Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Na hii tabia ya kipumbavu ya kumwita muuaji mwenzenu magufooli kuwa shujaa wa Tanzania komeni kabisa mi simuoni kama shujaa na ningefurahi kutangulia kaburini kabla ya Lissu.Kwahiyo we unatakaje?
Alafu tabia ya kipumbavu ya kusema sisi watanzania tuliumia sana unakosea ina manisha umenijumuisha na mimi.Ukwel ni kuwa sikuumia kabisa angekufa tu.Jiseme nafsi yako.
Wewe hutakufa?Nakuapia utakufa Kama Jiwe, utakufa waliowako wasivyofikiria. Kama Jiwe alivyokufa kimzaha nawe uko njiani kumfuata. Nakuapia walah!
Ndugu IGP Sirro
Nimesikiliza mahojiano yako uliyofanya na mwanahabari mmoja hapa nchini ,katika mahojiano yako umeonyesha bila chembe ya shaka kuwa hauna interest ya kufuatilia, kuchunguza na hatimaye kuwafikisha katika mkono wa sheria wahalifu walitenda tendo baya na la kinyama kabisa la kutaka kutoa roho ya Ndugu Tundu Antipass Lissu. Ndugu IGP umetusikitisha sana kwa sababu hizi zifuatazo:
1. Mosi, Unamshutumu Mhanga badala ya wewe kudeal na Wahalifu waliotekeleza jaribio la mauaji:
Ndugu Sirro, nimekusikia maneno yako uliyotoa kwenye kile chombo cha habari, umesema kuwa Lissu ni mkaidi, ukasema eti hakutoa ushirikiano wowote katika kipindi cha kampeni ulipomuita ili umhoji kuhusiana na tukio la shambulio lake. Ndugu Sirro nataka nikukumbushe tu kuwa hata wakaidi wanaowajibu wa kutii sheria bila shuruti. Sasa naomba uueleze umma huu wa Watanzania kwa kuwa Lissu alikataa kutoa ushirikiano katika kuhojiwa Je mlimchukulia sheria gani? Maana kosa alilotendewa Lissu ambalo ni jaribio la mauaji ni kosa dhidi ya Jamhuri na siyo kosa la madai kumhusu Lissu binafsi. Kwa kweli ndugu Sirro, sababu uliyoitoa ya Jeshi la polisi kutofanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa ndugu Lissu ni sababu nyepesi sana inayotufanya tuanze kuwa na mashaka na jeshi la Polisi, Je, Jeshi lako lina kitu gani cha kuficha katika shambulio lile?, Je wewe binafsi una kitu gani cha kuficha katika shambulio. Tueleze sisi wananchi tujue, maana nyie ndo mna dhamana ya ulinzi wa mali na raia. Majibu yako yanaacha wasiwasi mwingi sana
2. Hoja yako kuwa Lissu hajawahi kuripoti popote juu ya kushambuliwa kwake ina walakini:
Ndugu Sirro, usitake kutwambia kuwa kila Jinai ya wazi lazima aliyetendewa jinai ndo akaripoti. Ndugu Sirro, Lissu alikaa kwenye coma zaidi ya wiki moja na amekaa hospitali takriban mwaka mzima, na mpaka leo hii anaendelea bado na operesheni za kujitibia (imebaki moja), Ndugu Sirro je Jeshi la Polisi lilikuwa linangoja mhanga apone ndo muanze uchunguzi? Je, mhanga angekufa maana yake ni kwamba na uchunguzi wa tendo la jinai ndo ungeishia palepale?
Ndugu Sirro kwa nini Jeshi la polisi halijafungua jalada la upelelezi wa suala hilo, Je shahidi wa hilo tukio ni mmoja tu yaani yeye?, kwa nini hamjamuita dereva wake popte alipo kumhoji, na kama ni suspect kwa nini hamkutumia Interpol kumtafuta ili kumhoji?, Mbona hamjahoji majirani, hata wabunge waliokuwa na mheshimiwa Lissu siku hiyo mbona hamkuwaita kuchukua maelezo yao?, Sirro tueleze wewe na Jeshi la Polisi mnajua nini na mnaficha nini?
3. Sirro haukutimiza ahadi yako, uliwaahidi wanasiasa waliokimbia nchi warudi utawapa ulinzi sasa umebadilika:
Mara baada ya uchaguzi mkuu, ulitoka kwenye vyombo vya habari ukiwaambia wanasiasa waliokimbia nchi kufuatia sintofahamu za baada ya uchaguzi kuwa warejee nchini utawapa ulinzi maalum, lakini juzi wakati ukiongea na mwandishi wa habari ulibadili kauli, ukasema hakuna cha ulinzi maalum na kwamba hao wanasiasa ni kama watanzania wengine tu, ukasema kuwa hata watanzania wengine huwa wanashambuliwa na majambazi n.k. Ndugu Sirro, Je unafahamu mtu aliyesurvive risasi 16 atakuwa na hali gani katika kuhofia usalama wake hasa ukizingatia kuwa alitamka mara nyingi kuwa anafuatiliwa na watu kabla ya shambulio lake lakini Jeshi la polisi liliamua kukaa kimya tu?-
Je Ndugu Sirro unataka kutwambia kuwa haimo katika utendaji wa jeshi la polisi kufanyia kazi vitisho, na kauli zenye viashiria vya jinai kutendeka mpaka mtu aripoti polisi? Kama ni hivyo basi jeshi hilo chini yako litakuwa jeshi la ajabu sana!. Kwa hiyo leo kiongozi wa serikali akisema kuwa kuna kitisho dhidi yake hamtofanya lolote mpaka akaripoti polisi?-Sasa inakuwaje mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaita press conference kueleza kufuatiliwa na watu wasiojulikana na kuhofia maisha yake lakini jeshi la polisi lipolipo tu?- Tuambie Sirro, Jeshi lako linajua nini katika hili sakata?
4. Jinai haifi, wananchi tunataka tujue kwa nini Jeshi la polisi halifanyi uchunguzi juu ya tukio la jaribio la mauaji la ndugu Lissu:
Ndugu Sirro, maelezo uliyotoa kwenye vyombo vya habari juu ya hatua ya jeshi la polisi kutofanya lolote juu ya jaribio la mauaji ya ndugu Lissu ni maelezo mepesi sana, hayajasheheni sababu kuntu za kipolisi, za kiupelelezi na kwa kweli za kisheria. Sasa tunataka tujue ni lini jeshi la polisi litafungua jalada la upelelezi wa tukio la kumpiga risasi ndugu Lissu?, tunataka kuona wito wa kisheria wa kipolisi wa kuita mashahidi ili tuone kweli uchunguzi umefanyika, wahalifu wanafikishwa katika mkono wa sheria na haki inatendeka. Tunapotaka hivi hatumaanishi kuwa matukio yaliyowakumba wengine yasifanywe, lakini uchunguzi wa tukio fulani hauzuii uchunguzi wa tukio jingine. Ndugu IGP tunaomba majibu
5. Mwisho kabisa ndugu IGP naomba ufahamu yafuatayo:
Sisi watanzania tuliumizwa sana na tukio la kinyama alilofanyiwa mtanzania mwenzetu ndugu Lissu, tulilia naye, tulimuombea Kwa Mwenyezi Mungu amponye. Ukatili ule uliofanywa juu yake wa kumpiga risasi zote zile utadhani watu walitaka kuua Chatu ni ukatili usio na mithili. Kila nikiufikiria ukatili roho yangu inagumia. Sisi Watanzania tuna haki ya kujua akina nani walihusika ili mkono wa sheria uwe juu yao. Ndugu Sirro unavyopiga chenga au kujivutavuta katika kufanya uchuhunguzi wa hili suala, na kadri unavyoongea kwa nguvu nyingi kulifunika ndivyo nasi tunakuwa tukufikiria vibaya sana. Tafadhali usistaafu huku damu ya Lissu iliyomwagika bila hatia pale Dodoma ikiwa inakulilia kudai haki yake. Wewe hapo ulipo unaweza kuamua uchunguzi wa hili suala ufanyike ili tujue umetimiza wajibu wako, na ukishindwa unawe mikono kama Pilato tujue. Ndugu Sirro, Watanzania tuna interest ya kujua juu ya jinai ile kwa sababu inahusu maslahi ya viongozi wetu tunaowachagua, kama mkiwaachia wahalifu kwenda free basi watarudia tena hayo matendo huko mbeleni, ndiyo maana sisi watanzania tunataka mfanye uchunguzi, wahalifu wajulikane na sheria ichukue mkondo wako!
IGP SIRRO KABLA HUJASTAAFU TANATAKA KUONA UKITENDA HAKI KATIKA DHULMA HII MBAYA KABISA ILIYOWAHI KULIKUMBA TAIFA LETU
watanzania siyo makatili? hao wanaoshangilia kifo cha magufuli unawaitaje?
kwani unawahi wapi unakimbizwa kwani andika taratibu kitu kinacho eleweka.Kuna mtu alikifa badaya yake.
Vipi hapo
EeeenHeee,Kwahiyo we unatakaje?
Alafu tabia ya kipumbavu ya kusema sisi watanzania tuliumia sana unakosea ina manisha umenijumuisha na mimi.Ukwel ni kuwa sikuumia kabisa angekufa tu.Jiseme nafsi yako.
Isaidiwe Jamhuri, kosa la jinai ni kosa dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!
Hii bangi inakuharibu akili.Lissu anakataa kutoa ushirikiano na IGP anakataa kufanya uchunguzi! Ngoma droo. Na nyinyi wapambe wa Lissu msifikiri watanzania wote tumeumizwa na matatizo ya Lissu! Hata wakina Amsterdam wamemkacha.
Na wewe Lissu, usiwe una andika humu JF kwa identity ya bandia ukitafuta huruma! Maana huyu alie andika haya ni wewe Lissu.
Jeshi la polisi lina msaspect dereva wa lisu.Mwambieni amtoe huko alipo.Sirro njoo utueleze Watanzania, Je Wewe na Jeshi la Polisi linamsuspect nani katika shambulio dhidi ya Lissu
Tunataka jeshi la polisi lifanye kazi yake siyo kukwepa majukumu ya msingi!
Ni kweli kama ambavyo siyo wote walioumizwa na kifo cha mwendazakeLissu anakataa kutoa ushirikiano na IGP anakataa kufanya uchunguzi! Ngoma droo. Na nyinyi wapambe wa Lissu msifikiri watanzania wote tumeumizwa na matatizo ya Lissu! Hata wakina Amsterdam wamemkacha.
Na wewe Lissu, usiwe una andika humu JF kwa identity ya bandia ukitafuta huruma! Maana huyu alie andika haya ni wewe Lissu.
Huo ndio ukweli mwache mtu awonge ukwel au upendi kusikia kweli.Hii bangi inakuharibu akili.
Jeshi la polisi lina msaspect dereva wa lisu.Mwambieni amtoe huko alipo.
chadema bana nyie kichwani ni matope matupu.Mtu akishangilia ya lisu ni katili akishangilia ya JPM ni malaika.Kweli nyie ni hamnazo.Ni kweli kama ambavyo siyo wote walioumizwa na kifo cha mwendazake
Choo cha walemavu ni muhimu sana Ulaya una lingine?
Kuna haja gani kuwatarifu interpol wakati aliye shambuliwa ndiye aliyemficha akae nae tu apambane na hali...kama dereva ni suspect basi jeshi la polisi linatakiwa kuwataarifu Interpol na polisi wa Ubelgiji ili dereva huyo akamatwe na kurejeshwa nchini.
..huo ndio utaratibu unaotumika kuwakamata watuhumiwa waliotoroka nchini kwao, au eneo walikotenda uhalifu.
Kuna haja gani kuwatarifu interpol wakati aliye shambuliwa ndiye aliyemficha akae nae tu apambane na hali.