Ifike mahali Wanakwaya kanisani na wahudumu wa Kanisani Walipwe mishahara Kwa mwezi

Ifike mahali Wanakwaya kanisani na wahudumu wa Kanisani Walipwe mishahara Kwa mwezi

Mambo ya Huduma za burebure yalikuwa zamani Enzi za UTUMWA. Kwa sasa kila mtu yu Huru. Yesu alisema mkiujua ukweli utwaweka huru. Kwa nini umtumikie Mungu burebure Kama vile mtumwa wake. Wewe sio mtumwa. Wala wewe sio MATEKA, Wengi hutumia Kauli kuwa mtumikie Mungu atakulipa yeye mwenyewe, wakati wao tunawalipa Sisi kwa Zaka na Sadaka zetu. Mtu akikuambia hivyo mwambie amtumikie yeye huyo Mungu burebure. Mbona wao wanalipwa?
Wachungaji wanalipwa,
Waalimu wanalipwa,
Watangazaji wanalipwa,
Waandishi wanalipwa,
Maaskofu wanalipwa,
Madaktari wanalipwa,
Madereva wanalipwa,,
Hao wote wanamfanyia kazi Mungu kila mmoja Kwa nafasi yake,
Iweje hawa Wanakwaya na wahudumu wa Kanisani wafanye kazi burebure Kama watoto wadogo au kama Watumwa?
Ndiyo maana kuna Askofu alisema siku hizi Kanisa limeingiliwa na wahuni kama wahuni wengine tu ila tofauti ni kwamba hawa wengine wanafanyia uhuni madhabahuni
 
Unazidi kuonyesha uchanga wako kwenye neno. Uchungaji, uanakwaya, uhudumu wa kanisani SIYO kazi. Ni huduma za kujitolea zisizo na malipo. Achana na hawa viongozi matepeli wanabadilisha magari kila kukicha.

Ndio nakuuliza unajua maana ya kazi?

Na aliyekuambia kazi sio huduma ni Nani?
Kila KAZI ni huduma, unahudumia watu Kwa kitu Fulani.

Kuimba ni KAZI wanayoifanya wanakwaya Kuwahudumia watu katika ibada ya kusifu na kuabudu kupitia nyimbo.

Wachungaji wanafanya kazi ya kuhubiri na kuchunga makanisa. Wanatoa Huduma ya neno la Mungu.

Hao unaowaita matapeli hawana tofauti na hao unaowaona ni watumishi wa kweli
 
Akiwa nje kihuduma ndiyo anapewa posho ya kujikimu na siyo mshahara. Nimesema tena na tena, wanapata posho na siyo mshahara. Unajua sifa za malipo kuitwa mshahara wewe?
Na akiongoza ibada ya mazishi anakabidhiwa sadaka zote za ibada hiyo
 
Ndio nakuuliza unajua maana ya kazi?

Na aliyekuambia kazi sio huduma ni Nani?
Kila KAZI ni huduma, unahudumia watu Kwa kitu Fulani.

Kuimba ni KAZI wanayoifanya wanakwaya Kuwahudumia watu katika ibada ya kusifu na kuabudu kupitia nyimbo.

Wachungaji wanafanya kazi ya kuhubiri na kuchunga makanisa. Wanatoa Huduma ya neno la Mungu.

Hao unaowaita matapeli hawana tofauti na hao unaowaona ni watumishi wa kweli
Narudia tena: Viongozi wa dini wanapata posho na siyo mshahara. Ndiyo maana hawana mkataba wa malipo, wala malipo yao hayakatwi kodi, na wala hayako fixed. Kina siku matumizi yao yanategema mapato.
 
Mambo sio marahisi kama unavyokaa ukafikiria kujiandikia.
Kupitia hii unayoiita dhulma watu wamepona, wamebadili tabia, maisha yamewanyookea na wanajivunia imani zao.

Ujitahidi kuepuka kufakamia jambo lisilokufaidisha wewe yupo mtu anajivunia kuwa kwenye hiyo imani yake.

Mwisho kabisa kila mtu anasaka amani ya moyo wake


Huwezi nielewa kama hautotumia AKILI.
Hakuna sehemu nilipokataza watu wasijivunie hizo Dini.
Ninachojaribu kukieleza watu wafanye reformation Kwa maana dini zinaumiza wengi kuliko wanaofaidika nazo.

Kinachowatisha watu ni ukosefu wa elimu sahihi ya Dini ndio maana wanaogopeshwa, wengi wanaabudu kinafiki ili wazikwe wengine wakiogopa kuchomwa Moto😀
Huku wakiendelea kuteswa Kwa vitu ambavyo vinaweza kufanyiwa marekebisho.

Hizi Dini unavyoziona hivi leo zimepitia Reformations nyingi mno.
Hivyo hata ninachokisema kinaweza baadaye kuingizwa katika mfumo wa Dini
 
Ni kweli Kabisa
Unaona unavyojikanyaga mwenyewe hapa. Sasa wewe unazungumzia viongozi matapeli na siyo viongozi wa kweli wa dini. Kama ni viongozi wa dini matapeli, basi wako wengi na wanapata zaidi ya mshahara. Wamejimilikisha majumba, magari na wanaisha maisha ya kifahari sana. Hawa ndiyo unasema wanatakiwa kulipa wahudumu na wanakwaya wao mishahara? Unataka kushauri matapeli kufanya mambo ya uhalali? Huna hoja yoyote wewe.
 
Narudia tena: Viongozi wa dini wanapata posho na siyo mshahara. Ndiyo maana hawana mkataba wa malipo, wala malipo yao hayakatwi kodi, na wala hayako fixed. Kina siku matumizi yao yanategema mapato.

Unajua Kwa nini malipo Yao hayakatwi Kodi?

Ndio hivyohivyo nikasema, hizo unazoziita posho ambazo wanalipwa Kwa mwezi wapewe pia Hao wahudumu wengine kama wanakwaya.
Wapi sijaeleweka Mkuu
 
Unaona unavyojikanyaga mwenyewe hapa. Sasa wewe unazungumzia viongozi matapeli na siyo viongozi wa kweli wa dini. Kama ni viongozi wa dini matapeli, basi wako wengi na wanapata zaidi ya mshahara. Wamejimilikisha majumba, magari na wanaisha maisha ya kifahari sana. Hawa ndiyo unasema wanatakiwa kulipa wahudumu na wanakwaya wao mishahara? Unataka kushauri matapeli kufanya mambo ya uhalali? Huna hoja yoyote wewe.

Kitu usichokijua ni kuwa kila mtu huona dini ya mwenzake ni matapeli.
Ndio maana nikakuambia wote wawalipe wahudumu wengine wanaosaidia makanisa Yao kukua Kwa kutafuta Wateja wapya(waumini wapya).

Walipwe Kwa mwezi iwe mi posho au Mshahara unaolingana na Huduma zao
 
Huwezi nielewa kama hautotumia AKILI.
Hakuna sehemu nilipokataza watu wasijivunie hizo Dini.
Ninachojaribu kukieleza watu wafanye reformation Kwa maana dini zinaumiza wengi kuliko wanaofaidika nazo.

Kinachowatisha watu ni ukosefu wa elimu sahihi ya Dini ndio maana wanaogopeshwa, wengi wanaabudu kinafiki ili wazikwe wengine wakiogopa kuchomwa Moto😀
Huku wakiendelea kuteswa Kwa vitu ambavyo vinaweza kufanyiwa marekebisho.

Hizi Dini unavyoziona hivi leo zimepitia Reformations nyingi mno.
Hivyo hata ninachokisema kinaweza baadaye kuingizwa katika mfumo wa Dini
Kama kutumia akili kwako ndiko huku basi tuachane kwani hoja yako inaelea hewani. Cha msingi ni wewe kutofautisha viongozi wa dini matapeli (ambao ndiyo wengi) na viongozi wa ukweli.
 
Unazidi kuonyesha uchanga wako kwenye neno. Uchungaji, uanakwaya, uhudumu wa kanisani SIYO kazi. Ni huduma za kujitolea zisizo na malipo. Achana na hawa viongozi matepeli wanabadilisha magari kila kukicha.

Aliyesema hazina malipo ni Nani?

Mtu akifanya kazi madhabahuni anapaswa aliyemadhabuni hayo ndio malipo yake.

Ndio maana ni lazima kulipa zaka ili HAO watumishi wapate malipo Yao.
 
Kitu usichokijua ni kuwa kila mtu huona dini ya mwenzake ni matapeli.
Ndio maana nikakuambia wote wawalipe wahudumu wengine wanaosaidia makanisa Yao kukua Kwa kutafuta Wateja wapya(waumini wapya).

Walipwe Kwa mwezi iwe mi posho au Mshahara unaolingana na Huduma zao
Siyo kila mtu anayeona dini ya mwingine ni matapeli, hili ni kosa jingine umefanya. Mimi ni mkristo lakini siwezi kuona eg kila kiongozi wa dini ya kiisalam ni tapeli. Na zaidi kuna viongozi wa dhehebu langu nawaona ni matapeli tu. Tapeli hategemei dini bali ni matendo.
 
Ni sahihi kabisa, viongozi wa dini hutajirika kwa kukusanya zaka na sadaka kisha huzitumia peke yao na kusahau watenda kazi wengine
 
Kama kutumia akili kwako ndiko huku basi tuachane kwani hoja yako inaelea hewani. Cha msingi ni wewe kutofautisha viongozi wa dini matapeli (ambao ndiyo wengi) na viongozi wa ukweli.

Viongozi wa dini matapeli ni Wale wasiofuata maandiko, wanaojitungia mambo na kudhulumu wengine.

Biblia iko wazi Kabisa kuhusu wanaohudumu madhabahuni
 
Aliyesema hazina malipo ni Nani?

Mtu akifanya kazi madhabahuni anapaswa aliyemadhabuni hayo ndio malipo yake.

Ndio maana ni lazima kulipa zaka ili HAO watumishi wapate malipo Yao.
Huna hoja kwa sababu msingi ya dini huijui. Tunaweza kukesha hapa. Kajifunze kwanza misingi ya dini.
 
Viongozi wa dini matapeli ni Wale wasiofuata maandiko, wanaojitungia mambo na kudhulumu wengine.

Biblia iko wazi Kabisa kuhusu wanaohudumu madhabahuni
Huna hoja kwa sababu msingi ya dini huijui. Tunaweza kukesha hapa. Kajifunze kwanza misingi ya dini.
 
Nadhani labda neno mshahara ndio limekua tatizo kwako maana wewe unadai ni posho tu.
Sasa ninachopenda kujua ni kuwa iweje hiyo posho astahili kuhani na mkuu wa dini pekee na sio wahudumu wote wa madhabahuni kwa pamoja na wanakwaya wakiwepo? Maana mwanakwaya anatakiwa kuwepo kanisani muda na siku zote za ibada, anatakiwa kuwa na muda wa ziada kukutanika kwa ajili ya mazoezi ya kwaya, anatakiwa kukaa na kutafakari kutunga tungo nzuri ambazo zitawagusa waumini na hapo hapo aendane na policy ya kanisa, lakini kwa kawaida kuna sare na vitu kama hivyo mwanakwaya anatakiwa ajihudumie.
Sasa hauoni kuwa kuna haja ya kuwalipa posho ya kujikimu hawa wanakwaya kama tunavyofanya kwa makuhani na wakuu wa dini?
Fedha za zaka siyo malipo kwa makuhani. Ni fedha za kuwasaidia kuendesha maisha yao kwa sababu hawana kazi nyingine bali kazi yao ni hiyo tu. Zinatumika kuwalisha na kulipia huduma mbali mbali za maisha. Kwa mfano padri hana mshahara. Naomba sana utofautishe kati ya watumishi wa Mungu wa ukweli na matapeli waliovaa ngozi ya kondoo na kujifanya ni watumishi.
 
Ni sahihi kabisa, viongozi wa dini hutajirika kwa kukusanya zaka na sadaka kisha huzitumia peke yao na kusahau watenda kazi wengine

Unakuta Vijana wanalitumikia Kanisa miaka nenda Rudi lakini familia zao hazina la maana.
Umasikini, ujinga Kwa kushindwa kulipia Karo za Shule lakini wameahidiwa ati watapewa malipo Yao na Mungu wakati wachungaji na viongozi WA dini wakichukua malipo yetu Sisi Wanadamu
 
Iwe pisho, mshahara, marupulupu vyote ni pesa yenye lengo la kumuwezesha mwanadamu kukidhi mahitaji yake ya kila siku. Hayo ni majina tu ya kufumba macho ni sawa na tozo, kodi sijui sitting allowance, per diem, etc.

Kifupi watumishi kama wanakwaya wanatumia mda mwingi kwenye shughuri za kikanisa zahidi ya kuhudumia familia zao. Wanatakiwa walipwe posho ya kujikimu.

Kumbuka sio dini inayomuwezesha mwanadamu kuwasiliana na muumba wake bali ni usafi wa roho na matendo mema ndio yanayomuunganisha mwanadamu na Muumba wake.(Mungu)
 
Back
Top Bottom