Ifike mahala Watanzania tuache kusomea ualimu, supply imekuwa kubwa mno kuliko demand

Ki ukweli kazi ya ualimu ina vimelea vingi vya umasikini na ufukara wa kutukuka japo ni kazi ya heshima, ila inakimbiliwa kwa sababu ajira yake ipo kwa wingi. Elimu ya ufundi ilidharaulika sana na ilionekana inawafaa zaidi darasa la saba, lakini mambo yamebadilika. Mafundi sasa hivi ndio wanatengeneza hela kuliko mwalimu, kijana mdogo tu anamiliki nyumba aliyojenga bila kukopa kutokana na hela za ufundi. Basi tu, kwa kuwa walimu wanahitajika kufundisha wanafunzi, wakusomea ualimu wakasome tu waridhike na mshahara wa mwezi mpaka watakapostaafu, maana ni fungu walilolichagua maishani.
 
  • Ongezea na fani za ufundi wa magari/bajaji/pikipiki nao sii haba wanafyonza vijiasali wanatupiga spea za uongo mpaka tunakoma.😀
  • Kuna ufundi mwingine wala huitaji kwenda veta, mfano hawa wanaoweka urembo/tinted/stika/rim kwenye magari
  • Kuna watu wanafyonza asali vibaya mno kwa kuweka urembo kwenye milango/madirisha ya nyumba dirisha 1 utaambiwa 60,000 na material zote zakwako
  • Kuna watu wa garden siku izi kuotesha ukoka na kuulea utaambiwa 300k kwa mwezi.. vijana changamkieni fursa hizi
 
Kwa hio suluhisho ni VETA tu, hao mafundi wakijazatazana watamtengenezea nani?
Mtaani mafundi ni wengi sana tu.

Jambo la msingi vijana wawe competent na wawe na confidency.
Ukiwa na hivyo viwili ajira utapata au utajiajiri. Wekeza kijifunza life skills sio tu vocational skills haisaidii sanaa.
Vijana wajifunze teknolojia za kisasa hasa computer nabna online bussiness .

Wajifunze kujiajili kupitia mitandao, mfano wewe unasema hakuna ajira za kufundisha wakati kuna ajira nyingi tu za kufundisha mitandaoni.

Wekeza ktk lifelong learning, kuwa multi purpose, angalia soko ka dunia linataka nini.
Elimu ya ualimi ina kufindisha how to be critical thinker, presentation skills, personality, communication skill hata teknolojia. Tatizo lipo kwa wasomaji wenyewe wana focus katika nini.

I tell you education is multidisciplinary discipline inaingiaa kila eneo kuanzia ujasiliamali,ufundi, uhasibu,sayansi, saikolojia, fslsafa, teknolojia, jamii , lugha(hizi ni nyanja zote za maisha ya mwanadamu, acheni ujinga)

Msio elewa hii fani mtabaki kuiponda lakini ndio fani inayoongoza kwa ajira nyingi na uwanja mpana hata viongozi wengi wanatokana na fani ya elimu.

Kuna usemi unasema elimu ni ufunguo wa maisha haujabainisha kuwa ualimu si ufunguo wa maisha bsli ni ufunguo wa umasikini.
Poor young boy! Open up your mind.
 
Asee mi naona ni vzur wakaanzisha elimu ya ufundi Hadi kwa shule za sekondari yani mtu anachagua fani moja tu anaisomea na ataifanyia mtihani wa form 4 pale au ata form six akifika atasomea fani ile ile aliyochagua ,,,kwa kufanya ivyo ikitokea mtu amefeli kabs form 4 pale ile fani aliyosomea itamwezesha ata kwenda veta kujiendeleza na kuwa na ujuzi mzur zaid.
 
Ni kweli, Lakini kwa standard za kimataifa walimu bado hawatoshi kabisa. Ni kama madaktari tu, Tanzania ipo chini sana kwenye uwiano wa daktari kwa mgonjwa lakini bado madaktari wanakosa kazi.
 
Hivi mpaka sasa hapa Tanzania bado watu wanahimizwa kusoma ili kuja kuajiriwa? Tumechelewa sana.
Zama zimeshabadilika, usomi wa kuja kuzurura na bahasha ya kusaka ajira mitaani ni zaidi ya kubet.
 
Na wale Assistant clinical officer huwa wanaajiriwa?
Kwa mbinde sana, kuna course ukisoma inakua kama ngazi ya kupandia kielimu tu na sio kwa ajili ya ajira, mfano kwa sasa hiyo clinical medicine ni ya kusoma na kupambana kupata GPA ya at least 4.5 on the way to degree, period.
 
Hapa duniani hakuna taaluma yenye upungufu ya watendaji, bali kuna upungufu wa pesa za kuwaajiri. Tunaposema supply imekuwa kubwa kuliko demand, tunamaanisha wanaosomea ni wengi kuliko uwezo wa soko la ajira kuwafyonza, tumeelewana?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…