Ibrahim Class 'Mawe' na mabondia wengine wa Tanzania wanatakiwa kujifunza baada ya tukio alilolifanya Ibrahim

Ibrahim Class 'Mawe' na mabondia wengine wa Tanzania wanatakiwa kujifunza baada ya tukio alilolifanya Ibrahim

Ali Nassor Px

JF-Expert Member
Joined
May 6, 2022
Posts
2,384
Reaction score
3,926
Boxer ni mchezo ambao unahitaji umpelekee mashambulizi mwenzako ili wewe ushinde. Lakini pamoja na mashambulizi hayo, yupo refa na Masecond ambao wote kazi yao ni kuwalinda mabondia ndani ya uwanja.

Lakini ni kazi ya bondia pia yeye mwenyewe kujilinda. Lakini la ziada kabisa ambalo mabondia nadhani wengi hawalijui ni kumlinda pia mpinzani wako pale inapofikia hatua ya hatari kama hatua ya kumuona jamaa anaelekea kupoteza fahamu au kufa.

Tarehe 16 mwezi wa kwanza Mwaka 1999 Mike Tyson alipigana na Francois Botha na akampiga Botha akadondoka vibaya sana, lakini Tyson hakushangilia. Alichokifanya alishirikiana na refa kumnyanyua Botha ili asianguke tena.

Huo unaitwa ubinadamu ndani ya mchezo, ule ni mchezo na sio vita.

Alichokifanya Ibrahim Classic kwa mpinzani wake Allan Pinna sio kitendo cha kiungwana kabisa, na sijapenda maana Pinna alikuwa keshalewa anaenda chini mwenyewe Ibrahim Classic alikuwa na haja gani ya kutumia nguvu za ziada kumpeleka chini haraka?

Lakini leo hii watu wapo kimya kwa vile labda Ibrahim Classic ni bondia wetu kampiga bondia wa kigeni. Imagine kama pinna ndiyo angempiga jamaa hivyo.

Leo hii watu wengi wangemtukana sana Pinna, tungekilaani kile kitendo kwa nguvu zote.

Pinna jana katoka salama ndani ya uwanja hilo ni jambo la kushukuru, ila kama Pinna atakuja kufa kutokana na athari zilizotokana na lile pambano nadhani Ibrahim Classic hawezi kukaa kwa amani kamwe katika maisha yake.

Mabondia wanatakiwa wapewe elimu ya kujilinda, kuwalinda wapinzani wao na utu na ubinadamu ndani ya ulingo.

 
Boxer ni mchezo ambao unaitaji umpelekee mashambulizi mwenzako ili wewe ushinde. lakini pamoja na mashambulizi hayo yupo refa na masecond ambao wote kazi yao ni kuwalinda mabondia ndani ya uwanja...
Tanzania kwa ujumla hatujui thamani ya utu.
Vinginevyo Ndugai asingemfanyia Lissu ukatili na watu walikaa kimya kama hakuna kilichotokea.

Hapohapo kuna wabunge hawana chama wanakula good time.

Chunguza vizuri utajua tu hatuna utu
 
Nilidhani Ibrah kafanya kitendo fulani kibaya na cha hatari, kumbe kafanya finishing.

Anyway, wabongo ni kama Chadema tu, hatujui tunatakaga nini

Mara kaletewa bondia mbovu, mara kabebwa kisa mtz, Haya kamtwanga vizuri mmeshaanza kubwabwaja.

Mleta mada utakuwa na matatizo ya akili
 
Nilidhani Ibrah kafanya kitendo fulani kibaya na cha hatari, kumbe kafanya finishing.

Anyway, wabongo ni kama Chadema tu, hatujui tunatakaga nini

Mara kaletewa bondia mbovu, mara kabebwa kisa mtz, Haya kamtwanga vizuri mmeshaanza kubwabwaja.

Mleta mada utakuwa na matatizo ya akili
Hujaielewa mada umejiandaa kupinga tu
 
Wakati pambano linaendelea mlianza kusema ibra kapigwa while alikuwa ana score vizuri tu. Kapiga mtu mnaanza ooh ibra kazingua!

Mara ngapi mandonga kapigwa vitasa kama vile anaanguka hajielewi na mpinzani wake anashangalia hamjawahi kulisemea? Wabongo mtaacha lini shobo na kuthamini vyenu! Zile ngumi sio rede
 
Tanzania kwa ujumla hatujui thamani ya utu.
Vinginevyo Ndugai asingemfanyia Lissu ukatili na watu walikaa kimya kama hakuna kilichotokea.

Hapohapo kuna wabunge hawana chama wanakula goid time.

Chunguza vizuri utajua tu hatuna utu
Nailed
 
Nimetokea kumchukia huyo ibra tokea jana alifanye Hilo tukio baya sna .kila saa Hilo tukio linanirudia na naumia sna naisi yule bondia hatakuwa sawa na hata pigana Tena Kama akipona mnk amepata shambulio baya San

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Angepigwa ibra vile leo mngekuwa mshamgeuza meme!
 
Nafikiri Makocha Wa Mabondia wetu Waongeze hayo Mafunzo Ya Tahadhari Kwa Mabondia.

Niliona Pambano La Mwisho La Mandonga, Refa Amesimama Katikati hajaruhusu ngumu Ziendelee Lkn Yule Bondia pinzani akawa anataka Kuendelea kupiga...!

Hii michezo Japo ina Mikwara mingi Lkn ni sehemu Ya Furaha.
 
Nimetokea kumchukia huyo ibra tokea jana alifanye Hilo tukio baya sna .kila saa Hilo tukio linanirudia na naumia sna naisi yule bondia hatakuwa sawa na hata pigana Tena Kama akipona mnk amepata shambulio baya San

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
hahaahahha, wabongo ndomaana tunawahi kufa mapema na mapresha na mistress isiyokua na maana

Sasa unamchukia jamaa kwa lipi? ivi kabla ya jana ulikua unamjua Ibra kweli weweeee?!!!

Acha kujibebesha mafeelings yasikupa faida yoyote ile kwenye maisha yako...Ishi peacefully mkuu, relax!!!
 
Nilidhani Ibrah kafanya kitendo fulani kibaya na cha hatari, kumbe kafanya finishing.

Anyway, wabongo ni kama Chadema tu, hatujui tunatakaga nini

Mara kaletewa bondia mbovu, mara kabebwa kisa mtz, Haya kamtwanga vizuri mmeshaanza kubwabwaja.

Mleta mada utakuwa na matatizo ya akili
Nilidhani Ibrah kafanya kitendo fulani kibaya na cha hatari, kumbe kafanya finishing.

Anyway, wabongo ni kama Chadema tu, hatujui tunatakaga nini

Mara kaletewa bondia mbovu, mara kabebwa kisa mtz, Haya kamtwanga vizuri mmeshaanza kubwabwaja.

Mleta mada utakuwa na matatizo ya akili
ibra alikuwa kashamaliz finishing alichez foul ambay ilkuw inapelk hatar kwa mpinzan wake eb tazma vzr hy video boss.... acha kutetea vitu tazm vzr mtazam pinna mtazm ibra mtazm na refree njau
 
Upo sahihi 100% hata mimi kijiweni tumelizungumza sana. Ibra na kambi yake hawakufanya fea. Ona yule mhindi alivyomtandika ndugu yetu jamaa alivyoona anaanguka hakumfuata akaweka mikono nyuma akatulia kabisa. Na hata mwisho alishangilia kishkaji sana kwa kunyanyua bendera ya India akatoka ulingoni.
 
Back
Top Bottom