IGP Sirro, huyo ni mtoto wa nani?

IGP Sirro, huyo ni mtoto wa nani?

My Son drink water

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2016
Posts
4,932
Reaction score
13,306
IGP Sirro jana umetoa kauli nzito na ngumu mno kutolewa na kiongozi wa aina yako na mtu mwenye umri mkubwa kama wewe na mtu anayeheshimika kwa cheo chake kama wewe.

Angalia sana ulimi wako jinsi unenavyo, muombe sana Mungu akupe hekima ili kabla ya kutamka neno lolote hekima ikutangulie.

Jana ulitamka maneno haya nami nakunukuu.

"Watanzania kuweni makini msije mkazaa mtoto wa hovyo hovyo kama Hamza aliyetuletea majanga Watanzania, wazazi wa Hamza mnajisikiaje kuzaa mtoto kama huyo? Na nyie ndugu zake mnajisikiaje kuwa na ndugu kama Hamza?". Mwisho wa kunukuu.

IGP Sirro, hakuna mzazi anayepanga azae mtoto wa aina gani, Binadamu tunazaa mwili hatuzai Roho.

Kuna kijana anasumbua sana mitaani, anajitapa kwamba hakuna wa kumfanya lolote kwa sababu Baba yake ana cheo kikubwa mno serikarini, kijana huyo huvuta unga na kwenda hadi kwenye Hotel ya Baba yake iliyoko Chanika ambako hufanya vituko vya ajabu, ukiwemo kupiga watu.

Je, unajua huyo mtoto ni wa nani? Tafadhali sana, wazazi wa Hamza hawakujua kama wanazaa mtoto wa aina gani, hata wazazi wako wewe Sirro hawakujua kama ipo siku utakuja kuwa IGP.

JITOKEZE UIOMBE MSAMAHA FAMILIA YA HAMZA ILI ULINDE HESHIMA YAKO.
 
Siro ukimwangalia mwonekano wake kimwili utadhani ni mtu wa kuheshimika sana!

Hapana, kuna wakati hata matamshi yake yalionekana kuwa ya mtu mwenye busara.

Haieleweki ni kitu gani hasa kimembadilisha akili kiasi hiki alivyokuwa sasa?

Unajua, inasemekana damu za binaadam zikimwagwa kwa uonevu tu, hazimwachi mtu anayesababisha zimwagike, ni lazima atadhurika tu kwa njia moja au nyingine.

Siro ni mhanga wa umwagaji wa damu za waTanzania ambao hawakustahili kuuliwa au kuumizwa.

Maisha yake ya uhai wake uliosalia yatakuwa ya matatizo tupu.
 
Sirro tumbo Ni mithili ya shamba hutoa mazao ya Kila aina,hivyo huwezi kutukana wazazi na familiya Kisha tukupigie makofi kwa ubora wa matusi. Sirro ulichofanya Ni utoto na ulevi wa madaraka, tubu mapema. Sirro unahisi Kama kizazi chako hakifahamiki? Mbona na wewe ulizaa, kulea, na kukuza mvuta bangi anayesumbua chanika. Hotel zako za mwanza ulizijenga kwa mshahara na lesheni ya upolisi gani. Usitake tuseme yasiyotakiwa kusemwa. Kitendo Cha kudhihaki familiya HAPANA HAPANA HAPANA HAKIKUBALIKI.
 
Kaka yake hamza amesema hamza ni mbabaifu tangu utotoni kitu kilichopekekea baba yake kumpeleka Egypt kusoma dini....... kwa kauli za igp atakua anayajua mengi sana ya malezi ya hamza, sio kwamba ameropoka

Haipingiki kwamba kuwa na raia wema malezi mema lazima yaanzie kwa wazazi. Hakuna mzazi bingwa wa malezi lakini wazazi tupambane kulea tukimtanguliza Mungu huku tukikubali kurekebishwa pale tunapokosea kwenyebmalezi.

Mambo ya hamza ni mengi sana
Na bado akawa kiongozi wa CCM na ubabaifu wake.
 
Huyo ni Mtoto wa Sirro anasumbua watu sana mtaani kwa ubabe wake na anavuta bangi hadharani. Muda Mwingi anashinda Chanika kwenye Bar ya Baba yake.
Ohhoo even yule mtangulizi ana kijana sampuli hiyo hiyo even the top top lady wana kijana sampuli hiyo hiyo.

Mwambieni afute hiyo kauli aende kwa gwajima akarudishwe kwenye line
 
Back
Top Bottom