IGP alitusihi wazazi tusizae majambazi, vipi yeye kuongoza wauaji huko Jeshi la Polisi

IGP alitusihi wazazi tusizae majambazi, vipi yeye kuongoza wauaji huko Jeshi la Polisi

Wazazi tulianza kufanyia kazi ushauri wa IGP alitushauri vizuri tu tena kwa roho safi kua wazazi tusizae majambazi na magaidi kama HAMZA naamini lengo lilikua kudumisha amani na utulivu nchini ni sawa wazazi tulipokea ushauri huo kwa mikono yote miwili.

Vipi yeye sasa kuongoza waporaji wa mali za Raia wema na wauwaji wa raia wasio kua na hatia kwenye jeshi lake kama wazazi na sisi tunamshauri aache kuongoza majambazi huko kwenye taasisi yake bali alitakiwa kuongoza askari wenye weledi wa kutosha na sio kuongoza wauwaji wa mfanyabiashara wa madini.

Wazazi tunamshauri pia IGP Siro kamwe asiongoze majambazi wanaofanya uhalifu huko polisi.

Kama tulivopokea ushauri wake naamini nae atapokea ushauri wetu na kwa kuanzia tu ni vyema ajiuzuru nafasi yake.

‘IGP soma hii maneno, kuna ujumbe wako muhimu’​

 
Back
Top Bottom