Ibrahim Class 'Mawe' na mabondia wengine wa Tanzania wanatakiwa kujifunza baada ya tukio alilolifanya Ibrahim

Hata mimi naunga mkono hoja. Labda Ibra alitakiwa tu aoneshe uungwana kwa kutoshangilia sana, japo hata kushangilia siyo kosa.

Kama refa hajasimamisha mchezo kwa kweli lazima upeleke masumbwi kadri uwezavyo ukipata fursa ya kufanya hivyo. Ukijifanya msamaria mwema, round ijayo kibao kinaweza kugeuka.

Mchezo wa ngumi ni hatari, kila bondia analijua hilo.
 
Halafu mnaanzaje kumshangaa Ibra kushangilia kama kichaa jamani?

Mna uhakika gani kama Ibra akili zipo sawa, wakati mnajua kabisa mabondia wanapigwa ngumi za kichwa na kuvuruga akili?
 
Sijawahi penda hii michezoa ya kupigana pigana. Labda mieleka kwakua najua ni acting.

Yaani mtu from nowhere anakuja mnaanza kupigana ili wengine wafurahie. Unyama huo. Ni kama zile movie za Spartacus yaani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…