Idris Sultan afikishwa katika Mahakama ya Kisutu. Ashtakiwa kwa kumiliki laini ya simu isiyo na jina lake. Aachiwa kwa dhamana

Hivi kuicheka picha ya rais ni kitu kimoja na kumcheka rais??
rejea kisa cha Abunuwas na mlio wa punda



SIKU moja abunuwas alipata dinari zake mia. Akaenda sokoni akanunua punda mzuri, akampanda. Akaenda naye mpaka nyumbani kwake. Hata siku moja akaja mtu kuazima punda wake Abunuwas. Abunuwas akanena, Punda hayuko. Mara Yule punda akalia. Yule mtu akanena, punda si huyo analia, na wewe wasema hayuko? Abunuwas akajibu, sasa wewe umekuja kuazima punda ama umekuja kuazima mlio? Kama umekuja kuazima mlio na mimi nitalia. Abunuwas akalia, Ho! Ho! Ho! Akamwambia, haya panda uende zako.
 
Alicheka picha ya mfalme
Anaweza akakana kwamba hakujua kama yule ndio huyuhuyu John Pombe Joseph wa sasa

Anaweza akasema alikuwa anasmile kwa furaha baada ya kuona lile koti XXXXXXXL na kujiuliza vijana wa sasa wanawezaje kujibana na “slim fit”😎

Bahati nzuri ile clip haikuwa na maneno wala caption yoyote!
 
Naskia harufu ya Idris kupewa kesi ya kukwepa kodi,yani zile m500 zisipotafutiwa kosa sijui
 
Hv kwel kucheka picha ni sawa na kamcheka raisi?,vp kama alicheka lile koti kubwa?
 
nchi (y) africa mtoto chini ya miaka 14 tu alichora picha ya mkuu wao wa nchi ila kisanga walichopata ile familia nahisi hawatokuja kusahau kwenye ulimwengu huu.Simwombei mabaya kijana idd ila nawaza tu alithubutu vp kupost ile video.
 
Aise inashangaza watu mnavyojitoa ufahamu kutetea ujinga wa huyu dogo, hizi siasa zinatupeleka mahali tunasahau maadili yetu kama watanzania. Watanzania tumelelewa katika maadili ya kuheshimu watu waliotuzidi umri, chukulia mfano angekuwa baba yako mzazi amepostiwa na Idris Kama alivyo fanya we ungejisikiaje kama mtoto. Achilia mbali siasa Raisi JPM ana familia ana watoto, wanajisikiaje wanapoona mzee wao amespostiwa kwa kejeli namna ile. Jpm kiumri ni mzazi kwa Idris kwa hiyo kwa mtu uliyelelewa katika maadili ya Kitanzania na ni mfuasi wa dini muislamu au mkristu huwezi kusapoti ujinga aliofanya Idris.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwenye picha ya mzazi/wazazi wake tafadhali aiweke hapa alafu tuite comedian waifanyie mambo yao then tuanze kuizodoa, kucheka, kuikejeli nk, ili tupate taswira ya hiki kinnachoendelea.
 
Suti kama ile ningegaragara kabisa hata kama ingekuwa picha ya baba mzazi, na zipo mbona majumbani huwa tunazicheka saanaa, ni comedy tosha

Ila wametusaidia sana kipindi hiki cha Corona there were a lot to distract us from the distress
 
Amekosea saana Idris kwa kumshiaki na kumcheka Rais. Imagine hata watoto wa Rais wanajisikiaje Baba wanahemuheshimu anadhiakiwa hovyo hovyo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…