IGP kwenye suala la Lissu chutama, umatusononesha sana Watanzania kwa kumshambulia mhanga kwa maneno badala ya kutafuta wahalifu

IGP kwenye suala la Lissu chutama, umatusononesha sana Watanzania kwa kumshambulia mhanga kwa maneno badala ya kutafuta wahalifu

Hiyo hatakuwa hiari tena! Nasema aje mwenyewe asaidie, kwa mapenzi yake siyo interpol kuhusika. Kwani yeye haoni kuwa ni muhimu katika upelelezi huu. Akija, na Lissu akatoa ushirikiano, basi tutabaki tunalaumu polisi kwamba hawafanyi kazi au Walihusika! Hawa watu wawili walikuwepo wanapaswa waisaidie polisi iwasaidie.

..kwa mtizamo wangu Polisi haina haja na Lissu wala dereva.

..Lissu alikuwepo hapa Tz na alifika mpaka kwa Rpc Muroto wa Dodoma kudai apewe gari yake lakini polisi hawakumhoji.

..Kama polisi wanaamini dereva ana taarifa zinazowafaa wangeweza kuwatumia polisi wa Ubelgiji kumhoji. Huo ndio utaratibu unaotumika kwa mashahidi walioko nje ya nchi.

..Kama polisi wanaamini dereva ameshiriki tukio lile wanaweza kuwaomba Interpol na polisi wa Ubelgiji wamkamate na kumrejesha Tanzania. Huo ndio utaratibu unaotumika kukamata watuhumiwa waliovuka mipaka ya nchi yetu.

..Waliomshambulia Lissu wanaweza kukodishwa tena wakashambulia Mtanzania mwingine. Ni vizuri jeshi letu la polisi lifanye uchunguzi wa haraka kuwabaini waliohusika.
 
..kwa mtizamo wangu Polisi haina haja na Lissu wala dereva.

..Lissu alikuwepo hapa Tz na alifika mpaka kwa Rpc Muroto wa Dodoma kudai apewe gari yake lakini polisi hawakumhoji.

..Kama polisi wanaamini dereva ana taarifa zinazowafaa wangeweza kuwatumia polisi wa Ubelgiji kumhoji. Huo ndio utaratibu unaotumika kwa mashahidi walioko nje ya nchi.

..Kama polisi wanaamini dereva ameshiriki tukio lile wanaweza kuwaomba Interpol na polisi wa Ubelgiji wamkamate na kumrejesha Tanzania. Huo ndio utaratibu unaotumika kukamata watuhumiwa waliovuka mipaka ya nchi yetu.

..Waliomshambulia Lissu wanaweza kukodishwa tena wakashambulia Mtanzania mwingine. Ni vizuri jeshi letu la polisi lifanye uchunguzi wa haraka kuwabaini waliohusika.
Nafikiri hatuelewani hapa, hayo yote uliyo sema ni sawa kwa upande wa Polisi. Je! Kwa upande wa dereva na Lissu huoni kuwa sasa waende polisi wenyewe bila shinikizo? Kusudi upelelezi uanze na pasiwe na kisingizio cha kutupiana mpira! Maana bila hivyo tunachotea maji kwenye tenga (orugega)!
 
Mambo hubadilika sana...nilidhani msiba wa Magufuli umewafundisha kujua Dunian tunapita lakini hamna.
 
Nafikiri hatuelewani hapa, hayo yote uliyo sema ni sawa kwa upande wa Polisi. Je! Kwa upande wa dereva na Lissu huoni kuwa sasa waende polisi wenyewe bila shinikizo? Kusudi upelelezi uanze na pasiwe na kisingizio cha kutupiana mpira! Maana bila hivyo tunachotea maji kwenye tenga (orugega)!

..usichoelewa ni kwamba Lissu alishafika ofisini kwa Rpc Muroto wa Dodoma hakuhojiwa.

..Lissu pia alikamatwa baada ya uchaguzi na kushikiliwa na Polisi kabla Balozi wa Ujerumani hajamgomboa. Polisi hawakumhoji wakati wamemshikilia.

..Hiyo inadhihirisha kwamba Polisi hawana nia ya kumhoji Lissu.

..Kwa upande wa dereva imepita miaka 3 tangu tukio litokee. Kwanini Polisi hawashirikiani na wenzao wa Ubelgiji kumhoji? Au hawatumi maombi kwa Interpol ili arejeshwe nyumbani?

..Hivi kwa akili ya kawaida unadhani Polisi wanaweza kusubiri miaka 3 na zaidi ikiwa wanaamini dereva ana taarifa muhimu, au amehusika na tukio?
 
Anawasemea wale wote walioguswa na kuumizwa na kadhia hiyo ya kinyama.
Atafute lugha sahihi mf anaweza kusema ''sisi wana chadema"siyo kujumuisha umma wa waTanzania wote
 
Atafute lugha sahihi mf anaweza kusema ''sisi wana chadema"siyo kujumuisha umma wa waTanzania wote


Wewe unadhani hata wale waliompiga risasi wamo katika kundi la "sisi" ?!!----- common sense haikubali kabisa!! , ni wale touched tu ndio wanaozungumziwa hapa.
 
Wewe unadhani hata wale waliompiga risasi wamo katika kundi la "sisi" ?!!----- common sense haikubali kabisa!! , ni wale touched tu ndio wanaozungumziwa hapa.
Mkuu nimekutolea mf kabisa bado uwelewi?
 
Mkuu nimekutolea mf kabisa bado uwelewi?


Maana yangu ni hii haikuwa lazima awe specific kwani neno SISI linawakilisha uwingi na walioguswa kwenye kadhai ile ya kinyama ya Lissu ni wengi na sio lazima kwamba Chadema wote waliguswa kwani kuguswa ni jambo la moyoni mwa mtu hivyo neno SISI linawahusu wale ambao ni touched tu ama awe CCM, Chadema, Cuf, Act au mtu yeyote touched atakuwa kaingia kwenye SISI, na wapo CCM walikuwa touched na walienda kumtembelea hospitali Nairobi, mf, Mzee Ruksa hivyo naye yumo kwenye Sisi japo ni CCM.
 
Maana yangu ni hii haikuwa lazima awe specific kwani neno SISI linawakilisha uwingi na walioguswa kwenye kadhai ile ya kinyama ya Lissu ni wengi na sio lazima kwamba Chadema wote waliguswa kwani kuguswa ni jambo la moyoni mwa mtu hivyo neno SISI linawahusu wale ambao ni touched tu ama awe CCM, Chadema, Cuf, Act au mtu yeyote touched atakuwa kaingia kwenye SISI, na wapo CCM walikuwa touched na walienda kumtembelea hospitali Nairobi, mf, Mzee Ruksa hivyo naye yumo kwenye Sisi japo ni CCM.
Usiongele hisia jikite kwenye point mtoa mada alipo sema "sisi waTanzania"unaniondoaje mimi ambaye sikuguswa kabisa na tukio lile
 
Ndugu IGP Sirro

Nimesikiliza mahojiano yako uliyofanya na mwanahabari mmoja hapa nchini ,katika mahojiano yako umeonyesha bila chembe ya shaka kuwa hauna interest ya kufuatilia, kuchunguza na hatimaye kuwafikisha katika mkono wa sheria wahalifu waliotenda tendo baya na la kinyama kabisa la kutaka kutoa roho ya Ndugu Tundu Antipass Lissu. Ndugu IGP umetusikitisha sana kwa sababu hizi zifuatazo:

1. Mosi, Unamshutumu Mhanga badala ya wewe kudeal na Wahalifu waliotekeleza jaribio la mauaji:
Ndugu Sirro, nimekusikia maneno yako uliyotoa kwenye kile chombo cha habari, umesema kuwa Lissu ni mkaidi, ukasema eti hakutoa ushirikiano wowote katika kipindi cha kampeni ulipomuita ili umhoji kuhusiana na tukio la shambulio lake. Ndugu Sirro nataka nikukumbushe tu kuwa hata wakaidi wanaowajibu wa kutii sheria bila shuruti. Sasa naomba uueleze umma huu wa Watanzania kwa kuwa Lissu alikataa kutoa ushirikiano katika kuhojiwa Je mlimchukulia sheria gani? Maana kosa alilotendewa Lissu ambalo ni jaribio la mauaji ni kosa dhidi ya Jamhuri na siyo kosa la madai kumhusu Lissu binafsi. Kwa kweli ndugu Sirro, sababu uliyoitoa ya Jeshi la polisi kutofanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa ndugu Lissu ni sababu nyepesi sana inayotufanya tuanze kuwa na mashaka na jeshi la Polisi, Je, Jeshi lako lina kitu gani cha kuficha katika shambulio lile?, Je wewe binafsi una kitu gani cha kuficha katika shambulio. Tueleze sisi wananchi tujue, maana nyie ndo mna dhamana ya ulinzi wa mali na raia. Majibu yako yanaacha wasiwasi mwingi sana

2. Hoja yako kuwa Lissu hajawahi kuripoti popote juu ya kushambuliwa kwake ina walakini:
Ndugu Sirro, usitake kutwambia kuwa kila Jinai ya wazi lazima aliyetendewa jinai ndo akaripoti. Ndugu Sirro, Lissu alikaa kwenye coma zaidi ya wiki moja na amekaa hospitali takriban mwaka mzima, na mpaka leo hii anaendelea bado na operesheni za kujitibia (imebaki moja), Ndugu Sirro je Jeshi la Polisi lilikuwa linangoja mhanga apone ndo muanze uchunguzi? Je, mhanga angekufa maana yake ni kwamba na uchunguzi wa tendo la jinai ndo ungeishia palepale?

Ndugu Sirro kwa nini Jeshi la polisi halijafungua jalada la upelelezi wa suala hilo, Je shahidi wa hilo tukio ni mmoja tu yaani yeye?, kwa nini hamjamuita dereva wake popte alipo kumhoji, na kama ni suspect kwa nini hamkutumia Interpol kumtafuta ili kumhoji?, Mbona hamjahoji majirani, hata wabunge waliokuwa na mheshimiwa Lissu siku hiyo mbona hamkuwaita kuchukua maelezo yao?, Sirro tueleze wewe na Jeshi la Polisi mnajua nini na mnaficha nini?

3. Sirro haukutimiza ahadi yako, uliwaahidi wanasiasa waliokimbia nchi warudi utawapa ulinzi sasa umebadilika:
Mara baada ya uchaguzi mkuu, ulitoka kwenye vyombo vya habari ukiwaambia wanasiasa waliokimbia nchi kufuatia sintofahamu za baada ya uchaguzi kuwa warejee nchini utawapa ulinzi maalum, lakini juzi wakati ukiongea na mwandishi wa habari ulibadili kauli, ukasema hakuna cha ulinzi maalum na kwamba hao wanasiasa ni kama watanzania wengine tu, ukasema kuwa hata watanzania wengine huwa wanashambuliwa na majambazi n.k. Ndugu Sirro, Je unafahamu mtu aliyesurvive risasi 16 atakuwa na hali gani katika kuhofia usalama wake hasa ukizingatia kuwa alitamka mara nyingi kuwa anafuatiliwa na watu kabla ya shambulio lake lakini Jeshi la polisi liliamua kukaa kimya tu?-

Je Ndugu Sirro unataka kutwambia kuwa haimo katika utendaji wa jeshi la polisi kufanyia kazi vitisho, na kauli zenye viashiria vya jinai kutendeka mpaka mtu aripoti polisi? Kama ni hivyo basi jeshi hilo chini yako litakuwa jeshi la ajabu sana!. Kwa hiyo leo kiongozi wa serikali akisema kuwa kuna kitisho dhidi yake hamtofanya lolote mpaka akaripoti polisi?-Sasa inakuwaje mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaita press conference kueleza kufuatiliwa na watu wasiojulikana na kuhofia maisha yake lakini jeshi la polisi lipolipo tu?- Tuambie Sirro, Jeshi lako linajua nini katika hili sakata?

4. Jinai haifi, wananchi tunataka tujue kwa nini Jeshi la polisi halifanyi uchunguzi juu ya tukio la jaribio la mauaji la ndugu Lissu:
Ndugu Sirro, maelezo uliyotoa kwenye vyombo vya habari juu ya hatua ya jeshi la polisi kutofanya lolote juu ya jaribio la mauaji ya ndugu Lissu ni maelezo mepesi sana, hayajasheheni sababu kuntu za kipolisi, za kiupelelezi na kwa kweli za kisheria. Sasa tunataka tujue ni lini jeshi la polisi litafungua jalada la upelelezi wa tukio la kumpiga risasi ndugu Lissu?, tunataka kuona wito wa kisheria wa kipolisi wa kuita mashahidi ili tuone kweli uchunguzi umefanyika, wahalifu wanafikishwa katika mkono wa sheria na haki inatendeka. Tunapotaka hivi hatumaanishi kuwa matukio yaliyowakumba wengine yasifanyiwe uchunguzi, la hasha, lakini uchunguzi wa tukio fulani hauzuii uchunguzi wa tukio jingine. Ndugu IGP tunaomba majibu

5. Mwisho kabisa ndugu IGP naomba ufahamu yafuatayo:
Sisi watanzania tuliumizwa sana na tukio la kinyama alilofanyiwa mtanzania mwenzetu ndugu Lissu, tulilia naye, tulimuombea Kwa Mwenyezi Mungu amponye. Ukatili ule uliofanywa juu yake wa kumpiga risasi zote zile utadhani watu walitaka kuua Chatu ni ukatili usio na mithili. Kila nikiufikiria ukatili roho yangu inagumia. Sisi Watanzania tuna haki ya kujua akina nani walihusika ili mkono wa sheria uwe juu yao. Ndugu Sirro unavyopiga chenga au kujivutavuta katika kufanya uchuhunguzi wa hili suala, na kadri unavyoongea kwa nguvu nyingi kulifunika ndivyo nasi tunakuwa tukufikiria vibaya sana. Tafadhali usistaafu huku damu ya Lissu iliyomwagika bila hatia pale Dodoma ikiwa inakulilia kudai haki yake. Wewe hapo ulipo unaweza kuamua uchunguzi wa hili suala ufanyike ili tujue umetimiza wajibu wako, na ukishindwa unawe mikono kama Pilato tujue. Ndugu Sirro, Watanzania tuna interest ya kujua juu ya jinai ile kwa sababu inahusu maslahi ya viongozi wetu tunaowachagua, kama mkiwaachia wahalifu kwenda free basi watarudia tena hayo matendo huko mbeleni, ndiyo maana sisi watanzania tunataka mfanye uchunguzi, wahalifu wajulikane na sheria ichukue mkondo wako!

IGP SIRRO KABLA HUJASTAAFU TANATAKA KUONA UKITENDA HAKI KATIKA DHULMA HII MBAYA KABISA ILIYOWAHI KULIKUMBA TAIFA LETU
kichwa kipo mchangani, nanii nje.
 
Usiongele hisia jikite kwenye point mtoa mada alipo sema "sisi waTanzania"unaniondoaje mimi ambaye sikuguswa kabisa na tukio lile
Siwazungumzii nyie mliofurahishwa na Kitendo cha Lissu kutaka kuuawa, nazungumzia wale walioguswa moyoni na jaribio lile
 
Usiongele hisia jikite kwenye point mtoa mada alipo sema "sisi waTanzania"unaniondoaje mimi ambaye sikuguswa kabisa na tukio lile


Mkuu, Angalisema; "sisi watanzania wote"--- hapo ingalikuwa ni issue, lakini kasema; "sisi Watanzania" bado maana yake ni wale watz waliokuwa touched tu,it is just a matter of common sense tu.
 
Ndugu IGP Sirro

Nimesikiliza mahojiano yako uliyofanya na mwanahabari mmoja hapa nchini ,katika mahojiano yako umeonyesha bila chembe ya shaka kuwa hauna interest ya kufuatilia, kuchunguza na hatimaye kuwafikisha katika mkono wa sheria wahalifu waliotenda tendo baya na la kinyama kabisa la kutaka kutoa roho ya Ndugu Tundu Antipass Lissu. Ndugu IGP umetusikitisha sana kwa sababu hizi zifuatazo:

1. Mosi, Unamshutumu Mhanga badala ya wewe kudeal na Wahalifu waliotekeleza jaribio la mauaji:
Ndugu Sirro, nimekusikia maneno yako uliyotoa kwenye kile chombo cha habari, umesema kuwa Lissu ni mkaidi, ukasema eti hakutoa ushirikiano wowote katika kipindi cha kampeni ulipomuita ili umhoji kuhusiana na tukio la shambulio lake. Ndugu Sirro nataka nikukumbushe tu kuwa hata wakaidi wanaowajibu wa kutii sheria bila shuruti. Sasa naomba uueleze umma huu wa Watanzania kwa kuwa Lissu alikataa kutoa ushirikiano katika kuhojiwa Je mlimchukulia sheria gani? Maana kosa alilotendewa Lissu ambalo ni jaribio la mauaji ni kosa dhidi ya Jamhuri na siyo kosa la madai kumhusu Lissu binafsi. Kwa kweli ndugu Sirro, sababu uliyoitoa ya Jeshi la polisi kutofanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa ndugu Lissu ni sababu nyepesi sana inayotufanya tuanze kuwa na mashaka na jeshi la Polisi, Je, Jeshi lako lina kitu gani cha kuficha katika shambulio lile?, Je wewe binafsi una kitu gani cha kuficha katika shambulio. Tueleze sisi wananchi tujue, maana nyie ndo mna dhamana ya ulinzi wa mali na raia. Majibu yako yanaacha wasiwasi mwingi sana

2. Hoja yako kuwa Lissu hajawahi kuripoti popote juu ya kushambuliwa kwake ina walakini:
Ndugu Sirro, usitake kutwambia kuwa kila Jinai ya wazi lazima aliyetendewa jinai ndo akaripoti. Ndugu Sirro, Lissu alikaa kwenye coma zaidi ya wiki moja na amekaa hospitali takriban mwaka mzima, na mpaka leo hii anaendelea bado na operesheni za kujitibia (imebaki moja), Ndugu Sirro je Jeshi la Polisi lilikuwa linangoja mhanga apone ndo muanze uchunguzi? Je, mhanga angekufa maana yake ni kwamba na uchunguzi wa tendo la jinai ndo ungeishia palepale?

Ndugu Sirro kwa nini Jeshi la polisi halijafungua jalada la upelelezi wa suala hilo, Je shahidi wa hilo tukio ni mmoja tu yaani yeye?, kwa nini hamjamuita dereva wake popte alipo kumhoji, na kama ni suspect kwa nini hamkutumia Interpol kumtafuta ili kumhoji?, Mbona hamjahoji majirani, hata wabunge waliokuwa na mheshimiwa Lissu siku hiyo mbona hamkuwaita kuchukua maelezo yao?, Sirro tueleze wewe na Jeshi la Polisi mnajua nini na mnaficha nini?

3. Sirro haukutimiza ahadi yako, uliwaahidi wanasiasa waliokimbia nchi warudi utawapa ulinzi sasa umebadilika:
Mara baada ya uchaguzi mkuu, ulitoka kwenye vyombo vya habari ukiwaambia wanasiasa waliokimbia nchi kufuatia sintofahamu za baada ya uchaguzi kuwa warejee nchini utawapa ulinzi maalum, lakini juzi wakati ukiongea na mwandishi wa habari ulibadili kauli, ukasema hakuna cha ulinzi maalum na kwamba hao wanasiasa ni kama watanzania wengine tu, ukasema kuwa hata watanzania wengine huwa wanashambuliwa na majambazi n.k. Ndugu Sirro, Je unafahamu mtu aliyesurvive risasi 16 atakuwa na hali gani katika kuhofia usalama wake hasa ukizingatia kuwa alitamka mara nyingi kuwa anafuatiliwa na watu kabla ya shambulio lake lakini Jeshi la polisi liliamua kukaa kimya tu?-

Je Ndugu Sirro unataka kutwambia kuwa haimo katika utendaji wa jeshi la polisi kufanyia kazi vitisho, na kauli zenye viashiria vya jinai kutendeka mpaka mtu aripoti polisi? Kama ni hivyo basi jeshi hilo chini yako litakuwa jeshi la ajabu sana!. Kwa hiyo leo kiongozi wa serikali akisema kuwa kuna kitisho dhidi yake hamtofanya lolote mpaka akaripoti polisi?-Sasa inakuwaje mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaita press conference kueleza kufuatiliwa na watu wasiojulikana na kuhofia maisha yake lakini jeshi la polisi lipolipo tu?- Tuambie Sirro, Jeshi lako linajua nini katika hili sakata?

4. Jinai haifi, wananchi tunataka tujue kwa nini Jeshi la polisi halifanyi uchunguzi juu ya tukio la jaribio la mauaji la ndugu Lissu:
Ndugu Sirro, maelezo uliyotoa kwenye vyombo vya habari juu ya hatua ya jeshi la polisi kutofanya lolote juu ya jaribio la mauaji ya ndugu Lissu ni maelezo mepesi sana, hayajasheheni sababu kuntu za kipolisi, za kiupelelezi na kwa kweli za kisheria. Sasa tunataka tujue ni lini jeshi la polisi litafungua jalada la upelelezi wa tukio la kumpiga risasi ndugu Lissu?, tunataka kuona wito wa kisheria wa kipolisi wa kuita mashahidi ili tuone kweli uchunguzi umefanyika, wahalifu wanafikishwa katika mkono wa sheria na haki inatendeka. Tunapotaka hivi hatumaanishi kuwa matukio yaliyowakumba wengine yasifanyiwe uchunguzi, la hasha, lakini uchunguzi wa tukio fulani hauzuii uchunguzi wa tukio jingine. Ndugu IGP tunaomba majibu

5. Mwisho kabisa ndugu IGP naomba ufahamu yafuatayo:
Sisi watanzania tuliumizwa sana na tukio la kinyama alilofanyiwa mtanzania mwenzetu ndugu Lissu, tulilia naye, tulimuombea Kwa Mwenyezi Mungu amponye. Ukatili ule uliofanywa juu yake wa kumpiga risasi zote zile utadhani watu walitaka kuua Chatu ni ukatili usio na mithili. Kila nikiufikiria ukatili roho yangu inagumia. Sisi Watanzania tuna haki ya kujua akina nani walihusika ili mkono wa sheria uwe juu yao. Ndugu Sirro unavyopiga chenga au kujivutavuta katika kufanya uchuhunguzi wa hili suala, na kadri unavyoongea kwa nguvu nyingi kulifunika ndivyo nasi tunakuwa tukufikiria vibaya sana. Tafadhali usistaafu huku damu ya Lissu iliyomwagika bila hatia pale Dodoma ikiwa inakulilia kudai haki yake. Wewe hapo ulipo unaweza kuamua uchunguzi wa hili suala ufanyike ili tujue umetimiza wajibu wako, na ukishindwa unawe mikono kama Pilato tujue. Ndugu Sirro, Watanzania tuna interest ya kujua juu ya jinai ile kwa sababu inahusu maslahi ya viongozi wetu tunaowachagua, kama mkiwaachia wahalifu kwenda free basi watarudia tena hayo matendo huko mbeleni, ndiyo maana sisi watanzania tunataka mfanye uchunguzi, wahalifu wajulikane na sheria ichukue mkondo wako!

IGP SIRRO KABLA HUJASTAAFU TANATAKA KUONA UKITENDA HAKI KATIKA DHULMA HII MBAYA KABISA ILIYOWAHI KULIKUMBA TAIFA LETU
Missile of the Nation missiles are dangerous things sijui kama nia yako ni njema. Tuhuma ya kwanza ni ya kitoto, huwezi kuchunguza kama mhusika hatoi ushirikiano. Kwa mafunzo ya Kipolisi, ukikuta victim hatoi ushirikiano anakuwa treated kama ni hostile witness, atakuharibia kila kitu. Kwa nini tundulissu asiende polisi mwenyewe, kwa nini afuatwe? Aliitwa kwa IGP akakataa hadharani kwa dharau na kebehi, nadhani kuwafurahisha EU na mabwana zake mabeberu kama Sirro alivyosema. Kesi hii ni ya mchana kweupe, majambazi walionekana kwa tundulissu na dereva wake. It is pointless kumbembeleza tundulissu ajitokeze; kama hataki basi basi.

Watanzania tuko milioni 60 hatuwezi wote kuwa na body guard. CHADEMA wako milioni 10 (according to John Mrema) huwezi kuwapa wote police escort. Kuna NCCR, na Waarabu wa CUF, na UAMSHO, na Yanga, na wewe, wote mtapewa Police Escort? Why is tundulissu so special? Who is he?

La mwisho: kwa nini tundulissu kaumia upande wa kulia (kwa dereva) huku dereva hakuumia? Siku ile tundulissu alienda lunch peke yake kwa nini hata wa CHADEMA ngine hawakuenda?

Hii ya kuombewa kwa mungu barabani na viwanja vya kakobe ni private business kati yako na mungu wako, hakuna aliyewakataza. Ukitaka kuwa na T-shirt hapo hapo msikitini pia ni sawa, wewe na Paroko wako na Ustaadh na hata wakitaka ibadan kweye ubalozi wa ujerumani
 
Nimesikiliza mahojiano yako uliyofanya na mwanahabari mmoja hapa nchini ,katika mahojiano yako umeonyesha bila chembe ya shaka kuwa hauna interest ya kufuatilia, kuchunguza na hatimaye kuwafikisha katika mkono wa sheria wahalifu waliotenda tendo baya na la kinyama kabisa la kutaka kutoa roho ya Ndugu Tundu Antipass Lissu. Ndugu IGP umetusikitisha sana kwa sababu hizi zifuatazo:
IGP Sirro ulikuwa kioo cha jamii, lkn kadiri muda unavyokwenda mvuto wako unaporomoka kwa kasi ya kutisha!
Najua unakaribia kustaafu mkuu, legacy utakayoacha sidhani kama ni ile uliyoongia nayo. Jitafakari tena Mkuu wangu.
 
Missile of the Nation missiles are dangerous things sijui kama nia yako ni njema. Tuhuma ya kwanza ni ya kitoto, huwezi kuchunguza kama mhusika hatoi ushirikiano. Kwa mafunzo ya Kipolisi, ukikuta victim hatoi ushirikiano anakuwa treated kama ni hostile witness, atakuharibia kila kitu. Kwa nini tundulissu asiende polisi mwenyewe, kwa nini afuatwe? Aliitwa kwa IGP akakataa hadharani kwa dharau na kebehi, nadhani kuwafurahisha EU na mabwana zake mabeberu kama Sirro alivyosema. Kesi hii ni ya mchana kweupe, majambazi walionekana kwa tundulissu na dereva wake. It is pointless kumbembeleza tundulissu ajitokeze; kama hataki basi basi.

Watanzania tuko milioni 60 hatuwezi wote kuwa na body guard. CHADEMA wako milioni 10 (according to John Mrema) huwezi kuwapa wote police escort. Kuna NCCR, na Waarabu wa CUF, na UAMSHO, na Yanga, na wewe, wote mtapewa Police Escort? Why is tundulissu so special? Who is he?

La mwisho: kwa nini tundulissu kaumia upande wa kulia (kwa dereva) huku dereva hakuumia? Siku ile tundulissu alienda lunch peke yake kwa nini hata wa CHADEMA ngine hawakuenda?

Hii ya kuombewa kwa mungu barabani na viwanja vya kakobe ni private business kati yako na mungu wako, hakuna aliyewakataza. Ukitaka kuwa na T-shirt hapo hapo msikitini pia ni sawa, wewe na Paroko wako na Ustaadh na hata wakitaka ibadan kweye ubalozi wa ujerumani
Huchunguzi jinai kwa ajili ya manufaa ya mtendewa jinai, unachunguza kwa ajili ya manufaa ya Jamhuri. Ndiyo maana lile ni kosa la jinai na si la madai!
Halafu wa kuhojiwa siyo mhanga peke yake bali mashahidi wengi, lini umewahi kusikia jeshi la polisi limemhoji yeyote?
 
Back
Top Bottom