Ijue Mwanza jiji

Ijue Mwanza jiji

Ameongelea Jiji la Mwanza na sio Mkoa wa Mwanza.
Hivi ni vitu viwili tofauti.
Unapoongelea jiji la Mwanza unamaanisha ni Ilemela na Nyamagana hizi wilaya mbili ndio zinaunda jiji LA Mwanza. Na wanaobeba gharama za uendeshaji ni Nyamagana kama ilivyo kwasasa Dar es salaam Ilala ndio inabeba gharama. Jiji LA Dar es salaam wilaya zake zote zimo ndani ya jiji tofauti na Mwanza, Kwa Mwanza wilaya zenye hadhi ya Manspaa ni mbili tu yaani ilemela na nyamagana tu, zilizobaki zote ni halmashauri za mji wilaya tofauti na Dar wilaya zake zote zina hadhi ya manispaa.
Umeeleza vizuri sana, ila unachanganya kati ya wilaya na Halmashauri.

Majiji yanaundwa na Halmashauri wala sio wilaya.

Ndio maana utakuta yanaitwa HALMASHAURI YA JIJI LA ...
 
Umeeleza vizuri sana, ila unachanganya kati ya wilaya na Halmashauri.

Majiji yanaundwa na Halmashauri wala sio wilaya.

Ndio maana utakuta yanaitwa HALMASHAURI YA JIJI LA ...


Majiji yanaundwa na wilaya zenye hadhi ya Manispaa,

1.Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni(Kinondoni Municipal Council) hii ni wilaya lakni hadhi yake ni manispaa.
2.Halmashauri ya Mji Sengerema (Sengerema Town Council) hii ni wilaya lakni hadhi yake ni mji.

3.Halmashauri ya Jiji Dodoma (Dodoma City Council) hii ni wilaya yenye hadhi ya jiji.

Kwahiyo kuna majiji yanaundwa na wilaya zaidi ya mbili, mfano ni jiji LA Dar es salaam na Mwanza halafu kuna jiji linaundwa na wilaya moja tu yenye hadhi ya jiji kama jiji LA Dodoma, jiji LA Tanga, jiji LA mbeya na Arusha.
 
Majiji yanapata wp maeneo ya mashamba,!? Sheria za majiji ikoje kuhusu mashamba?


Hakuna sheria inayokataza kulima au kufanya shughuli za Kilimo na ufugaji ndani ya jiji.
Sheria iliyopo inakataza kufanya shughuli za Kilimo na ufugaji mkubwa katikati ya jiji.
Kwahiyo kama upo nje ya jiji kama huko Chanika,kigambani, mabwapande huko ruksa, ndio maana Sumaye alikuwa na ekari 300 za Kilimo na ufugaji huko mabwepande, mji unavyosogea ndio mashamba yanapoteza sifa.
Manji alikuwa na mashamba ya Ng'ombe Kijichi Temeke lakni baada ya mji kukua manispaa ya Temeke wakamlipa fidia na kupima viwanja mwaka 2000, mpaka Leo majiji yetu bado yana mapori pembezoni ndio maana unasikia miradi ya upimaji na uuzaji wa viwanja mpaka sasa.
 
Kwa wengi msioifahamu Mwanza jiji ( Mwanza city) au The Rock City , ni jiji la pili Tanzania baada ya jiji la Dar es salaam.

Jiji hili lilipewa hadhi ya kuwa Manispaa mwaka 1978 na mwaka 2002 tarehe 07 mwezi wa 07 likapandishwa hadhi ya kuwa jiji la Mwanza , lenye wilaya mbili za Ilemela na Nyamagana na jumla ya kata 20, 9 Ilemela na 11 Nyamagana . Nyamagana ndio yalipo makao makuu ya jiji la Mwanza.

UTAWALA
Baada ya jiji la Mwanza kupanuka , liligawanywa sehemu mbili yaani halmashauri ya jiji la Mwanza yenye wilaya moja ya nyamagana, hapo kuna mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Mwanza, mkuu wa wilaya ya Nyamagana pia halmashauri ya Manispaa ya Ilemela yenye wilaya ya Ilemela , Kuna mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela, mkuu wa wilaya wa wilaya ya Mwanza.

Hapo Ni kiutawala tu lakini huwezi kuitenganisha Mwanza ( Ilemela na Nyamagana) zilizokuwa tarafa za halmashauri ya manispaa ya Mwanza hadi mwaka 2002.

IDADI YA WATU
Kwa sasa tunasubiri takwimu za watu na makazi za mwaka 2022, hata hivyo inakadiriwa kuwa na watu milioni tatu hadi sasa.

VYANZO VYA MAPATO
Biashara, kilimo na ufugaji, kwa takwimu za mwaka huu hadi kufikia mwezi wa 6 mwaka huu halmashauri ya jiji imeweza kuchangia Tsh bilioni 17 Kama pato la ndani huku halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ikichangia Tsh bilioni 10 na kufanya Mwanza jiji kuchangia Tsh bilioni 27 kwa mujibu wa TAMISEMI.

ELIMU
Jiji la Mwanza lina vyuo vikuu kamili viwili , vyenye makao yake makuu jijini Mwanza yaani SAINT AUGUSTINE UNIVERSITY OF TANZANIA ( SAUT) na CATHOLIC UNIVERSITY OF HEALTH AND ALLIEND SCIENCE ( CUHAS) zamani au maarufu Weill Bugando University vyote vinamilikiwa na kanisa katoliki Tanzania kupitia TEC ( Tanzania Episcopal Conference) , hakuna chuo kikuu cha serikali jijini Mwanza ( Serikali Sasa ione umuhimu kujenga chuo kikuu Mwanza, University of Mwanza, ( UoM) kiweze kushinda na UdSm, UDOM, na Nelson Mandela.

WENYEJI
Wenyeji wa jiji la Mwanza ni kabila la Wasukuma ( Wang'weri) , yaani wasukuma wa magharibi .
Karibuni jijini Mwanza kwa fursa mbalimbali.

Imeandikwa na mimi Malika.
Kwa maoni ushauri, karibuni kwenye uzi.
Sio mwaka 2002 ni mwaka 2000 ndo Mwanza ilikuwa Jiji
 
Hapo kwenye wilaya mbili, mzee umetupiga kakamba flani hivi. Kuna wilaya nyingine kama magu, sengerema, ukerewe, misungwi n.k
Kuna vitu vingi sana hapa vinapwaya, but all in all tunashukuru kwa
Kwamba jiji la Mwanza lina kata 20?Yaani tumekukaribisha juzi juzi unaanza kujifanya kujua hili jiji?
 
Kwamba jiji la Mwanza lina kata 20?Yaani tumekukaribisha juzi juzi unaanza kujifanya kujua hili jiji?
Kata? Wapi nmeongelea kata mkuu?
Besides, i was born and raised in mwanza, how come umenikaribisha?
 
Jiji la mwanza haliwezi kufika watu mil 3 never, sensa iliyopita population ilikua laki sita na nusu ilemela na nyamagana sasa itafikaje mil 3 kwa muda mfupi hivi ?,mwanza iko over rated
Laki 6 ilikua Arusha na Mwanza ilikua 1.2 milion,ukiondoa Dar es Salaam mji wa Mwanza ni mji wa pili kwa kua na watu wengi zaidi

Hii ya miaka ya nyuma huko
View attachment 2321185
 
Mwanza nilijua ni jiji lenye hela kuliko Arusha, lakin kumbe limepitwa na Arusha banah,,
1. Dar-75.3B
2. Dom-45.1B
3. Arsh-24.3B
4. Mwnz-17.7B
5. Tanga-17.4B
6. Mby-16B
Yaani ikizubaa Tanga wanapga kiwiko
Hapo Ilemela ipo omitted soma vizuri uzi
 
Kata? Wapi nmeongelea kata mkuu?
Besides, i was born and raised in mwanza, how come umenikaribisha?
Mkuu inaonekana hujui hata ulichoandika.Hujazungumza habari za kata?🤣🤣
 
Hapo kwenye wilaya mbili, mzee umetupiga kakamba flani hivi. Kuna wilaya nyingine kama magu, sengerema, ukerewe, misungwi n.k
Kuna vitu vingi sana hapa vinapwaya, but all in all tunashukuru kwa kupaisha jiji letu
👆👆👆👆 this is exactly what i wrote
Mkuu inaonekana hujui hata ulichoandika.Hujazungumza habari za kata?🤣🤣
Haya mtaalam mwenye PHD ya mwandiko, kusoma na ku-quote comments kutoka chuo cha Jamii Forum , nisaidie kunionyesha wapi nmeandika masuala ya kata hapo juu?
Au ulikurupuka usingizini vidole vinawasha kutype?
 
👆👆👆👆 this is exactly what i wrote

Haya mtaalam mwenye PHD ya mwandiko, kusoma na ku-quote comments kutoka chuo cha Jamii Forum , nisaidie kunionyesha wapi nmeandika masuala ya kata hapo juu?
Au ulikurupuka usingizini vidole vinawasha kutype?
🤣🤣🤣🤣🤣Sorry mkuu nilikosea kuquote post yako nilimtarget mleta mada
 
Hapo kwenye wilaya mbili, mzee umetupiga kakamba flani hivi. Kuna wilaya nyingine kama magu, sengerema, ukerewe, misungwi n.k
Kuna vitu vingi sana hapa vinapwaya, but all in all tunashukuru kwa kupaisha jiji letu
Amezungumzia Jiji la Mwanza siyo mkoa was Mwanza
 
Back
Top Bottom