I want to die a judge

I want to die a judge

Hadithi: I Want to Die Judge (Nataka Kufa Hakimu)
Mtunzi: Febiani Babuya
Maimuliaji: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com


SEHEMU YA KWANZA.
Saa mbili za usiku ndani ya jiji la mwanza katika barabara kubwa ambayo pia ni nzuri kimwonekano ikiwa inaelekea ndani ya Capri point linaonekana gari moja zuri sana aina ya Land cruiser Prado likiwa kwenye spidi sana wakati huo kulikuwa na manyunyu manyunyu ya Mvua zilizofanya usiku kuwa mtulivu ndani ya jiji lenye utajiri wa mawe ya kutosha.

Ndani ya hili gari anaonekana mzee mmoja wa makamo ya kawaida akionekana kuwa na miaka isiyopungua 50 hivi ila kwa sababu ya ukwasi aliokuwa nao bado alionekana kama ni kijana na ana safari ndefu ya kuufikia uzee. Alikuwa anarejea nyumbani kwake baada ya kutoka kwenye mihangaiko yake ya kila siku ili kuhakikisha familia yake inakuwa na furaha muda wote. Alikuwa anatamani sana afike nyumbani haraka baada ya kununua zawadi nyingi za kutosha alijua watazifurahia hao wana familia wake ambao aliwapenda kuliko kitu chochote kile. Akiwa kwenye hiyo furaha kubwa ndani ya gari gari yake alihisi kama kuna kitu amekikanyaga baada ya gari hiyo aliyokuwa nayo kuyumba nusu ipoteze uelekeo ikamlazimu kuisimamisha ghafla tu huku akiwa anahema kwa nguvu hakutarajia hilo tukio.

Aligeuka kuangalia nyuma alikokuwa ametoka ni kweli alikuwa amemkanyaga paka ambaye alikuwa anakatiza kwenye barabara hiyo majira ya usiku, yule paka baada ya kugongwa hakuwa na maisha marefu hata kidogo alipoteza maisha pale pale, hiyo ilikuwa ni ishara mbaya sana majira hayo ya usiku, alikuwa mtu wa dini sana huyu mzee hivyo hiyo ishara alijua wazi ni ishara mbaya na huenda kuna mambo hayako Sawa, kama imani yake inavyo mruhusu alifanya maombi kwa dakika tatu baada ya hapo aliliondoa gari kwa mwendo wa taratibu kuelekea nyumbani kwake, ile hamu na furaha kubwa aliyokuwa nayo tangu mwanzo ilimpotea kabisa usoni pake, akawa anawaza kuhusu tukio ambalo halikuwa zuri kwa dakika kadhaa zilizoweza kupita nyuma.

Alifika nje ya nyumba yake alisimamisha gari kama dakika tano akiwa ameulalia usukani akiwaza, alionekana anawaza mbali sana, aliichukua simu yake akaandika meseji ambayo haikuwa na maneno mengi sana akaituma mahali kisha akaizima hiyo simu. Alipiga honi kwenye hilo geti la nyumba yake, dakika moja mbele geti lilifunguliwa na mlinzi wale ambaye walikuwa wanataniana sana lakini siku hii ilikuwa ni tofauti kidogo kwa huyu mlinzi alijaribu kumtania bosi wake alinyamaza baada ya kumuona mzee huyo hakuwa sawa.

Jina lake halisi alikuwa anaitwa Jonson Malisaba, alikuwa amebahatika kupata familia kubwa na nzuri yenye furaha muda wote, alikuwa na mke wake aliyefahamika kama Anastazia Lewin pamoja na watoto watatu mmoja ambaye ndiye mkubwa zaidi alikuwa anaitwa Cleopatra Jonson na wawili ambao walikuwa ni wadogo kwa Cleopatra walikuwa ni mapacha wawili wakiume alikuwa anaitwa Lenovatus Jonson na wakike alifahamika kama Octavian Jonson pia humo ndani walikuwa wakiishi na mfanya kazi wakike pamoja na wa kiume bila kumsahau mlinzi wa getini, hawakuwa na utofauti kati ya wafanyakazi na wana familia wote waliishi kwa usawa na furaha kiasi kwamba kwa mgeni ilikuwa ni ngumu sana kuweza kuwatambua kama wengine ni wafanyakazi tu wa ndani.

Kabla ya kurudi kwa mzee huyu familia ilikuwa ipo mezani wakati huo wakiwa wanaandaa chakula kwa sababu walijua baba mwenye nyumba muda wowote ule alikuwa anafika na ndiyo ilikuwa mida yake ya kurudi kila siku, hakuwa mtu wa kuchelewa kwa vile alikuwa anayajua vizuri majukumu yake kama baba bora wa familia.
"Octavian nenda ukamuamshe mwenzako maana naye kwa kulala lala huyo kisa anajua ndo wamwisho basi ndo anajidekesha wewe subiri nife atakoma mbona na itokee ndo aletewe mama wa kambo ataelewa" ni mama wa familia Anastazia Lewin mke wa Mr Jonson alikuwa akimtania binti yake mdogo Octavian ambaye alimtuma akamuamshe pacha wake wa kiume Lenovatus aliyekuwa amelala mpaka muda huo wanakaribia kupata chakula cha usiku huku akiwa anacheka.

"Mama kwa sababu yeye ni doto basi unaona kama mimi sio wa mwisho sitakiwi kudeka sawa tu" binti huyu mdogo aliye barikiwa kuwa na uzuri wa mama yake alimjibu mama yake meno yake yote yakiwa nje kwa kicheko kwa sababu alipenda sana kumtania sana pacha wake huyo huku mara kadhaa akiwa anamwambia kwamba hata afanyaje yeye ni dada yake kwani alimzidi dakika thelathini za kuzaliwa. Mapacha hawa walikuwa na miaka 14 kwa muda huo na dada yao Cleopatra alikuwa ana miaka 20.

"Heee heee nitokee hapa nawewe unamuonea wivu mwenzako sasa wewe nayeye si ni mtu mmoja" mama huyu aliongea tena na familia nzima ilikuwa kwenye kicheko kikubwa wakiwa na furaha sana.

"Hahahahahaaa mama na hao watoto wako mtanivunja mbavu zangu mie mwisho wa siku nishindwe kupata watoto mimi" dada mtu Cleopatra alimtania mama yake ambaye aliishia kutabasamu humu akiwa anapakua chakula kwenye hiyo meza.

"Anakuja lastborn wako huyo" Octavian baada ya kutoka chumbani alimtania tena mama yake huku akienda kukaa kwenye sehemu yake, mama yao alitabasamu sana alikuwa mtu mwenye furaha kubwa kubahatika kupata familia bora iliyojaaliwa amani na furaha ya kutosha.

Mr Jonson baada ya kuingiza gari ndani ya geti la nyumba yake alienda sehemu alipokuwa anatumia kupaki magari yake akalipaki vyema hilo ambalo alikuwa amelitumia hii siku, aligeuka ili aelekee ndani akawaite waje wamsaidie kushusha mizigo ndani ya hilo gari ila wakati anageuka alishangaa kuona bado geti liko wazi haikuwa kawaida kwani ilitakiwa akiingia tu humo ndani geti lifungwe ilikuwa ni usiku tayari na hilo geti halikutakiwa kuwa wazi.

Alitaka kuita jina la mlinzi wake huyo wa getini lakini alisita kidogo baada ya kuona mwili wa mtu umelala chini alihisi huenda mlinzi wake huyo amepatwa na tatizo hivyo anapaswa kumsaidia, alisogea hatua mbili akiwa anaelekea sehemu ulipokuwa huo mwili ila alisimama baada ya kuhisi kuna mtu hiyo sehemu ni kweli mbele yake walikuwa wamesimama wanaume wawili waliokuwa wamevaa suti safi na hawakuonekana kabisa kuhofia manyunyu ya Mvua mida hiyo ya jioni.

"Kwanini umeamua kutukimbia na kuja kuishi huku bila taarifa yoyote" ni swali la mmoja ya wale wanaume wawili waliokuwa na suti safi nyeusi na kofia kubwa vichwani.

"Mnataka nini mpaka mnifuate na huku? nilishaamua kutoka kwenye maisha yenu ndio maana sijawahi kuwatafuta tena ni miaka miwili sasa imepita hivyo sitarajii kunifuatilia tena ondokeni hapa" Mr Jonson alionekana kuwajua kwa undani hao watu walio onekana kumtafuta kwa muda mrefu sana.

"Leo umekuwa jasiri wa kutufukuza watu kama sisi kweli? mbona unajisahau sana namna hii mkuu, umemdanganya mpaka mke wako hakuwahi kuujua uhalisia wako kwamba wewe ni nani na tulikusaidia kulilinda hilo saivi unaanza kujibu jeuri.

Bosi ametuagiza vitu vitatu kwako cha kwanza ni kuchukua mzigo wetu tukuache hai, chapili uende wewe mwenyewe ukamkabidhi huo mzigo na umpe sababu za msingi kwanini umekuwa msaliti mkubwa sana namna hii kwa mtu ambaye uliaminiwa na kupewa nafasi kubwa mno, lakini cha tatu kama vyote hivyo viwili vikishindikana basi tuue familia yako yote" yalikuwa ni maelezo yaliyo jitosheleza vyema hayakuhitaji maswali mengi sana ili yaeleweke.

"Siendi mahali na hakuna kitu ambacho mtakifanya kwangu siwezi kurudi kwenye maisha yale ya utumwa mimi" Mr Jonson alitamka kijasiri wakati huo aliichomoa bastola yake kwa nguvu ila kabla hajafanya chochote alipigwa yeye risasi ya bega iliyo mtoa kilio kikubwa kilicho washtua mpaka ndani, familia karibia nzima ilitoka nje kasoro Lenovatus ambaye ndo alikuwa anaamka, ni baada ya kusikia kelele za Mr Jonson walihisi huenda anahitaji msaada wa ghafla hivyo wote walikuwa wametoka nje ila waliogopa baada ya kuona mzee huyo amewekewa bastola ya kichwa akiwa anaamriwa kuwakabidhi hazina yao kama walivyokuwa wanadai wao.

Watu hao walionekana kufurahia baada ya kuona familia ya mzee huyo yote ipo nje, mmoja wa wale wanaume aliwasogelea na kuwamiminia risasi wote bila hata kuuliza, Mr Jonson alinyanyuka akihitaji kwenda kumzuia mtu huyo alipigwa risasi mbili za miguu akawa hana hata uwezo wa kutembea tena, alitoa machozi kwa kushindwa kabisa kuisaidia familia yake ambayo alikuwa anaona kabisa inakufa Kwa sababu ya uzembe wake, hakuwa na cha kufanya mzee huyu hakupata hata nafasi ya kuwaaga wana familia hao ambao kwenye kuangaza kwake hakumuona mtoto wake wa mwisho ambaye alikuwa ni pacha wa Cleopatra kidogo alipata matumaini na aliomba MUNGU amlinde huko aliko hata amtumie malaika wake amlinde mtoto huyo asiweze kuonekana hiyo sehemu.

"Umeshindwa kuilinda familia yako kwa sababu ya ujinga wako mwenyewe ungetupatia tunacho kihitaji haya yasingetokea kabisa, sasa tunaua familia nzima hakuna shahidi atakaye baki wa kuendelea kuificha hiyo hazina ambayo haupo tayari kuitoa haya yanaishia hapa hapa mkuu naomba unisamehe sana japo umekuwa mkuu wangu kwa muda mrefu kidogo leo sina namna ya kufanya" mwanaume huyo aliyekuwa amesimama karibu yake alikuwa anampa wosia wa mwisho mwisho Mr Jonson.

"Ipo siku haya yote yataisha najua yupo mtu atayafanya haya tu na mtaisha wote" hakuongeza neno lingine alipigwa risasi nyingi sana za kichwa, milio mingi ya risasi nyingi nje ya nyumba hiyo ndiyo iliyokuwa imemshtua Lenovatus na kumaliza usingizi wake wote, alifika sebuleni lastborn huyu wa familia kwani ilikuwa lazima akadeke kwa mama yake kwanza ndo aendelee na mengine ila hakumkuta mtu yeyote sebuleni hapo chakula kikiwa kimeandaliwa tayari, alichukua zake paja la nyama ya kuku akaendelea kulitafuna taratibu ndipo alipokumbuka alisikia sauti kubwa nje na mlango ulikuwa upo wazi kabisa, alielekea kwenye huo mlango ili ajue nini kinaendelea huko nje ambako kulikuwa kuna mwanga wa kutosha wa umeme.

Baada ya kufika hapo mlangoni nyama ilimdondoka mkononi baada ya kuona damu imetapakaa alimuona mama yake amelala chini akiwa na damu nyingi sana inamtoka kichwani pembeni ya mama yake alikuwa amelala pacha wake ambaye walipendana kuliko kitu chochote kile kwenye huu ulimwengu, Lenovatus alikuwa bado ni mdogo ila uchungu ulio mpata ulikuwa ni mkubwa sana alikuwa anaelewa vyema kwa sababu alikuwa anaona kwenye movie nyingi namna watu wanavyokufa alitambua hao wote hapo chini walikuwa hawapo tena duniani, aliyainua macho yake mbele kidogo ambapo aliona kuna mwanaume mwenye suti yake nzuri sana akiwa anakata shingo ya baba yake kisu.

"Baba" aliita kwa nguvu mtoto huyu akitaka kukimbilia kule nje ili akamzuie mtu huyo kufanya hicho kitu kwa baba yake mzazi, sauti yake iliwashtua wale wanaume ambapo yule mmoja alikuwa amekamilisha kukikata hicho kichwa na alikuwa amekishika mkononi. Kabla huyo mtoto hajatoka kwenye huo mlango ikiwa ndo anaanza kukimbia kuelekea nje mlango ulipigwa na teke la ghafla ulijifunga pembeni mwa huyo mtoto alitokea mwanaume mmoja aliye onekana kuwa wa makamo kidogo akiwa na barakoa iliyo uziba uso wake kwa usahihi alimziba Lenovatus mdomo aliyekuwa anapiga makelele kwa mambo aliyo yaona hapo nje kwa familia yake, baada ya kuona mtoto huyu anahangaika ajinasue kwenye mikono yake ili atoke kwenda huko nje alipitisha kidole chake kwenye mshipa wa shingoni Lenovatus akatulia kimya.

Wanaume hao walikuwa wanakuja kwa tahadhali sana baada ya kugundua walikuwa hawajaimaliza familia nzima, mmoja aliupiga mlango kwa teke wakati huo wanafika kwenye huo mlango yule mtu aliyemziba Lenovatus mdomo alijirusha juu ya kabati kubwa la vyombo hapo sebuleni akatulia kimya akiwa amempakata mtoto huyo. Hao watu waliingia humo ndani na kukagua kila chumba lakini hawakuona chochote kile.

"Kwa nilivyo muona bado ni bwana mdogo sana hata kama ameona kilicho tokea hawezi kukumbuka atakapokuwa mkubwa, tukienda kwa bosi tutamwambia wote wamekufa kwani hata hatujui alikuwa na watoto wangapi kwa maisha ya siri aliyokuwa anaishi na familia yake" baada ya kuonekana kukubaliana na hilo walitoka humo ndani wakaondoka na kichwa cha Mr Jonson. Yule mtu aliyekuwa amemsaidia Lenovatus kutoka kwa hao watu baada ya kuhakikisha watu hao wameondoka alishuka kule juu ya kabati akaangaza huku na huku kisha akaelekea mlango wa nyuma wa nyumba na alionekana kuijua vyema sana hiyo nyumba akatokomea zake gizani akiwa amembeba kijana mdogo sana Lenovatus.

Mr Jonson Malisaba ni nani?, Siri gani ambayo aliificha familia yake?, Huyu aliye msaidia Lenovatus ni nani hasa mpaka afike muda kama huu?, kuna nini kinaendelea kati ya hawa watu waliompa Mr Jonson machaguo matatu ya kuchagua? Na hicho kitu kilikuwa na umuhimu gani mkubwa mpaka wafikie hatua kama wakikikosa waue familia nzima ili kusiwe na Shahidi yeyote??......

Ndio kwanza tunaianza hadithi mpya ndani ya sehemu ya kwanza kabisa , utakuwa nami mpaka mwisho wa kisa hiki kinacho mhusu bwana mdogo Jamal utajua kwa undani Jamal yeye ni nani hasa na alipitia nini kweye maisha yake kikubwa usibanduke ungana namimi mpaka mwisho kabisa wa hadithi hii.

Bux the story teller.View attachment 2310192
TITLE YA KITOTO SIWEZI SOMA UPUUZI
 
TITLE YA KITOTO SIWEZI SOMA UPUUZI
Usijali ndugu, TITLE inaweza kuonekana ya kitoto kwa sababu haujui dhamira ya kuiita hivyo ni nini, kwenye literature huwa tunaambiwa elezea jinsi TITLE yako inavyohusiana/endana na kilicho andikwa ndani, nadhani ni ngumu sana kuielewa title kama tu mindset yako ishaamua kuselect hivyo kabla hata hujasoma kilichopo, by the way shukrani sana kwa maoni ndugu[emoji122][emoji122][emoji122]

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
Usijali ndugu, TITLE inaweza kuonekana ya kitoto kwa sababu haujui dhamira ya kuiita hivyo ni nini, kwenye literature huwa tunaambiwa elezea jinsi TITLE yako inavyohusiana/endana na kilicho andikwa ndani, nadhani ni ngumu sana kuielewa title kama tu mindset yako ishaamua kuselect hivyo kabla hata hujasoma kilichopo, by the way shukrani sana kwa maoni ndugu[emoji122][emoji122][emoji122]

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Kwenye literature title means a lot since inaweza mfanya mtu atake au asitake kusoma hadith. So hapo ndo unapaswa utulize kichwa. Wewe umachagua title ambayo mimi kama mchambuzi naona imemaliza kila kitu.

But pia haina ubunifu ni kama unaandika makala ya ndoto ya mtoto flani. Ndo maana nikasema ya Kitoto sana. Sijaweza soma hata hadithi sababu ya kuona title utadhani ya makala ya mtoto siku ya shule darasa la 4-7.
 
Kwenye literature title means a lot since inaweza mfanya mtu atake au asitake kusoma hadith. So hapo ndo unapaswa utulize kichwa. Wewe umachagua title ambayo mimi kama mchambuzi naona imemaliza kila kitu.

But pia haina ubunifu ni kama unaandika makala ya ndoto ya mtoto flani. Ndo maana nikasema ya Kitoto sana. Sijaweza soma hata hadithi sababu ya kuona title utadhani ya makala ya mtoto siku ya shule darasa la 4-7.
Unaweza ukanipa sifa hata tatu za title nzuri mkuu na why title huwa zinatungwa?

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
Unaweza ukanipa sifa hata tatu za title nzuri mkuu na why title huwa zinatungwa?

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
1. Title isimalize hadithi husika
2. Title iweze mfanya msomaji kutaka kujua nini kitakuwa ndani
3. Isiwe conclusive ( asiye sikia la mkuu huvunjika mguu)

Fikiria kama title hii

1. Sifi Mara Mbili
2. Chumba namba 215
3. Hakimu wa Mwisho
4. .....
 
1. Title isimalize hadithi husika
2. Title iweze mfanya msomaji kutaka kujua nini kitakuwa ndani
3. Isiwe conclusive ( asiye sikia la mkuu huvunjika mguu)

Fikiria kama title hii

1. Sifi Mara Mbili
2. Chumba namba 215
3. Hakimu wa Mwisho
4. .....
Ok, shida ya hiyo tittle ni ipi? then nikuletee list ya vitabu vya waandishi wakubwa duniani unitajie title zao zinafit vipi kwenye hizo sifa zako

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
1. Title isimalize hadithi husika
2. Title iweze mfanya msomaji kutaka kujua nini kitakuwa ndani
3. Isiwe conclusive ( asiye sikia la mkuu huvunjika mguu)

Fikiria kama title hii

1. Sifi Mara Mbili
2. Chumba namba 215
3. Hakimu wa Mwisho
4. .....
From what i know hizi ndizo sifa ambazo title inatakiwa kuwa nazo; descriptive, direct, accurate, appropriate, interesting, concise, precise, unique, and should not be misleading

Kwa mfano The Beautyful Ones Are Not Yet Born....rejea kwenye sifa yako ya tatu then itumie kuchambua hii title

It's true title inatakiwa kuwa clear, ya kuvutia, kuleta hamu ya msomaji kuisoma, kitu cha mhimu zaidi unatakiwa kujua why imetumika title kama hiyo lengo au dhamira kuu ni nini?


I WANT TO DIE JUDGE....ukinambia ipo conclusive nitakukatalia....unless uwe na uwezo wa kuchambua kitu ambacho kimeandikwa humo kwa kutumia hiyo title bila kusoma kilichopo, nadhani huwa ni vizuri sana kitu ukijue ndo ujudge....

Sanaa ni pana sanae, sana sometime inatumika ironically huwezi kuielewa bila kuipitia, mpaka sasa haujui why nimetumia title kama hiyo, rejea kwenye hadithi zangu kama ULIMWENGU WA WATU WABAYA, GEREZA LA HAZWA, INNOCENT KILLER hizo title nazitengeneza kulingana na lengo la mimi kuziandika na zinakuwa zinabeba kilichopo ndani iwe ni ironically au ya kudirect kitu kama kilivyo.

I WILL MARRY WHEN I WANT hii nayo tittle utaniambia ya hovyo kwa sababu ipo conclusive?


Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA AROBAINI NA NANE

TULIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA SABA........

Aliye anzisha ni yule komando ambaye alikuwa nyuma ya kiongozi wake alipiga makelele sana alilalamila kwa maumivu makali ya sikio, sikio lake halikuwepo sehemu ambapo lilitakiwa kuwa lilikuwa lipo chini kisu kikali sana kilipita na sikio hilo haikujulikana ilikuwaje na kwa muda gani, kwa kiongozi wa hawa makomando alikuwa anavuja damu nyingi sana kwenye tumbo lake, alikuwa amecharangwa mithili ya mishikaki MUNGU wake utumbo haukuguswa japokuwa tumbo lilikuwa linahitaji apewe matibabu ya haraka sana vinginevyo lingemletea madhara makubwa, kwa Jamal alitaka kitingisha hata mkono wake lakini alishindwa, alihisi labda hakufanya vizuri alijaribu tena lakini ilikuwa ni vile vile tu hakuna kiungo chochote kwenye mwili wake ambacho kilikuwa kinaweza kusogea hakuelewa imekuaje, uso wake ulianza kukumbwa na usingizi ambao hata yeye mwenyewe hakuelewa umetokea wapi alianza kukakamaa mwili mzima, mwili wake ulilegea sana alidondoka chini na kuyafumba macho yake.

ENDELEA........................

Wakati makomando wawili wale wanakuja Jamal alikuwa na kisu mkononi mwake, kiongozi wao alivyorusha mikono yake alikuwa ameshika sindano zenye sumu kali sana mkononi mwake ndizo ambazo aliziachia wakati ule anairusha mikono yake kwa nguvu ilikuwa ni kazi ngumu sana kuweza kuziona kiurahisi ndio maana Jamal hakuweza kulitambua hilo mpaka zinazama mwilini mwake, sumu iliyokuwa ndani ya sindano hizo ilikuwa ikimaliza nguvu zote za mwili na kuufanya mwili uweze kukakamaa na kama zikiachwa kwa zaidi ya dakika tano bila kutolewa basi huwa ni lazima mtu aliye chomwa apoteze maisha.


Kitendo cha kumkwepa kiongozi huyo wa hao makomando mwanume aliinama kidogo na kupitisha kisu hake kidogo hicho kwenye tumbo la mwanaume mkomavu huyo na kulifanya lichanike hovyo hovyo baada ya hapo kisu kilirushwa kwa nguvu kwa komando wa nyuma ambaye alikuwa amebakiza hatua mbili tu amfikie Jamal.



***************************
Kukamatwa kwa gaidi aliyehusika kumuua mheshimiwa makamu wa raisi wa nchi ambaye alisemekana kuwa komando mkubwa sana ndiyo habari ambayo ilikuwa ikizungumziwa kila pande ya Tanzania, Afrika pamoja na dunia kwa ujumla, hakuna sehemu ambayo habari hiyo haikufika. Watu wana siri sana ila sio kwa utandawazi mkubwa uliopo kwa sasa hasa pale Jambo linapofika kwenye mkono wa mitandao ya kijamii, kila sehemu hiyo ndiyo iliyokuwa topic bora zaidi ndani ya nchi ya Tanzania, watu walikuwa wapo busy sana kuzungumzia jambo hili huku habari za chini chini ikisemekana kwamba mtu huyo alikuwa akifikishwa mahakamani siku ya mchana huo na kesi yake ilikuwa inasomwa siku hiyo hiyo watu walikuwa wapo makini sana kufuatilia kila hatua ili waweze kuujua mwafaka wa mwanaume kijana mdogo sana ambaye alikuwa amefanya tukio la kihistoria tangu nchi hii iweze kupata uhuru.



Moyo huwa ni kitu cha hovyo na cha ajabu zaidi kuwahi kutokea kwenye maisha ya mwanadamu yeyote yule, moyo ndicho chanzo cha lawama zote ambazo wanazitoa wanadamu kwa sababu walishajihalalishia kwamba moyo kazi yake kubwa ni kupenda kitu ambacho huwa kinakuja kuwaletea maumivu mazito sana baadaye na huwa wanakosa kabisa msaada kwa sababu wanatengeneza imani kwa wanadamu ambao wamekutana nao ukubwani tu na hawakuwahi hata kujuana huko nyuma.


Nimeuita ni kitu cha hovyo kwa sababu ukitoa umaskini moyo ndicho kitu ambacho kinaongoza kuleta maafa mengi duniani, unapo bahatika kuwa mbali na magonjwa ya moyo yanayo sababishwa na mapenzi basi unatakiwa umshukuru sana MUNGU kukuepusha na kikombe cha mwana haramu mapenzi.

Ndani ya nchi ya Cuba Catheline Yudel mtoto wa mr Yudel ambaye alikuwa ni kiongozi mkuu wa kambi kubwa zaidi ya kikomando ndani ya nchi hiyo alikuwa ametoka kuoga wakati anafika chumbani kwake baada ya kuvaa nguo yake laini ili aweze kumpumzika aliweza kuiona taarifa ya habari ya mheshimiwa raisi wa Tanzania kuhusu mtu mmoja ambaye alijulikana kwa jina la LENOVATUS kutafutwa baada ya kumuua makamu wa raisi wa nchi, picha aliyo iona ndicho kitu kilicho mshtua alikuwa ni mpori pori wake Jamal ambaye siku ya mwisho alimuahidi atakuwa naye kwenye sehemu yoyote ile duniani na popote pale atakapokuwa, hakuamini hicho kitu alikuwa amepanga kukikucha aanze rasmi kulifuatilia hilo jambo lakini baada ya asubuhi kukucha alijutia sana kuchelewesha maamuzi yake.

Alikuwa akitokwa na machozi mengi sana muda huo kwani baada ya kuwasha simu yake na kuingia kwenye mitandao ya kijamii taarifa za kukamatwa kwa mtu huyo ambaye alipewa jina la gaidi zilisambaa mno na mchana wake ilisemekana ndio muda ambao kesi yake ilikuwa inaenda kusomwa mahakamani.

Ilimhitaji sio chini ya masaa 23 kuweza kufika kwenye nchi ya Tanzania maana yake hakuwa na uwezo wa kuwahi mahakamani kwa sababu ilikuwa ni siku nzima kuweza kufika Tanzania hata hivyo hakukata tamaa mwanadada huyu mrembo ambaye alikuwa jasusi wa nchi ya Cuba, alipanga vitu vyake vya mhimu na kutoka ndani kwake, alikuwa anakuja Tanzania kulipigania penzi la mwanaume wa kwanza kwenye maisha yake ambaye ndiye aliye mtoa bikra yake hawezi kuusahau usiku ule hata siku moja ilikuwa ni miongoni mwa siku bora sana yeye kuwahi kuipitia. Alijisahau kabisa kwamba yeye ni komando wa nchi na hakuruhusiwa kabisa kwenda popote bila ruhusa ya mkubwa wake, mapenzi yalimchanganya hakuna kitu ambacho angeweza kuelewa kwa mtu ambaye angehitaji kumzuia.


*****************
Muda na umri ndivyo vitu pekee duniani ambavyo huwa havisimami kabisa hilo unatakiwa kulielewa kwa umakini sana, unavyo yaishi maisha yako inabidi uende kwa usahihi na hizo hesabu mbili kama ukiikosea hata moja basi utayaishi maisha yako kwa majuto sana. Mchana ulikuwa umefika jua kali sana la jiji la Dar es salaam haikuwa sababu ya kuwafanya watu washindwe kufika kwenye mahakama kuu ya nchi inayo husika na makosa ya jinai hapo ndipo palipo amuliwa kwenda kutoa hatima ya kesi ya kijana Jamal, kila kituo cha habari siku hiyo kilikuwa na soko sana waliuza mno walitamani habari za aina hiyo ziwe zinatokea kila siku kwani habari mbaya ndizo huwa zinauza sana, mchana huo hakuna hata mwananchi mmoja ambaye alikuwa akizurura mtaani, watu walikuwa wameyakaza macho yao kwenye kila runinga zao mtaani majenereta yaliandaliwa ili kama ikitokea umeme ukikatika kusiwe na tatizo lolote lile la umeme kukatika wasiweze kuikosa hiyo kesi, ndiyo ilikuwa kesi ya kwanza ya mauaji kuweza kuonyeshwa laivu ikiwa ni kama onyo kali kwa watu ambao walikuwa na tabia za hovyo kama za Jamal kwa kuziasi nchi zao kitu ambacho sheria ilikuwa hairuhusu kabisa.


Watu walijazana nje ya mahakama kumshuhudia kijana huyo ambaye wengi wao walishangaa sana kwani alionekana bado ni mdogo sana hakuna ambaye alitegemea kwamba anaweza kufanya tukio kama hilo la kutisha, watu walikuwa na simu zao wakirekodi tukio hilo moja kwa moja ili wakasambaze kwenye mitandao kama ilivyokuwa kawaida yao watu wengi kuliko kuwaza mambo ya maendeleo kwao mitandao ndilo chaguo sahihi zaidi kwa maisha yao, mwanaume alikuwa amechakaa damu kwenye mwili wake kuonyesha wazi alipigwa vikali mno ni shehemu ya uso tu ndiyo ilikuwa inatazamika hakuwa kwenye hali nzuri kitu ambacho hata wananchi kiliwatisha kwani hata kama alifanya makosa basi hakustahili kufanyiwa hivyo kwa kuzingatia haki za binadamu.

***************************
“Ndugu Jamal umahusishwa na kesi ya mauaji ya mheshimiwa makamu wa raisi wa nchi ya Tanzania, je kuna ukweli gani wa hili tukio ni kweli wewe ndiye uliye lifanya kwa mikono yako na ukiwa timamu kabisa kichwani?” ilikuwa ni sauti ya jaji baada ya kuingizwa ndani ya mahakama.


“Sijaua” ni sauti nzito sana yenye mkwaruzo kutoka kwa Jamal akiwa kwenye pingu pale kizimbani ambapo alikuwa amesimama


“Kama hujaua wewe kwanini wewe ndiye ukamatwe?”

“Nadhani hilo swali ungewauliza walio nikamata”

“Ninavyo kuuliza swali Mr Jamal unatakiwa kutoa ushirikiano na sio kunijibu jeuri utakuwa unaenda kinyume na sheria za mahakama kitu ambacho ni hatari sana”

“Sawa”

“Sasa kwanini tuamini kwamba wewe haujaua?” sauti ya jaji ilisikika na ndiyo iliyo mfanya atabasamu japo alikuwa na maumivu makali sana


“Wewe kama jaji una ushahidi gani wa kujihakikishia kama mimi ndiye niliye ua?” swali la Jamal lilimfanya jaji mkuu amkazie macho Jamal

“Vipi kama ushahidi ukiletwa mbele ya mahakama utafanyaje”

“Kama ni hivyo kweli basi nataka kufa hakimu (I WANT TO DIE JUDGE) niue nitaipokea adhabu ” mwanaume aliongea akiwa hana hata tone la wasi wasi watu walikuwa kimya wakimshangaa kijana huyo alivyokuwa anajiamini sana kwenye sehemu ambayo binadamu wengi huwa wanaiogopa mno, Mahakama sio sehemu ya kuombea kupelekwa panatisha sana hususani kama unapelekwa kwa makosa ya jinai, kama ni kijana hakikisha unayaishi maisha kwa usahihi kukwepana na dhahama hii ya kwenda mahakamani ni hatari sana jela sio sehemu nzuri kwa mtu mwenye ndoto. Mheshimiwa jaji alinyoosha mkono wake kama ishara ya kuweza kumuita mtu, kuna mwanaume mrefu alikuwa akiingia hapo ndani akiwa na miwani yake safi usoni hakuwa hata na presha, nguo zake tu zilitosha kumuaminisha mtu yeyote mwenye macho kwamba huyo ni mwanasheria lakini aina ya vazi lake lilikuwa ni tofauti sana na ya wanasheria wengine.

Nicolous Philemone ndilo lilikuwa jina halisi la mtu huyo ambaye ndiye mwana sheria mkuu wan nchi ya Tanzania, alikuwa yupo hapo baada ya Jamal kugoma kabisa kwamba yeye hakuhusika kabisa kwenye hayo mauaji ambayo walisema ameyafanya, aliulizwa kama akikutwa na hatia wamfanye nini alisema mwenyewe kwamba wamuue sasa huyu aliyekuwa amekuja hapa alikuwa yupo kwa ajili ya kulithibitisha hilo, aliijua sheria kuliko hata jina lake na ndiye aliyekuwa akizisimamia sheria zote za nchi kazi ilikuwa ipo kwake.

“Mr Jamal umesema sio wewe uliye husika na hili tukio na mbele ya mahakama umekana kabisa huku ukidai kwamba kama ukikutwa na hatia basi upo tayari kupokea adhabu yoyote hususani ukidai kufa una uhakika na maamuzi yako na hauta yajutia?” wanasheria ni watu hatari sana maelezo yako ndiyo yanayo kufunga ukiwa mbele ya hao watu angalia kila aina ya neno ambalo linakutoka kinywani kwani linaweza kukuharibia kila kitu ndicho alichokuwa anakifanya mwanaume huyu kesi kwake ilikuwa ni rahisi sana kupitia tu maelezo yake ndiyo aliyokuwa anaenda kuwashangaza mamilioni ya watanzania ambao walikuwa wakishuhudia kila kitu.

“Yes, nipo tayari”

“Sawa” hakuongea sana kuna frashi ndogo alienda kuichomeka kwenye skrini kubwa iliyokuwa ikitumika kutolea ushahidi wa video pamoja na sauti za mfumo wa audio pale inapo hitajika, kilichokuwa kinaonekana kwenye hiyo video kiliwashangaza watu wengi sana kila aliyekuwa anaangalia alimfumba mtoto wake macho, unyama ambao ulikuwa unafanyika ndani ya hiyo video ulikuwa unatisha sana sura ya Jamal ilikuwa inaonekana kwa usahihi akiwa ndani ya gwanda ambalo huwa linavaliwa na makomando tu pekee hata mwanajeshi wa kawaida haruhusiwi kabisa hata kuligusa.

Silaha nzito ya maangamizi aliyo itumia kuvamia msafara huo ilitisha namna alivyokuwa akiwatoboa maaskari kwa risasi, aina ya kisu ambacho alikitumia kukata baadhi ya shingo za watu hao namna kilivyokuwa kinazungushwa kiliwatisha watu wenye roho nyepesi waliyafumba macho yao hakuna ambaye aliamini binadamu anaweza kuwa na roho ngumu kiasi hicho kiasi kwamba anachinja wenzake mithili ya kuku.

Tukio lililo leta msisimko zaidi ni pale wakati mtu huyo amemfikia makamu wa raisi namna mzee huyo alivyokuwa anaomba msamaha akitoa kilio kiliwafanya wengi wamuonee huruma sana hata hivyo hakuna ambacho kilisaidia kwani ilikuwa ni tayari alishakufa alimmiminia risasi nyingi sana mtu huyo alikufa hapo hapo kisha mwanaume akapotelea kwenye vichochoro na kutokomea huko. Video hiyo ilizalisha minong’ono mingi sana hiyo sehemu wenye roho nyepesi walibaki wanaangua kilio mahakamani na hata wale ambao walikuwa wanaangalia kwenye video zao nchi ilikuwa imefikia sehemu mbaya sana matukio kama hayo kuweza kufanyika.

Nisiwe muongeaji sana mtuhumiwa alitaka kuuawa, ushahidi upo wazi ni yeye kweli ndiye aliyeua hukumu mikononi mwa jaji, Mr mind mwanasheria mkuu ameshamaliza kazi yake nini kinatokea?.......48 naweka nukta hapa tukutane tena wakati ujao[emoji3578]

Bux the story teller

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Hiki kipande ni kirefu mno kitausindikiza usiku wako

Enjoy

Bux the story teller

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
From what i know hizi ndizo sifa ambazo title inatakiwa kuwa nazo; descriptive, direct, accurate, appropriate, interesting, concise, precise, unique, and should not be misleading

Kwa mfano The Beautyful Ones Are Not Yet Born....rejea kwenye sifa yako ya tatu then itumie kuchambua hii title

It's true title inatakiwa kuwa clear, ya kuvutia, kuleta hamu ya msomaji kuisoma, kitu cha mhimu zaidi unatakiwa kujua why imetumika title kama hiyo lengo au dhamira kuu ni nini?


I WANT TO DIE JUDGE....ukinambia ipo conclusive nitakukatalia....unless uwe na uwezo wa kuchambua kitu ambacho kimeandikwa humo kwa kutumia hiyo title bila kusoma kilichopo, nadhani huwa ni vizuri sana kitu ukijue ndo ujudge....

Sanaa ni pana sanae, sana sometime inatumika ironically huwezi kuielewa bila kuipitia, mpaka sasa haujui why nimetumia title kama hiyo, rejea kwenye hadithi zangu kama ULIMWENGU WA WATU WABAYA, GEREZA LA HAZWA, INNOCENT KILLER hizo title nazitengeneza kulingana na lengo la mimi kuziandika na zinakuwa zinabeba kilichopo ndani iwe ni ironically au ya kudirect kitu kama kilivyo.

I WILL MARRY WHEN I WANT hii nayo tittle utaniambia ya hovyo kwa sababu ipo conclusive?


Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Bahati mbaya sijazisoma zote hizo. Ila title ambayo ningeipenda ni
1. Gereza la Hazwa
2. Ulimwengu wa watu wabaya

I will marrry when i want ni ironical au sarcastic.
 
IMG_9645.jpg
 
Back
Top Bottom