Idrisa abadili mawazo. Hatojiuzulu tena

Idrisa abadili mawazo. Hatojiuzulu tena

  • Thread starter Thread starter MegaPyne
  • Start date Start date
wanaposhindwa huleta vioja ! nimekuuliza na ww unauliza wapi na wapi kunguru kunyea manati mzee ? jibu kwanza. kama huwezi lets keep it moving lakini sio kusema kila kitu rais hivi rais vile hadi saa nyingine inakuwa tooo much yaani ni sawa na kusema huyo rais anafanya toooo much skendos zaidi ya kazi iliyomuweka pale KITU AMBACHO SI KWELI !![/QUOTE]

tatizo ni kuwa unaamini kuwa kauli yako ina ukweli na na kauli za wengine hazina ukweli. Umejuaje kuwa "si kweli"?
 
ULICHOONA WEWE HAPO NI TATIZO TU ??hapa tutakesha, ni either nikuache usijibu swali au niendelee kujibizana na wewe ! kama utataka kujibu utajibu usipotaka hautojibu, acha niendelee kurumagia mzinga wangu hapa !
 
ULICHOONA WEWE HAPO NI TATIZO TU ??hapa tutakesha, ni either nikuache usijibu swali au niendelee kujibizana na wewe ! kama utataka kujibu utajibu usipotaka hautojibu, acha niendelee kurumagia mzinga wangu hapa !

nimeshakula bata mzinga wangu so kama kukesha tutakesha hadi uone makosa ya hoja yako na ukubali kuwa I'm right and you are wrong... so lets get it on!
 
heheee, KUKUBALI AM WRONG i will unless i am wrong, but if you want me agree am wrong just to agree with you i will also !
 
heheee, KUKUBALI AM WRONG i will unless i am wrong, but if you want me agree am wrong just to agree with you i will also !

sipendi ushindi wa chee bwana.. na ushindi wa mezani hauna filimbi! so, tunakubaliana kuwa you are left and I'm right?
 
Waziri Karamagi aunga mkono TANESCO kupandisha umeme


Na Joseph Lugendo

WAZIRI wa Nishati na Madini Bw. Nazir Karamagi ameunga mkono mapendekezo ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kupandisha bei ya huduma zake kwakuwa shirika hilo linatakiwa kujiendesha kibiashara.

Akijibu maswali ya waandishi wa habari muda mfupi baada ya kufungua Warsha ya Wadau wa Mafuta ya Petroli iliyohusu majukumu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Dar es Salaam jana, Bw. Karamagi alisema ongezeko la bei limetokana na kuondolewa kwa ruzuku ya Serikali iliyokuwepo kabla ya mapendekezo hayo.

"Si busara kuendelea kutumia fedha za bajeti kutoa ruzuku kuendeshea TANESCO," alisema Waziri Karamagi na kuongeza kwamba wahisani wataishagaa Tanzania ikiwa fedha wanazotoa kupitia mfuko wa bajeti zitatumika kutoa ruzuku kwenye shirika ambalo linazalisha.

Alitaka jamii ielewe kwamba hakuna shinikizo lolote kutoka kwa wahisani kutaka kuondolewa kwa ruzuku hiyo na kuongeza kwamba ni vyema shirika hilo likajiendesha kibiashara.

Hata hivyo, Bw. Karamagi alisema Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) wanayo mamlaka ya kupunguza bei inayopendekezwa kwa kuangalia upotevu wa mapato ulio ndani ya TANESCO kwa kuagiza shirika hilo kufidia sehemu itakayo punguzwa kwa kuziba pengo la upotevu wa mapato litakalobainika.

Kuhusu malalamiko ya wananchi yanayoashiria kupinga ongezeko hilo, Bw. Karamagi alisema wananchi wanaopata huduma ya nishati nchini ni asilimia 10 tu na kwamba wanaopinga ongezeko hilo ni asilimia 8 wanaoishi mjini na ambao wanauwezo ukiwemo wa kusema na kusikika.

"Tunapozungumza ongezeko la bei lazima tulinganishe na wengine ndio tufahamu hali halisi," alisema Bw. Karamagi na kuongeza kuwa hakuna mtu anayependa kuongezewa bei na kwamba wengi wangefurahi kama ingekuwa bure.

Alifafanua kwamba Serikali haihusiki kwenye upangaji wa bei na kwamba ikiwa ongezeko la asilimia 40 ya bei litakubaliwa na EWURA, bado bei hizo hazitazidi zilizopo katika nchi za Afrika Mashariki.

Akielezea hali ya mahitaji ya huduma hizo kwa wateja wapya wa vijijini Bw. Karamagi, alisema Serikali itaendelea kutoa ruzuku vijijini kupitia chombo kilichopo cha Wakala wa Umeme Vijijini.

Kuhusu taarifa za kujiuzulu kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Dkt. Idris Rashid, Waziri Karamagi, alisema shirika hilo lina Bodi ya Wakurugenzi ambayo imepeleka ripoti ofisini kwake wakati anakwenda kufungua warsha hiyo na kuwataka kusubiri mpaka atakapopitia ripoti ya Bodi hiyo.

Aliitaka jamii kuelewa kwamba Dkt. Rashid hakufukuzwa ila atakuwa amejiuzulu mwenyewe jambo ambalo ni hiyari yake kama ilivyo kwa mtu yeyote kuacha kazi anapoona hayupo tayari kuendelea nayo.

Source: Majira

Kwa maelezo haya Dr Idris Rashid amejiuzulu au hajajiuzulu?
 
Kada, Si kila asemalo mwanakijiji ni uongo simply bcoz he is a member of Chadema.

Kilichofanyika ni siasa kuchukua mkondo wake baada ya kuharibu.

Sasa bei itapanda, na Tanga cement watashikishwa adabu. Dr alikuwa anataka hayo tu.

MMempa mfupa uliomshinda FISI sasa anaanza KULILA mnamuingilia. Balozi inabidi apishe wengine tu AMECHOOOOKA!
Fikra zake zimefilisika.
 
Kada, Si kila asemalo mwanakijiji ni uongo simply bcoz he is a member of Chadema.

imani ni imani tu, mtu unaweza kuamini fulani hakuiba kwa sababu ya imani, na mtu anaweza kuamini kuwa mwezi umetengenezwa kwa jibini na ya kuwa kwenye sayari ya Zebaki kuna sura ya mtu. Wenzio wamekuwa wakiamini unachoamini wewe na kwa vile ni imani bora uishikilie maana inaleta mantiki katika unayoyafanya.
 
nini kinaendelea hapa ??

kile kile kilichokuwa kinaendelea toka mwanzo na ambacho kuendelea kwake watu wanaona bora kuendelee. Sasa wanapotokea watu wanaohoji kuendelea kwa kitu hicho basi inaonekana kuwa kuendelea kwake kunatishiwa hivyo wanaotaka kiendelee wanakataa kuendelea kwa wanaohoji; kwa hiyo wanaamua kulinda kile kinachoendelea ili kiendelee...
 
namkumbuka mwalimu wangu anaitwa msembele gademu alikuwa na majibu kama yako wewe ! unamuuliza swali anakujibu reja reja afu anauliza umeelewa, ukimwambia sijaelewa anakwambia kesho natoa quiz ndio wewe !
 
At least we have some alternatives:

1. Plenty of Natural Gas

2. Solar Power.

Kazi kwenu, kwani Lazima mtumie TANESCO... Naungana na FD kama kweli mlikubali jamaa aendeshe shirika kibiashara na hamumpi ruzuku, muache apandishe bei atakavyo provided anaonyesha rationale!!!

In terms of Energy Zote zimepanda bei kwa nini TANESCO mnawakatalia, hivi mbona OILCOM, BP, GAPCO, ORYX hamjawaletea shida?
 
heheee, KUKUBALI AM WRONG i will unless i am wrong, but if you want me agree am wrong just to agree with you i will also !

..habari za siku!

..mzee wewe hata siku moja kukaa kwa amani na watu huwezi?

..wakati mwingine kataa hoja au kitu positively!ujenge hoja!

..hamna haja ya kugombana na watu!watapuuza unachosema hata kama kina maana kuliko walichosema wao!

..ni maoni na ushauri wangu tu!
 
Kwa kweli hata sielewi kwa nini Dr. anaamua kutengua uamuzi wake. Lakini labda niulize huyu jamaa amewahi kushika madaraka makubwa sana kwenye nchi hii... Gavana wa BOT halafu baadaye kuajiriwa kwenye normal Bank kwangu mimi ni demotion... alitakiwa afungue firm yake awe anaisimamia sio kuajiriwa.. Amekuwa MD wa Vodacom hakuweza kufanya cha maana ilikuwa tuu ni juhudi za R.A kuonyesha kuwa na sisi wabongo tunaweza. ila aliprove failure mapema mno.. kwa sasa Meneja mkubwa Tanesco hakuna cha maana kinachofanyika huko.. aliwahi kusema kuwaondoa vishoka sio rahisi (Failure)
Sijui ni kwa nini hatuna PHD holder tanzania ambao wanaweza kusimama na kusema hiki hapana hiki ndio... Ndio maana kuna wau wengine wanasema hakuna haja ya kusoma hadi kwenye level ya Phd kwani sioni wanachokifanya kwenye taif hili... wamekuwa wanasiasa zaidi.
Lini wasomi wetu wata- add value kwa nchi hii??? na sio kwenye mambo yao binafsi?
 
Back
Top Bottom