Ifahamu Mahenge (Ulanga, Morogoro) na siri zake

Ifahamu Mahenge (Ulanga, Morogoro) na siri zake

Mbingu nilifika na kulala siku moja tu na kesho yake kuondoka. Hivyo sikufanikiwa kuyasoma mazingira

Ila niligundua ni eneo lenye chakula cha kutosha sana mf. Mpunga, ndizi, na mahindi eneo la Ikule kutokana na uwepo wa udogo wa rutuba na hali ya hewa nzuri.
Upo sahihi kabsa kule pesa ndo ngumu ila chakula kipo cha kutosha….+nyama na samaki
 
Dah! Hayo maeneo ya Mang'ula A, Mang'ula B, Mwaya, Mgudeni, Kisawasawa, Kiberege, Signal (Ziginali), Sonjo, Mkula, Kidatu, Nyandeo, Mkamba, Ruaha, Ifakara yote, Mahenge, Malinyi, Mngeta kurudi nyuma, nk. Nimepiga sana mishe huko miaka ya 1990's.
Mkuu umesahau Kikwawila na Sagamaganga
 
Kitonga hamna mlima pale ule ni muinuko tu mlima gani unapanda umenyooka,hio ndororo unacheza na kona 24 na zote ni fupi fupi kupanda na kushuka,ila waliozoea kina kidinilo wanapanda na kushuka kwa 60 wanacheza na stopper sana.
Usie mzoefu lazima wakakuokote chini mita elf 3 Kama Sio 6 bondeni huko
 
Kitonga hamna mlima pale ule ni muinuko tu mlima gani unapanda umenyooka,hio ndororo unacheza na kona 24 na zote ni fupi fupi kupanda na kushuka,ila waliozoea kina kidinilo wanapanda na kushuka kwa 60 wanacheza na stopper sana.
Usie mzoefu lazima wakakuokote chini mita elf 3 Kama Sio 6 bondeni huko
Ndororo ya miaka ya 90 ilikuwa ni noma sana hasa nyakati za masika. Tulikuwa tunaupanda huo mlima kwa kutumia gari aina ya Landrover 109, huku tukikaa juu ya machuma na chini ikiwa imejaza mizigo ya kutosha.

Na hapo kulikuwa hakuna lami kwenye huo mlima. Yaani ni full utelezi.
 
Ndororo ya miaka ya 90 ilikuwa ni noma sana hasa nyakati za masika. Tulikuwa tunaupanda huo mlima kwa kutumia gari aina ya Landrover 109, huku tukikaa juu ya machuma na chini ikiwa imejaza mizigo ya kutosha.

Na hapo kulikuwa hakuna lami kwenye huo mlima. Yaani ni full utelezi.
Mmetoka mbali aisee angalau wameweka lami kuondoa utelezi
 
Mahenge ni wilaya inayopatikana kusini mwa mkoa wa Morogoro na kabila la Wapogoro ndio wanapatikana huko. Ikiwa eneo la juu (Mlimani) na hali ya hewa ya ubaridi na mvua mvua.

Wilaya hii ina vivutio na siri nyingi mno, kihistoria,kiserikali na hata kidini (Je, umewahi kuisikia Wilaya hii na unapata picha gani juu yake?)

Vivutio; kwa upande wa vivutio kuna;
1. Kabila lenyewe linalopatikana huko (wapogoro) asili yao na lugha yao,tamaduni na style yao ya maisha. (kuoana ndugu mradi wasitike nababu mmoja) Uzuri wa wanawake wao wana miili yenye nguvu mno..

2. Ardhi na landscape yake, jinsi kulivyo na miinuko na misitu na vile ambavyo mji umechongwa.

3. Majengo ya mjerumani (boma) ambalo linatumika kama ofisi kuu za serikali (wilayani) na jengo la mkuu wa wilaya . Lakini pia majengo ya wamisionari (kanisa katoliki la tatu kwa ukubwa la tanzania lilojengwa kwa mawe tupu na mji wake ikijumuisha na shule zilojengwa na wao)

4. Misitu na miti pekee, na alama zilowekwa juu ya milima na misituni na wakoloni, hivyo ni baadhi.

Siri zilizoko;
1. Kuna madini ya aina mbali mbali yanayopatikana na kuchimbwa huko (rubi, spinal, greentomalin, uno, dhahabu na hata almasi)

2. Kutokana ni mji wa kikoloni, Mjerumani na Muingereza walikuwako huko hivyo alama zao juu ya milima na misitu zinamaana fulani, je ni ipi?

3. Kwanini wilaya hii licha ya kuwa na vyote hivi lakini bado imefungwa kimawasiliano ya barabara??? njia ni mbovu lakini pia haitoki inatoka kwa njia za mikato pekee.

4. Toka miaka viongozi wake wamekuwa wakinifaidisha wao, maajabu maendeleo yao pia yamekuwa hayaonekani sio kwa wao tu hata kwa ndugu zao (viongozi walowahi kutoka huko kwa uchache Late Amati liyumba aliwahi kuwa BOT, Late Mama Celina kombani alikuwa mbunge kabla CCM hawakumpa asante ya kumuweka mwanae kuwa mbunge baada ya mama yake Bw. Goodluck Mlinga ambae ameshindwa kuchukua jimbo mara baada ya miaka mitano kuisha .Sasa linashikiliwa na Bw. Almasi.

Je, kwanini hakuna maendeleo?

Je, kwanini viongozi wa huko ni kama wanaogopwa na wapogoro?

Je, kwanini mpaka leo barabara ni ya vumbi na kuna muda inakuwa mbaya na chafu kabisa?? kama unaogopa mlima kitonga basi usiendeshe kwenda Mahenge kuna mlima unaitwa ndororo ni hatari mno..

Kwa nini Viongozi wanaweza kaa msimu mzima wakaenda tembelea jimbo mara moja? especially walopita!!

Mimi nimeeleza vitu baadhi, waeza jazia vingine vile unafahamu kuhusu mji huu pia kuweza kualika kiongozi unae mjua aje ajibu baadhi ya hoja. Pia hata kueleza maswahibu au vituko ulivyowahi kutana navyo kwa mji huu maana na hata uchawi upo na wanatumia live.

cc: Goodlucky Mlinga
cc: Mkuu wilaya Mahenge Ulanga na mkurugenzi wake..
cc: Mbunge wa sasa Bw. Almasi
mbona sijaona sehemu umeitoa hiyo siri
 
Mpogoro katoka kwao mahenge huko, kuja dar...

Kurudi ndio anawasimulia wenzie kuwa yeye ni mjanja saanna,

"kondakta kusema, ubungu, ubungu nikabanishi, njwii, mpaka manzese kumkomoa dereva" 😂 🤣

Yaani akimaaisha konda gari ilipofika ubungo akatangaza kituo, yeye hakushuka akabana kwenye gari, kaenda kushukia manzese kwa kumkomoa dereva. 😂
Mpogoro akiwa anatuma salamu ukawasalimie utasikia "mpe shikamo yangu mama ,mpe shikamo baba,mpe shikamo kaka...." Ha ha

Ni watani zangu hao
 
Dah! Hayo maeneo ya Mang'ula A, Mang'ula B, Mwaya, Mgudeni, Kisawasawa, Kiberege, Signal (Ziginali), Sonjo, Mkula, Kidatu, Nyandeo, Mkamba, Ruaha, Ifakara yote, Mahenge, Malinyi, Mngeta kurudi nyuma, nk. Nimepiga sana mishe huko miaka ya 1990's.
Loh! Umepataja nyumbani moyo wote umenisisimka, mkula ndio nyumbani mkuu
 
Epanko ni Rubi yachimbwa.. ila kuna maeneo mengine ambayo nilibahatika kufika ... Lukande, ketaketa,mwaya na hata huko mbele kama una enda selous kunaitwa ibuyu
Shikamooo umekikumbusha miaka ya 2006 Lukande, ketaketa, mwaya, ipundi, mbuga palikuwa na barabara mbaya ajabu kipindi cha masika siku 3 ketaketa morogoro hapo ni crusier mpyaaa
 
Kitonga hamna mlima pale ule ni muinuko tu mlima gani unapanda umenyooka,hio ndororo unacheza na kona 24 na zote ni fupi fupi kupanda na kushuka,ila waliozoea kina kidinilo wanapanda na kushuka kwa 60 wanacheza na stopper sana.
Usie mzoefu lazima wakakuokote chini mita elf 3 Kama Sio 6 bondeni huko
Wale jamaa wa Kidinilo walipata wapi uzoefu wa ule Mlima ?
 
Mbona hujasema kwamba kuna Junior Seminari ya St Francis maarufu kama Kasita Seminari ambayo imezalisha vipanga mbalimbali wanaokimbiza kwenye sekta nyingi hapa nchini.

Kwiro secondary
Regunamundi
Kasita
St Agnes
 
[emoji23] Wale wamama wanaokuja kuuza vyakula jioni?! Haujaacha mtoto kule wewe?
😂😂😂 Sina uhakika japo nakumbuka kuna mama mmoja nilikuwa nakula free na kupiga shoo tu, nakumbuka nilimpaga ada ya shule nikasingizia kwa baba nimeibiwa🤣🤣🤣
 
Shikamooo umekikumbusha miaka ya 2006 Lukande, ketaketa, mwaya, ipundi, mbuga palikuwa na barabara mbaya ajabu kipindi cha masika siku 3 ketaketa morogoro hapo ni crusier mpyaaa
Kaka nimetoka ketaketa mwezi wa 12 mwaka 2024. Nakuhakikishia barabara ni mbaya Sana. Ilibidi tupaki gari pale ilonga niende na bodaboda adi ketaketa.
 
Back
Top Bottom