Uchaguzi 2020 IGP Simon Sirro, mchukulie hatua kali OCD wilaya ya Hai

Uchaguzi 2020 IGP Simon Sirro, mchukulie hatua kali OCD wilaya ya Hai

Prof Koboko

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
350
Reaction score
2,550
Ni wazi kabisa kwamba huyu OCD amelichafua na kulidhalilisha kwa kiasi kikubwa sana Jeshi la polisi nchini. Haiwezekani kiongozi ambaye ni well trained kwenye maduka ya kijeshi anaongea ujinga kiasi hicho. Polisi ni kazi ya shurba siku zote, ukitaka kuifanya upendavyo wewe utamaliza watu. Ni kazi ya heshima na hekima inayohitaji utulivu na busara katika kuamua.

IGP SIRO, wananchi tunaomba uchukue hatua stahiki kwa huyu askari kabla hali haijawa mbaya, huyu OCD ameweka historia na rekodi mbaya kwa mara ya kwanza katika Tanzania. Afande IGP usipochukua hatua kwa huyu askari chochote kitakachotokea nawe itahusika, tunaamini umeona na umesikia. Huyu OCD ni wazi kuwa anatumiwa kisiasa na hatutakubali kuwa na askari kama huyu atatuletea maafa, huyu siyo kiongozi.

 
Ameonesha ushabiki na uzalendo wa waziwazi.
Jeshi la polisi mnatakiwa kutokuonesha hisia zenu za kisiasa.

Hata kama una sababu binafsi za kuhakikisha kuwa unaemtaka ashinde utampigania kwa gharama yeyote ile.

Hata kama ni ndg yako.
 
Kwa vipi hali itakuwa mbaya? Bona wafuasi humu JF mnakariri kauli za vitisho vya viongozi wenu?

Hujui kilichojiri kurushiana hayo maneno unakuja na bandiko la kulaumu!

Wagombea wenu wanalaumu, kubeza na kudharilisha mwaona wao wana haki, ni upuuzi mtupu.

Alichosema Kamanda halisi, siyo wenu wa kujipachika, ni sawia. Amemkumbusha kuwa kwa ulevi wake wa kupindukia, ambao wapiga kura wake wanautambua na kujua kwa kina, zamu hii hachaguliwi.
 
Amchukulie hatua anathubutu???

Ajaribu kama hajarudishwa yeye nyumbani kumsaidia mkewe kukata kata vitunguu,huyo OCD wa hai tactically ameshachukua uelekeo wa maisha,awamu hii wengi wanakula na kipofu.
Mkuu tayari OCD kashaweka tabaka kubwa kati ya Wananchi wa Hai na Jeshi la Polisi. Kumbuka kuwa wako Askari wengi tu wanaoishi Uraiani. Siyo suala la kumuacha mtu kama yule kuwabeep Raia waliozoea kuishi na Polisi ktk maisha ya kawaida. Ni hatar sana.
 
Mkuu tayari OCD kashaweka tabaka kubwa kati ya Wananchi wa Hai na Jeshi la Polisi. Kumbuka kuwa wako Askari wengi tu wanaoishi Uraiani. Siyo suala la kumuacha mtu kama yule kuwabeep Raia waliozoea kuishi na Polisi ktk maisha ya kawaida. Ni hatar sana.
Awamu hii kinachoangaliwa unasimama vipi na mshika kiti kikuu,mara ngapi Magufuli amewagawa Watanzania?hivi kuna kauli mbovu na ya kizandiki kama unasimama mbele ya watu unaowahimiza kulipa kodi na kuwaambia uso kwa macho kwamba “msipoichagua ccm siwaletei maendeleo”

Kuna ubaguzi m'baya zaidi ya huo mkuu?
 
Mkuu Polisi hana nafasi hiyo. Angemuachia Mgombea wa CCM ayajibu yeye kazi yake ni kilinda amani tu. Siyo msemaji wa CCM. Hili siyo suala la siasa ni suala la Maadili ya kazi yake ya Kipolisi.
 
Tatizo kazi nyingi zinazoingiliana na siasa au kupata vyeo kisiasa ni tatizo, wachini wanafanya kazi kujionyesha ili kuchukua vyeo vya mabosi wao, Sasa inakuwa nikuharibu tu kwasababu ya cheo, hata waziri mkuu na spika wangekuwa wanatenguliwa ungeona fujo za wabunge bungeni, kikubwa mifumo ibadilike.
 
Hana CV ,Sana Sana ni mtu wa Mara kapandishwa cheo kuwa OCD kea sababu IGP ni mtu wa Mara. Ikachofanyika hai ni ugaidi Ili DC apandishwe cheo awe RC na OCD awe RPC
OCD NA RPC sio vyeo ni madaraka.

October 28 kura zote ni kwa JPM.

JPM ANATOSHA
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Back
Top Bottom