika tano ukifanikiwa kuzimaliza sitakuwa na swali la kukuuliza kuhusu maisha yako nitakuacha uende ila kama zitakushinda basi taarifa ya habari ya leo inaenda kuzitangaza habari za kifo chako mtu ambaye kile mtu anajua ulishakufa” kauli ya Alexander ilifuatiwa na uchomolewaji wa visu viwili kwenye kiuno chake.

ENDELEA...................

Visu viwili mkononi ndizo silaha ambazo alikuwa akiziheshimu sana Alexander akiwa kwenye sehemu yoyote ile ya hatari kwenye maisha yake, licha ya kukatwa na kisu kwenye sehemu yake ya tumbo bado mwili wake ulikuwa una joto la kutosha kuhitaji mapigano, ni dakika tano tu pekee ambazo ndizo alikuwa amezitoa kwa Ashrafu kama angefanikiwa kuzimaliza angeweza kumuacha akiwa hai kabisa na akaenda mbali ila kama angeshindwa kuzimaliza basi alitakiwa kuyajibu maswali yote aliyo ulizwa kwa usahihi ambayo ni mawili tu pekee yeye ni nani na ni mtoto wa nani serikalini hata hivyo kuachwa kwake ilikuwa ni ngumu sana kwani aliahidiwa kuuawa kikatili sana kiasi kwamba baba yake mzazi angejutia sana kwenye taarifa ya habari ya kifo cha kijana huyo. Hakuwahi kumuogopa binadamu yoyote yule Ashrafu lakini kwa siku hiyo kwa mara ya kwanza kabisa aliingiwa na hofu kwenye maisha yake mpaka muda huo mbavu zake zilikuwa kwenye hali mbaya sana ya maumivu ni mazoezi makali mno ndiyo yalikuwa yakimlinda mpaka muda huo ila kama angekuwa ni mtu wa kawaida asingeweza hata kumeza mate wala kuongea kwa usahihi.

Kisu kimoja kilikuwa kinakuja kwenye kifua cha Ashrafu, kilipanguliwa na upanga wake alijikuta yuko mbali sana baada ya kudondokea miguuni mwa moja ya walinzi wake, ujio wa kisu ulikuwa uko sambamba kabisa na spidi alizokuwa anakuja nazo Alexander mtu wa Kagera, Ashrafu alijinyanyua kwa maumivu akiwa haelewi mtu huyo alikuwa anapiga vipi dakika tatu ndizo zilikuwa zinamfanya ayasaidie maisha yake alijinyoosha na upanga wake akisukumizia na mateke yote mawili ambapo moja lilifanikiwa kumugusa Alexander kwenye paji la uso, alihisi pamechanika lakini alitikisa kichwa chake na kukiweka sawa, alijinyoosha akakiokota kisu chake kimoja ambacho kilipanguliwa na upanga wa Ashrafu, aliuma meno kwa hasira sana hakuamini kama mtu huyo angeweza kumsumbua sana namna hiyo, Ashrafu alibetuka tiktaka moja safi sana ili kuitegua shingo ya Alexander mwanaume aliinama chini kidogo akapitiliza Ashrafu wakati anageuza kichwa chake alikutana na teke la uso hakuamini kama ni teke limempiga ilikuwa ni mithili ya jiwe la chuma ndilo alikutanishwa nalo kwa mawazo yake yalivyo mtuma, alipoteza kabisa uwezo wa kuona alianza kupiga kelele kwa kupoteza uwezo wa kuona, kichwa kilikuwa kinauma na macho yalikuwa yanauma, alianza kurusha upanga bila mpangilio akipiga makelele.

Alexander aliangalia saa yake dakika moja ilikuwa imebaki zikamilike tano, alizungusha ngumi yake kwa hasira na kuituliza kwenye kifua cha Ashrafu ambaye alicheua damu, visu viwili vilipita kwenye bega lake mkono mmoja haukuwa na kazi tena ulichanika vibaya sana, alipiga kelele za kutisha zilizowafanya walinzi wake waingilie sasa baada ya kuona bosi wao amezidiwa hana uwezo wa kujilinda tena mbele ya mwanaume mkatili mno aliyekuwa yupo mbele yake. Alexander hakuwa na muda wa kupoteza humo ndani alikuwa anaenda kufa kwa spidi alijipindua na kumdaka Ashrafu ambapo mwili wa kijana huyo aliutumia kama kinga ya kujilindia baada ya kukoswa na risasi kadhaa kutoka kwa hao watu, aligeuza macho ule upande ambako walikuwa wale vijana wawili wenye kufanana na Ashrafu Hamad hakuona kitu chochote kile aligundua tayari walishakimbia, mkononi mwake alikuwa ameshika kitu kama bomu alilifungua juu yake moshi mwingi sana ulitanda humo ndani walinzi wote walianza kukohoa na kuishiwa nguvu hatimaye wakadondoka chini kabisa baada ya kukosa pumzi haikujulikana kama Alexander alipona kwenye huo moshi mkali au alipatwa na nini.

Mheshimiwa makamu wa raisi alikuwa ndani ya ofisi yake akiwaza mambo mengi sana ambayo yalikuwa yanaendelea kwenye maisha yake, stori ya maisha yake ndiyo iliyokuwa ikimfanya awe na mawazo mengi sana kichwani mwake, miaka kadhaa nyuma alikumbuka alikuwa mtu mwenye furaha kubwa sana wakati alipokuwa akiishi na mwanamke aliyekuwa akimpenda sana, alimshukuru MUNGU kwa kumpa zawadi hiyo ya pekee kabisa kwenye maisha yake, ni mwanamke ambaye hakuwa na uwezo wa kuelezea ni namna gani aliweza kumpata.

“Mbali na siasa ni kitu gani ambacho ndicho unakipenda sana kwenye maisha yako?”
“Kama ningeambiwa nichague maisha na mapenzi basi mapenzi kingekuwa kitu ambacho nisingekosa kukitaja, hakuna maisha bila mapenzi niamini mimi ila kunaweza kuwa na mapenzi bila maisha, kauli yangu inaweza kuwa tata na nisieleweke kirahisi hususani kwa binadamu wa sasa ambao wamepoteza imani kabisa ila ina maana kubwa sana, nakumbuka kwenye maisha yangu nilifanikiwa kukisoma kitabu kimoja kizuri sana cha mapenzi kinacho wahusu Romeo and Juliet tangu siku ile nilijifunza kwamba hakuna maisha bila mapenzi ila kuna mapenzi bila maisha kwa sababu watu wawili wapendanao waliamua kuyatoa maisha yao kwa sababu ya mapenzi ila hawakuwa tayari kuwa na maisha bila mapenzi. Tumeumbwa ili tuishi kwenye kuishi ni lazima upate mtu wa kuishi naye kwa wakati wako ambao MUNGU amekupendelea, mimi ni moja ya watu ambao nimebahatika kuishi kwenye maisha ambayo kila mwanaume anayatamani. Kukupata mwanamke kama wewe najihisi naweza kuufundisha ulimwengu juu ya nini maana ya mapenzi yalivyo, Asiana ni jina la mwanamke ambaye ninampenda sana kwenye maisha yangu, ni mwanamke ambaye kila nikimuona naelewa maana halisi ya mapenzi, nampenda sana huyo mpori pori wangu, na sio siasa tu hata ningeambiwa kwenye vitu vyote ambavyo vipo chini ya ulimwengu huu nataka nini, penzi la huyu mwanamke kwangu ni zawadi kubwa sana kwenye bustani nzuri ya huba la moyo wangu” sio wimbo wala hadithi ya kwenye kitabu ni maneno adhimu yalikuwa yakimtoka kijana mmoja pembezoni ya mto mdogo maeneo ya Kibiti akiwa kando ya mwanamke aliyekuwa akimpenda sana.

Hamad Hamad ndiye kijana aliyekuwa akielezea namna alivyokuwa akimpenda mwanamke wake huyo aliyepatwa kuitwa Asiana, mara ya kwanza mwanamke huyo alikuwa akijisikia vibaya sana kwa kuhisi mwanaume aliyekuwa akimpenda sana alikuwa akiipenda siasa kuliko anavyo mpenda yeye lakini hicho kitu kilikuwa ni cha tofauti kabisa na mawazo yake leo mwanaume alikuwa akimpa tasnia ya tungo nzuri zilizopo kwenye mdomo wake kuelezea namna anavyo mpenda, ni jambo lililompa furaha ambayo asingeweza kuielezea mwanamke huyo kwa namna alivyo kuwa amefurahi kupitiliza, kicheko ndiyo ilikuwa sehemu ya kuupamba uso wake mpana majira ya jioni maeneo ya Kibiti kwa walima mihogo huko.

Makamu wa raisi alishtuka kutoka kwenye hayo mawazo ambayo alitamani yasingekuwa yanaisha kirahisi sana namna hiyo, ule ulikuwa ni wakati sahihi sana wa yeye kuyaishi maisha hayo aliona kabisa alistahili kuipata furaha hiyo kwenye maisha yake yote lakini liwalo na kicheko leo basi kilio chaliita kesho yake ni tamathali ambazo baadhi ya watu wenye maarifa waliwahi kuzitamka na makamu huyo alikuwa akizikumbuka kwa usahihi sana. machozi yalimtoka kwenye macho yake usingeweza kuamini kama mwanaume wa aina hiyo alikuwa akililia mapenzi ni jambo la kuchekesha sana ila kama unalishuhudia upande wa pili, ni ugonjwa ambao hata wanao yachambua mapenzi kwa usahihi hawawezi kujitibu wenyewe, alisimama hapo alipokuwa amekaa akaenda kwenye kabati moja kubwa sana ambalo lilikuwa pembeni yake kidogo, aliingiza nywila hapo akatoka na Album moja nzuri sana ya picha, aliufungua ukurasa wa kwanza wa album hiyo kulikuwa na picha za watu watatu, picha moja alikuwa anaonekana yeye wakati akiwa kijana, picha ya pili kulikuwa na mwanamke mmoja mrembo sana lakini katikati ya picha hizo alikuwa amekaa mtoto mdogo sana mchanga tabasamu likiwa limeiangaza nuru ya uso wake. Alitoa kitambaa baada ya chozi lake kudondokea kwenye hiyo picha akajifuta kwa uchungu mkubwa.

“Mlinde mwanangu kwa namna yoyote ile huyo ndiyo alama ya uwepo wangu duniani hakuna mwingine zaidi yake, ukimuona yeye ni sawa na kwamba umeniona mimi” ni sauti ya mwanamke ambayo ilijirudia kichwani kwake, aliiheshimu mno hiyo sauti, alikurupuka humo ndani akatoka nje kwa kasi.

“Bosi kuna nini mpaka upo kwenye hiyo hali saivi?” mlinzi wake wa karibu sana aliweza kumuuliza bosi wake baada ya kumuona kama hakuwa sawa kabisa.
“Andaa msafara nahitaji kwenda kumuona mwanangu sasa hivi” aliitamka sentensi yake kwa jazba kiasi kwamba hakuhitaji maelezo mengi kutoka kwa hao watu.
“Sawa bosi lakini inadaiwa kwamba nyumbani kwake hayupo jana ameaga anaenda kwenye nyumba ndogo Kinondoni”
“Alienda kufanya nini huko bila mimi kujua”
“Sijui bosi ni tarifa ambayo nimeipata usiku wa leo kabla hakujapambazuka”
“Nahitaji kwenda huko haraka sana huyo mtoto kwangu ni mhimu sana andaa kila kitu nahitaji kufika huko haraka sana kwa muda mfupi” kauli yake ilikuwa ni amri na ilitekelezwa mara moja safari ya kuelekea Kinondoni ilianza mara moja. Dakika thelathini hakukuwa na foleni sana alfajiri hiyo na mapema walikuwa wamefika nje ya geti la nyumba hiyo iliyokuwa ikimilikiwa na Ashrafu Hamad mtoto wa mheshimiwa makamu wa raisi walishtuka kidogo baada ya kukuta nje kulikuwa na pikipiki ambayo ilionekana imetoka kulipuliwa muda sio mrefu sana kwani bado ilikuwa na mto unawaka. Mzee huyo alifika getini na kuingiza namba kadhaa geti likafunguka kwanza walistaajabu kuona kuna vijana wawili wameuawa kikatili mno hapo nje, makamu wa raisi alikimbilia ndani ya nyumba hiyo wakati huo moshi ulikuwa umeisha ila humo ndani kulikuwa na harufu kali ya kutisha. Aliangaza huku na huku kama ataona mtu lakini hakuona chochote kile wakati anageuza macho yake aliona alama za damu chini na mfumuko wa sofa ambao alijua wazi ni risasi zilipita hapo, hofu iliongezeka kwenye moyo wake sana.

Nyuma yake kulikuwa na miili ya wanaume kama kumi na wawili ambao walikuwa wapo chini wamelala, hakuelewa sababu ni nini aliinama ili kuwagusa na kuwageuza lakini alizuiwa na mlinzi wake ambaye alimuonyeshea alama ya kukataa kwa kichwa.

“Hii ni sumu kali sana ambayo huwa inamlevya kwanza mtu, anakosa nguvu kabisa kisha baada ya dakika thelathini kama atakosa matibabu basi hawezi kupona tena ataanza kubadilika taratibu” Mlinzi wa mzee huyo alikuwa anaongea huku akumvalisha bosi wake usoni mashine ya kuvutia hewa safi kwa sababu mazingira ya humo ndani hayakuwa rafiki kabisa kwa afya ya mtu wa kawaida.
“Atakuwa ni nani huyu mwenye ujasiri wa kuingia kwenye nyumba ya mwanangu bila wasi wasi wowote akatenda haya kwa wepesi sana namna hii?” swali kidogo lilikuwa gumu kwani wote ndo walikuwa wanafika muda huo hakuna mtu ambaye angeweza kujua kama nini kilitokea bila kuwa na ushahidi. Kabla hajajibiwa ili miili ya wale walinzi wa Ashrafu Hamad pale chini ilianza kubadilika rangi na kuwa myeusi.

“Huyu mtu anaonekana sio wa kawaida kwa sababu kuu mbili, yakwanza sio rahisi kumuingilia Ashrafu kwa ninavyo mjua mimi ni mtu wa kutisha sana kwenye mapigano ina maana kama huyu mtu amevamia na kumpata hapa akapata mpaka ujasiri wa kuyafanya haya basi ni mtu hatari mno, lakini sababu ya pili hii sumu iliyo tumika huwa inapatikana ndani ya nchi ya Urusi tu pekee duniani na haijawahi kuruhusiwa kusambaa kwenye nchi yoyote duniani kwa kuhofia usalama wa binadamu, hapa ndani ya saa moja lijalo hakuna kiumbe ambacho kimeivuta hiyo hewa kwa muda mrefu kitakuwa hai mpaka kwa muda huo” maelezo ya mlinzi wake yalimpa wasi wasi sana makamu wa raisi, hii nyumba aliijenga mwenyewe hivyo aliijua vyema sana aliingia mpaka kwenye chumba ambacho kilikuwa kinatumika kwa ajiri ya kamera za ulinzi zilizokuwa ndani ya nyumba hiyo.

Mjongeo wa kamera hizo uliionyesha sura ambayo baada ya kuiona tu mbele yake alionekana kuogopa mno hakutegemea hicho kitu kabisa kwenye maisha yake kama kinawezekana, hakuwa na nguvu tena za kusimama mzee huyu alilegea kiasi kwamba alidondokea kwenye kiti.

“Nooooo haiwezekani haiwezekani, imewezekanaje yupo hai mpaka leo nooooooooooo” aliongea kwa hasira akiinuka na kupiga ngumi kwenye ukuta kwa hasira kali, akiwa kwenye huo mshtuko na hasira simu ya kwenye hicho chumba cha kamera ilianza kuita kwa fujo, ni kitu ambacho hawakukitegemea hata kidogo ni vipi mpigaji aliweza kujua kwamba huo muda wangekuwa hapo alfajiri hiyo na mapema sana, aliinua na kuipokea simu yake midomo yake ikiwa inatetemeka sana, hakuwa na imani na usalama wa hiyo simu.

Nani kaanza kumgusa sehemu mbaya makamu wetu wa raisi? Hatima ya Alexander na Ashrafu ni ipi? Unadhani mpigaji wa simu atakuwa nani?...........

Naachia kalamu 28, tukutane sehemu ijayo baada ya Jamal kuujua ukweli wa maisha yake, unadhani anaenda kufanya nini?

Bux the story teller
 
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE

TULIPO ISHIA SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA.......

“Leo kama utapona siku nyingine unatakiwa ukiniona unikimbie nadhani kwa hiki kinacho enda kutokea hapa leo hata baba yako atajitokeza hadharani akiwalilia watu kwa kitu unacho enda kufanyiwa ni bora ungeendelea kujificha tu, dakika tano ukifanikiwa kuzimaliza sitakuwa na swali la kukuuliza kuhusu maisha yako nitakuacha uende ila kama zitakushinda basi taarifa ya habari ya leo inaenda kuzitangaza habari za kifo chako mtu ambaye kile mtu anajua ulishakufa” kauli ya Alexander ilifuatiwa na uchomolewaji wa visu viwili kwenye kiuno chake.

ENDELEA...................

Visu viwili mkononi ndizo silaha ambazo alikuwa akiziheshimu sana Alexander akiwa kwenye sehemu yoyote ile ya hatari kwenye maisha yake, licha ya kukatwa na kisu kwenye sehemu yake ya tumbo bado mwili wake ulikuwa una joto la kutosha kuhitaji mapigano, ni dakika tano tu pekee ambazo ndizo alikuwa amezitoa kwa Ashrafu kama angefanikiwa kuzimaliza angeweza kumuacha akiwa hai kabisa na akaenda mbali ila kama angeshindwa kuzimaliza basi alitakiwa kuyajibu maswali yote aliyo ulizwa kwa usahihi ambayo ni mawili tu pekee yeye ni nani na ni mtoto wa nani serikalini hata hivyo kuachwa kwake ilikuwa ni ngumu sana kwani aliahidiwa kuuawa kikatili sana kiasi kwamba baba yake mzazi angejutia sana kwenye taarifa ya habari ya kifo cha kijana huyo. Hakuwahi kumuogopa binadamu yoyote yule Ashrafu lakini kwa siku hiyo kwa mara ya kwanza kabisa aliingiwa na hofu kwenye maisha yake mpaka muda huo mbavu zake zilikuwa kwenye hali mbaya sana ya maumivu ni mazoezi makali mno ndiyo yalikuwa yakimlinda mpaka muda huo ila kama angekuwa ni mtu wa kawaida asingeweza hata kumeza mate wala kuongea kwa usahihi.

Kisu kimoja kilikuwa kinakuja kwenye kifua cha Ashrafu, kilipanguliwa na upanga wake alijikuta yuko mbali sana baada ya kudondokea miguuni mwa moja ya walinzi wake, ujio wa kisu ulikuwa uko sambamba kabisa na spidi alizokuwa anakuja nazo Alexander mtu wa Kagera, Ashrafu alijinyanyua kwa maumivu akiwa haelewi mtu huyo alikuwa anapiga vipi dakika tatu ndizo zilikuwa zinamfanya ayasaidie maisha yake alijinyoosha na upanga wake akisukumizia na mateke yote mawili ambapo moja lilifanikiwa kumugusa Alexander kwenye paji la uso, alihisi pamechanika lakini alitikisa kichwa chake na kukiweka sawa, alijinyoosha akakiokota kisu chake kimoja ambacho kilipanguliwa na upanga wa Ashrafu, aliuma meno kwa hasira sana hakuamini kama mtu huyo angeweza kumsumbua sana namna hiyo, Ashrafu alibetuka tiktaka moja safi sana ili kuitegua shingo ya Alexander mwanaume aliinama chini kidogo akapitiliza Ashrafu wakati anageuza kichwa chake alikutana na teke la uso hakuamini kama ni teke limempiga ilikuwa ni mithili ya jiwe la chuma ndilo alikutanishwa nalo kwa mawazo yake yalivyo mtuma, alipoteza kabisa uwezo wa kuona alianza kupiga kelele kwa kupoteza uwezo wa kuona, kichwa kilikuwa kinauma na macho yalikuwa yanauma, alianza kurusha upanga bila mpangilio akipiga makelele.

Alexander aliangalia saa yake dakika moja ilikuwa imebaki zikamilike tano, alizungusha ngumi yake kwa hasira na kuituliza kwenye kifua cha Ashrafu ambaye alicheua damu, visu viwili vilipita kwenye bega lake mkono mmoja haukuwa na kazi tena ulichanika vibaya sana, alipiga kelele za kutisha zilizowafanya walinzi wake waingilie sasa baada ya kuona bosi wao amezidiwa hana uwezo wa kujilinda tena mbele ya mwanaume mkatili mno aliyekuwa yupo mbele yake. Alexander hakuwa na muda wa kupoteza humo ndani alikuwa anaenda kufa kwa spidi alijipindua na kumdaka Ashrafu ambapo mwili wa kijana huyo aliutumia kama kinga ya kujilindia baada ya kukoswa na risasi kadhaa kutoka kwa hao watu, aligeuza macho ule upande ambako walikuwa wale vijana wawili wenye kufanana na Ashrafu Hamad hakuona kitu chochote kile aligundua tayari walishakimbia, mkononi mwake alikuwa ameshika kitu kama bomu alilifungua juu yake moshi mwingi sana ulitanda humo ndani walinzi wote walianza kukohoa na kuishiwa nguvu hatimaye wakadondoka chini kabisa baada ya kukosa pumzi haikujulikana kama Alexander alipona kwenye huo moshi mkali au alipatwa na nini.

Mheshimiwa makamu wa raisi alikuwa ndani ya ofisi yake akiwaza mambo mengi sana ambayo yalikuwa yanaendelea kwenye maisha yake, stori ya maisha yake ndiyo iliyokuwa ikimfanya awe na mawazo mengi sana kichwani mwake, miaka kadhaa nyuma alikumbuka alikuwa mtu mwenye furaha kubwa sana wakati alipokuwa akiishi na mwanamke aliyekuwa akimpenda sana, alimshukuru MUNGU kwa kumpa zawadi hiyo ya pekee kabisa kwenye maisha yake, ni mwanamke ambaye hakuwa na uwezo wa kuelezea ni namna gani aliweza kumpata.

“Mbali na siasa ni kitu gani ambacho ndicho unakipenda sana kwenye maisha yako?”
“Kama ningeambiwa nichague maisha na mapenzi basi mapenzi kingekuwa kitu ambacho nisingekosa kukitaja, hakuna maisha bila mapenzi niamini mimi ila kunaweza kuwa na mapenzi bila maisha, kauli yangu inaweza kuwa tata na nisieleweke kirahisi hususani kwa binadamu wa sasa ambao wamepoteza imani kabisa ila ina maana kubwa sana, nakumbuka kwenye maisha yangu nilifanikiwa kukisoma kitabu kimoja kizuri sana cha mapenzi kinacho wahusu Romeo and Juliet tangu siku ile nilijifunza kwamba hakuna maisha bila mapenzi ila kuna mapenzi bila maisha kwa sababu watu wawili wapendanao waliamua kuyatoa maisha yao kwa sababu ya mapenzi ila hawakuwa tayari kuwa na maisha bila mapenzi. Tumeumbwa ili tuishi kwenye kuishi ni lazima upate mtu wa kuishi naye kwa wakati wako ambao MUNGU amekupendelea, mimi ni moja ya watu ambao nimebahatika kuishi kwenye maisha ambayo kila mwanaume anayatamani. Kukupata mwanamke kama wewe najihisi naweza kuufundisha ulimwengu juu ya nini maana ya mapenzi yalivyo, Asiana ni jina la mwanamke ambaye ninampenda sana kwenye maisha yangu, ni mwanamke ambaye kila nikimuona naelewa maana halisi ya mapenzi, nampenda sana huyo mpori pori wangu, na sio siasa tu hata ningeambiwa kwenye vitu vyote ambavyo vipo chini ya ulimwengu huu nataka nini, penzi la huyu mwanamke kwangu ni zawadi kubwa sana kwenye bustani nzuri ya huba la moyo wangu” sio wimbo wala hadithi ya kwenye kitabu ni maneno adhimu yalikuwa yakimtoka kijana mmoja pembezoni ya mto mdogo maeneo ya Kibiti akiwa kando ya mwanamke aliyekuwa akimpenda sana.

Hamad Hamad ndiye kijana aliyekuwa akielezea namna alivyokuwa akimpenda mwanamke wake huyo aliyepatwa kuitwa Asiana, mara ya kwanza mwanamke huyo alikuwa akijisikia vibaya sana kwa kuhisi mwanaume aliyekuwa akimpenda sana alikuwa akiipenda siasa kuliko anavyo mpenda yeye lakini hicho kitu kilikuwa ni cha tofauti kabisa na mawazo yake leo mwanaume alikuwa akimpa tasnia ya tungo nzuri zilizopo kwenye mdomo wake kuelezea namna anavyo mpenda, ni jambo lililompa furaha ambayo asingeweza kuielezea mwanamke huyo kwa namna alivyo kuwa amefurahi kupitiliza, kicheko ndiyo ilikuwa sehemu ya kuupamba uso wake mpana majira ya jioni maeneo ya Kibiti kwa walima mihogo huko.

Makamu wa raisi alishtuka kutoka kwenye hayo mawazo ambayo alitamani yasingekuwa yanaisha kirahisi sana namna hiyo, ule ulikuwa ni wakati sahihi sana wa yeye kuyaishi maisha hayo aliona kabisa alistahili kuipata furaha hiyo kwenye maisha yake yote lakini liwalo na kicheko leo basi kilio chaliita kesho yake ni tamathali ambazo baadhi ya watu wenye maarifa waliwahi kuzitamka na makamu huyo alikuwa akizikumbuka kwa usahihi sana. machozi yalimtoka kwenye macho yake usingeweza kuamini kama mwanaume wa aina hiyo alikuwa akililia mapenzi ni jambo la kuchekesha sana ila kama unalishuhudia upande wa pili, ni ugonjwa ambao hata wanao yachambua mapenzi kwa usahihi hawawezi kujitibu wenyewe, alisimama hapo alipokuwa amekaa akaenda kwenye kabati moja kubwa sana ambalo lilikuwa pembeni yake kidogo, aliingiza nywila hapo akatoka na Album moja nzuri sana ya picha, aliufungua ukurasa wa kwanza wa album hiyo kulikuwa na picha za watu watatu, picha moja alikuwa anaonekana yeye wakati akiwa kijana, picha ya pili kulikuwa na mwanamke mmoja mrembo sana lakini katikati ya picha hizo alikuwa amekaa mtoto mdogo sana mchanga tabasamu likiwa limeiangaza nuru ya uso wake. Alitoa kitambaa baada ya chozi lake kudondokea kwenye hiyo picha akajifuta kwa uchungu mkubwa.

“Mlinde mwanangu kwa namna yoyote ile huyo ndiyo alama ya uwepo wangu duniani hakuna mwingine zaidi yake, ukimuona yeye ni sawa na kwamba umeniona mimi” ni sauti ya mwanamke ambayo ilijirudia kichwani kwake, aliiheshimu mno hiyo sauti, alikurupuka humo ndani akatoka nje kwa kasi.

“Bosi kuna nini mpaka upo kwenye hiyo hali saivi?” mlinzi wake wa karibu sana aliweza kumuuliza bosi wake baada ya kumuona kama hakuwa sawa kabisa.
“Andaa msafara nahitaji kwenda kumuona mwanangu sasa hivi” aliitamka sentensi yake kwa jazba kiasi kwamba hakuhitaji maelezo mengi kutoka kwa hao watu.
“Sawa bosi lakini inadaiwa kwamba nyumbani kwake hayupo jana ameaga anaenda kwenye nyumba ndogo Kinondoni”
“Alienda kufanya nini huko bila mimi kujua”
“Sijui bosi ni tarifa ambayo nimeipata usiku wa leo kabla hakujapambazuka”
“Nahitaji kwenda huko haraka sana huyo mtoto kwangu ni mhimu sana andaa kila kitu nahitaji kufika huko haraka sana kwa muda mfupi” kauli yake ilikuwa ni amri na ilitekelezwa mara moja safari ya kuelekea Kinondoni ilianza mara moja. Dakika thelathini hakukuwa na foleni sana alfajiri hiyo na mapema walikuwa wamefika nje ya geti la nyumba hiyo iliyokuwa ikimilikiwa na Ashrafu Hamad mtoto wa mheshimiwa makamu wa raisi walishtuka kidogo baada ya kukuta nje kulikuwa na pikipiki ambayo ilionekana imetoka kulipuliwa muda sio mrefu sana kwani bado ilikuwa na mto unawaka. Mzee huyo alifika getini na kuingiza namba kadhaa geti likafunguka kwanza walistaajabu kuona kuna vijana wawili wameuawa kikatili mno hapo nje, makamu wa raisi alikimbilia ndani ya nyumba hiyo wakati huo moshi ulikuwa umeisha ila humo ndani kulikuwa na harufu kali ya kutisha. Aliangaza huku na huku kama ataona mtu lakini hakuona chochote kile wakati anageuza macho yake aliona alama za damu chini na mfumuko wa sofa ambao alijua wazi ni risasi zilipita hapo, hofu iliongezeka kwenye moyo wake sana.

Nyuma yake kulikuwa na miili ya wanaume kama kumi na wawili ambao walikuwa wapo chini wamelala, hakuelewa sababu ni nini aliinama ili kuwagusa na kuwageuza lakini alizuiwa na mlinzi wake ambaye alimuonyeshea alama ya kukataa kwa kichwa.

“Hii ni sumu kali sana ambayo huwa inamlevya kwanza mtu, anakosa nguvu kabisa kisha baada ya dakika thelathini kama atakosa matibabu basi hawezi kupona tena ataanza kubadilika taratibu” Mlinzi wa mzee huyo alikuwa anaongea huku akumvalisha bosi wake usoni mashine ya kuvutia hewa safi kwa sababu mazingira ya humo ndani hayakuwa rafiki kabisa kwa afya ya mtu wa kawaida.
“Atakuwa ni nani huyu mwenye ujasiri wa kuingia kwenye nyumba ya mwanangu bila wasi wasi wowote akatenda haya kwa wepesi sana namna hii?” swali kidogo lilikuwa gumu kwani wote ndo walikuwa wanafika muda huo hakuna mtu ambaye angeweza kujua kama nini kilitokea bila kuwa na ushahidi. Kabla hajajibiwa ili miili ya wale walinzi wa Ashrafu Hamad pale chini ilianza kubadilika rangi na kuwa myeusi.

“Huyu mtu anaonekana sio wa kawaida kwa sababu kuu mbili, yakwanza sio rahisi kumuingilia Ashrafu kwa ninavyo mjua mimi ni mtu wa kutisha sana kwenye mapigano ina maana kama huyu mtu amevamia na kumpata hapa akapata mpaka ujasiri wa kuyafanya haya basi ni mtu hatari mno, lakini sababu ya pili hii sumu iliyo tumika huwa inapatikana ndani ya nchi ya Urusi tu pekee duniani na haijawahi kuruhusiwa kusambaa kwenye nchi yoyote duniani kwa kuhofia usalama wa binadamu, hapa ndani ya saa moja lijalo hakuna kiumbe ambacho kimeivuta hiyo hewa kwa muda mrefu kitakuwa hai mpaka kwa muda huo” maelezo ya mlinzi wake yalimpa wasi wasi sana makamu wa raisi, hii nyumba aliijenga mwenyewe hivyo aliijua vyema sana aliingia mpaka kwenye chumba ambacho kilikuwa kinatumika kwa ajiri ya kamera za ulinzi zilizokuwa ndani ya nyumba hiyo.

Mjongeo wa kamera hizo uliionyesha sura ambayo baada ya kuiona tu mbele yake alionekana kuogopa mno hakutegemea hicho kitu kabisa kwenye maisha yake kama kinawezekana, hakuwa na nguvu tena za kusimama mzee huyu alilegea kiasi kwamba alidondokea kwenye kiti.

“Nooooo haiwezekani haiwezekani, imewezekanaje yupo hai mpaka leo nooooooooooo” aliongea kwa hasira akiinuka na kupiga ngumi kwenye ukuta kwa hasira kali, akiwa kwenye huo mshtuko na hasira simu ya kwenye hicho chumba cha kamera ilianza kuita kwa fujo, ni kitu ambacho hawakukitegemea hata kidogo ni vipi mpigaji aliweza kujua kwamba huo muda wangekuwa hapo alfajiri hiyo na mapema sana, aliinua na kuipokea simu yake midomo yake ikiwa inatetemeka sana, hakuwa na imani na usalama wa hiyo simu.

Nani kaanza kumgusa sehemu mbaya makamu wetu wa raisi? Hatima ya Alexander na Ashrafu ni ipi? Unadhani mpigaji wa simu atakuwa nani?...........

Naachia kalamu 28, tukutane sehemu ijayo baada ya Jamal kuujua ukweli wa maisha yake, unadhani anaenda kufanya nini?

Bux the story teller
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA

TULIPO ISHIA SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE.......
“Nooooo haiwezekani haiwezekani, imewezekanaje yupo hai mpaka leo nooooooooooo” aliongea kwa hasira akiinuka na kupiga ngumi kwenye ukuta kwa hasira kali, akiwa kwenye huo mshtuko na hasira simu ya kwenye hicho chumba cha kamera ilianza kuita kwa fujo, ni kitu ambacho hawakukitegemea hata kidogo ni vipi mpigaji aliweza kujua kwamba huo muda wangekuwa hapo alfajiri hiyo na mapema sana, aliinua na kuipokea simu yake midomo yake ikiwa inatetemeka sana, hakuwa na imani na usalama wa hiyo simu.

ENDELEA.....................


“Muda huwa unaenda kwa kasi sana hapa duniani kama ilivyokuwa kawaida hauwezi kusimama, wiki tatu zilipita nikiwa napatiwa matibabu pale kitandani hatimaye niliweza kunyanyuka nikiwa kamili , yule mtu alitumia pesa nyingi sana kuhakikisha nasimama tena maana waliletwa madaktari bingwa kutoka nje za nchi ambao walinishughulikia wakati huo kiongozi wangu hakuwa akijua lolote kuhusu hayo ambayo yalikuwa yamenitokea kwa muda huo. Huenda ni miongoni mwa wanadamu ambao nilikuja kuwaheshimu zaidi kwenye maisha yangu yote, kwanza alinilindia siri kwa wenzake kwamba mimi ni usalama wa taifa kwa sababu kama wangejua basi wangenitafuta sehemu yoyote ile waweze kuniua, mpaka muda huo sikuwa na uwezo wa kumpatia mwanamke yeyote mimba kwa sababu sikuwa na sehemu ambazo zingenipa huo uwezo kwenye maisha yangu lakini sikuwa mchoyo wa fadhila kwa mwenyezi MUNGU kwa kunipendelea nafasi nyingine ya kuendelea kushuhudia ubaya wa ulimwengu, pumzi ndicho kiburi kikubwa sana kwa mwanadamu yeyote yule, ndiyo huwa inawafanya wanadamu wanakuwa jeuri mno ila ikifika siku ukiwa huna uwezo wa kuivuta hiyo pumzi vizuri upo kitandani malaika wa kifo anakung’ang’ania uondoke naye ndipo utakapo elewa thamani ya maisha ambayo unayachezea kwa sasa hapa duniani. Baada ya kuweza kusimama kwa mara nyingine tena nilifanya mazoezi kwa nguvu sana sikuhitaji kukutana na mkuu wangu kwa hali niliyokuwa nayo isingekuwa vyema kukaa naye kuongea ningeonekana mwanadamu dhaifu sana.

Wiki moja baadae nilijihisi kuwa vizuri sana hivyo nilifanikiwa kutoka kwenye hospitali ambayo nilikuja kugundua baadae kwamba ilikuwa ni nyumba ya mtu binafsi ambayo ilikuwa nje ya jiji kabisa, gari moja nilipewa na wale madaktari ambao walihakikisha usalama wangu, nikiwa ndani ya suti yangu nilirudi ndani ya jiji la Dar es salaam bila wasi wasi, mtu wa kwanza kuonana naye alikuwa ni mkurugenzi wa usalama wa taifa baada ya kupotea kwa zaidi ya mwezi mzima nilijua lazima watakuwa wamenitafuta sana.
“Ni mwezi sasa umepita haupo wala hauonekani ni kipi kimetokea huko ulikokuwa” baada ya kukutana na mzee yule hakuihitaji hata salamu yangu swali lake ndiyo ilikuwa salamu. Nilimsimulia kila kitu kilichokuwa kimetokea mpaka wakati huo, alinisikitikia sana mambo yaliyonikuta yalikuwa yanatisha sana ilihitaji moyo kuweza kuyamudu. Alishtuka sana baada ya mimi kumwambia Jonson Malisaba alikuwa akifanya kazi chini ya viongozi wakubwa wa serikali, ni kitu ambacho ilikuwa ni ngumu sana kwake kukiamini lakini ndio ulikuwa ukweli wenyewe alitamani sana akutane na Malisaba mwenyewe. Baada ya kutoka hapo maisha yaliendelea bila kuweza kuongea na baba yako ni mwaka mmoja ulikuwa umeisha, siku moja saa sita za usiku niliamua kuipiga ile namba ambayo alikuwa amenipa kwamba nikimhitaji muda wowote nitampata 911 niliipiga bila kusita kwa kutumia simu yangu ya mezani, simu moja kwa moja ilipokelewa kituo cha polisi sikuogopa kwa sababu hilo nilikuwa nikilijua mapema sana yalifuata maongezi ya kawaida tu kisha ikakatwa, dakika zaidi ya tano zilipita kukiwa kimya lakini haikuchukua muda simu yangu iliita niliipokea kwa wepesi mno.
“Hello” sauti yenye mgandamizo kutoka upande wa pili niliisikia majira hayo ya usiku wa manane kwa usahihi kabisa.
“Naomba tuonane” nilimjibu kwa ufupi kwa sababu ilikuwa ni hatari sana kuanza kutambulishana kwenye simu ni kitu cha hatari sana unaweza kukamatwa muda wowote ule.
“Toka nje ndani ya dakika saba kuna gari inakuja kukuchukua hapo” aliongea kwa msisitizo ila nilishangaa kwani nilikuwa naishi sehemu ya siri sana sasa sikujua amepajuaje
“Unajua nilipo mpaka useme nakuja kuchukuliwa” swali langu lilionekana la kipuuzi kwani alikata simu, nilitoka nje ili nijue kama hicho kitu ni cha kweli au alikuwa ananitania tu, nilishuka ngazi kwa wepesi nikatoka nje kweli sio muda niliona kuna gari nyeusi inafika hapo sikuwa na shaka niliingia ndani. Tulizunguka nyuma tu ya mtaa huo gari ikasimama kwa mbele alikuwa amesimama mwanaume ambaye alinipa mgongo ila nilimfahamu vyema nilitabasamu tu.
“Unaonekana kuwa mtu wa kutisha sana kama umefanikiwa kuweza kuijua sehemu ambayo ninaishi mtu kama mimi” niliongea huku nikiwa nasogea mahali alipokuwa akiendelea kuivuta sigara yake kubwa
“Haya maisha ni wajinga tu pekee ndio huwa wanajihisi wao wana akili kupita kiasi hasa pale wanapokuwa kati kati ya wajinga wenzao ila huwa ni tofauti kwa watu wenye akili sana kwao mjinga ndiye huwa anatumika kurahisisha kazi zao kupitia kujisifia kwake hivyo usije ukakaa ukajiona kwamba wewe unaishi kwa siri hata kidogo ni wajinga tu ndo wanajua hivyo ila kuna watu tunaweza kukupata muda wowote ule ambao tunataka sisi na hii ndiyo dunia tunayo iishi leo kila kitu kipo mkononi” alimaliza maelezo yake akinirushia kichupa cha pombe kali ambacho kwa kiasi fulani kingenipatia joto kutokana na upepo wa bahari uliokuwa ukivuma mpaka hayo maeneo.
“Hii ndiyo sababu serikali haiwezi kuwapata kirahisi sana watu kama nyie mna kila kitu cha kuwafanya muwe salama muda wote, kwa nchi hili jambo ni la kutisha kupita kiasi kama kuna raia tu wa kawaida wanaweza kuyafanya haya mambo bila vyombo vya usalama kujua inatishia amani ya nchi” nilimjibu huku nikikunja ndita kwa ukali wa pombe niliyokuwa nimepewa.
“Tatizo ni pesa, inapokuwepo pesa basi hakuna haki wala hakuna uzalendo, nchi haina pesa wanazishikilia watu wachache tu ambao wanafanikiwa kupata nafasi za juu unadhani kinatokea nini hapo, sisi tuna pesa nyingi sana, serikalini tuna watu wengi mno ambao ndio hao mnategemea waitengeneze nchi, mimi ukinikamata saivi baada ya saa moja tu baadae natoka nawewe unauawa unadhani ni kitu gani nchi itatufanya? Ujio wa pesa umebadilisha aina ya maisha ambayo wanadamu wa kawaida walitakiwa kuyaishi hivyo usipoteze muda sana kuwaza hilo jambo. Kesho ni siku ambayo unaenda kukutana na ndugu yako kwa mara ya kwanza tangu utoke nchini ni miaka sita nadhani imepita sasa, ni mwanajeshi sasa na ana nyota tatu kwa sababu yako tu kukubali kufanya kazi na serikali basi mwenzako naye anaishi vizuri kwa sasa, usijiulize nimejuaje nimekwambia hii nchi ipo kwenye mikono ya watu ambao wana uwezo wa kufanya jambo lolote lile na asiwepo mtu yeyote yule wa kuwazuia.

Hiyo siku ya kesho una kazi kubwa ya kulikomboa taifa lako kama ukishindwa basi hii nchi mtakuwa mmeikabidhi rasmi kwenye mikono ya watu ambao ninafanya nao kazi kwa sasa” maelezo yake yalikuwa yakinichanganya sana sikumuelewa vitu vyangu vingi namna ile ameweza kuvijua vipi ila nilifurahi sana moyoni kusikia ndugu yangu alikuwa na nyota tatu mpaka wakati huo ulipita muda mrefu sana bila kumuona wala kupata taarifa zake lakini hilo sikuliwaza sana kitendo cha kuniambia kwamba nilikuwa na kazi kubwa sana ya kulilinda taifa langu ndicho hicho kilichoweza kuniumiza kichwa sana huku yeye akiwa hana hata wasi wasi kwenye uso wake.
“Una maanisha nini kusema kwamba natakiwa nilikomboe taifa kwa mikono yangu mwenyewe?”
“Kesho raisi wa nchi anaenda kuuawa”
“Raisi anaenda kuuawa? Kivipi? Na nani anaenda kufanya hilo tukio?” maswali yalinitoka kwa mkupuo jasho likiwa linanitoka kwa kasi lakini yeye alikuwa anacheka sana
“Vipi unaogopa sana?” aliniuliza akiitupa sigara yake chini
“Unajua mimi nashindwa kabisa kukuelewa, uliniambia mheshimiwa raisi ndiye aliyekupa kazi ya kuisaidia nchi leo unaniambia raisi anaenda kuuawa nitakuamini vipi kwa hayo yote unayo yaongea?” nilimuuliza kwa hasira jina raisi huwa linapaswa kutajwa kwa heshima sana tofauti nayeye alivyokuwa akilitaja kiwepesi mno tena akisemea kifo cha mheshimiwa kwa urahisi sana namna hiyo
“Nadhani uliwahi kuathirika sana na madhara ya upigaji wa punyeto kwenye ukuaji wako hiyo michezo ni hatari kwenye kuwafanya watu kupoteza sana kumbu kumbu, kazi nilipewa na mkuu wa majeshi na ndiye aliye nikutanisha na mheshimiwa raisi ila hata hivi hilo halihusiani na kufa kwake” wakati huu sasa alinigeukia akionekana sura yake kuiweka kwenye hali ya usiriasi sana.
“Unamaanisha nini kuniambia hivyo”
“Nilikwambia unitafute mapema ukitoka kitandani lakini wewe ukapuuzia ni mwaka sasa ndo umenitafuta muda ukiwa umeenda sana, ungenitafuta mapema huenda hili ungekuwa umelizuia mapema sana kwa sasa sina imani sana kama utafanikisha ila jaribu kila linalowezekana kama utaweza kuifanya hiyo kazi. Huyu raisi aliyepo madarakani ni mtu ambaye anafanya baadhi ya mambo yetu kukwama hivyo kinacho fanyika ni kumtoa kwenye kile kiti na kumtoa kwake ni kumuua tu hakuna njia nyingine. Kesho majira ya saa nane usiku ndio muda ambao anatakiwa kufa kwahiyo kama mkishindwa kumsaidia mpaka muda huo keshokutwa asubuhi taifa litapokea taarifa mbaya sana hivyo ni kazi kwako wewe pamoja na wenzako wahini mapema kama mtalifanikisha hilo ila kumbuka tu kwamba wanao kuja kuifanya hii kazi ni watu wa kutisha na ni hatari mno” baada ya maelezo yake alianza kuondoka.
“Itakuaje kama hilo jambo litafanikiwa kukamilika?” swali langu lilimfanya akageuka tena pale nilipokuwa.
“Vyombo vya usalama mtakuwa kwenye hatari kubwa sana kwa sababu mtaonekana hampo makini na kazi yenu mpaka mheshimiwa raisi anauawa mkiwa mpo jiandaeni kwa hilo”
“Hili tukio limepangwa kufanyikia wapi? ili ikiwezekana ratiba zote za mheshimiwa ziweze kuvunjwa hiyo kesho”
“Bahati mbaya sana hata kama ungeipata nafasi huna hiyo nguvu ya kuweza kuzifuta ratiba za mheshimiwa raisi kwa nafasi uliyo nayo kumbuka umeingizwa kwenye usalama kiholela hivyo haujulikani. Hilo tukio linaenda kufanyikia ikulu”
“Haiwezekani, hakuna binadamu anayeweza kulifanya hilo tukio ndani ya ikulu hata kama angekuwa nani, hiyo ndiyo sehemu inayo lindwa zaidi kwenye ardhi hii inawezekana vipi raia afanye hilo tukio kule”
“Mhhhhhhhhh, hauna hata miaka mingi kwenye hiyo kazi ndo kwanza unaanza hiyo jeuri ya kupinga hicho kitu unaitolewa wapi? watu wanaiba mpaka benki kuu ya dunia ambayo ndiyo sehemu unapo hifadhiwa utajiri wa dunia nzima sasa kwenye nchi moja watashindwa? Usipende kukurupuka sana hasa kwa watu ambao huwajui, mna masaa ishirini na manne pekee ya kumkomboa kiongozi mkuu wa nchi. Kesho mchana kaonane na ndugu yako ukiwa kwenye sura tofauti na hiyo hautakiwi kujulikana kabisa kwa watu halafu baada ya kesho nitafute ni mhimu sana” alimaliza maelezo yake kisha akaangalia saa yake na kuingia kwenye gari ambayo ndiyo iliyokuja kunichukua kwangu na kupotea hayo maeneo.

Niliishia tu kuishuhudia gari hiyo ikipotelea kwenye barabara kuu, midomo yangu ilikuwa mizito kupita kiasi, mbele yangu nilikuwa nimepewa kazi ngumu mno ya kuweza kumlinda mheshimiwa raisi wa Tanzania ambaye sikujua nitamlinda vipi na kwa bahati mbaya sana tukio lilikuwa linaenda kufanyikia Ikulu, hakuna mtu ambaye ningemwambia hicho kitu akaniamini kabisa kwenye maisha yangu, nilitoa machozi na kukaa chini nilitamani sana kumsaidia raisi wangu mtu ambaye usalama wa nchi upo kuhakikisha yeye ndiye mtu wa kwanza anayekuwa salama kwa gharama yoyote ile na ndipo wangefuata wananchi.

Raisi atakufa kweli? Na mtekelezaji wa hilo tukio ni nani mwenye ujasiri wa kwenda kufanyia hilo tukio ndani ya Ikulu sehemu inayo lindwa kuliko kitu chochote kile kwenye nchi?.............29 natundika daruga uwanja umejaa maji ungana nami wakati ujao tena.

Bux the story teller
 
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA

TULIPO ISHIA SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE.......
“Nooooo haiwezekani haiwezekani, imewezekanaje yupo hai mpaka leo nooooooooooo” aliongea kwa hasira akiinuka na kupiga ngumi kwenye ukuta kwa hasira kali, akiwa kwenye huo mshtuko na hasira simu ya kwenye hicho chumba cha kamera ilianza kuita kwa fujo, ni kitu ambacho hawakukitegemea hata kidogo ni vipi mpigaji aliweza kujua kwamba huo muda wangekuwa hapo alfajiri hiyo na mapema sana, aliinua na kuipokea simu yake midomo yake ikiwa inatetemeka sana, hakuwa na imani na usalama wa hiyo simu.

ENDELEA.....................


“Muda huwa unaenda kwa kasi sana hapa duniani kama ilivyokuwa kawaida hauwezi kusimama, wiki tatu zilipita nikiwa napatiwa matibabu pale kitandani hatimaye niliweza kunyanyuka nikiwa kamili , yule mtu alitumia pesa nyingi sana kuhakikisha nasimama tena maana waliletwa madaktari bingwa kutoka nje za nchi ambao walinishughulikia wakati huo kiongozi wangu hakuwa akijua lolote kuhusu hayo ambayo yalikuwa yamenitokea kwa muda huo. Huenda ni miongoni mwa wanadamu ambao nilikuja kuwaheshimu zaidi kwenye maisha yangu yote, kwanza alinilindia siri kwa wenzake kwamba mimi ni usalama wa taifa kwa sababu kama wangejua basi wangenitafuta sehemu yoyote ile waweze kuniua, mpaka muda huo sikuwa na uwezo wa kumpatia mwanamke yeyote mimba kwa sababu sikuwa na sehemu ambazo zingenipa huo uwezo kwenye maisha yangu lakini sikuwa mchoyo wa fadhila kwa mwenyezi MUNGU kwa kunipendelea nafasi nyingine ya kuendelea kushuhudia ubaya wa ulimwengu, pumzi ndicho kiburi kikubwa sana kwa mwanadamu yeyote yule, ndiyo huwa inawafanya wanadamu wanakuwa jeuri mno ila ikifika siku ukiwa huna uwezo wa kuivuta hiyo pumzi vizuri upo kitandani malaika wa kifo anakung’ang’ania uondoke naye ndipo utakapo elewa thamani ya maisha ambayo unayachezea kwa sasa hapa duniani. Baada ya kuweza kusimama kwa mara nyingine tena nilifanya mazoezi kwa nguvu sana sikuhitaji kukutana na mkuu wangu kwa hali niliyokuwa nayo isingekuwa vyema kukaa naye kuongea ningeonekana mwanadamu dhaifu sana.

Wiki moja baadae nilijihisi kuwa vizuri sana hivyo nilifanikiwa kutoka kwenye hospitali ambayo nilikuja kugundua baadae kwamba ilikuwa ni nyumba ya mtu binafsi ambayo ilikuwa nje ya jiji kabisa, gari moja nilipewa na wale madaktari ambao walihakikisha usalama wangu, nikiwa ndani ya suti yangu nilirudi ndani ya jiji la Dar es salaam bila wasi wasi, mtu wa kwanza kuonana naye alikuwa ni mkurugenzi wa usalama wa taifa baada ya kupotea kwa zaidi ya mwezi mzima nilijua lazima watakuwa wamenitafuta sana.
“Ni mwezi sasa umepita haupo wala hauonekani ni kipi kimetokea huko ulikokuwa” baada ya kukutana na mzee yule hakuihitaji hata salamu yangu swali lake ndiyo ilikuwa salamu. Nilimsimulia kila kitu kilichokuwa kimetokea mpaka wakati huo, alinisikitikia sana mambo yaliyonikuta yalikuwa yanatisha sana ilihitaji moyo kuweza kuyamudu. Alishtuka sana baada ya mimi kumwambia Jonson Malisaba alikuwa akifanya kazi chini ya viongozi wakubwa wa serikali, ni kitu ambacho ilikuwa ni ngumu sana kwake kukiamini lakini ndio ulikuwa ukweli wenyewe alitamani sana akutane na Malisaba mwenyewe. Baada ya kutoka hapo maisha yaliendelea bila kuweza kuongea na baba yako ni mwaka mmoja ulikuwa umeisha, siku moja saa sita za usiku niliamua kuipiga ile namba ambayo alikuwa amenipa kwamba nikimhitaji muda wowote nitampata 911 niliipiga bila kusita kwa kutumia simu yangu ya mezani, simu moja kwa moja ilipokelewa kituo cha polisi sikuogopa kwa sababu hilo nilikuwa nikilijua mapema sana yalifuata maongezi ya kawaida tu kisha ikakatwa, dakika zaidi ya tano zilipita kukiwa kimya lakini haikuchukua muda simu yangu iliita niliipokea kwa wepesi mno.
“Hello” sauti yenye mgandamizo kutoka upande wa pili niliisikia majira hayo ya usiku wa manane kwa usahihi kabisa.
“Naomba tuonane” nilimjibu kwa ufupi kwa sababu ilikuwa ni hatari sana kuanza kutambulishana kwenye simu ni kitu cha hatari sana unaweza kukamatwa muda wowote ule.
“Toka nje ndani ya dakika saba kuna gari inakuja kukuchukua hapo” aliongea kwa msisitizo ila nilishangaa kwani nilikuwa naishi sehemu ya siri sana sasa sikujua amepajuaje
“Unajua nilipo mpaka useme nakuja kuchukuliwa” swali langu lilionekana la kipuuzi kwani alikata simu, nilitoka nje ili nijue kama hicho kitu ni cha kweli au alikuwa ananitania tu, nilishuka ngazi kwa wepesi nikatoka nje kweli sio muda niliona kuna gari nyeusi inafika hapo sikuwa na shaka niliingia ndani. Tulizunguka nyuma tu ya mtaa huo gari ikasimama kwa mbele alikuwa amesimama mwanaume ambaye alinipa mgongo ila nilimfahamu vyema nilitabasamu tu.
“Unaonekana kuwa mtu wa kutisha sana kama umefanikiwa kuweza kuijua sehemu ambayo ninaishi mtu kama mimi” niliongea huku nikiwa nasogea mahali alipokuwa akiendelea kuivuta sigara yake kubwa
“Haya maisha ni wajinga tu pekee ndio huwa wanajihisi wao wana akili kupita kiasi hasa pale wanapokuwa kati kati ya wajinga wenzao ila huwa ni tofauti kwa watu wenye akili sana kwao mjinga ndiye huwa anatumika kurahisisha kazi zao kupitia kujisifia kwake hivyo usije ukakaa ukajiona kwamba wewe unaishi kwa siri hata kidogo ni wajinga tu ndo wanajua hivyo ila kuna watu tunaweza kukupata muda wowote ule ambao tunataka sisi na hii ndiyo dunia tunayo iishi leo kila kitu kipo mkononi” alimaliza maelezo yake akinirushia kichupa cha pombe kali ambacho kwa kiasi fulani kingenipatia joto kutokana na upepo wa bahari uliokuwa ukivuma mpaka hayo maeneo.
“Hii ndiyo sababu serikali haiwezi kuwapata kirahisi sana watu kama nyie mna kila kitu cha kuwafanya muwe salama muda wote, kwa nchi hili jambo ni la kutisha kupita kiasi kama kuna raia tu wa kawaida wanaweza kuyafanya haya mambo bila vyombo vya usalama kujua inatishia amani ya nchi” nilimjibu huku nikikunja ndita kwa ukali wa pombe niliyokuwa nimepewa.
“Tatizo ni pesa, inapokuwepo pesa basi hakuna haki wala hakuna uzalendo, nchi haina pesa wanazishikilia watu wachache tu ambao wanafanikiwa kupata nafasi za juu unadhani kinatokea nini hapo, sisi tuna pesa nyingi sana, serikalini tuna watu wengi mno ambao ndio hao mnategemea waitengeneze nchi, mimi ukinikamata saivi baada ya saa moja tu baadae natoka nawewe unauawa unadhani ni kitu gani nchi itatufanya? Ujio wa pesa umebadilisha aina ya maisha ambayo wanadamu wa kawaida walitakiwa kuyaishi hivyo usipoteze muda sana kuwaza hilo jambo. Kesho ni siku ambayo unaenda kukutana na ndugu yako kwa mara ya kwanza tangu utoke nchini ni miaka sita nadhani imepita sasa, ni mwanajeshi sasa na ana nyota tatu kwa sababu yako tu kukubali kufanya kazi na serikali basi mwenzako naye anaishi vizuri kwa sasa, usijiulize nimejuaje nimekwambia hii nchi ipo kwenye mikono ya watu ambao wana uwezo wa kufanya jambo lolote lile na asiwepo mtu yeyote yule wa kuwazuia.

Hiyo siku ya kesho una kazi kubwa ya kulikomboa taifa lako kama ukishindwa basi hii nchi mtakuwa mmeikabidhi rasmi kwenye mikono ya watu ambao ninafanya nao kazi kwa sasa” maelezo yake yalikuwa yakinichanganya sana sikumuelewa vitu vyangu vingi namna ile ameweza kuvijua vipi ila nilifurahi sana moyoni kusikia ndugu yangu alikuwa na nyota tatu mpaka wakati huo ulipita muda mrefu sana bila kumuona wala kupata taarifa zake lakini hilo sikuliwaza sana kitendo cha kuniambia kwamba nilikuwa na kazi kubwa sana ya kulilinda taifa langu ndicho hicho kilichoweza kuniumiza kichwa sana huku yeye akiwa hana hata wasi wasi kwenye uso wake.
“Una maanisha nini kusema kwamba natakiwa nilikomboe taifa kwa mikono yangu mwenyewe?”
“Kesho raisi wa nchi anaenda kuuawa”
“Raisi anaenda kuuawa? Kivipi? Na nani anaenda kufanya hilo tukio?” maswali yalinitoka kwa mkupuo jasho likiwa linanitoka kwa kasi lakini yeye alikuwa anacheka sana
“Vipi unaogopa sana?” aliniuliza akiitupa sigara yake chini
“Unajua mimi nashindwa kabisa kukuelewa, uliniambia mheshimiwa raisi ndiye aliyekupa kazi ya kuisaidia nchi leo unaniambia raisi anaenda kuuawa nitakuamini vipi kwa hayo yote unayo yaongea?” nilimuuliza kwa hasira jina raisi huwa linapaswa kutajwa kwa heshima sana tofauti nayeye alivyokuwa akilitaja kiwepesi mno tena akisemea kifo cha mheshimiwa kwa urahisi sana namna hiyo
“Nadhani uliwahi kuathirika sana na madhara ya upigaji wa punyeto kwenye ukuaji wako hiyo michezo ni hatari kwenye kuwafanya watu kupoteza sana kumbu kumbu, kazi nilipewa na mkuu wa majeshi na ndiye aliye nikutanisha na mheshimiwa raisi ila hata hivi hilo halihusiani na kufa kwake” wakati huu sasa alinigeukia akionekana sura yake kuiweka kwenye hali ya usiriasi sana.
“Unamaanisha nini kuniambia hivyo”
“Nilikwambia unitafute mapema ukitoka kitandani lakini wewe ukapuuzia ni mwaka sasa ndo umenitafuta muda ukiwa umeenda sana, ungenitafuta mapema huenda hili ungekuwa umelizuia mapema sana kwa sasa sina imani sana kama utafanikisha ila jaribu kila linalowezekana kama utaweza kuifanya hiyo kazi. Huyu raisi aliyepo madarakani ni mtu ambaye anafanya baadhi ya mambo yetu kukwama hivyo kinacho fanyika ni kumtoa kwenye kile kiti na kumtoa kwake ni kumuua tu hakuna njia nyingine. Kesho majira ya saa nane usiku ndio muda ambao anatakiwa kufa kwahiyo kama mkishindwa kumsaidia mpaka muda huo keshokutwa asubuhi taifa litapokea taarifa mbaya sana hivyo ni kazi kwako wewe pamoja na wenzako wahini mapema kama mtalifanikisha hilo ila kumbuka tu kwamba wanao kuja kuifanya hii kazi ni watu wa kutisha na ni hatari mno” baada ya maelezo yake alianza kuondoka.
“Itakuaje kama hilo jambo litafanikiwa kukamilika?” swali langu lilimfanya akageuka tena pale nilipokuwa.
“Vyombo vya usalama mtakuwa kwenye hatari kubwa sana kwa sababu mtaonekana hampo makini na kazi yenu mpaka mheshimiwa raisi anauawa mkiwa mpo jiandaeni kwa hilo”
“Hili tukio limepangwa kufanyikia wapi? ili ikiwezekana ratiba zote za mheshimiwa ziweze kuvunjwa hiyo kesho”
“Bahati mbaya sana hata kama ungeipata nafasi huna hiyo nguvu ya kuweza kuzifuta ratiba za mheshimiwa raisi kwa nafasi uliyo nayo kumbuka umeingizwa kwenye usalama kiholela hivyo haujulikani. Hilo tukio linaenda kufanyikia ikulu”
“Haiwezekani, hakuna binadamu anayeweza kulifanya hilo tukio ndani ya ikulu hata kama angekuwa nani, hiyo ndiyo sehemu inayo lindwa zaidi kwenye ardhi hii inawezekana vipi raia afanye hilo tukio kule”
“Mhhhhhhhhh, hauna hata miaka mingi kwenye hiyo kazi ndo kwanza unaanza hiyo jeuri ya kupinga hicho kitu unaitolewa wapi? watu wanaiba mpaka benki kuu ya dunia ambayo ndiyo sehemu unapo hifadhiwa utajiri wa dunia nzima sasa kwenye nchi moja watashindwa? Usipende kukurupuka sana hasa kwa watu ambao huwajui, mna masaa ishirini na manne pekee ya kumkomboa kiongozi mkuu wa nchi. Kesho mchana kaonane na ndugu yako ukiwa kwenye sura tofauti na hiyo hautakiwi kujulikana kabisa kwa watu halafu baada ya kesho nitafute ni mhimu sana” alimaliza maelezo yake kisha akaangalia saa yake na kuingia kwenye gari ambayo ndiyo iliyokuja kunichukua kwangu na kupotea hayo maeneo.

Niliishia tu kuishuhudia gari hiyo ikipotelea kwenye barabara kuu, midomo yangu ilikuwa mizito kupita kiasi, mbele yangu nilikuwa nimepewa kazi ngumu mno ya kuweza kumlinda mheshimiwa raisi wa Tanzania ambaye sikujua nitamlinda vipi na kwa bahati mbaya sana tukio lilikuwa linaenda kufanyikia Ikulu, hakuna mtu ambaye ningemwambia hicho kitu akaniamini kabisa kwenye maisha yangu, nilitoa machozi na kukaa chini nilitamani sana kumsaidia raisi wangu mtu ambaye usalama wa nchi upo kuhakikisha yeye ndiye mtu wa kwanza anayekuwa salama kwa gharama yoyote ile na ndipo wangefuata wananchi.

Raisi atakufa kweli? Na mtekelezaji wa hilo tukio ni nani mwenye ujasiri wa kwenda kufanyia hilo tukio ndani ya Ikulu sehemu inayo lindwa kuliko kitu chochote kile kwenye nchi?.............29 natundika daruga uwanja umejaa maji ungana nami wakati ujao tena.

Bux the story teller
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA THELATHINI

TULIPO ISHIA SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA..........

Niliishia tu kuishuhudia gari hiyo ikipotelea kwenye barabara kuu, midomo yangu ilikuwa mizito kupita kiasi, mbele yangu nilikuwa nimepewa kazi ngumu mno ya kuweza kumlinda mheshimiwa raisi wa Tanzania ambaye sikujua nitamlinda vipi na kwa bahati mbaya sana tukio lilikuwa linaenda kufanyikia Ikulu, hakuna mtu ambaye ningemwambia hicho kitu akaniamini kabisa kwenye maisha yangu, nilitoa machozi na kukaa chini nilitamani sana kumsaidia raisi wangu mtu ambaye usalama wa nchi upo kuhakikisha yeye ndiye mtu wa kwanza anayekuwa salama kwa gharama yoyote ile na ndipo wangefuata wananchi.

ENDELEA...........................


“Nina imani tayari ulishanijua na unanisikia vizuri sana mzee hivyo haina haja ya kuzunguka sana kwenye hili, mwanao yupo kwenye mikono yangu sina shida naye sana japokuwa dharau zake ndizo zimemponza mpaka yamemptokea haya, miaka kadhaa nyuma alionekana kunitafuta sana kitu ambacho kilifanya mpaka amuue rafiki yangu na kufanikiwa kunipiga risasi moja kwenye mwili wangu, sikuwahi kumuona baada ya hiyo miaka miwili nimemtafuta sana na kwa bahati mbaya alikuwa akitumia miili ya vijana wenye njaa wa mtaani kwa kuwatengenezea sura za bandia ili yeye awe salama, kushindwa kwake kunijibu maswali yangu marahisi sana ndiko kumempelekea yeye kuishia kuwa kwenye hii hali ambayo sikupenda sana tufikie huku lakini nimekuwa sina namna zaidi ya kuyafanya haya kwa mtu ambaye ameonekana kuwa hatari sana kwangu. Sasa mimi nahitaji tuonane ndani ya dakika tano zijazo maswali yake uyajibu wewe hapo vinginevyo likiisha lisaa limoja kabla hajapatiwa matibabu hatakuwa na nafasi ya kuwa hai tena kwa hali aliyokuwa nayo mpaka sasa, uamuzi ni wako kuamua kuyaokoa maisha ya mwanao au kuyaacha yateketee ndani ya dakika tano naisubiri simu yako baada ya hapo hautanipata hewani tena nadhani umenielewa vizuri sana” sauti nzito ndiyo iliyokuwa inasikika kwenye simu ambayo ilikuwa ipo mkononi mwa waziri mkuu akiwa anatetemeka sana, alibahatika kupata mtoto mmoja tu kwenye maisha yake, mkewe alikuwa amemuusia sana kumtunza mtoto huyo kwa nguvu zake yote na kwa gharama yoyote ile.

“Pumbavu sana, hivi ni nani ambaye kwenye hii nchi anaweza kuwa na huo uwezo wa kujiamini mpaka kufikia hatua ya kunitishia mimi bila kuwa na uoga wowote ule juu ya kile ambacho kinaweza kumtokea yeye na familia yake? Kama nikimkamata hakuna hata chembe ndogo ya familia yake itabaki hai amepita kwenye mikono yangu mwenyewe leo hii anakuja kunitishia hadi mimi hahahahaha nitamfanyia kitu kibaya sana” makamu wa raisi alikuwa anaongea kwa hasira sana akiwa ameikunja sura yake baada ya simu kukatwa, alichukia sana kijana ambaye hakuwa mgeni kwake kuwa na ujasiri wa kuweza kumpigia simu na kumtisha huku akimpa dakika kadhaa za kuweza kufanya maamuzi ya kukutana nae vinginevyo alikuwa anaenda kumpoteza mwanae wa pekee Ashrafu Hamad, alikuwa mwenye hasira mno alirudi kwenye marejeo ya zile video akihitaji kujua ni kipi kilikuwa kimetokea mpaka mtoto wake akamatwe kizembe sana namna hiyo. Video ilikuwa inaonyesha kwa usahihi tukio tangu Alexander anaingia humo ndani mpaka muda ambao Ashrafu aliwakataza walinzi wake kuingilia huo ugomvi alisikitika sana mzee huyu kwa sababu mtu ambaye mwanae alikuwa anang’ang’ania kupigana naye yeye alimjua vyema sana hakuwa mtu wa kawaida hata kidogo na mpaka muda huo alikuwa anashangaa imekuaje mpaka mtu huyo yuko hai na anaishi.

Mapigano ambayo yalifanyika hapo ndani na namna mwanaume huyo alivyofanikiwa kukwepa risasi za zaidi ya walinzi 12 iliwafanya hata mlinzi wa makamu wa raisi mwili kumsisimuka, mwanaume huyo alikuwa anayajua mapigano kama aliyatengeneza yeye hakuwa na roho ya huruma kabisa kwenye mishipa yake tukio la kutisha lilipita kwenye macho ya makamu wa raisi wakati visu viwili vikipitishwa kwenye mkono wa mtoto wake na kumfanya kupiga kelele sana akihitaji msaada lakini hata walinzi wake hawakuwa na msaada tena baada ya kuweza kuachiwa sumu kali moshi ulijaa humo ndani kiasi kwamba hata kamera hazikuwa na uwezo wa kuchukua matukio hayo tena moshi ulipokuja kuisha hapakuwa na mtu yeyote ambaye alikuwa akionekana hapo. Makamu wa raisi aliipiga kwa ngumi skrini ndogo ambayo ilikuwa inasaidia kuonyesha matukio yote kwenye hizo kamera za ulinzi humo ndani kwa hasira na kuipasua.

“Bosi kwani huyu mtu unamjua?” swali lilitoka kwa mlinzi wake baada ya kuhisi kama hao watu walikuwa wanajuana hivi
“Huyu tumemtengeneza mwenyewe kwa mikono yetu, sio mtu wa kuombea kukutana naye kirahisi sana kwenye maisha yako hana ubinadamu pale alipo, mpaka sasa huwa tunajua alishakufa kwa sababu aliuawa nikiwa naona kwa macho yangu sasa mpaka leo nashangaa yupo hai ni kitu ambacho kinanipa wakati mgumu sana kuamini hili tukio kama ni la kweli au mimi ndiye nipo ndotoni” maelezo yake yalimfanya mpaka mlinzi wake ahisi kuchanganyikiwa inakuaje mtu ambaye umemshuhudia anauawa leo hii umshuhudie yupo hai tena wa afya tele hiki kitu huwa kinatisha sana na kwa mwanadamu mwenye roho nyepesi ya kawaida huwa hawezi kuhimili haya mambo. Aliinyanyua simu na kupiga hiyo namba ambayo muda sio mrefu alitoka kuongea nayo.

“Nije wapi?” aliongea kwa jazba akiwa na hamu ya kumtia Alexander kwenye mikono yake ili aweze kujua aliponaje na aweze kumuonyesha ni wapi ambako alikuwa amemhifadhi mtoto wake.
“Ukitoka nje ya huo mlango wa hiyo nyumba piga hesabu hatua tano kisha kunja kulia ukitembea hatua kumi simama nitakufuata ulipo, hakikisha unakuja wewe mwenyewe nataka tuzungumze kwa kina tukiwa wawili tu ukienda kinyume na hilo utakikuta kichwa cha mtoto wako” maelekezo hayakuhitaji kuelezewa sana moja kwa moja yalikuwa yanaeleweka kwa usahihi sana. Mheshimiwa makamu wa raisi alianza kutoka nje ya hicho chumba kwa mwendo wa haraka sana alihitaji kuyasaidia maisha ya mwanae kwa namna yoyote ile, mlinzi wake hakuwa tayari kuona hilo jambo linatokea kwa sababu kama mtu huyo angepata tatizo yeye ndiye ambaye angepaswa kuieleza serikali ni kipi kimetokea alianza kumfuata nyuma lakini alipewa ishara ya kuto mfuata mzee huyo.

“Mzee ni hatari sana kirahisi namna hiyo kwenda kwa mtu ambaye tayari alisha onyesha kila dalili za kuwa sio salama kwa maisha yako mimi siwezi kuruhusu hilo” mlinzi wake aliongea kwa msisitizo akionekana wazi hakuwa tayari kuruhusu hilo jambo lifanyike lakini alikatwa jicho kali mno na mzee huyo ambaye aligeuka na kuanza kutoka humo, mlinzi wake alikimbia kwa spidi akauweka mkono wake mbele ya makamu wa raisi huyo

“Bosi hatuwezi kukuruhusu kwenda huko nje bila kuhakiki usalama ambao utakuwepo huko hata kama ukit….” Hakumalizia sentensi yake alipigwa kofi moja kali kwenye shavu lake hata hivyo hata hakutikisika kilikuwa kitu cha kawaida mno kwake.

“Hivi wewe mpuuzi unaelewa hata nini maana ya familia wewe? ulishawahi kuwa na mtoto wewe? au unaropoka tu hapa vitu ambavyo huvielewi, hujui lolote kuhusu uchungu wa familia hapo ulipo unawaza tu ukidhani hayo mabunduki kila muda yanaweza yakatatua kila tatizo, huyo mtu mwenyewe ambaye yupo huko unamjua au unaropoka tu, nitokee mbele yangu nisije nikakupiga risasi bure unahisi mimi naweza kuuawa kirahisi sana kama unavyo fikiria hivyo mpuuzi wewe” aliongea kwa hasira sana mheshimiwa baada ya kuona mlinzi wake huyo haelewi maumivu yoyote yale pale mtu anapogusiwa familia yake anayo ipenda sana, aliyafuata maelekezo kwa usahihi sana na hatimae alifanikiwa kufika alipokuwa ameambiwa. Mbele yake chini ya mti ambao ulikuwa una majani marefu kiasi kwamba ukiwa mbali huwezi kuona kilichopo hapo chini ndani ya geti la nyumba ya mwanae ndipo alipo muona mtu akiwa anakizungusha kisu chake, Alexander alijisogeza mbele kidogo alicho kiona hakuamini hata kidogo hakuwahi kufikiria kama huyo mtu ndiye baba wa huyo mtoto ambaye mpaka muda huo alikuwa mkononi mwake, ni muda mrefu sana amemtafuta mtu huyu na hakujua ni lini atapata bahati ya kukutana naye maana moyoni alikuwa na kisasi naye kizito sana ila leo alikuwa yupo mbele yake uamuzi ulikuwa ni wake ni nini akifanye kwa mtu huyo japo sio kazi nyepesi kama inavyoweza kufikirika kirahisi.


Nilichanganyikiwa sikujua ni nani nitamfikishia ile habari akawa na uwezo wa kunisikiliza, hakuna mtu ambaye ungemwelekeza kwamba raisi anakuja kufia Ikulu akakuelewa kirahisi, sikuwa na namna nilienda kwa mkurugenzi wa usalama wa taifa ambaye ndiye alikuwa mlezi wangu nilikuwa nina imani kwamba ndiye mtu ambaye angeweza kunisikiliza. Nilikutana naye na kumweleza kile kitu kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu niliona mzee yule akiyapuuzia maneno yangu nilimsisitiza sana kwamba hicho kitu kilikuwa cha kweli aliishia tu kuniambia kwamba nikapumzike tu hakuna binadamu ambaye alikuwa na huo uwezo wa kufanya tukio kama hilo, sikuwa na cha kufanya ukizingatia kwa wakati ule hakuna watu wengi ambao walikuwa wananifahamu nilikuwa agenti wa siri sana nilirudi nyumbani kwangu kinyonge sana nikiwa najua wazi mheshimiwa raisi alikuwa na maisha mafupi sana maana nilisisitiziwa kwamba kama tungepuuza ilikuwa ni lazima afe.

Jioni ile nilikuwa nimekaa kwangu nikiwa naangalia televisheni yangu wakati huo raisi huyo alikuwa ana mkutano na waandishi wa habari kuweza kuongea na wananchi wake kwani ulikuwa umepita muda mrefu sana bila kuongea na watu wake hao, alikuwa kipenzi cha watu na wengi walikuwa wakimtakia maisha mema kiongozi yule niliamua kuizima na kwenda kujipumzisha kitandani kwangu machozi yalikuwa yananitoka, nilijua wazi tunaenda kumpoteza mheshimiwa raisi kizembe sana kwa sababu hakukuwa na mtu ambaye aliyachukulia maanani maneno yangu, niliinua simu yangu na kumpigia tena simu mkurugenzi lakini jibu lake lilikuwa ni lile lile, nilichanganyikiwa siku hiyo sikukumbuka hata kwenda kumuona ndugu yangu ambaye ilikuwa imepita miaka sita bila kuonana. Nilipitiwa na usingizi nilikuja kushtuka majira ya saa tisa na nusu usiku moyo ulinienda mbio sana baada ya kukumbuka saa nane ndio muda ambao mheshimiwa raisi alikuwa anatakiwa kuuawa, nilikurupuka kitandani nikaiwasha televisheni yangu ila nilisikia milio ya gari za polisi nje zikiwa zinapishana kwa kasi sana, niliiangalia simu yangu ilikuwa na simu nyingi sana ambazo zilikuwa zimeingia kutoka kwa kiongozi wangu huyo niliinyanyua na kuipiga ambayo haikuchukua muda ilipokelewa nilikuwa nikitetemeka kwani sikuhitaji kukisikia kile ambacho nilikuwa nikikifikiria kwenye maisha yangu, alipokea simu akionekana wazi ni mtu aliye changanyikiwa sana alinihitaji nifike ikulu mara moja nilishituka sana kuambiwa hivyo kwa mara ya kwanza nilikuwa naenda kutia mguu wangu kwenye sehemu takatifu zaidi ndani ya nchi.

“Nilitoka nje haraka sana sikutaka kutumia gari yangu nilitembea kwa mguu kwa mbele kidogo nilibahatika kupata boda boda ambayo ilibidi nimuelekeze kupitia vichochoroni ili kuweza kutokea ilipokuwa ikulu hiyo ya nchi, alikuwa na wasi wasi alitulia baada ya mimi kumuonyesha kitambulisho safari ikaanza, wakati tunakaribia kufika karibu na maeneo ikulu ilipo tulipishana na msafara wenye gari zaidi ya ishirini za ikulu zikiwa kwenye mwendo mkali mno njia zote zilizuiliwa hakuna mtu yeyote ambaye alikuwa anaruhusiwa kukatiza popote pale. Nilishuka na kumsihi boda boda yule atafute sehemu ya kujihifadhi asije akaonekane muda huo ingekuwa ni hatari sana kwake ule muda, nilimlipa pesa ngingi sana kisha nikaondoka, kwenye geti kuu la kuingilia Ikulu kulikuwa na ukaguzi wa kutisha ila kwa mimi nilishangaa baada ya kuonyesha tu kitambulisho sikukaguliwa kabisa nadhani taarifa yangu ilikuwa imefika kule mapema, kuna mtu alinipa ishara ya kidole nimfuate basi nilinyoosha kwenye jengo moja kubwa sana ambalo lilikuwa limejengwa kwa ustadi mno nilikuwa naishangaa sana ikulu ilivyokuwa sehemu nzuri mno, panalindwa sana kiasi kwamba hata sisimizi hawezi kukatiza bila kuonekana, tuliipita kordo moja ambapo ndani watu walikuwa na heka heka kibao wakiwa wamevaa nguo za usalama, tulipishana na mrembo mmoja ambaye alikuwa mapokezi aliniangalia sana lakini sikuwa na muda naye nilielekezwa mlango wa kuingilia kwenye chumba kimoja.

Baada ya kuingia nilifanikiwa kumuona kiongozi wangu ambaye alikuwa kama vile amechanganyikiwa, vitu vilikuwa vimevurugwa sana mle ndani
“Mzee” alishtuka baada ya mimi kumuita na kumpa heshima kwa kuinama sikuwa nikijua chochote mpaka muda huo aligeuka machozi yakiwa yamejaa kwenye macho yake.

“Ooooh damn it…. Mr President…… oooh my God” aliongea kwa sauti ya ukali akikaa chini, sikuwahi kumuona kwenye hali kama hiyo hata siku moja nilijua kutakuwa na tatizo kubwa sana

“What happened to Mr President (nini kimetokea kwa mheshimiwa raisi)?” swali langu lilikuwa zito sana kunijibu alitumia zaidi ya dakika tano ndipo akaufungua mdomo wake.

“He is no more (amekufa)” ……… Nani ameweza kufanya hili tukio sehemu yenye ulinzi kama hii kirahisi sana namna hiyo kumuua kiongozi mkubwa zaidi wa nchi tena akiwa ikulu?........ Alexander alifanikiwa kulipa kisasi chake kwa makamu wa raisi na kisasi chake kimetokana na nini?

Binafsi sina la ziada kwenye sehemu ya 30 sehemu zifuatazo zitatupa majibu zaidi ya nini kinajiri kwenye tamthilia moja nzuri sana ya kusisimua.

Langu jina naitwa Bux the

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA THELATHINI NA SABA

TULIPO ISHIA SEHEMU YA THELATHINI NA SITA........
Leonard Makachi ndilo jina lake mzee huyu, huyu ndiye mtu ambaye alikuwa ni mkurugenzi wa usalama wa taifa ambaye ndiye aliye mlea Timotheo Jordan baada ya kumuokota kwenye uoshaji wa magari na kumtengeneza kuwa jasusi mkubwa sana ndani ya Tanzania, alifungwa jela kwa kosa la uzembe mkubwa sana ambao aliufanya kuruhusu raisi kuuliwa ndani ya ikulu ambapo tukio hilo lilitekelezwa na kijana ambaye alifahamika kwa jina la Alexander akiwa na miaka 21 tu kwa wakati huo.
ENDELEA.................................

Kwenye chumba kimoja kikubwa sana ambacho kilikuwa na Meza moja tu pekee ndefu sana ambayo ilikuwa na viti viwili ikimaanisha ni watu wawili tu ndio waliokuwa wanahitajika kuwepo ndani ya hicho chumba, taa moja yenye mwanga hafifu sana ndiyo ilikuwa ikionekana juu ya hiyo meza kitu ambacho ingekuwa ni vigumu sana mtu wa upande mmoja kumuona kwa usahihi mtu ambaye angekuwa upande wa pili yake, upande wa kulia alikuwa amekaa mwanaume mmoja ambaye hakuwa mnyonge kwenye mwili wake alionekana ni mtu imara sana miwani yenye rangi nyeusi ikiwa sehemu ya kuupamba uso wake, Julius Makasi ndilo jina lake mtu huyu. Ni masalia na ndo pekeyake ambaye alifanikiwa kutoka akiwa hai ndani ya Buguruni siku ambayo walipewa kazi na wenzake ya kwenda kumuua ama kumchukua Timotheo Jordan lakini ilivyo shindikana kuna watu walitokea na kuwaua wenzake wote pona pona yake ni baada ya kuingia kwenye tenki kubwa la maji ambapo alipigwa risasi mbili kwenye mwili wake ambapo alitoka akiwa na hali mbaya mno lakini baadae alikuja kusaidiwa na mtu ambaye hata yeye mwenyewe hakuweza kumjua kabisa kwamba alikuwa ni nani.
Akiwa hapo alikuwa anakumbuka matukio mengi sana ambayo yalimpata kwenye maisha yake mwili ulimsisimka mno kwa namna alivyoweza kupona kwenye tukio lile, MUNGU alikuwa upande wake na hilo alilithibitisha bila kipingamizi chochote, mlango wa hicho chumba ulifunguliwa kisha akaingia mtu mwembamba mrefu ambaye alionekana akiwa na miwani yenye mwanga mkali kidogo hata hivyo alikuwa haonekani kutokana na kuvaa kwake nguo nyeusi ndani ya mwili wake, mlango ulifungwa kisha akaketi baada ya kuilegeza tai yake kwa usahihi.
"Habari yako bwana Julius" alijikoholesha kidogo kisha akaufungua mdomo wake kwa ustaarabu usiokuwa na haraka ndani yake.
"Ni vizuri kama tukienda moja kwa moja kwenye pointi ya msingi iliyokufanya mpaka uniite hapa muda huu" aliongea kwa kujiamini sana huyu mwanaume maisha aliyokuwa ameyapitia yalimfunza kuwa mtu imara ambaye hakuwahi kutetereka kwa kumhofia mwanadamu mwenzake yeyote yule.
"Kwa sasa nina imani utakuwa umepona vyema sasa na unaweza kufanya kazi kwa usahihi" hiyo kauli ilimshtua kidogo, mtu aliyekuwa anaongea naye alionekana kwamba anamjua kwa usahihi sana ndio sababu aliweza mpaka kumwambia siri yake hiyo.
"Sina kumbukumbu kama tulishawahi kuonana kabla lakini unaonekana kunifahamu vizuri sana" kauli yake haikujibiwa zaidi ya mtu huyo kusimama na umeme ukawaka humo ndani kitu ambacho kilimfanya Julius ashangae sana, ilikuwa ni mara ya pili anaiona hiyo sura mbele yake, hawezi kuisahau kabisa ni muda mrefu kidogo umepita lakini alikumbuka waliwahi kukutana hospitalini akiwa hana hata uwezo wa kunyanyua mguu wake, mtu huyo alimuahidi kwamba angerudi siku akiwa amepona mpaka hapo hakuwa na swali lingine juu ya hilo alihitaji kumjua huyu mtu anahitaji nini kwake alikuwa anaelewa vizuri msaada huwa hauendi bure lazima Kuna vitu alitakiwa kuvilipa.

"Malipo gani unayahitaji kwangu?" Swali lake lilipuuziwa sana badala ya kujibiwa waliingia wanaume wanne humo ndani.
"Kill him" ndio kauli ambayo mtu huyo aliitoa kwenye mdomo wake, ni mwanadamu ambaye alikuwa anaaminika sana kwenye macho ya kila mtanzania, ni mtu ambaye kila mtu alikuwa anajua kwamba yupo pale kwa sababu ya kuilinda sheria lakini huenda macho huwa ni kitovu cha kuwalaghai wanadamu wengi sana, Mwanasheria mkuu wa nchi ya Tanzania ndiye mtu ambaye alikuwa yupo humo ndani na ndiye ambaye alitoa hiyo amri ya kuuawa kwa Julius Makasi, mpaka sasa mwanaume huyo ni mtu mmoja pekee ambaye alikuwa amebahatika kumuona sura yake Alexander pekeake lakini wengine walikuwa wakikutana na sura tofauti kabisa hivyo hakuna mtu ambaye angeweza kujua kwamba huyo mtu alikuwa ni Mwanasheria mkuu wa nchi.
Urefu wake na wembamba wake ukijumlisha na miwani aliyokuwa anaivaa kwenye macho yake vilikuwa vikiwaaminisha wengi sana kwamba huyu ni kiumbe dhaifu mno ila bahati mbaya sana hakuna aliyekuwa anaijua siri kubwa ya huyu mtu ambayo alishi nayo kwenye moyo wake. Julius alijua wazi hakuna namna ya yeye kuwa salama zaidi ya kujitetea vinginevyo alikuwa anauawa, wanaume wanne wenye visu vikali walikuwa mbele yake wakati anawahesabia vizuri alihisi kama shingo yake imevunjia ni kiatu safi cha mwanaume mmoja ambaye alikuwa amevaa suti safi kilipita na shingo yake alijishika kwa maumivu wakati huo mateke mawili yalipita kwenye tumbo lake uso ukipokea ngumi kali sana, wote walikuwa wakija pamoja kwa kumchangia alijuta kuingia kwenye hicho chumba, akiwa ameegamia ukuta anaisikilizia ngumi ya usoni ambayo iliivunja miwani yake aliona kisu kikiwa kimelenga jicho lake alikuwa na hasira mno baada ya kugundua alikuwa ameitwa humo ndani kuweza kuuawa, mikono yake ilikuwa imepona mifupa yake ilikuwa migumu mithili ya mtu anayebeba zege kila siku alikikwepa hicho kisu ngumi yake akiilenga kwenye mdomo wa huyo mtu aliyehitaji kumchoma kisu alipiga makelele baada ya kutema meno yake, visu vitatu vilikuwa vimemlenga na kuja kwake alitembea ukutani kwa nguvu akajirushia upande wa pili ambapo alipita na mkono wa mmoja wao aliuvunja bila huruma yoyote, akakiokota kisu ambacho mtu huyo aliyevunjwa mkono alikidondosha.

Wawili ambao walibakia hawakuwa kwenye mahesabu yake alijua kabisa hawamuwezi kwa chochote aliwachonganisha kwa kujifanya anaingia kati kati walivyo jisogeza mmoja wao alimpiga mtama kwa hasira akisindikiza na ngumi nzito tumboni kisha akajirusha kwa juu alijigeuza na kutua na teke zito kwenye paji la uso la aliyekuwa amebaki amesimama ambaye alipasuka kwenye paji la uso na kukaa chini.

"Stop" ilikuwa ni sauti kali ya mamlaka kutoka kwa Mwanasheria mkuu ambaye hakuna mtu alijua kama huyo ni yeye wafanyakazi wake wote walimzoea kwa sura tofauti sana mtu huyo, aliongea kwa sauti hiyo nzito huku akiwa amekidaka kisu mkononi mbele ya uso wake ambacho kilirushwa na Julius Makasi ili kuweza kummaliza mtu huyo lakini kilidakwa kwa namna ambayo kila mtu alishangaa kidogo kwa sababu walimjua mtu huyo ni mdhaifu mno wakati huo aliamua kusimamisha pambano hilo baada ya kuona mlinzi wake mmoja amemuweka Julius chini ya ulinzi akihitaji kumpiga na bastola kichwani.
"Tuacheni wawili nendeni nje" kauli yake ilikuwa ni amri walinzi wote walitoka wakikokotana kwani wengine walikuwa wamevunjika tayari.
"Kaa chini hapo" kauli yake ilimshangaza Julius ambaye bado alikuwa kwenye hasira Kali mno na mtu huyo ambaye sio muda alihitaji kumuua, hakumuamini tena alijikunja kwa sarakasi moja kali sana akiwa amepiga mahesabu ya kumpiga eneo la shingo mtu huyo kwa teke lake lakini alishangaa amepiga hewa na mtu huyo alikuwa amekaa hapo hapo kwenye kiti, maana yake ni kwamba alikuwa ni mwepesi hata karatasi inasubiri alimuangalia bila kummaliza mtu huyo ambae ni dhaifu mno kwa mwonekano wake ulivyo.
"Acha hicho unachotaka kukifanya huwa sipigani na watoto wadogo nisije nikakuua wakati nina kazi nawewe" maneno ya mtu huyo yalimpa hasira za kuzidi yeye kuitwa mtoto kwenye mapigano ilikuwa ni dharau kubwa sana ambayo asingeweza kabisa kuivumilia, alijiandaa kushambulia lakini kisu kilikuwa kipo singoni kwake hakuelewa mtu huyo amenyanyuka muda gani mpaka kumfikishia kisu hicho.
"Kwanini unataka kuniua?" Julius aliuliza kwa hasira
"Huwa sifanyi kazi na watu wazembe ungefanya ujinga ulikuwa unakufa kweli" maneno hayo yalimfanya Julius ameze mate kwa shida.
"Wewe ni nani hasa na unataka nini kwangu?" Aliuliza baada ya kuruhusiwa kukaa na mtu huyo kukitupa hicho kisu chini.
"Dunia inatisha sana siku hizi ni watu wenye pesa tu na akili ndio wanaishi vizuri bila shida yoyote ila ukikosa hivi vyote viwili basi unakuwa mwanadamu usiye na bahati zaidi kuishi Ulimwenguni msaada wako pekee itakuwa ni kulalamika ukihisi kwamba kulalamika ndiko kutakako kufariji kumbe ndipo unajichongeshea shimo ambalo hata wewe mwenyewe hutaweza kabisa kulikwepa. Nimetumia pesa zangu nyingi sana kuhakikisha unapona na kuwa salama sio kwamba sikuwa na kazi ya kufanyia hizo pesa mpaka nikazileta kwako ila hata wewe pia ilikuwa ni kazi ya kuzifanyia hizo pesa, ili kuweza kuzirudisha pesa zangu Kuna kazi moja ndogo sana ambayo nataka uifanye kwa siri kubwa sana baada ya hapo nitakuacha uendelee na maisha yako au utaamua wewe kama utahitaji kulipa kisasi kwa watu ambao walikupa kazi na wakataka kukuua kwa muda huo, hii ndio dunia yenyewe usishangae kwa hilo" Mwanasheria mkuu akiwa kwenye Sura ambayo hakuna mtu alikuwa anamtambua zaidi ya Alexander alimwambia haya maneno Julius yeye akiwa amekunja nne bila hofu.
"Wewe umeyajua vipi haya yote kwamba unafuatilia sana kila kinacho endelea nchini wewe ni nani hasa" swali lake halikujibiwa kwa maneno bali kwa vitendo, mtu huyo alijigusa kidogo shingoni kwake awamu hii sura hakuivua bali ilijibadilisha kwa kujivuta ya ndani ikaja nje na ya nje ikaingia ndani, Julius aliogopa sehemu ambayo wanadamu wenzake walikuwa wamefikia ilikuwa inatisha, sio rahisi sana mtu wa kawaida kufanya haya mambo hii ni teknolojia ambayo hata nchini bado haijaingia kabisa alijifuta jasho baada ya jambo hilo kukamilika na mbele yake alikuwa anamuona na kuiona sura halisi ya Mwanasheria mkuu wa nchi, haikuwa shida kubwa kuweza kumtambua kwani alikuwa ni mtu maarufu sana ndani ya nchi hususani kwenye harakati zake za kuweza kuwatetea watu wanyonge na kuwagandamiza vigogo ndivyo vilivyo mpa umaarufu zaidi.
"How is this possible Mr attorney general? (hili linawezekanaje mheshimiwa Mwanasheria mkuu?)" Julius aliuliza akiwa ameuacha mdomo wake wazi, mbele yake ilikuwa inakuja ndoto moja hivi ya kutisha sana ila alishangaa huo ni uhalisia sio ndoto Mwanasheria mkuu wa nchi iliwezakana vipi kuwa hii sehemu akionekana kumiliki watu wa kutisha namna hiyo.

"Hapa duniani hakuna kinacho shindikana ukiamua tu hata wewe leo unaweza kuwa Elon musk kama ukitaka unakuwa, rejea kauli yangu ya mwanzo nimekwambia watu hatari zaidi hapa duniani ni watu wenye pesa pamoja na watu ambao wanatumia sana akili kwenye maisha yao kwahiyo inatakiwa uombe sana MUNGU akupe hata kimoja kati ya hivyo basi wewe utaishi utakavyo mwenyewe ila kama ukikosa vyote utayaishi maisha yako yote ukiwa mtumwa. Hili sio mhimu sana lililo tukutanisha hapa kazi yako ambayo nataka uifanye nataka unitafutie mtoto mmoja hivi"

"Mtoto yupi?"

"Miaka kadhaa nyuma wakati kijana wangu ameenda kufanya mauaji kwenye familia moja huko mwanza alifanya makosa makubwa sana kuna mtoto mmoja wa kiume aliweza kusaidiwa na mtu mmoja ambaye nadhani saivi atakuwa amekufa hivyo kazi yako kubwa namhitaji huyo mtoto japo kwa sasa sio mtoto tena alishakuwa ni mtu mzima ni miaka mingi kidogo imepita" Mwanasheria mkuu aliongea bila kupepesa macho wala kuuma uma maneno yake yalikuwa yanaeleweka moja kwa moja kwenye macho ya mtu huyo.
"Lengo lako kubwa ni nini akisha patikana?" Alitabasamu sana mtu huyu Mwanasheria mkuu
"Nataka kuichukua hii nchi ila Kuna vikwazo vidogo vidogo naviona mbele yangu kwahiyo nahitaji niisafishe njia mapema, Kuna wajinga wamekaa mahali wanacheza michezo ya kitoto sasa nataka niitumie michezo yao kufanikisha malengo yangu kwa urahisi mkubwa mno"aliongea kwa kujiamini sana.
"Huyo mtoto unaye msema wewe anajua juu ya uwepo wako na malengo yako na anajua mtu aliye husika na hayo mauaji ya familia yake?" Julius bado alihitaji maelezo ta kutosha alielewa kama ametafutwa kufanya kazi lazima kulikuwa na ugumu kiasi chake kuifanikisha kazi hiyo hivyo alihitaji kuielewa vyema.
"Sina hakika sana kwani nilichelewa kupata taarifa hiyo ila lazima atajihaji kumjua mtu ambaye amefanya hicho kitu na kama atakuwa ana kumbukumbu vizuri basi atakuwa anakitafuta kichwa cha baba yake mpaka leo hilo linaweza likamfanya atambue uwepo wangu"
"Kichwa cha baba yake? Ina maana wewe ndiye ambaye unacho?"

"Huwa napenda sana maelezo mafupi mafupi ya kueleweka sipendi kupotezewa muda kwa vitu ambavyo ni vya kipuuzi mbele yangu, fanya nilicho kuagiza sio kuanza kunihoji hoji kama vile wewe ni usalama wa taifa, picha zake unaletewa za huyo kijana japo hatuna uhakika sana za mahali alipo maana picha zake zipo za utotoni, za ukubwani sina uhakika nazo sana hapo maelezo yanaonyesha kwamba kwa mara ya mwisho alipotea Dar es salaam kwa miaka kadhaa kisha akarudi na kukaa siku chache tu halafu akasafirishwa kwenda nje ya nchi kwahiyo nahitaji kujua haraka sana taarifa zake halafu uniletee huyo mtoto nina kazi naye" baada ya kumaliza Mwanasheria mkuu alijirudisha kwenye Sura yake ambayo huwa hatambuliki na kutoka nje bila kusubiri jibu kwani maswali ya Julius yalikuwa yakimkera mno aliamua kuondoka ili asije akamuua bure mtu huyo, kwa Julius alibaki anashangaa tu asielewe kinacho endelea huyo binadamu wengi walikuwa wakimjua na kumsifu kwa upole sana lakini alikuwa ni mtu wa kutisha mno.

Wenye akili ndio huwa washindi wa michezo yenye akili zaidi, huyu ndiye mtu ambaye alikuwa na kichwa cha Jonson Malisaba kwenye mkono wake huku akiwa amewaachia msala watu wengine wahangaike na hilo suala kisha yeye anakuja kula nyama tu mwishoni.
Ni mtu wa aina gani Mwanasheria mkuu? Mchezo gani anataka kuucheza kwa watu ambao amewaita ni wajinga? Julius atampata Jamal? Vip kwa Jamal itakuaje na yeye tayari amesha ujua ukweli wa maisha yake na kugundua kwamba Alexander ndiye mtu ambaye alikikata kichwa cha baba yake atamfanya nini huyu mwanadamu ambaye ndiye pekee aliyeweza kuingia ikulu na kutoka akiwa mzima wa afya? Kazi ya Black Widow ni ipi??

Naweka kalamu pembeni nakuacha ushuhudie huu mchezo unavyochezwa. 37 natia nanga tukutane wakati ujao.

Bux the story tellerView attachment 2384203

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Kwa shilingi 5000 tu isome hadithi hii mpaka mwisho kabisa sehemu ya 100 uweze kuiburudisha akili vya kutosha.

Namba za malipo ni

0621567672 (WhatsApp)
0745982347

Jina FEBIANI BABUYA

Ukituma pesa unatumiwa muda huo huo[emoji3578]

Wako

Bux the story teller

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
Kwa shilingi 5000 tu isome hadithi hii mpaka mwisho kabisa sehemu ya 100 uweze kuiburudisha akili vya kutosha.

Namba za malipo ni

0621567672 (WhatsApp)
0745982347

Jina FEBIANI BABUYA

Ukituma pesa unatumiwa muda huo huo[emoji3578]

Wako

Bux the story teller

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Kwa shilingi 5000 tu isome hadithi hii mpaka mwisho kabisa sehemu ya 100 uweze kuiburudisha akili vya kutosha.

Namba za malipo ni

0621567672 (WhatsApp)
0745982347

Jina FEBIANI BABUYA

Ukituma pesa unatumiwa muda huo huo[emoji3578]

Wako

Bux the story teller

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA

TULIPO ISHIA SEHEMU YA THELATHINI NA NANE........
"Kukiwa na tatizo la aina yoyote au msaada wowote nitafute muda wowote ule" maneno hayo yalimfanya Rashid aitikie kwa kichwa kuonyesha anakubaliana na hilo Jambo kisha mwanaume akapanda kwenye gari moja aina ya Land Rover na kutoka humo ndani kwa kasi kubwa mno, kazi yake rasmi ilikuwa imeanza ndani ya jiji la Dar es salaam akiwa ana mpango kwanza wa kumpata huyo mtu ambaye ndiye aliyeweza kukikata kichwa ya baba yake mzazi.
ENDELEA..................
Kwenye chumb kimoja chenye joto kali sana na kiza cha kutosha, dirisha moja dogo ambalo lilikuwa juu ya chumba hicho halikutosha kutoa mwanga wa kufanya kila kitu kiweze kuonekaka humo ndani. Kuna mtu alikuwa amekaa humo kwa takribani masaa sita akiwa hajui nini hatima yake, ni chumha ambacho kilifanya ajutie sana kuwepo wapo kwani hali yake ilikuwa haizoeleki hata kidogo. Dakika tano baadaye mlango ulifunguliwa wakaangia wanaume watatu wakiwa na miili iliyoshiba vyema, wawili walienda na kumnnyanyua mwanaume ambaye alikuwa amekaa hapo kwa muda mrefu sana na kwenda kumkalisha kwenye kiti cha chuma kisha wakamfunga vizuri.
"Unajua huwa sipendi sana kuzungushwa kwa sababu nina mambo mengi sana ya kuyafanya huko nje saivi unaweza kuniambia huyu mtu yuko wapi?" Mapande Dikson ndiye mwanaume ambaye alikuwa akiongea kwa sauti kubwa yenye mamlaka ndani yake akionekana kutohitaji kuzungushwa sana kujibiwa maswali yake, alikuwa ni mtu mwenye cheo kikubwa sana cha DCI akiwa yupo kwa ajili ya kupambana na makosa ya jinai nchini.
"Mtu gani huyo ambaye unamhitaji huku ukiwa umenifunga mikono kwamba wewe ni muoga sana au hahahahahahahaha" sauti ya dharau ilimfanya mtu huyo apigwe ngumi nzito kwenye mdomo wake huenda alijutia sana kujifanya kiburi kwa kumjibu kwa dharau mtu huyo.
"Mfungueni mikono yake haraka sana" aliongea huku akiwa anaikuja shati ya jeshi la polisi kwa wepesi mno
"Mkuu huyu ni mshtakiwa kivipi tumfungulie tena?" Vijana wake waliuliza wakiwa na mashaka ya kuweza kusababisha madhara kwa mtu huyo.
"Pumbavu sana nitawafukuza kazi sasa hivi nyie ndio watu wa kuanza kunipangia mimi cha kufanya?" Aliongea kwa ukali kiasi kwamba vijana wake walihofia wanaweza na wao wakachanganywa kwenye hiyo kesi kwani kiongozi wao walimjua vyema sana iliwalazimu kufanya kila ambacho walikuwa wameambiwa wakifanye.
"Haya sasa umefunguliwa mikono njoo upigane namimi" aliongea kwa dharau sana mikono yake ikiwa ipo nyuma, hakumhofia mtuhumiwa wake ambaye alionyesha tambo kwamba anahojiwa akiwa amefungiwa kumaanisha kwamba DCI alikuwa ni muoga sasa alikuwa amefunguliwa ili waongee kiume. Kijana aliyekuwa ameletwa hapo ni Rashid kijana wa Timotheo Jordan, haikueleweka sababu ya msingi mpaka kumkuta kwenye hiki kituo akiwa ndani ya selo kwa ajili ya mahojiano. Rashid hakuwahi kuwa mnyonge hata siku moja linapokuja suala la kucheza michezo ya ngumi mtu wa usalama wa taifa huyu wa siri sana na haikutakiwa mtu yeyote kutoka nje aweze kulitambua hilo, mikono yake ilikuwa na spidi kali sana alikuwa amemfikia Mapande Dickson teke lake lilimkosa kiongozi huyo wa jeshi la polisi na kubaraza kwenye ukuta mpaka ukatikisika mtu huyo alikuwa peku lakini miguu yake ilikomaa sana mpaka yeye mwenyewe alishangaa sana, Rashid alikuwa anarusha ngumi kwa nguvu ambapo tatu zilitua kwenye uso wa kiongoz huyo pua yake ilipasuka wakati anapepesuka alipigwa na kifuti kizito kwenye mbavu zake alicheka na kujinyoosha vizuri kisha akautoa mkanda wake kiunoni alielewa mtu aliyekuwa mbele yake alikuwa mzito hivyo naye alitakiwa kumchukulia kwa uzito huo huo.

Alizipanga ngumi zake mbili akiwa anauchezesha mguu, Rashid kama kawaida yake alijizungusha ticktaka moja ambayo Dickson aliikwepa kisha akarusha ngumi moja mithili ya jabali iliyotua kwenye kifua cha Rashid akacheua damu mwanaume huyo hakuweza kumpa nafasi alimchota mtama Rashid na kumpiga na ngumi zote mbili tumboni ambazo zilimpeleka kwenye nondo za humo ndani alijibamiza vibaya sana mgongoni kabla hajajinyanyua alipigwa na teke la kichwa aliona dunia inazunguka zaidi ya mara mia saba ila haikuwa hivyo kilikuwa ni kipigo kutoka kwenye mguu ulioshiba mno, Dickson alikuwa anampiga kwa hasira sana kijana huyo hakuwa level zake kabisa kwenye mapigano ilifika hatua mpaka vijana wake wakaenda kumushika kwa sababu alikuwa anaenda kumuua kwa hasira alizokuwa nazo.
"Mjinga mkubwa wewe yaani nakuuliza maswali unanijibu mimi jeuri" aliongea macho yake yakiwa yana rangi nyekundu tayari alimnyanyua Rashid akiwa amezimia na kumkalisha kwenye kiti ambapo alimmwagia maji ya baridi sana yenye barafu ambayo yalimzindua kutoka kwenye usingizi mzito, kichwa chake kilikuwa kizito mno mbele yake alikuwa anaona wanaume wawili wawili. Baada ya kutulia mbele ya uso wake kulikuwa na picha ya watu wawili Timotheo Jordan pamoja na Jamal ambayo walipigwa na kamera za usalama siku ya kwanza tu wanavyo ingia kutoka ndani ya Kyela kuingia Dar es salaam.
"Huyu mzee kwenye hii picha unamfahamu?" Rashid alikuwa anaulizwa wakati shingo hake ikiwa imekamatwa kikakamavu sana
"Hapana simjui" jibu lake lilimfanya mtu huyo achukua mkasi ambao ulikiwa upo pembeni yake aliuzamisha kwenye paja la Rashid ambapo alipiga kelele za kuomba msaada lakini hakukuwa na mtu yeyote yule ambaye alikuwa anamjua wa kumsaidia kwenye maisha yake, kufa kwa Timotheo Jordan kulimfanya kukosa tumaini la kuwa na mtu yeyote yule mwingine wa kuyajali maisha yake.

Wakati tukio hilo linaendelea humo ndani nje ya kituo kikubwa cha polisi kwa Dar es salaam OSTERBAY POLICE STATION kuna gari moja aina ya Land Rover ilipaki kwa nje akashuka kijana mmoja ambaye alikuwa ana suti ndani ya mwili wake, hakuonekana kuwa mtu wa kuvaa sana suti kwani tai iliyokuwa shingoni mwake ilimfanya ahisi inamsumbua sana japo tai ilimpendeza sana, ni kijana wa mdogo tu wa takribani miaka kama ishirini na mitatu au minne hivi, alionekana kuwa mgeni ndani ya hizo ofisi akaulizia kwa askari mmoja ambaye alikuwa anatoa heshima kila muda baada ya kujua huenda kijana huyo alitoka mwenye familia yenye ukwasi sana. Moja kwa moja alinyoosha mpaka kwenye ofisi ya mkuu wa kituo hicho kikubwa cha polisi.
"Habari ya kazi mzee wangu" aliongea huku akiwa anaangaza kwenye ofisi hiyo ambayo aliona wazi vitu vilipangwa hovyo hovyo tu kuonyesha kwamba mtu aliyekuwa humo ndani hakuwa akijali chochote juu ya hicho chumba.
"Nikusaidie nini kijana" aliongea huku akiwa amegeukia upande wa pili akiwa na gazeti mkononi mwake
"Mhhhhhh hivi ndivyo mnavyoweza kuwahudumia watu hapa sio" kauli yake ilimfanya mkuu wa kituo hicho ageuke na kumwangalia kijana huyo ambaye kwake alikuwa ni mdogo sana kwa hasira mno aliongea
" We mpumbavu usitake nikutie ndani muda huu acha kunipigia kelele kama huwezi kuelezea kilicho kuleta hapa naomba utoke ofisini kabla sijakupatia kesi hapa, mwanaume mzima umekalia kulalamika lalamika kama mtoto wa kike si ukaolewe huko" haya ndiyo maisha halisia kwenye sehemu kama hizi watu ambao wamepewa mamlaka makubwa ya dola huwa wanayatumia kwa manufaa yao binafsi bila kujali shida zozote zile wanazo zipitia watu.
"Naitwa Lenovatus Jonson nina ndugu yangu hapa ambaye kwangu ni kama kaka anaitwa Rashid nasikia amekamatwa sasa nimekuja kumchukua kwa sababu hakuna kosa lolote lile ambalo ameweza kulifanya, kwa leo nitahesabia kwamba ni makosa madogo madogo ambayo yameweza kufanyika ila kama kitu kama hiki kitakuja kujirudia tena sidhani kama nitakuja kama nilivyoweza kuja hii leo" baada ya kumaliza maneno yake mkuu wa kituo alitaka kutoa bastola ili amuweke mtu huyo chini ya ulinzi lakini alisita baada ya mtu huyo kumuonyesha kitambulisho chake, kitambulisho chake kilikuwa kikubwa sana alikuwa ni komando wa ngazi za juu sana serikalini mzee huyu alielewa watu hao huwa hawaonekani mara kwa mara maana yake mpaka amefika hapo ilikuwa ni ishara mbaya sana, alijifuta jasho alikuwa anakosa kazi kama hilo jambo lingefika kwa IGP aliogopa mno akiwa anatetemeka alitaja namba ya selo ambako ndiko Rashid alikuwa amefungwa, Jamal alikuwa na hasira sana baada ya kutamkiwa maneno ya kashfa na mtu huyo ila alijitahidi kuvumilia ili mambo yaende kwa uharaka sana hakuhitaji kuwasumbua watu ambao walikuwa wamekuja hiyo sehemu kwa shida zao aligeuka na kuanza kutoka humo ndani baada ya kufika mlangoni aligeuka akamtazama mzee huyo kwa umakini sana
"Nadhani hili halijaishia hapa nitakutafuta tuongee vizuri" Jamal aliacha maneno ambayo yalimuweka kwenye hali mbaya kiongozi wa kituo ya Osterbay huyu, hawa watu huwa anawajua vizuri sana ukiingia kwenye 18 zao nafasi ya wewe kupona huwa ni ndogo sana. Safari ya Jamal ilimpeleka mpaka karibu na selo ambayo alikuwa amepewa maelekezo kuwa ndugu yake amefungwa huko, ndani ngumi nzito ilikuwa inashuka kwenye uso wa Rashid ambaye alikuwa tayari alishakata tamaa ya kuendelea kuishi bahati nzuri haikufanikiwa kufika baada ya kuzuiwa na mkono wa mtu kisha uzito mkubwa sana uliielemea shingo ya Mapande Dickson baada ya kuteguliwa na uzito wa ngumi ambayo ilirushwa na Jamal, Mapande Dickson alishangaa akiwa mwenye hasira sana alijizoa pale chini ili kumkabili mtu huyo ambaye alikuwa bado hajamjua vizuri kutokana na kiza totoro ambacho kilikuwa humo ndani na kwa bahati mbaya hakujua mtu huyo ameingia muda gani humo ndani, ujio wake wa hasira ulimponza alishangaa kiganja kizito sana kinashuka kwenye bega lake akachuchumaa chini kwa maumivu, kiatu kiligongeshwa kwenye kichwa chake ambacho kilijipigiza kwenye smenti chini damu zikaanza kumtoka
"Washa taa washa taaa" alipiga kelele ili taa ziwashwe hakuelewa ni mtu gani anampiga vibaya sana namna hiyo kwenye kiza kwani kiliwashwa kibatari kidogo tu ambacho kilikuwa kinatumika kumulikia picha ambazo alikuwa anamuuliza Rashid aweze kuwataja hao watu walipo, taa ziliwashwa na maaskari wawili ambao walikuwa mlangoni walikuwa hawaelewi mtu huyo amewezaje kuingia wakiwa wamesimama pale pale, Dickson kichwa chake hakikuwa Sawa hata kidogo alikuwa kwenye maumivu makali alijikaza na kusimama mbele yake alikuwa amesimama mwanaume ambaye kwa sura alikuwa ni kijana japo sura yake ilikuwa imekomaa kiasi kuonekena kwamba shida ni sehemu ya maisha yake ya kila siku.
"Ni nani wewe unaye thubutu kuurusha mkono wako ukafika kwenye mwili wangu bila kuwa na wasi wasi wowote ule" alikuwa amechukia sana raia wa kawaida kumpiga hivyo tena mbele ya vijana wake.
"Mimi ndiye ninapaswa nikuulize wewe hapo ni nani hasa kwenye hii nchi mpaka uwafanyie watu mambo kama haya, kwani umeambiwa huyu ni gaidi aliye iasi nchi au kahujumu uchumi mpaka umtese sana namna hii bila hata kuuliza kwa ustaraabu kwamba kosa lake ni nini" sauti yake ilikuwa ya kistaarabu sana akiwa anampa hayo maneno Mapande Dickson wakati huo aligeuka pembeni alipokuwa amekalishwa Rashid alikuwa amepigwa mno hakuwa akitamanika hata kumwangalia usoni alisikitika sana Jamal pembeni aliona picha mbili, yakwanza ilikuwa ni yakwake yeye na baba yake mlezi Timotheo Jordan ambayo ilimfanya atabasamu baada ya kukumbuka mbali sana alikotoka na mzee huyo alimpenda sana lakini picha ya pili ilikuwa ni ya Rashid akiwa na Timotheo Jordan alisikitika baada ya kugundua huenda walikuwa wakimhitaji yeye na Timotheo Jordan ndiyo sababu Rashid akakamatwa bila kujua, wakati wote huo Dickson kichwa chake kilikuwa kinazunguka alikuwa hajatia neno lolote lile. Alishtuka sana baada ya kutulia vizuri sura ambayo ilikuwa kwenye picha ndiyo hiyo hapo ambayo alikuwa akiiona mbele yake.
"Chanzo cha kumkamata huyu ni kwa sababu ulikuwa unanitafuta mimi na huyo mzee hapo kwenye picha au kuna lingine" kidogo ilimtisha Dickson lakini alikuwa mtu wa kujiamini mno kwenye maisha yake.
"Kamata huyo awekwe ndani kama mwenzake mpuuzi huyu anatafutwa alafu anakuja kuongeza kesi zingine za kuleta fujo kituoni" kipigo alichopewa kiliwafanya askari wale wawili wameze mate huku wakiwa wanasukumiziana kila mmoja akihitaji mwenzake aanze kwenda, Jamal alitabasamu sana baada ya kulijua hilo walikuwa wanamuogopa ndio sababu hawakutii amri ya kiongozi wao.
"Jina lako unaitwa Dickson Mapande au Mapande Dickson kama unavyopenda kujiita, ni mtu mpenda rushwa mno na taarifa zako zote ninazo kiasi kwamba zikifika juu ya mikono ya Sheria au kwa wakubwa wako kazi hauna. Unaishi kwa kuwatesa watu huku mjini wakati familia yako na mtoto wako wa kiume umewaficha huko Kilombero wanakula tu maisha ya rushwa unazo zichukua hapa mjini kwa kudhulumu watu. Leo sijaja kwa hilo hapa ila nataka nikuonye kitu kimoja jitahidi sana ujifunze namna ya kuishi na watu ambao huwajui kwenye maisha yako inaweza kukuharibia kila kitu kwenye maisha yako, najua kuna watu wamekupa kazi ya kunitafuta mimi sasa nakuagiza wewe kawaambie hao wanao kufuga kwamba nimerudi rasmi kama kuna ambaye yupo kwenye huu mchezo basi ana bahati mbaya sana kwenye maisha yake kwani moyo wa ubinadamu nimetoka kuuzika siku ya jana saivi nina sura tu ya ubinadamu ila kilichopo kwenye moyo wangu ni cha kutisha mno, leo tumeongea kistaarabu sana ila kama tukionana kwa mara ya pili usiruhusu tukutane tena utakufa" Jamal hakutaka kuwa mtu wa kuhubiri sana aligeuka na kwenda kumfungua Rashid kwenye kiti hicho cha chuma akachukua na zile picha kisha akaanza kutoka akiwa amemshikilia Rashid kabla hajafika mlangoni alimgeukia Mapande Dickson ambaye bado alikuwa ameyatoa macho kama amebanwa na mlango
" Kuhusu hiki ulicho kifanya kwa kijana wa watu mimi sitaingilia hukumu yake itakuwa kwa namna atakavyo pendezwa yeye, kama akiamua kukusamehe basi mimi sina tatizo ila kama hajaridhika na hili jambo basi sio muda tunakutana tena" maneno yake yalimtisha sana Dickson hususani kuhusu familia yake ambayo hakuna binadamu ambaye alikuwa anamjua ilipo lakini mtu huyo alimtajia mpaka sehemu aliyokuwa ameificha na ni kweli alikuwa ni mtu mwenye mke na mtoto mmoja wa kiume, aliwaogopa sana wanadamu leo mbele ya vijana wake kiongozi huyu mkubwa sana nchini wa kupambana na makosa ya jinai alikuwa akitetemeka wakati huo mwanaume aliingia kwenye gari na kutoka kwenye kituo hicho taratibu kila askari akiwa anamtolea macho asielewe kinacho endelea.

Mcheza kwao hutunzwa usipotunzwa wanao jua kutunza wanauchukua mchezo, rasmi baba mwenye nyumba Jamal amejiingiza kwenye mchezo vipi atatunza au yeye ndo atatunzwa baada ya kujitambulisha rasmi jina lake na kuwapa taarifa kwamba rasmi yeye karudi anakitaka kila kilicho potea kirudi?????......
Binafsi sijui itakuaje niseme tu 39 kwa leo naweka nukta muda utaamua zaidi kipi kinajiri.

Langu jina naitwa

Bux the story teller
Ofa ya leo tu kwa sababu ya kumuenzi Baba yetu wa taifa vipande vilivyobaki 62 ili kufika final sehemu ya 100 nakupatia kwa shilingi 4500 tu pekee.

Hivyo usijisikie unyonge kukaa mwenyewe nyumbani siku ya leo wakati Bux the story teller yupo kwa ajili yako.

0621567672 (WhatsApp)
0745982347

lipia kwa hizo namba jina FEBIANI BABUYA.

Unapewa hadithi muda huo huo ili siku yako iishe vyema ukiupa ubongo burudani ya madini ya kutosha

Bux the story teller
 
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA AROBAINI NA TATU

TULIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA MBILI........
Jamal baada ya kupanda kwenye gari aliondoka kwa kasi hiyo sehemu lakini wakati yupo njiani alihisi kuna gari inamfuatilia, alipaki sehemu kujipa uhakika kama hicho kitu kilikuwa ni kweli, gari hiyo nayo ikapaki kwa nyuma kidogo alisikitika kuona hicho kitu huyo mtu alikuwa anafanya kitu cha hatari sana kumfuatilia mtu kama yeye ambaye kwa sasa hakuwa na moyo wa kibinadamu, kwenye gari ya nyuma Julius Makasi ndiye mwanaume ambaye alikuwa anakula sahani moja na Jamal leo, hili ni deni ambalo alikuwa anamlipa mwanasheria mkuu wa nchi baada ya kumuokoa kwenye kifo ambacho hata yeye alijua atakufa.

ENDELEA..............................
Gari ilikuwa kwenye mwendo mkali sana kiasi kwamba kama kingetokea hata kitu kidogo tu mbele ya hiyo gari hakuna ambaye angesalimika, Alexander baada ya kuitwa na dada yake hakuwa na amani moyoni alijua wazi kwamba lazima alikuwa kwenye hatari kubwa sana ndio sababu hakuwa na muda wa kupoteza licha ya kuwa kwenye huo mwendo hakuwa na taarifa kabisa kwamba kuna mtu alikuwa anamfuatilia kwa siri nyuma yake, tangu anatoka maeneo ya Buguruni kuna gari ilikuwa inamfuatilia kwa umakini mkubwa sana bila yeye kujua, Ashrafu Hamad ndiye mtu aliyekuwa akimfuatilia kwa umakini sana alikuwa na hasira sana na mtu huyu alihitaji kuweza kujua udhaifu wa kiumbe huyu ili aweze kulipa kisasi, siku mbili alizo lala kitandani bila kuwa na uwezo wa kunyanyuka kwa kupokea kipigo kutoka kwa Alexander zilimtia hasira mno hakuamini kama anaweza kupigwa kirahisi sana namna hii kwani alijiaiminisha kwamba hakuna mwanadamu anayeweza kumpiga.
Navy force kwa zaidi ya miaka minne alipitia mafunzo makali sana kwenye jeshi la maji aliwahi kuwa komando namba moja kwa uimara kwenye kikosi hicho ndiyo sababu aliweza mpaka kudanganya umri ili aingie huko kwani kwa umri ambao alikuwa nao mwanzo alikuwa haruhusiwi kabisa kuwa kwenye hiyo sehemu ndio maana kwa sasa alikuwa anasema ana miaka 32 ila haikuwa ukweli alikuwa na miaka 27 tu bado alikuwa kijana mdogo sana, haikuwa kazi ngumu kupata nafasi kwa sababu alikuwa ni mtoto wa kigogo akiwa na miaka 17 pekee alikuwa tayari ni komando wa kuogopwa sana lakini wakati huo kilitokea kisingizio kwamba ana matatizo ya moyo hivyo ilililazimu jeshi kumpa nafasi ya kuachana na kazi za jeshi kwa ajili ya afya yake ila hiyo miaka aliitumia kufanya utafiti ndani ya Buguruni ili aweze kujua kitu cha thamani ambacho walikuwa wanakitafuta walikuwa wamekihifadhi wapi hata hivyo hakuwahi kuambulia chohote kile kwa maiaka yake yote ile ndani ya nchi hii licha ya kuwa omba omba na kichaa kwenye mitaa hiyo ya Buguruni sokoni hakuwahi kufanikiwa kujua chochote kile kwani watu ambao alikuwa akiwatafuta walionekana kufanya kazi kwa weledi mkubwa mno baada ya kumuua rafiki yake Alexander na Alexander kupotea alikuwa na usongo naye mkubwa sana. Leo alikuwa amebahatika kumuona maeneo ya Buguruni karibu na sehemu ile ile ambayo alipoteleaga kwa mara ya kwanza japo hakujua ametokea mlango upi maana hakukuwa na dalili yoyote ya mtu kukaa maeneo hayo leo alikuwa anamfuatilia binadamu katili sana huyu bila yeye mwenyewe kujua, nini hatima yake? Chukua bisi tafuna kisha endelea kuenjoy……….

Kwa mwendo aliokuwa ameondoka nao haikuchukua muda mrefu sana wa yeye kuweza kufika sehemu ambayo alikuwa anaenda, Mbezi Beach karibu na Sea Breeze ndiko safari yake ilikoweza kuishia alivyofika tu kwenye nyumba moja kubwa sana geti lilijifungua lenyewe mwanaume akaingia ndani kisha geti hilo ambalo alikuwa anatumia limoti control kuweza kulifungua lilijifunga tena, hakukumbuka hata kuzima gari yake alitoka haraka akawa anakimbilia ndani ya jengo hilo la kifahari, alicho kiona kilimshangaza sana dada yake alikuwa amekaa pembeni mwa meza moja kubwa ya kifahari mbele yake kukiwa na pombe kali sana ambazo kwa umri wake halafu ukizingatia yeye ni mwanamke hatakiwi kabisa kuzigusa pombe hizo. Alexander baada ya kuona hicho kitu alichukia sana Troni ambaye ndiye alikuwa mlinzi mkuu wa mdogo wake alikuwa amekaa kando akionekana wazi hana la kufanya kwa sababu kazi yake ilikuwa ni kusikiliza binti huyo anataka nini tu na kumfanyia na sio vinginevyo, Deodata Romeo aliichukua chupa ya pombe na kuigugumia kwa spidi kitu ambacho kilimpa hasira sana Alexander aliichukua chupa hiyo kwenye mkono wa Deodata

“una matatizo gani wewe” aliongea kwa hasira akiivunja chupa hiyo
“Niache niache nilewe tu sina cha kupoteza hapa duniani mpaka inafika muda huwa najuta sana kuzaliwa ninaishi maisha ya kifahari lakini sina furaha kabisa naishi kama vile mimi ni mtumwa hahahahahaha niache nilewe mimi” Deodata alikuwa akiongea huku akiyumba yumba pale alipokuwa amekaa akionekana kabisa alikuwa amekolea kwenye pombe hiyo ambayo aliibugia.
“Hiki ndicho ulicho niitia hapa unajua ni kazi ngapi nimeacha huko nilikokuwa kwa ajili yako halafu unaniitia pombe una akili kweli wewe?”
“Ahaaaaa kwaiyo kazi zako ni mhimu sana kuliko mimi ndugu yako sio? Aya ondoka hapa sitaki kukuona kwenye macho yangu usije ukajitokeza tena kwenye maisha yangu” Deodata alikuwa anaongea kwa hasira sana huku akiwa anatoa machozi, maneno yake yalifanya apigwe kibao kimoja kizito mno kitu ambacho mpaka Troni alishangaa na kuogopa mno hakuwahi kushuhudia mtu huyo akimgusa mdogo wake leo alimpiga kibao kwa mara ya kwanza Troni ilimbidi kuwapisha ndugu hao wawili maana hiyo kesi yeye ilikuwa haimhusu kabisa.

“ Unavyokuwa unaongea namimi unatakiwa kuwa na mipaka na kujua unaongea na nani, unaniongelea kirahisi sana namna hiyo unajua nilikotoka nawewe? Unajua nimepitia mangapi ili wewe uishi? Naishi kama popo huwa silali ili uishi maisha mazuri leo umekuwa na jeuri ya kuniambia mimi nitoke kwenye maisha yako una akili kichwani mwako humo wewe” Leo kwa mara ya kwanza alikuwa anaongea kwa hasira sana mbele ya dada yake ambaye kwa miaka yote ameweza kumlea kama yai hakuhitaji ateseke kwa kitu chochote kile ndiyo sababu alimpa maisha yaliyobora kwa kila namna lakini alisahau kwamba pesa sio kila kitu kwenye maisha ya mwanadamu ndiyo sababu Deodata aliishi akiwa hana hata furaha japo alikuwa na maisha mazuri sana ila alikuwa mpweke mno.

“Unasema unafanya kazi? Haya nambie unafanya kazi gani ambayo inakufanya kuwa na pesa nyingi sana kiasi hicho, niambie kazi gani unafanya mjini hapa wewe, kazi ipi hiyo ambayo unaishi kwa kunificha ficha kama nimekuwa mke wa raisi” swali la Deodata lilikuwa ni gumu sana kwa upande wa Alexander hakuwa na kitu cha kujibu kwani alikuwa ni mafia aliua watu wengi sana ambao hata kama atasema awahesabu hana idadi kamili.
“Huna jibu la kunipa kwa sababu unajua unacho kifanya, ona sasa mimi naishi kama mtumwa siwezi kwenda sehemu hivi sasa natafutwa kila kona na watu yote kwa sababu yako, natamani nisingezaliwa pamoja nawewe kwanini umekuwa mtu wa namna hiyo kumbe kunilinda kote huko unajua kwamba una maadui kila kona? Sitaki kuamini siku nikija kuambiwa kwamba kaka yangu ni muuaji tafadhali isije kuwa hivyo” aliongea kwa uchungu sana kwa sababu walikuwa wamezaliwa wawili tu kwao hakuwa tayari kumpoteza kaka yake wa pekee alichukia sana kwani alihisi ni wazi mtu huyo alikuwa akifanya kazi za haramu, alikuwa na pesa nyingi sana na hakujua kabisa kwamba alikuwa akizitoa wapi hata kama angekuwa ameajiriwa hakukuwa na mtu wa kumlipa pesa nyingi sana namna hiyo.

“Ni nani ambaye anakutafuta wewe?” Alexander aliuliza kwa sauti ya upole alimjua vizuri dada yake huyo kama angemuuliza kiukali asingepata jibu kamili alikuwa na hamu sana ya kuweza kumjua binadamu ambaye alikuwa na jeuri ya kumtafuta dada yake hapa mjini ingali yeye yupo hai.
“Mimi ndo Black Widow”
“Whaaaaaaaaaaaaat?”
“Yes hiyo ndiyo sababu ambayo inafanya mimi natafutwa sana” Alexander ilimbidi akae kwanza hakuwa na nguvu za kuendelea kusimama eti dada yake ndiye Black Widow ambaye hata yeye alikuwa akimtafuta sana kwani hakuna ambaye aliwahi kumjua binti huyo zaidi ya Jamal ambaye ndiye aliyeenda kumpa taarifa hizo, wanadamu wana siri sana mdogo wake wa damu ndiye mtu ambaye alikuwa na soko kubwa sana kwenye mitandao ya kijamii kuliko hata pesa inavyo tafutwa, yeye pekee ndiyo ilikuwa njia ya kuwafanikishia kile ambacho walikuwa wanakitafuta kwa miaka mingi sana.
“Unamjua huyu mtu?” Deodata aligeuza laptop yake kuelekea sehemu ambayo alikuwa amekaa kaka yake, kwenye hiyo picha alikuwepo yeye pamoja na Jamal siku ile wakiwa wamekaa kwenye fukwe ya Ununio na mpaka leo siku mbili zilikuwa zimetimia tayari. Alexander alisimama akiwa haamini kijana ambaye ilikuwa inatakiwa amtie mkononi kwa garama yoyote na ndiyo kazi ambayo alitoka kupewa leo alikuwa anamuona akiwa kwenye tabasamu na dada yake.
“Amekufanya nini huyu mpumbavu?” aliuliza kwa ghadhabu akiwa anahitaji hata kumkunja dada yake kwani mtu huyo kwake alikuwa kama pilipili ambayo mtu anahitaji kuiweka kwenye kidonda namna inavyowasha, alimhitaji sana huyo kijana kazi yao itakuwa imeishia hapo.
“Unaogopa sana kuona alikutana namimi eeh, au unaogopa atakuchukulia dada yako sio, au unaogopa atanioa?, sasa sijui umemfanyia nini ila alinipa maagizo juzi japo hata simu ulinizimia ndiyo sababu taarifa imechelewa kukufikia maana alitoa siku mbili tu uwe umemtafuta kuna maswali anataka umjibu ilia toe hatima ya maisha yako vinginevyo sitakuona tena. Who are you brother?” maelezo ya Deodata yalifuatiwa na swali ambalo hata hivyo halikuweza kujibiwa kabisa, Alexander alichukia sana kwa kile alicho kisikia alitoka humo ndani bila hata kuaga bila kujulikana anaelekea wapi, dada yake alibaki anamuita kwa sauti yake ya kilevi kwani alikuwa hajamjibu maswali yake hata hivyo mwanaume hakusimama aliingia kwenye gari yake na kuondoka kwa spidi ambayo ungedhani kwamba kuna mtu anaenda kuuawa kama angechelewa kufika.

Mita kadhaa kutoka hapo ilipokuwa hiyo nyumba, kuna gari ya kifahari ilikuwa imepaki kwenye hilo eneo ndani ya hiyo gari alikuwa anaonekana Ashrafu ambaye alionekana kuridhika baada ya kumuona mwanaume huyo akiwa anaingia na kutoka kwenye hiyo nyumba bila shaka alijua wazi kwamba alikuwa akihusiana moja kwa moja na nyumba hiyo, upande wa pili alikuwa amekaa Travace ndani ya gari nyingine huyu alikuwa ni dereva wa Ashrafu ambapo ndani ya gari alikuwa na wanaume wengine watano, Ashrafu hakuwa amepona vizuri mkono wake ambao alichomwa visu kikatili na Alexander hivyo alikuwa akitembea na walinzi kila anapokuwa japo haya mambo aliamua kuyafuatilia mwenyewe bila baba yake mzazi kuweza kuelewa chochote kile.

*******************
Jamal alikuwa anaikata mitaa kuelekea maeneo ya External akiwa anajua wazi kwamba kuna mtu anamfuatilia nyuma, alivyofika hapo hakuweza kusimama bali alipitiliza mpaka Ubungo ambapo alikunja njia ya Kibo baada ya kufika mbele kidogo akakunja njia ya Kibamba ambapo alienda kusimamisha gari yake karibu na godauni moja kubwa ambalo ndani yake walikuwa wakizalishia chakula na dawa za kuku, hapakuwa na mtu yeyote yule risasi moja ilitosha kuivunja kufuli ambayo ilikuwa hapo akaingia ndani, muda mfupi mbele Julius Makasi alikuwa amefika karibu na hilo godauni, aliitoa silaha yake kwenye kiuno na kuishika mkononi ili aweze kukabiliana na namna yoyote ile ya hatari ambayo ingeweza kutokea mbele yake hivyo bastola ilimsaidia kumfanya kuwa salama kwa asilimi za kutosha, aliingia humo ndani kwa tahadhari sana palikuwa kimya mno hakukuwa na aina yoyote ile ya kelele zaidi ya nyayo zake ambazo alikuwa akinyata nazo taratibu bila kelele, aliona kisu kikija upande wake kwa nguvu alikikwepa kikambaraza kwenye mkono ambao ulikuwa na bastola hivyo ilimfanya bastola iruke juu wakati anaruka kuifuata alipigwa mtama akajigeuza na kusimama bastola ikadondokea upande wa pili.

“Mbona unanifuata kwa kuninyemelea sana ndugu yangu si ungekuja tu mbele yangu?” ilikuwa sauti ya Jamal kijana mdogo sana
“Hahahahahahah nilijua nitakuwa na kazi ngumu sana kukupata kumbe mtu mwenyewe mwepesi sana namna hii halafu bado mtoto mdogo sana ulitakiwa uwe shule unasoma saivi” majigambo yalichukua sehemu yake kwenye mdomo wa Julius Makasi, baada ya kupewa kazi ya kumpata mtu huyu kutoka kwa mwanasheria mkuu alidhani ingemchukua muda mrefu lakini ilikuwa ni tofauti ilikuwa ni kazi nyepesi sana kuweza kujua alipo kwani mtu huyo alikuwa anajiweka wazi sana lengo lake aweze kuwajua maadui zake kwa sababu alijua ni lazima anatafutwa sana na hao watu, Jamal alikuwa yupo mbele yake tayari sasa ilikuwa ni kazi kwake kuweza kumchukua na kuweza kumpeleka mbele ya huyo kiongozi wake kama yeye mwenyewe alivyokuwa ameahidi kuweza kuifanya kazi hiyo.

Jamal kwenye mikono ya mlipa madeni Julius Makasi atatoka?, Ashrafu yupo nyumbani kwa Alexander, Deodata yupo kwenye hatari kubwa mno je nani atamsaidia binti huyu mdogo waweza kumuita Blak Widow?...........43 inafika tamati tukutane tena wakati ujao.

Bux the story teller
Imalizie hadithi hii mpaka sehemu ya 100 kwa shilingi 4000 tu mpaka mwisho.

Hivyo usijisikie unyonge kukaa mwenyewe nyumbani siku ya leo wakati Bux the story teller yupo kwa ajili yako.

0621567672 (WhatsApp)
0745982347

lipia kwa hizo namba jina FEBIANI BABUYA.

Unapewa hadithi muda huo huo ili siku yako iishe vyema ukiupa ubongo burudani na kupata madini ya kutosha
 
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA AROBAINI NA TANO

TULIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA NNE........
. Mmoja wa walinzi wake alidakwa na ndiye ambaye risasi zote zilimuishia sasa walikuwa wamebaki yeye na mlinzi mmoja pamoja na Travace ambaye alikuwa mlaini sana kazi yake yeye ilikuwa ni kushughulika na usukani tu ukimkuta huko alikuwa mjanja kupita kiasi ila kwenye hili suala la mapigano ulikuwa ni ugonjwa mkubwa sana kwake na aliuogopa sana ugonjwa huo. Waliupanga mkono wanaume wawili ambao walidhani mtu huyu hakuwa na uwezo wa kuwashinda,mkono ulipigwa kwa dakika mbili tu yule mlinzi shingo yake ilikuwa imegeuzwa kwa sasa ni Ashraf tu ndiye aliyekuwa anahitajika kuyatetea maisha yake yeye mwenyewe dereva wake alikuwa amepiga magoti akiomba msamaha bila kujua anamuomba nani huku wanaume wakionyeshana umwamba wa mikono.

ENDELEA...............................
Ashrafu alikuwa hajapona mkono mmoj hivyo asingeweza kuhimili mbele ya mtu imara kama huyu, mkono wake ambao ulikuwa bado haujapona ulivunjwa pamoja na mguu wake mmoja alikuwa chini akiugulia maumivu mazito sana.
“Nisamehe bosi wangu mimi sijui wala sihusiki ni miaka kadhaa watu hawa huwa wananitishia maisha yangu hivyo ili kuilinda familia yangu walinigeuza kuwa dereva wao, hivi nina mke na watoto wadogo mapacha ambao wananitegemea kwa kila kitu” Ashrafu hakuamini dereva wake alimkataa wazi wazi hofu ya kifo ilimtia mbavuni alikuwa akitetemeka sana, alifanya anacho kiweza yeye ili kuhakikisha anakuwa salama mambo ya wengine aliona kabisa kwamba hayamhusu kilichokuwepo mbele yake ilikuwa ni kuokoa tu maisha yake kwanza ndipo mambo mengine yafuate. Alionyeshwa ishara ya kuondoka humo ndani alikimbia mno mtu huyu kuweza kusalimika maisha yake alipanda kwenye mnazi mkubwa bila hata kupumzika akiparamia ukuta na kurukia nje kwa hofu kubwa bila kujali kwamba angetua vipi huko nje kitu alicho kijali kwa huo muda ni kuiponya nafsi yake lilikuwa ni tukio la kuchekesha sana ila uhai ulikuwa ni mhimu zaidi hata ya kuchekesha hapo.

“ Sasa nakuhitaji uniambie huyu binti unamhitaji wanini?” Jamal alimkazia macho Ashrafu ambaye alikuwa chini akiendelea kuugulia maumivu ya mkono wake na mguu wake.
"Hauna mamlaka ya kuniamrisha mtu wa kawaida sana kama wewe" jeuri huwa ni mbaya sana pale unapo hitaji huruma ya mtu uli uweze kuishi, Ashrafu alikuwa ni mtu mwenye dharau sana ndiyo sababu alikuwa akijibu kile ambacho angejisikia yeye.
“Mhhhhhhh mimi unanijua mpaka unaniongelea kwa jeuri sana namna hiyo? Ni vyema ukazichanga karata za maisha yako kwa usahihi vinginevyo mdomo wako unaenda kukuponza” Jamal alichuchumaa chini alipokuwa amelala Ashrafu huku akiwa anaichomoa bastola yake kiunoni ambayo ilibakia bila wasi wasi, Deodata alikuwa bado ameduwaa sana hayo matukio kwake ilikuwa kama anaangalia movie ya kutisha sana ila alichokuwa anakiona ulikuwa ni uhalisia wa kila jambo.
“Paaaa ni mlio wa risasi ambayo ilizamishwa kwenye mguu wa Ashrafu alitamani dunia ijifungue azame huko ndani mambo ya binadamu yalikuwa yanamtisha mno alihisi kuna muda hata shetani huwa anakuwa na huruma lakini sio kukutana na mwanadamu kama huyu ambaye kwake utu ulikuwa ni kitu cha kutafutiza sana, Deodata alikumbuka juzi mwanaume huyu alivyokuwa amekuja kuongea naye kule ununio akiwa mwenye tabasamu sana leo mtu aliyekuwa anamuona hapa alikuwa ni tofauti sana na yule ambaye yeye alikuwa akimdhania kwamba anamjua.

“Mimi nilikuwa nina shida na kaka yake ambaye nina ugomvi naye hivyo nilijua kupitia huyu ingekuwa ni kazi rahisi sana kuweza kumpata mtu huyo”
“Unafanya kazi na nani”
“Mimi ni mmiliki wa kampuni ya M96 OWNER’Z”
“Whaaaaaaaat”
“Yes ni kampuni ambayo nimeachiwa na baba yangu”
“Baba yako ni nani”
“Hakramu Hamad”
“Unamaanisha makamu wa raisi”
“Ndiyo”
“Mpigie simu haraka sana” Jamal hakuweza kuamini kama huyo aliyekuwa mbele yake ndiye aliyekuwa mtoto wa kuzaliwa kwa makamu wa raisi alishtuka sana baada ya kusikia mtu huyu ndiye bosi wa hiyo kampuni ambayo alisimuliwa kwamba ndiyo chanzo cha kifo cha baba yake baada ya kusikia hilo aliamini moja kwa moja kuna watu wako nyuma ya hili, kijana kama huyu hawezi kumiliki kampuni kubwa ya namna hiyo, Ashrafu maumivu ya kifo yalimbana mbavu hakuwa na sehemu ya kukimbilia ilimlazimu kutii kila alichokuwa anaambiwa hakuwa na namna nyingine yoyote ya kuweza kufanya.
“Nitakuja kukuona leo” upande wa pili baada tu ya kupokea simu ulijibu kwa sauti nzito, makamu wa raisi moja kwa moja alijua kwamba anaongea na mtoto wake.
“Nisikilize kwa umakini sana mzee”
“Wewe ni nani ambaye upo na simu ya mwanangu? Na yuko wapi”
“Hatima ya maisha ya mwanao yapo kwenye mkono wangu mimi kama nikiamua atakuwa salama lakini nisipo amua pia hataweza kuwa salama kwahiyo naomba unisikilize kwa umakini sana”
“Unataka nini”
“Yes hilo ndilo swali la msingi sana ambalo ulipaswa kuniuliza kwa muda mrefu mno, anaye waumiza watu siku zote huwa anakuwa mtu wa kupoteza sana kumbukumbu tofauti na mtu ambaye anakuwa anaumizwa na watu, miaka mingi sana huko nyuma mlishawahi kuyafanya mambo ya kutisha sana na matukio ya hovyo mno, mliwahi kuua watu wasiokuwa na hatia yoyote mpaka leo mmeziacha familia nyingi sana kwenye maisha magumu kwa sababu ya tamaa zenu za muda mfupi je utaweza kuyalipa hayo ili mwanao aishi?” maneno ya Jamal yalikuwa kama mwiba kwa mzee huyo upande wa pili maneno aliyo ambiwa yalimfanya akose majibu ya haraka kwani walikuwa wameua watu wa familia nyingi sana hivyo kwake ilikuwa ni ngumu moja kwa moja kujua kwamba ni mtu gani ambaye alikuwa anaongea naye muda huo.

“Unaweza ukanikumbusha wewe ni kutoka familia ipi?”
“Unamkumbuka Jonson Malisaba” Hayo maneno yalimfanya makamu wa raisi aweze kupaliwa alitoa kikohozi cha nguvu sana kisha akajiweka sawa
“Wewe ndiye yule mtoto uliyepona?”
“Nacho kihitaji ni kichwa cha baba yangu kiko wapi na unipe sababu ya msingi ya mimi kukuelewa kwamba ni kipi kiliwafanya muyatende haya kwa familia yangu”
“Kuhusu kichwa cha baba yako mimi sijui kilipo kwani kuna mtu mwigine ambaye aliingilia kati kuhusu hili jambo kabla sisi hatujafika ila sababu ya msingi ya kufanya haya zipi mbili ya kwanza tulikuja kugundua baba yako alikuwa anatumiwa na serikali kutoa siri zetu kitu ambacho kilikuwa ni mwiko mkubwa sana kwetu lakini cha pili ni kitu cha thamani ambacho alikuwa anamiliki sisi lengo letu lilikuwa ni kukipata hiho kitu hivyo kabla hatujamtia mkononi kuna mtu mweingine ambaye mpaka leo hatujajua ni nani alihusika kuyatenda haya na kama unacho hicho kitu nipatie mapema sana kabla hujachelewa” Makamu wa raisi alikuwa anajibu hayo maswali lakini alikuwa na hasira mno ni kwa sababu tu mtoto wake alikuwa kwenye mikono ya huyo mtu ilikuwa ni dharau kubwa sana mtu kama yeye kuweza kuulizwa maswali na kijana kama huyo.

“Utakuja kuibeba maiti ya mwanao” Jamal alimalizia hayo maneno na kuikata simu yake
“Hello hello” makamu wa raisi upande wa pili alikuwa akiongea yeye mwenyewe hakukuwa na mtu yeyeote yule ambaye alikuwa akimjibu, aliwapigia watu wake simu haraka sana ili waweza kuangalia location ya simu hiyo ilipo waweze kumfuata haraka sana wakati huo yeye alikuwa ananyoosha sehemu ambayo wazi alijua yeye mwenyewe anaenda kufanya nini, aliingia kwenye gari yake na kuondoka kwa spidi kali sana kwenye hilo eneo, kwa Jamal baada ya kukata simu aliikoki bastola yake na kupiga kupiga risasi mbili akiwa na hasira sana zilimlenga Ashrafu.

Upande wa pili kwa Alexander alikuwa kwenye barabara ya mwenge, baada ya kupata taarifa ya jambo la hatari kupitia kinasa sauti ambaho alikuwa akikitumia kuwasiliana na Troni mlinzi wa dada yake ilimlazimu kugeuza gari kwa kasi sana kwa mbele kulikuwa na foleni ndogo kwa sababu kiongozi alikuwa akipita na msafara wake hivyo alichelewa kidogo. Baada ya barabara kuwa nyeupe gari iliendeshwa kwa spidi za hatari kiasi kwamba ungedhani alikuwa kwenye mashindano, bara bara ya Mbezi ilikuwa nyeupe hivyo alichukua muda mfupi kufika nyumbani geti lilifunguka lakini ndani palikuwa hakuna mtu yeyote yule wala hakukuwa na dalili yoyote ile ya mtu kuwepo kwenye hilo eneo, bada ya kugeuza shingo yake vizuri kwa chini aliona kuna wanaume wamelala wengine wakiwa wamepigwa risasi za kichwa na wengine walikuwa wamevunjwa, naweza kusema ni bahati mbaya sana mbele yake alikuwa anamuona Ashrafu Hamad akiwa kama mtu aliyeweza kukata tama ya maisha yake kabisa kuendelea tena kuishi hapa duniani. Miguu yake yote miwili ilikuwa imevunjika vibaya sana mmoja ukiwa umevunjwa na mtu namwingine ulionekana kabisa uliweza kuvunjwa kwa risasi ambazo zilikuwa zimepitishwa kwenye mfupa wa goti ni wazi kabisa kwamba mtu huyo alikuwa kwenye maumivu makali sana ambayo hayakuwa mepesi hata kuweza kuyaelezea.

“Wewe mjinga umeona haitoshi umeamua unifuate nyumbani kwangu? Siku ile nimekuacha ukiwa hai kabisa lakini bado tu haukomi sio where is my sister?” Alexander alikuwa anaongea kwa hasira sana, hakuwa tayari kwa mtu ambaye alikuwa anaonyesha kila dalili za kuweza kumgusa dada yake kipenzi ambaye alikuwa anampenda kuliko kitu chochote kile hapa duniani na hakuwa tayari kuona mwanamke huyo anateseka ingali yeye alikuwa yupo hai kabisa hana shida yoyote.
“Mimi nilikuja kumchukua dada yako ila kuna mtu ameingilia hili jambo na ndo huyo ambaye ameweza kuondoka naye” Ashrafu aliongea akiwa na wasi wasi mkubwa sana pamoja na maumivu makali aliyokuwa anayapitia huyo mwanaume ambaye alikuwa yupo mbele yake alikutana naye siku kadhaa nyuma na aliuona ukatili wake namna ulivyo na ndiye mwanaume ambaye aliweza kuingia ikulu ya nchi akafanya kile ambacho kwa yeye aliweza kuona kinamfaa na kuondoka bila tatizo lolote lile. Mwanaume alimwangalia kijana huyu ambaye zile tambo zake zote ambazo alikuwa amezoea kuzitoa kwenye mdomo wake pamoja na yale maneno ya majivuno ambayo kila siku ilikuwa kawaida yake hayakuwa sehemu yake siku hiyo, alimpiga risasi tano kwenye kichwa hakuwa na huruma naye hata kidogo hasira alizokuwa nazo zilimfanya asiwe na moyo wa mwanadamu kabisa, huyu mtu alikuwa na usongo naye kwa muda mrefu sana ni kama bahati mbaya sana siku ile Kindondoni aliweza kumponyoka na kupona baada ya baba yake kuweza kufika lakini leo hakukuwa na cha kumpa msaada.

Ombaomba wa Buguruni, kichaa wa Buguruni, mmiliki feki wa M96 OWNER’Z na kijana aliyekuwa anaishi kwenye sura tano leo hakuwa na kauli tena mbele ya uso wa dunia, Ashrafu Hamad mtoto wa pekee kabisa wa mheshimiwa makamu wa raisi wa nchi ya Tanzania alikuwa ameiaga dunia kwenye mikono ya mtu mbaya na binadamu wa kutisha sana Alexander. Mwanaume alipitiliza mpaka ndani ambapo aliskitika sana baada ya kumkuta kijana wake Troni amekufa vibaya sana kwa kupigwa risasi za kichwa alimfunika vizuri macho yake akapandisha kwenye chumba chake cha juu kabisa ambako huko kulikuwa na chumba cha siri cha kamera ambazo alikuwa ameziweka kwa siri sana kila sehemu ambayo ilikuwa ikizunguka kwenye hiyo nyumba.

Mwanaume aliiwasha mashine yake ndogo ambayo alikuwa ameuganisha kila kitu humo ndani ili kuweza kuona kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea ndani ya muda mfupi sana ambao yeye aliweza kutoka humo ndani, alishuhudia matukio yote tangu anatoka magari yaliyokuwa nje mpaka namna ambavyo Jamal aliweza kuingia na kuweza kufanya hicho alichoweza kukifanya pamoja na kuondoka na dada yake, alijilaumu sana kwani alijiona kuwa mzembe aliyepita kiasi kwa kitu ambacho alikiruhusu kifanyike kwa maamuzi yake ya kuondoka kwa hasira, aliizoom vizuri sura ya Jamal aliiangalia kwa umakini sana na ndipo alipoweza kuyakumbuka maneno ya dada yake ambaye alimpa taarifa mapema kwamba mtu huyo angefika hapo muda wowote ule ndani ya siku mbili kama yeye binafsi asingeweza kumtafuta mtu huyo. Aliharibu kila kitu humo ndani na kuchukua vitu vyake vyote vya mhimu kwani alijua wazi kwamba maaskari wangeweza kufika na kufanya uchunguzi kwa mauaji ambayo yalikuwa yamefanyika, visu vyake viwili vilikuwa kiunoni mwake, koti kubwa na kofia juu aliingia kwenye gari yake ya kifahari na kuondoka kwa spidi hilo eneo moja kwa moja alikuwa anaelekea kumtafuta mtu ambaye alikuwa amemshikilia dada yake moyoni mwake alikiri wazi kwamba akimkamata mtu huyo basi atakuwa miongoni mwa wandamu ambao watakufa kifo kibaya sana hapa duniani.

Maskini Ashrafu[emoji22]imekuwa mapema mno tulikupenda sana, makamu wa raisi atawafanya nini hawa binadamu walio igusa roho ya maisha yake??????, Nini Alexander anaenda kumfanya bwana mdogo huyu ambaye amemgusa mwanamke ambaye kwake hakuwahi kumpa ruhusa binadamu yeyote kumgusa hata ukucha wake, yaani kiufupi Jamal kayakanyaga kwa Alexander mtu kazi.
Kila mwanzo huwa una mwisho 45 natia nanga rasmi leo[emoji3578] tukutane majira yanayo fuata panapo majaaliwa ya mwenyezi MUNGU.

Bux the story teller

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Kwa shilingi 4000 tu unaisoma yote mpaka mwisho sehemu ya 100.

0621567672 (WhatsApp)
0745982347

Jina

FEBIANI BABUYA

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom