Pre GE2025 Idadi kubwa ya wapiga kura ndilo kaburi la CCM

Pre GE2025 Idadi kubwa ya wapiga kura ndilo kaburi la CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Duniani kote hakuna kitu kinachoogopwa na serikali dhalimu kama idadi kubwa ya wapiga kura.

Baada ya Tume inayosimamia uchaguzi TAMISEMI kudanganya idadi halisi ya waliojiandikisha, kazi iliyo mbele yao kwa sasa ni namna gani watabadilisha hiyo idadi ziwe kura.

Kwa mfano; Mwanza, Sensa ya 2022 idadi ilikuwa 1.95M zaidi ya nusu wakiwa ni watoto chini ya miaka 14, leo wameandikisha 2,08M. Siku ya kupiga kura watawatoa wapi hao watoto waje kupanga foleni wapige kura, mashuleni au mitaani?

Kwa hali halisi ilivyo mitaani na vijijini, chuki ya wananchi kwa CCM na viongozi wake wa mitaa na vitongoji ni kubwa sana, hasira ya ugumu wa maisha kwa wananchi hasa vijana wataimalizia kwenye sanduku la kura.

Mbali na hiyo chuki ya wananchi, ndani ya CCM kwenyewe kuna makundi hasimu yanayotaka mgombea wao apite hivyo kugawa kura.

Kwenye chaguzi zilizopita CCM ilikuwa inasingizia wananchi hasa vijana hawajitokezi kujiandikisha, walitoa hicho kisingizio kwa vile ilionekana vijana wengi walikuwa wanaviunga mkono vyama vya upinzani, safari hii takwimu zinaonesha vijana wengi wamejiandikisha.

Ukichukulia hali hii na idadi kubwa ya waliojiandikisha iwapo wote wataamua kujitokeza kupiga kura, basi CCM watakuwa na kazi kubwa ya kuiba zaidi ya nusu ya kura kitu ambacho ni next to impossible.

Kati ya kura 1,000,000 unaweza kuiba kura laki moja (100,000) lakini siyo laki tano (500,000), hilo likitokea basi utakuwa ni wizi mkubwa kuwahi kutokea na utaweka historia Tanzania.

Kwa idadi hii nadiriki kusema CCM wamejichimbia kaburi lao wenyewe kinachotakiwa kwa vyama vya upinzani sasa ni kuhamasisha watu hasa vijana wajitokeze kwa wingi siku ya kupiga kura.
 
Duniani kote hakuna kitu kinachoogopwa na serikali dhalimu kama idadi kubwa ya wapiga kura.

Baada ya Tume inayosimamia uchaguzi TAMISEMI kudanganya idadi halisi ya waliojiandikisha, kazi iliyo mbele yao kwa sasa ni namna gani watabadilisha hiyo idadi ziwe kura.

Kwa mfano; Mwanza, Sensa ya 2022 idadi ilikuwa 1.95M zaidi ya nusu wakiwa ni watoto chini ya miaka 14, leo wameandikisha 2,08M. Siku ya kupiga kura watawatoa wapi hao watoto waje kupanga foleni wapige kura, mashuleni au mitaani?

Kwa hali halisi ilivyo mitaani na vijijini, chuki ya wananchi kwa CCM na viongozi wake wa mitaa na vitongoji ni kubwa sana, hasira ya ugumu wa maisha kwa wananchi hasa vijana wataimalizia kwenye sanduku la kura.

Mbali na hiyo chuki ya wananchi, ndani ya CCM kwenyewe kuna makundi hasimu yanayotaka mgombea wao apite hivyo kugawa kura.

Kwenye chaguzi zilizopita CCM ilikuwa inasingizia wananchi hasa vijana hawajitokezi kujiandikisha, walitoa hicho kisingizio kwa vile ilionekana vijana wengi walikuwa wanaviunga mkono vyama vya upinzani, safari hii rekodi zinaonesha vijana wengi wamejiandikisha.

Ukichukulia hali hii na idadi kubwa ya waliojiandikisha iwapo wote wataamua kujitokeza kupiga kura, basi CCM watakuwa na kazi kubwa ya kuiba zaidi ya nusu ya kura kitu ambacho ni next to impossible.

Kati ya kura 1,000,000 unaweza kuiba kura laki moja (100,000) lakini siyo laki tano (500,000), hilo lilitokea basi utakuwa ni wizi mkubwa kuwahi kutokea na utaweka historia Tanzania.

CCM wamejichimbia kaburi lao wenyewe kilinachotakiwa kwa vyama vya upinzani sasa ni kuhamasisha watu hasa vijana wajitokeze kwa wingi siku ya kupiga kura.
acha upotoshaji gentleman,

Idadi kubwa ya wanachama wa CCM waliojiandikisha kupiga kura ndio hasa chachu na msingi wa ushindi wa kishindo kwa kila uchaguzi ambao CCM wanashiriki na si vinginevyo..

Ni upotoshaji wa kiwango cha juu zaidi kulinganisha matokeo ya sensa ambayo ambayo hayana kampeni wala sera na ambayo hufanyika katka kipindi cha zaidi ya miaka 10 na uchaguzi mkuu au wa serikali za ambao ni hufanyika kila baada ya miaka mi5.

Na ndiyo maana mara zote tunasema humu jukwaani na waTanzania wote wanajua, kwamba mchujo wa kura za maoni ndani ya CCM huwa una hamasa na shauku kubwa zaidi ya uchaguzi mkuu wenyewe, kwasababu, ndani ya chama hicho ndiyo waTanzania huamua mustakabali wa uongozi wa nchi yao.

Hata hivyo,
uchaguzi mkuu hua ni kukamilisha ratiba ya uchaguzi, taratibu za kisheria na kikatiba tu, kwasabb tayari wananchi wameshaamua mustakabali wao kupitia CCM 🐒
 
Ni upotoshaji wa kiwango cha juu zaidi kulinganisha matokeo ya sensa ambayo ambayo hayana kampeni wala sera na ambayo hufanyika katka kipindi cha zaidi ya miaka 10 na uchaguzi mkuu au wa serikali za ambao ni hufanyika kila baada ya miaka mi5.
Unabishana na takwimu?

Takwimu sio siasa ni facts, ila ukidanganya kama alivyofanya Mchengelwa zinakuwa siasa. After all hata wakati wa Sensa kulikuwa na kampeni.

Uongo ni kwamba watu wote wa mkoa wa Mwanza wameandikishwa kupiga kura wakiwemo watoto wa miaka mitatu, how?

20241024_062153.jpg
 
Unabishana na takwimu?

Takwimu sio siasa ni facts, ila ukidanganya kama alivyofanya Mchengelwa zinakuwa siasa. After all hata wakati wa Sensa kulikuwa na kampeni.

View attachment 3133870
kwahivyo sasa unataka takwimu zifanyaje kwa mfano gentleman 🤣

zipungue, zisipungue, ziongezekea au zisiongezeke zibaki static tu?

Kwa mfano,
kuna tatizo gani kwenye takwimu hizo ambazo ni very reasonable kabisa hata kama si halisi?🐒
 
kwahivyo sasa unataka takwimu zifanyaje kwa mfano gentleman 🤣

zipungue, zisipungue, ziongezekea au zisiongezeke zibaki static tu?

Kwa mfano,
kuna tatizo gani kwenye takwimu hizo ambazo ni very reasonable kabisa hata kama si halisi?🐒
Uongo ni kwamba watu wote wa mkoa wa Mwanza wameandikishwa kupiga kura wakiwemo watoto wa miaka mitatu, how?
 
Uongo ni kwamba watu wote wa mkoa wa Mwanza wameandikishwa kupiga kura wakiwemo watoto wa miaka mitatu, how?
hayo ni maoni na mitazamo wako potofu ambao ni haki na uhuru wako..

ukweli ni kwamba walioandikishwa kote nchini, ni wale tu wenye sifa na vigezo vya kikatiba vya kupiga kura na si vinginevyo 🐒
 
Duniani kote hakuna kitu kinachoogopwa na serikali dhalimu kama idadi kubwa ya wapiga kura.

Baada ya Tume inayosimamia uchaguzi TAMISEMI kudanganya idadi halisi ya waliojiandikisha, kazi iliyo mbele yao kwa sasa ni namna gani watabadilisha hiyo idadi ziwe kura.

Kwa mfano; Mwanza, Sensa ya 2022 idadi ilikuwa 1.95M zaidi ya nusu wakiwa ni watoto chini ya miaka 14, leo wameandikisha 2,08M. Siku ya kupiga kura watawatoa wapi hao watoto waje kupanga foleni wapige kura, mashuleni au mitaani?

Kwa hali halisi ilivyo mitaani na vijijini, chuki ya wananchi kwa CCM na viongozi wake wa mitaa na vitongoji ni kubwa sana, hasira ya ugumu wa maisha kwa wananchi hasa vijana wataimalizia kwenye sanduku la kura.

Mbali na hiyo chuki ya wananchi, ndani ya CCM kwenyewe kuna makundi hasimu yanayotaka mgombea wao apite hivyo kugawa kura.

Kwenye chaguzi zilizopita CCM ilikuwa inasingizia wananchi hasa vijana hawajitokezi kujiandikisha, walitoa hicho kisingizio kwa vile ilionekana vijana wengi walikuwa wanaviunga mkono vyama vya upinzani, safari hii takwimu zinaonesha vijana wengi wamejiandikisha.

Ukichukulia hali hii na idadi kubwa ya waliojiandikisha iwapo wote wataamua kujitokeza kupiga kura, basi CCM watakuwa na kazi kubwa ya kuiba zaidi ya nusu ya kura kitu ambacho ni next to impossible.

Kati ya kura 1,000,000 unaweza kuiba kura laki moja (100,000) lakini siyo laki tano (500,000), hilo likitokea basi utakuwa ni wizi mkubwa kuwahi kutokea na utaweka historia Tanzania.

Kwa idadi hii nadiriki kusema CCM wamejichimbia kaburi lao wenyewe kilinachotakiwa kwa vyama vya upinzani sasa ni kuhamasisha watu hasa vijana wajitokeze kwa wingi siku ya kupiga kura.
Hujui ukisemacho!
 
Ingekuwa sahihi kama ni kweli hao watu wamejiandikisha.
 
Kati ya kura 1,000,000 unaweza kuiba kura laki moja (100,000) lakini siyo laki tano (500,000), hilo likitokea basi utakuwa ni wizi mkubwa kuwahi kutokea na utaweka historia Tanzania.
Ilishatokea 2020 uchaguzi Mkuu, Jimbo la January Makamba, akiwa yeye Ndio msimamizi wa Ile tallying centre, waliojiandikisha walikua 20,000 na waliompigia Kura magufuli walikua 40,000
 
kwahivyo sasa unataka takwimu zifanyaje kwa mfano gentleman 🤣

zipungue, zisipungue, ziongezekea au zisiongezeke zibaki static tu?

Kwa mfano,
kuna tatizo gani kwenye takwimu hizo ambazo ni very reasonable kabisa hata kama si halisi?🐒
Uwe hata na aibu au angalau ka akili kidogo ndugu. Hizi takwimu zinaonesha uozo mkubwa kwenye uchaguzi huu, Ni takwimu za kupika hata mtoto wa darasa la sita mwenye akili nzuri ataona hilo.
 
hayo ni maoni na mitazamo wako potofu ambao ni haki na uhuru wako..

ukweli ni kwamba walioandikishwa kote nchini, ni wale tu wenye sifa na vigezo vya kikatiba vya kupiga kura na si vinginevyo 🐒
Kama una knowledge kidogo ya takwimu hizo data za Dar na Mwanza zina maana gani, kama huwezi ku interpolate data achana na mambo ya takwimu tuendelee na siasa taka.

20241024_062153.jpg
 
Kwa hizo takwimu maana yake ambao hata hatujafika kujiandikisha tayari tushaandikishwa kilazima. Kiufupi wamiliki wote wa card za CCM wameshaandikishwa maana ziko electronically controlled.
 
Watasema wagombea wa upinzani wamekosea ku sain…so wamekua disqualified…..Then wanapita bila kupingwa..
 
Back
Top Bottom