Ijue Rwanda, Kagame, Museveni na Uvamizi wao katika Ardhi ya Congo

Ijue Rwanda, Kagame, Museveni na Uvamizi wao katika Ardhi ya Congo

Du! ndo marayakwanza nasikia hilo,basi kama ni mkataba itabidi watimize ahadi,kwani mkataba ni mkataba mnasemaje hapo,hata mimi siwezi kubali kama nikweli yani wapoteze maisha yao kwa pimbi kabila,halafu awageuke? But kwahili hakuna ukweli wowote,huo niuzushi wa wakongo ili kesi ya M23 waifanye ya rwanda.

Nami naona kama kweli walisaini hiyo makubaliano basi ni lazima Kabila akubali,

Watu walipoteza maisha yao kwa hiyo makubaliana sharti watimiziwe
 
Mkuu MKAMASIMBA

Nimeweka vyanzo vingi sana vya makusanyo yangu ya makala haya, mimi ni Mtanzania tena Mhehe wa Nyololo Iringa, sina sababu ya kuwapendelea Watutsi ikiwa kuna habari zaidi za Wahutu,

Nimesimulia yale niyajuayo kupitia vyanzo vyangu, ikiwa kuna lolote unalolijua ambalo litaweka uwiano wakihistoria kati ya Watutsi na Wahutu basi ni vema uweke hapa wote tufaidi
 
Rwanda ilikuwa eneo penye utawala wa kifalme tangu karne ya 16 BK kabla ya kufika kwa ukoloni. Mwanzo wake ni katika eneo la Ziwa la Muhazi. Watawala wenye cheo cha "mwami" kutoka kikundi cha wafugaji (Watutsi) walitanua himaya zao tangu miaka ya karne ya 16 BK hadi kufika eneo la leo hii. Wafugaji wa ng'ombe Watutsi walikalia nchi pamoja na wakulima wa Kihutu na wawindaji Watwaa.

UKOLONI WA KIJERUMANI

Ukoloni ulichelewa kufika Rwanda, mwaka 1890 Ujerumani na Uingereza walipatana ya kuwa Rwanda na Burundi ziwe ni sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Lakini ilikuwa mwaka 1908 tu ya kwamba Wajerumani walimtuma afisa wa kudumu aliyekaa Rwanda kama mwakilishi wa serikali ya Ujerumani. Mwaka 1916 Ubelgiji na Uingereza walivamia Rwanda katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Baadae ikawa chini ya Ubelgiji pamoja na Burundi kama "Rwanda-Urundi" katika hali ya eneo la kudhaminiwa kutokana na azimio la Shirikisho la Mataifa (UNO).


Utawala wa Wabelgiji ulikuwa wa moja kwa moja na mkali zaidi kuliko wa Wajerumani. Wabelgiji walijaribu kutoa faida ya kiuchumi wakilazimisha wenyeji kupanda mikahawa na kutekeleza kazi za serikali ya kikoloni. Katika utawala wao Wabelgiji walitumia zaidi Watutsi wakiwapa nafasi za elimu na kuwatumia katika shughuli za serikali. Wataalamu wengine huamini ya kwamba siasa hii ilisababisha kukua kwa chuki dhidi ya Watutsi kwa upande wa wakulima Wahutu iliyoleta kumwaga kwa damu baadaye.

Katika miaka ya 1950 ilionekana na kudhihirika ya kwamba ukoloni unaelekea mwisho wake. Uhusiano kati ya Wahutu na Watutsi ukawa vigumu kwa sababu Wabelgiji walibadilisha siasa yao yakupendelea Watutsi wakidai haki zaidi kwa ajili ya Wahutu waliokuwa wengi. Ni hasa wamisionari wa katoliki Mapadre Weupe waliosimama upande wa Wahutu wakiona ndio wagandamizwa.

Mwami Mutara Rudahigwa aliyejiita pia Charles alijaribu kuleta upatanishi kati ya vikundi katika nchi. 1954 aligawa nchi ya kifalme kati ya Wahutu na Watutsi. Lakini alikuwa na wapinzani Watutsi waliomua mwaka 1959. Mtoto wake Mwami Kigeri V. alisimikwa kwenye kiti hicho. Hatua hii ilisababisha ghasia na vurugu nchini kwa sababu Wahutu walidai kuwa na neno katika mabadiliko ya serikali. Mwezi wa Novemba 1959 Mwami Kigeri V. alilazimishwa kuondoka nchini akikimbilia Uganda. Watutsi wenye siasa kali walijaribu kumwua kiongozi wa Mouvement Democratique Republicain (MDR) chama kikubwa cha Wahutu. Wahutu walijibu kwa kuwashambulia na kuua Watutsi. Wabelgiji walitumia wanajeshi wao kupoza hali hiyo nchini Rwanda. Katika uchaguzi wa kwanza wa halmashauri ya tarafa na miji kabla ya uhuru chama cha Parmehutu ndicho kilichopata kura nyingi. Viongozi wa Parmehutu walitangaza serikali mpya mwaka 1961. Uchaguzi wa Bunge ulileta kura ya 77% kwa ajili ya chama cha Parmehutu kilichomchagua kiongozi wake Grégoire Kayibanda kuwa Rais.

Tarehe 01.07.1962 Rwanda ilipata uhuru wake kamili. Wakati huo zaidi ya Watutsi 350,000 tayari walishakuwa wamekimbilia nchi za jirani. Mwaka uliofuata vikundi vya Watutsi kutoka nchi hizo za jirani walijaribu kufanya mapinduzi kwa kushambulia serikali mpya wakitokea uhamishoni. Kitendo hicho kilifuatiwa na uangamizaji wa kwanza wa Watutsi zaidi ya 100,000 waliouawa na Wahutu.
Hata katika miaka iliyofuata mauaji dhidi ya Watutsi iliendelea. Wanasiasa Wahutu walizoea kuita Watusi ndio "Wadudu". Kila kitu kilichokuwa si sawa kilielezwa ni kosa la Watutsi waliokuwa raia bila haki. Idadi kubwa ya Watutsi walikimbia Burundi, Uganda na Tanzania.

Mwaka 1973 Generali Habariyama alimpindua rais Kayibanda na kuanzisha serikali ya kijeshi akijaribu kupatanisha vikundi ndani ya taifa. Lakini hata mwaka uliofuata 1974 mauaji ya Watutsi yalitokea tena.

Mnamo 1990 ilikuwa wazi ya kwamba Rwanda ilikuwa na hali ngumu. Kwa upande moja nchi za mataifa zilisukuma serikali za Afrika kuruhusu kura huru za kisiasa.

Katika Rwanda ongezeko la wakazi lilileta msongamano mkubwa na uhaba wa ardhi ya kilimo na Ufugaji. Uchumi ulikuwa duni, Wakati huohuo wapinzani Wahutu walikusanyika nje ya nchi hiyo kudai demokrasia. Na katika makumi elfu ya watoto wa Watutsi waliokuwa nje ya nchi hiyo, sauti zikasikika zilizodai warudi tena kuijenga Rwanda.

Habyarimana alijaribu kutafuta suluhisho na ungamano wa kitaifa, akaanza kujadiliana na Watutsi wa nje lakini alikutana na upinzani kwa upande wa Wahutu wakali waliochukia uelewano na Watutsi.


Safari ya Kagame na RPF kurudu Rwanda kutoka Uganda.

Oktoba 1990 Watutsi waliokaa Uganda walianzisha chama cha RPF (Rwanda Patriotic Front) wakiwa na wafuasi wahutu wachache wakavamia Rwanda kwa silaha. Kiongozi wao alikuwa Paul Kagame aliyeondoka Rwanda akiwa mtoto wa miaka minne. Alikuwa amejiunga na jeshi la Yoweri Museveni na kupanda ngazi katika jeshi la Uganda hadi kuwa mkuu wa huduma ya usalama ya kijeshi ya Uganda. Walitaka kulazimisha serikali ibadilishe hali ya Watutsi kuwa raia bila haki. Lakini uvamizi huu ulisababisha kuongezeka kwa ukali wa Wahutu dhidi ya Watutsi ndani ya Rwanda na siasa kali kwa upande wa viongozi Wahutu. Kikundi cha kihutu cha Interahamwe kilipewa silaha kujibu mapigo dhidi ya uvamizi wa Kagame, Maelfu ya Watutsi Warwanda waliuawa. Vita kati ya wapinzani kutoka Uganda na jeshi la serikali iliendelea mpakani hadi pande zote mbili zilikutana hapa Arusha Tanzania na kupatana kukoma kwa vita 1992 chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika.

Sehemu ya viongozi Warwanda walijiandaa kutafuta utaratibu mpya lakini wengine walifanya mipango ya kumaliza swali la Watutsi kabisa wakipanga kuua Watutsi wote nchini.

Tarehe. 06.04.1994 rais Habariyama akirudi nchini kutoka safari ya Tanzania, Ndege yake ilipigwa kombora kabla ya kutua ikaanguka chini akafariki. Uwezekano ni mkubwa ya kwamba ni Wahutu wenye msimamo mkali ndio waliomua, lakini wengine walisema ni Jenerali Paul Kagame na RPF yake.

Tendo hili ilikuwa mwanzo wa mauaji ambayo hayakuwahi kutokea Afrika. Viongozi wa Interahamwe, wa jeshi la kitaifa na vikundi vikali vya Kihutu walitekeleza mipango ya kukusanya Watutsi kila mahali na kuwaua. Haiwezekani kuwa na idadi kamili lakini makadirio ya chini yanataja Watutsi 750.000 na Wahutu wasio wakali zaidi ya 100.000 waliuawa na Interahamwe na wanajeshi wa serikali ya Kihutu. Watu walikimbilia na kutafuta hifadhi makanisani lakini hata huko walichinjwa bila neema. Wahutu waliokataa kushiriki katika mauaji waliuawa pia.

RPF chini ya uongozi wa Paul Kagame iliamua kutumia nguvu zote kusimamisha machinjo haya. Kwa miezi miwili mauaji na vita yalienda sambamba hadi RPF iliposhinda Julai 1994 na kuchukua madaraka ya serikali.

Jeshi, Waparmehutu na serikali ya Kihutu walikimbilia Kongo wakiwalazimisha wakazi wengi kuongozana nao hali iliyosababisha kutokea kwa makambi ya wakimbizi makubwa sana katika Kongo ya mashariki yaliyokuwa na idadi ya Wahutu milioni mbili. Walio wengi wamerudi baada ya kuimarika kwa serikali mpya.

Tangu ushindi wa kijeshi mwaka 1994, RPF walianzisha serikali ya umoja wa kitaifa. Rais alikuwa Pasteur Bizimungu mwanasiasa Mhutu aliyeshikamana na RPF Kagame akiwa makamu wake. Baada ya kupinduliwa kwa Bizimungu mwaka 2000 Kagame akawa Rais. 2003 palitokea uchaguzi wa kwanza wa kirai ambapo chama cha RPF chimi ya Jenerali Paul Kagame kilishinda.

Jeshi la Rwanda limeendelea kuwa na vita ndani ya Kongo likipigana na mabaki ya Interahamwe waliokuwa wanashambulia Rwanda mara kwa mara kutoka Kongo.

Kutokana na mauaji hayo ya 1994, mahakama ya kimataifa iliyopo nchini Uholanzi imeendesha hukumu nyingi kwa wahusika wake, vilevile mahaka ya kimataifa ya Arusha nchini Tanzania nayo imeendesha huku stahiki kwa wahusika,

Ndani ya Rwanda mahakama za vijijini zinazoitwa "gachacha" vilevile zimejaribu kutoa hukuma juu ya waliohusija na mauaji ya mwaka 1994.

Mapatano ndani ya Rwanda yamezidi kushamiri, huku Paul Kagame akionsha kuijenga vema Rwanda kwa mkono wa chuma, Mathalani: D.Gasangwa wa EACU arisisitiza kwamba "Sometime in April(2004)" movie, ilikuwa "ETHNIC CLEASING", si HOLOCOSTI!, kama ilivyoandikwa na Wazungu wa Magazeti ya Ulaya. Watu karibu 600,000 waliuawa Rwanda, na hapo Mkoa wa Kivu, Congo.

Afrika ina ujuzi sasa; kama ujuzi wa Kiarabu, Kiswahili, Kilingala, Kiwolof, Kiamharic. Utengamano wa siasa mpya rasima utatupa na fasi ya kujenga inchi mpya kama EACU na Rwanda Kazembe.

Lakini huku mapambazuko mema yakitamalaki Rwanda, Kiongozi wa utawala wa nchi hiyo ndogo, anatajwa kuwa ni miongozi mwa viongozi makupe barani Afrika, ukupe wake sio waufisadi bali ukwasi wenye chembe za kiyunani

Lakini leo yale mabaki ya vikundi vile vya Interahamwe vilivyokimbilia uhamishoni kaskazini mwa Kongo mji wa Goma na Kivu si vikundi vya uasi dhidi ya Rwanda tena bali ni vitendea kazi muhimu dhidi ya upanuzi wa miliki mpya ya Watusi,

Wale watusi waliokimbilia Uganda enzi za Mwami Kigeri V, Inatajwa na kuaminika kuwa Jenerali Paul Kagame, Yoweri Mseveni na Watutsi waliokimbilia Goma baada ya kushika dola zao, walikuja na malengo mujarabu yanayotekelezwa kwa hatua na kwa vipindi virefu sana,

Mpango huo ulikuwa ni kusimika dola imara la Watutsi barani Afrika hasa nchini Kongo katika Goma-Kivu ya Kasiskani mpango siri walioupa jina la "Nchi mpya ya ahadi ya Watutsi". Ni mpango endelevu ulio na lengo la kuwakusanya Watutsi duniani kote na kuwaweka pamoja wakimiliki ardhi na rasilimali zake!

Hili linathibitika katika kile walicho "Mkataba wa kuigawa Kongo" ulisainiwa na Yoweri Mseveni, Paul Kagame na Laurent Kabila akiomba msaada wa kuingia madarakani kwa mtutu wa bunduki,

Naam baada ya Laurent Kabila kuingia madarakani kwamsaada wa Kagame na Mseveni kupitia ule mkataba, Kabila alikataa kuheshimu mkataba ule nakusema yale yalikuwa ni maneno ya porini tu hivyo hawezi kuiuza nchi kwa karatasi za mstuni!

Hapo sasa ndipo tunapoingia kwenye madhila ya Kongo tuliyoyaona tangu mauaji ya L. Kabila na tunayoyashuhudia hii leo chini ya J. Kabila, M23, Kagame na Mseveni

.........................................

MKATABA WA KUIGAWA na KUIUZA KONGO






Kinachoitwa vita vya sasa nchini Kongo ni utekelezaji wa “Makubaliano ya Lemera” ya mwaka 1996 yenye shabaha ya kuigawa nchi hiyo kubwa kuliko yoyote ile Afrika Mashariki na Kati.

Makubaliano yalifanywa kati ya Laurent Desire Kabila, akiwa kiongozi wa chama cha “kuikomboa Kongo” kutoka utawala wa dikteta Mobutu Sese Seko, kwa upande mmoja; na wapiganaji wa Kinyarwanda kutoka Rwanda na Mashariki mwa Kongo.

Makubaliano ambayo yalifanyika kwenye vilima vya Lemera vilivyoko Kivu ya Kusini na kujulikana kwa jina hilo, yalitaka Kabila, baada ya kuwa rais wa Kongo, aruhusu mikoa miwili ya Kivu Kaskazini na Kusini kuwa makazi ya Wanyarwanda wa kabila la Kitutsi.

Taarifa zilizopo zinaonyesha makubaliano yaliandaliwa mapema mjini Kigali na pale Lemera yalikuwa yanazinduliwa tu. Ilikubaliwa wakati huo kwamba hiyo ndiyo ingekuwa “asante” kwa Rwanda “kwa ukombozi wa Kongo.”

Desire Kabila alikuwa tayari amechoka. Kwa takriban miaka 20 alikuwa akipambana na utawala wa Mobutu Sese Seko. Alikuwa amefikia hatua ya kukata tamaa na kutulia jijini Dar es Salaam.

Mwaka 1996, mjini Kigali, Rwanda kilikuwa kimeundwa kikundi cha wapiganaji waliojiita “wapinzani wa dikiteta Mobutu.” Hawa walikuwa Wakongomani na Wanyarwanda kutoka Rwanda na wengine waliokuwa wakiishi mkoa wa Kivu Kusini, Mashariki mwa Kongo.

Katika kundi hilo alikuwemo Mkongomani, Jenerali Andre Kisasi Ngando; askari mtaalam wa kusomea. Anadaiwa kupata mafunzo nchini Cuba, Ujerumani na Bulgaria. Alikuwa akiongoza Wakongomani wapatao 600 katika kikundi hicho.

Wakati kikundi hicho kinataka kuanza vita, kilitaka kuwa na msemaji. Mungu akupe nini! Hakuna uthibitisho wowote, lakini taarifa zinaeleza kiliomba ushauri wa Mwalimu Julius Nyerere “ambaye aliwapa Laurent Desire Kabila kuwa msemaji wa wapiganaji.”

Mwanzoni mwa vita ya kumg’oa Mobutu kikundi hiki kilijulikana kama cha Wanyamulenge. Dunia nzima ikaambiwa na kuaminishwa kuwa hayo yalikuwa “maasi ya Wanyamulenge.”

Wanyamulenge ni watu wanaodaiwa kutoka kwenye vilima vya Mulenge vilivyoko wilaya ya Uvira katika mkoa wa Kivu Kusini. Makabila ya asili ya hapa ni Wavira na Wafuliro. Wanaojiita Wanyamulenge ni Wanyarwanda wakuja.

Vita vilianza kwa propaganda kuu kwamba serikali ya Mobutu haitambui Wanyamulenge ambao walidai ni raia wa Kongo; inawanyanyasa na inawanyima uraia. Haya yalikuwa madai makubwa sana yaliyovuta hisia kali na huruma kwa wapiganaji.

Wapinzani, chini ya Jenerali Andre Kisasi Ngando, na msemaji mkuu wao Laurent Kabila waliteka, kama mchezo, mji mkuu wa Kivu Kaskazini, Goma. Wakavuka Ziwa Kivu na kuingia Kivu Kusini.

Ilikuwa baada ya kukamata mji wa Bukavu, makao makuu ya Kivu Kusini na sehemu nyingi za mkoa huo, wapiganaji wa Kinyarwanda waliingiza pendekezo la rais ajaye wa Kongo, kutoa Kivu Kaskazini na Kusini kwa Rwanda.

Lakini kabla suala hilo nyeti kupewa uzito unaostahili, wapiganaji wa Kinyarwanda, baada ya kuteka Bukavu, wanadaiwa kuanza kupora mali – magari, vifaa vya nyumbani, dawa katika maduka – hatua ambayo ilielezwa kuwa uhamishaji wa mali za wakazi wa Bukavu na maeneo mengine.

Alikuwa Jenerali Ngando anayeripotiwa kupinga uporaji usiomithilika, jambo ambalo lilimletea uhasama kwa baadhi ya wapiganaji. Kuona hivyo, Laurent Kabila akamwasi Ngando.

Ngando anasemekana kuuawa siku chache baada ya kutofautiana na wapiganaji juu ya uporaji. Inaelezwa kuwa alimiminiwa risasi na kuuawa na mwili wake kuchomwa moto katika mbuga ya wanyama ya Virunga.

Kabila aliulizwa mara nyingi juu ya Ngando. Alikuwa na majibu tofauti. Akiwa bado msituni alisema Jenerali Ngando amekamatwa na majeshi ya serikali na mara ametekwa na wanamgambo wa Mai Mai.

Baadaye Kabila alisema Ngando alijeruhiwa na kupelekwa Ujerumani kwa matibabu. Na wakati akiwa rais, aliwaambia waandishi wa habari mjini Kinshasa kuwa Ngando alikuwa askari kama askari wengine na kwamba alikufa kwenye mapambano.

Ilikuwa baada ya kifo cha Jenerali Ngando ndipo Kabila aliingizwa kwenye makubaliano ya kumega Kongo. Kwanza, kikundi cha wapiganaji kiligeuzwa kuwa chama – AFDL – Alliance de front Democratique pour la Liberation du Congo.

Kabila akapanda cheo na kuwa kiongozi wa chama cha ukombozi wa Kongo kutoka kuwa msemaji tu wa wapiganaji.

Baada ya kuundwa kwa AFDL, jina la Wanyamulenge likatoweka kabisa. Wapiganaji wakaitwa waasi wa Kongo. Taarifa zinasema kabla wapiganaji kutoka Bukavu na kuanza safari iliyomfikisha Kabila madarakani, waliingia katika mkataba ambao ndio umekuja kuitwa “Makubaliano ya Lemera.”

Kuna madai kwamba viongozi wakuu wa wakati huo wa baadhi ya nchi walipata nakala ya makubaliano hayo ya kumega Kongo. Miongoni mwa nchi hizo ni Namibia, Uganda, Burundi, Zambia, Ethiopia, Eritrea, Zimbabwe, Angola, Namibia, Sudan na baadhi ya nchi za Ulaya na Marekani.

Imeelezwa kuwa makubaliano ni pamoja na kufanya mikoa ya Kivu Kaskazini na Kusini kutawaliwa na Wanyarwanda wa Kitutsi kutoka mataifa ya Rwanda, Burundi na Uganda; na kwamba utawala huo ambao ungefanya kazi kwa ushirikiano na serikali ya Kabila, ungetekelezwa kwa awamu tatu katika kipindi cha miaka 10 kuanzia 1998.

Chini ya mpango huo, raia wa Kongo, wakazi wa Kivu Kaskazini wangehamishiwa Kivu Kusini, “taratibu na kwa utulivu huku makazi yao yakichukuliwa” na wavamizi.
Imeelezwa kuwa hatua ya kwanza isingekuwa ngumu kwani Rwanda ingedai kuwa inapambana na wanamgambo wa Kihutu walioitwa Interhamwe ambao itaelezwa kuwa wanatishia amani nchini Rwanda. Hivyo ndivyo imekuwa ikifanya hadi sasa.

Makubaliano yanadaiwa kueleza kuwa kuchukuliwa kwa miji ya Goma na Butembo mkoani Kivu Kaskazini, sharti iwe hatua ya kwanza kwa kuwa hayo ndiyo maeneo yenye upinzani mkubwa. Kufanikiwa kwa awamu ya pili, kungetegemea mafanikio ya awamu ya kwanza, makubaliano yanadaiwa kueleza.

Wafuatiliaji wa mahusiano ya Rwanda na Kongo wanasema ingawa mpango huo ulishindikana kutekelezwa kuanzia mwaka 1998, kuingia kwa majeshi ya Rwanda nchini humo hivi sasa, ni utekelezaji wa hatua ya kwanza ya Makubaliano ya Lemera; na tayari miji ya Goma na Butembo iko chini ya kile kinachoitwa “majeshi ya ushirikiano” ya Rwanda na Kongo.

Kwa mujibu wa masimulizi juu ya makubaliano hayo, awamu ya pili ingekuwa kujaza wakazi wa Kaskazini katika Kivu Kusini na kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa ambapo wazawa wangeenguliwa, kukosa uongozi na hivyo kunyimwa sauti.

Hatua nyingine ilikuwa kuanzisha benki ya kusaidia wavamizi katika Kivu mbili, kujenga nyumba zipatazo 600,000 na kujiimarisha katika nchi ya kigeni – Kongo.

Imeelezwa kuwa Kabila alikubaliana na masharti ya makubaliano kwa kuwa lengo lake lilikuwa moja tu: Kuingia ikulu ya Kinshasa kwa msaada wowote kutoka kwa yeyote; Mungu au shetani.

Ilikuwa baada ya makubaliano hayo, Kabila alisonga mbele na hatimaye kushinda na kuingia ikulu ya Kinshasa akiwa na wapiganaji wa Rwanda, akiwemo mkuu wa sasa wa majeshi wa Rwanda, James Kabarebe.

Baada ya kuingia ikulu, Kabila anadaiwa kuwageuka wenzake. Ilikuwa baada ya miaka miwili ya urais, alitangaza, tena kwa jeuri, kuwa wageni wote waondoke nchini. Aliongeza kwa kufafanua, kwamba Wanyarwanda warudi kwao na kusema anawashukuru kwa kazi waliyofanya.

Kabila alikuwa tayari amesoma mwelekeo wa makubaliano yake na kuona kuwa yanatoa mwanya kwa kile kilichoitwa “Nchi ya Ahadi” ya Watutsi kutoka Rwanda, Burundi, Uganda, Somalia, Ethiopia, Eritrea na Tanzania.

Alitakiwa atangaze, akiwa rais, kuwa Kivu mbili zote ni makazi ya Watutsi; ili hata wananchi wa Kongo watakaobaki humo, wawe wanafahamu kwamba siyo kwao.

Kabila alinukuliwa akisema kuwa hayo (Makubaliano ya Lemera) ni “makubaliano ya porini” na kwamba yeye hakuwa na madaraka ya kuuza nchi. Alisema hakatai kuwepo mkataba, lakini akataka hilo “lipelekwe kwa wananchi – kupitia bungeni – ili wananchi wenyewe waamue.”

Kilichomshangaza zaidi Kabila, baada ya kutangaza kuwa Wanyarwanda warudi kwao, ni kwamba aliyekuwa wa kwanza kuondoka na kukimbilia Afrika Kusini, alikuwa waziri wake wa mambo ya nje aliyeitwa Bizima Karaha (Bizimana Karahamuheto).
Katika mshangao na labda kejeli, Kabila alisema, “Kumbe nchi ilikuwa imevamiwa! Hata waziri wangu wa mambo ya nje alikuwa Mnyarwanda?”

Hiyo ilifuatiwa na kufukuzwa kwa James Kabarebe aliyekuwa mkuu wa majeshi ya Kongo na sasa mkuu wa majeshi ya Rwanda. Hatua hizi na nyingine, ndizo zilisababisha kutotekelezwa kwa Makubaliano ya Lemera.

Lakini wachunguzi na wafuatiliaji wa mahusiano ya nchi hizi mbili wanasema, makubaliano yameandikwa na yapo; hayajafutika. Kilichofanyika ni “ukaidi wa Kabila” wa kutotaka kutimiza ahadi yake baada ya kuingia ikulu.

Kabila anasemekana alikuwa amesoma kitabu cha Raphael Ntibazokiza kikieleza mahusiano ya Watutsi na wabantu, kiitwacho Plan de la colonisation tutsi au Kivu et region centrale de l’Afrique – Mpango wa ukoloni wa Kitusi katika Kivu na eneo la Afrika ya Kati.

Raphael anaandika, “Mhutu ameumbwa kufanyia kazi watu wengine; hawezi hata kujaribu kupata uongozi. Chukua nafasi zote za mikoa na wilaya na atakayekuwa mtawala ahakikishe kuwa analinda maslahi yetu... Baadaye watakapokuja kustuka, watakuwa wamechelewa…”

Mmoja wa waliokuwa karibu na Laurent Kabila amenukuliwa akisema hakuna kitu kilichomsononesha Kabila kama kauli ifuatayo ndani ya kitabu cha Raphael:
“Tutumie ukarimu wao. Tujinyenyekeze kwao kama sisi ni watumishi wao.

Tukiishachukua nafasi zao tuwatelekeze na ‘kuwalipa ujira wa nyani’- payez-les en monnaie de singe pour montrer leur incapacite – ili kudhihirisha kuwa hawana uwezo.”

Kabila aliuawa kabla hajamaliza kunyukana na Rwanda. Aliuawa na mmoja wa “watoto” wake – vijana wadogo waliokuwa watu wa karibu sana na waliomlinda tangu akiwa msituni.

Kuna maelezo tatanishi juu ya kifo chake. Kuna wanaodai aliyemuua alitumwa na waliokuwa wakitaka atekeleze makubaliano ya Lemera; lakini wengine wanadai ni karata za nchi za Magharibi.

Kwa kuwa Jonas Savimbi aliuawa katika wiki moja tu baada ya kifo cha Kabila, inadaiwa kulikuwa na mkono wa mataifa makubwa; hili likitaka kuingia Kongo na hivyo kuomba msaada wa kuondoshwa kwa Kabila huku likiwezesha kukamatwa na kuuawa kwa Savimbi. Siasa hizi hazijafafanuliwa.

Kuingia kwa Joseph Kabila, anayedaiwa kuwa mtoto wa kufikia wa Laurent Kabila, kunaonekana kuleta mgeuko mwingine kuelekea kule ambako “baba” yake alikataa.
Kinachoitwa makubaliano kati ya serikali ya Rwanda na ile ya Kongo kinaonekana wazi kuwa utekelezaji wa mpango wa awali ambao Laurent Kabila alikataa.

Aidha, kukamatwa kwa Jenerali Laurent Nkundabatware na kuhifadhiwa nchini Rwanda kunaelezwa kuwa sura kamili ya “kuheshimu kazi ya maandalizi aliyokuwa akifanya nchini Kongo.”

Kuna madai kuwa Nkundabatware, Mnyarwanda kutoka Rwanda, lakini Rwanda inasema ni Mkongomani, hakuwa na jeshi lolote nchini Kongo. Aliongoza majeshi ya Rwanda hadi hapo ilipoonekana kuwa mazingira yamekuwa mazuri kwa Rwanda kuingilia kwa kisingizio cha “kufukuza Interhamwe na kuweka usalama mpakani.”

“Hata akipelekwa Kongo leo hii, Kabila atamlinda Jenerali Nkundabatware, labda kama wakuu wa Kongo na Rwanda watakuwa wamegundua kuwa amewasaliti,” kimeeleza chanzo cha habari hizi mjini Goma.

Rwanda imeingia Kongo. Nani ataiondoa? Baadhi ya nchi jirani zimekuwa watazamaji tu wakati nyingine zikiwa katika maandalizi ya kunufaika kutokana na mgogoro wa nchi hii.

Moses Byaruhanga, waziri katika ofisi ya rais (Siasa) nchini Uganda, amesema nchi yake inaunga mkono “shirikisho la Kivu na Kisangani” na kwamba wanasubiri kuona serikali ya Kinshasa inalionaje suala hilo.

Katika siku za karibuni kumekuwa na taarifa za kukamilisha kumegwa kwa mikoa miwili ya Kivu Kaskazini na Kusini kutoka Jamhuri ya Kongo na kuzifanya muungano wa Jamhuri ya Kivu.

Kauli ya msemaji wa ikulu Uganda inaongeza uwezekano wa kuimega Kongo pale inapohusisha jimbo jingine la Kisangani ambako majeshi ya Uganda yanadai kuwinda waasi wa Lord’s Resistance Army (LRA).

Kiongozi wa LRA, Joseph Kony amekuwa akipambana na majeshi ya serikali ya Yoweri Museveni kwa zaidi ya miaka 15. Uganda sasa inadai kuwa Kongo inatumika kama kichaka cha waasi hao.

Kauli ya Uganda haipishani na mipango inayodaiwa kufanywa na Rwanda ingawa Rwanda, kupitia balozi wake mjini Dar es Salaam ilikaririwa ikisema haina mpango wowote wa kuigawa Kongo.

Jumuiya ya kimataifa imetekwa kwa propaganda za Interhamwe, Wanyamulenge, waasi wa LRA na kumbukumbu za mauaji ya kimbari.

Isipokuwa Barrack Obama ambaye angalau amesema anataka Kongo tulivu na kwamba atasaidia kuleta hilo, mataifa mengine, pamoja na Ufaransa, yanataka kuimega Kongo.


Vielelezo:

Moabi KKK/BKK
Yunani
Wikipedia
Tutsi
Hutu
Twa
Paul Kagame
Laurant Kabila
Yoweri Mseveni
MwanaHalisi

Mimi Mwen
UMOJA WA WANYARWANDA WAKIMBIZI
Brazaville Dar es Salaam Cape townLondon​
Tel. +242069728747 +255755047545 +27795382019 +447413549095
E-mail: <hutubanturace@gmail.com>​





KWA MAANDALIZI YA KUREJEA KWENYE NCHI YETU
RWANDA, JIBU LA MAZUNGUMZO YA KISIASA








MATATIZO MAKUBWA YA WANYARWANDA NI YA KISIASA NA YANAGUSA KILA MUNYARWANDA. UFUMBUZI WAKE NI MAZUNGUMZO YA KISIASA KATI YA WANYARWANDA AMBAO WAKO KWENYE UONGOZI WA RWANDA LEO, WANANCHI, UPINZANI, NA UMOJA WA WANYARWANDA WAKIMBIZI.

KWA MAANDALIZI YA KUREJEA KWENYE NCHI YETU RWANDA: JIBU LA MAZUNGUMZO YA KISIASA.
MAZUNGUMZO KATI YA WANYARWANDA: NJIA PEKEE YA KUONDOKANA NA TATIZO LA KISIASA.
Mazungumzokatiyawanyarwandayanayoandaamazingirayamaelewanokatiyawanyarwanda, ndiyonjiapekeeyakuondokananamatatizoyoteya Rwanda. Viongoziwataifahilo, walitakiwakuzingatianafasihiimuhimunakufikiahatuayakubadilishamutazamowao.
Mdaumefikailiwanyarwandawotetuishipamojakwenyenchiyetu. Rwanda ninchiyetusisiwotenaitajengwatunaumojawawatwa, wahutunawatutsi. Hayomazungumzondiyodhamanayamatokeomazurikwenyemaswalayakisiasa, kiuchumi, kiutamaduni, nk,katikataifaletu.Wakimbiziwotewakinyarwandawanaotakakurejeakwao, huundiomsimamowao,bilauogawalakubabaisha.
Tangumiaka 19,tukiwanjeyanchiyetu, uongoziwaKagameunajuavizurisanakwambatumeachananafamiliazetu, tumepotezamalizetu; kwambanyumbazetuzimebomolewa au zimechukuliwanawatuwenginenakwambanduguzetuwengiwanasutanakuteswakwenyemagerezabilakesiyoyotebadayakuwatuwamesingiziwa. Hatunaimanitenana Paul Kagame, ndiyomanatunatakiwakuzungumzia kwanza maswalayausalama, namengineyotekablahatujarejea Rwanda.
Paul Kagameanajuavizurisanakwamba, wengimiongonimwawanajeshi wake, au wanachamawa RPF, ambaowamemwagadamuzawanyarwandawengi, wakohurubilahofuyoyote, nahiyohaliinaonyeshajinsiganimahakamazauongoziwa Kigali siyozakuaminika.

MADAI YETU MAKUBWA YANAHUSU VITU VIFUATAVYO:
- Mazungumzokatiyawanyarwanda
- National Reconciliation
- Kutambulikakwavyamavyasiasavyaupinzaniikiwandani au njeya Rwanda bilayakuviingizakwenyekitukinaitwa “forum”
- Kuingizawakimbiziwotewatakaorejeakwaokwenyemaishayakawaida
- Kuachiliahuruwafungwawotewakisiasa
- Mahakamazisizopendeleakwawanyarwandawote
- Kuingizawanajeshiwazamanikwenyejeshi la taifa
- Kuhakikishausalamawawatunamalizao
- Kusomeshawatotowoteambaowazaziwaohawanauwezobilaubaguziwowote
- Uhuruwakujielezanakutoamaoni
- Kuandaamazingiramazuriyauchaguzihuruna transparent kwenyengazitofautitofauti.


NATIONAL RECONCILIATION.

Nationa Reconciliation nikituambachohadileokimeupigachengauongoziwa RPF. Tanguinashikamadarakamwakawa 1994, RPF inaendeleakuenezauongokwamataifakwambainaupakipaombeleumojawakitaifa, wakatimatendoyakeyakisiasanakijeshiyanapelekeakwenyechuki. Viongoziwa RPF hawaachikuonyeshajeurikwambachamahichokimeshindakwamtutuwabundukinakwamanahiyokinatakiwakutawalakimabavu. Ndiyomanawahutuwotewaliyouawana RPF wamesahaulika, wakatiwatutsiwaliyokufawanakumbukwawakatiwote. RPF itadaijekwambakuna reconciliation ikiwawaliyokufawotepandezotehawakumbukwiwote?
Tunasisitizakwamba national reconciliation katiyawanyarwanda, inatakiwakutokananaumojakatiyawanyarwandawote. Ili tufikekwenyeumojahuo, kunavitu 4 muhimuvyakujua:

- Hukumusawakwawatuwapandezotembiliambaowameingizakwenyemachafukotaifa la Rwanda. Aidhakwakuundatuumeyakitaifayakufuatilia, au kwakupanuwa mandate ya ITPR kwaviongoziwaserikaliya Kigali naya RPF waliyohusikakuuawahutundaniya Rwanda nakwenyenchiambazowamekimbilia;
- Hakiyakumbukumbukwawaliyokufawotenasiyotukwaupandemmoja;
- Uchunguziwa kina au utafitikwenyeukwelikuhususababuzamsingikwenyematatizoyanayogonganishawanyarwanda;
- Hudumakwawahangawotebilaubaguzi.
Tunafikiritenatunaaminikabisakwamba “tuumeyakitaifayaukweli, uhuruwamahakamana reconciliation, ambayopekeendiyoyenyeuwezowakurejeshaamanikwenyetaifa la Rwanda, inaitajikasana”. Ndiyomanaumojawawanyarwandawakimbiziunaombaviongoziwa Rwanda kuchangamkiaharakatizakuundahiyotuume.
KUINGIZA ASKARI WA ZAMANI (EX FAR) KWENYE JESHI LA TAIFA
Ili matatizoya Rwanda yafikieukomo wake, tunatakiwakukubarianakwambakunasehemuyawanajeshiwazamani(ex FAR)ambaowanaishiukimbizinitakribanimiaka 19 imepita. Kwaajiliyausalamazaidiwataifa la Rwanda, wanajeshihaoambaoniwakimbizi, hawatakiwikubakimisituni. Wanaitajikurejeakwenyenchiyaokwanjiayamazungumzoitakayoandaamazingirayakuwaingizakwenyejeshijipya la taifa.Nikwanjiayamazungumzotukwenyeambayohawowanajeshiwakimbiziwanawezakurejea Rwanda bilakuwanawasiwasi.
MAANDALIZI YA UCHAGUZI HURU NA TRANSPARENT KWENYE NCHI YA RWANDA
Uchaguzihuruna transparent kwenyetaifa la Rwanda ukombalikwasababu Rwanda inatawaliwakimabavunachamakimojaambachondichokinaruhusiwakutoamgombeauraismmoja.
Kwenyenchiya Rwanda wakatiwauchaguzimkuu, wagombeauraiswavyamavyaupinzaniwanabugudhiwa, wanachukuliwakama negative forces, maranyinginewanakamatwanakutupwandaniiliwaregezwekisiasa, nahatimayekuwafanyawapotezesifazaozote. Mifanohainikama Madame INGABIRE Victoire, mwenyekitiwa FDU, mgombeakwenyeuchaguziwaraismwakawa 2010; Dr MUSHAYIDI Deogratias, mwenyekitiwa PDNnaMr Bernard NTAGANDA, mwenyekitimwanzilishiwa PS imberakuri….Wanyarwandawanakiukubwayakujichaguliaraiswanayemutakabilakulazimishwa.
KUJENGA RWANDA MPYA NI KAZI YA WANYARWANDA WOTE
Kwamtazamohuo, Paul Kagamekamaraisnayeyenimmojawawanaotakiwakujenga Rwanda mpya.
Kuna takribanimiaka 19 wanyarwandawanazururakutokananamachafukoyaliyoikumba Rwanda yakayipelekeakutumbukiakwenyegizanenemwakawa 1994. Lakini, wakatiwotetukiwaukimbizini, serikaliya Kigali haijabadilishasiasazakezaubaguzinaukandamizajiwaupandemmojawawananchi. Hiyosiasainazuiasanawakimbiziwakinyarwandakurejea Rwanda kwahiyariyao.
Ukwerinikwambaserikaliya Kigali, hainampangowalauhiyariwakujengamazingirayamazungumzonakuwekapamojawanyarwandawote.
Kinyumechake, serikalihiyoinaendeleakuchocheamauaji, ambayoyamekuwandiyosirahayake. Ukosekanajiwasiasayakweliyakujengataifaletukwenyemaeneoyote (uchumi, utamaduni, mahusiano, uhuruwakuabudu…), wakimbiziwotewanamashakakwenyemanenoya Paul Kagamekuhusukurejeakwao.
Kutokakwenyegazeti la Le Figaro la tarehe 24 December 2010 “Paul Kagamealijutiahadharanikuwahakuwezakuuawahutuwotewaliokimbilia DRC, naakaahidikwambaatakujakumalizananaobadaye”, wakimbiziwanawezakuwanasababunzurizakujiulizamaswalikwenyehabarihiyoyakurejea.

HITIMISHO
Kwamfanowanchiambazozimepitakwenyemigogoromikubwakama Rwanda, umojawawanyarwandawakimbizi, unaaminikwambaniwakatimwafakawakuandaa mambo yajaobilakusahauyaliyopita. Lakinipia, umojahuohuo, unajuakabisakwambawapowanaumenawanawakeambaowanajuaumuhimuwakusameheyana, umuhimuwakujiunganakupendakuishipamoja. Ndiyomana, umojahuowawakimbiziungependakuhusishwakwenyekujenga Rwandampya, nchiyetu, kwakuunganishawanyarwandawotebilaubaguzi (watwa, wahutunawatutsi) nahatimayekujenganchiyenyeamaninademokrasia.


MSEMAJI WA UMOJA WA WANYARWANDA
DEOGRATIAS KAREGEYA-DENMARK
+4591703492


COMMUNAUTE DES EXILES RWANDAIS
Brazaville Dar es Salaam Cape town LondonTel.+242069728747 +255755047545 +27795382019 +447413549095
POUR UN RETOUR DIGNE DES EXILES A LA MERE PATRIE: LE RWANDA
UNE REPONSE A L’OFFRE POLITIQUE DE RETOUR AU RWANDA
 
Mkuu hujamwelewa hasa anachozungumza,Katika hili tukiweka hisia tukautenga ukweli halisi tutakuwa tunakosea,
Mkuu YN, KOBA ana akili sana - tukumbuke ana wajibu wa kumtetea PK na ndugu zake which's healthy, binafsi nafikili wakati mwingine tusimulahumu SANA. Siku moja nilicheka sana, aliwahi kuanzisha thread za kumlahumu/shutumu PK na kutoa link zenye kuweka chumvi mno za kumsema sema sana PK. Kilicho nishangaza baadhi ya wana JF wali swallow hook, line, and sinker wakifikili ndugu KOBA kamugehuka PK!! Mimi nilijua hiyo ni janja ya KOBA anataka kuwachota akili wasomaji - ni hilo tu, na ndicho kilicho tokea. Kunisema kwamba kumbe mimi ni mtu wa Kigoma hiyo ni njia mmoja wapo ya kutuma ujumbe fulani kwa kuwa amekwisha nisoma na kujua kwamba deep down siwachukii Watutsi per se, kinacho nichukiza ni viongozi wao kupenda penda kupigana vita na kuwa na mawazo ya kifahidhina ambayo ndio yanaweza kuwa chanzo cha kufanya Raia wa maziwa makuu kushindwa kuelewana na kuanzisha vurugu zisizo na kikomo, mimi sina matatizo na Watutsi wahadirifu walio wengi, nilisha sema nimebahatika kukaa nao kwa karibu tangu nikiwa mdogo nimejifunza mambo mengi kuhusu tamaduni zao, lugha yao, falme zao, matazo yao ya jadi na Wahutu, imani zao nk.
 
Yericko Nyerere

Sasa nimeamini kuwa UKOO wa NYERERE ni WATUSI.

Umepotosha sana historia Ndugu yangu sijuhi kwanini.Ila Historia haiwezi kukamilika bila kuzungumzia yafuatayo:-

1. Uhusiano wa Kanisa Katoliki katika kuchochea chuki za Watusi na wahutu.

2. Mauji ya Wahutu zaidi ya 200,000. Miaaka ya 60. Maana wewe makala yako yote unaonyesha ni watusi tu ndio waliouwawa lakini wahutu hapana, Hii ni chuki ya moja kwa moja kwa wahutu.

3. Utunguaji wa ndege uwezi kuuzungumzia bila kutuambia kuwa na Raisi wa Burundi aliuwawa pia.

4. Huwezi kuzungumzia the Rise of Museven na Kagame bila kuzungumzia Vita vya Kagera zidi ya Idd amini, Pia kutukumbusha kuwa hawa Museven na Kagame Nyerere aliwafundisha mwenyewe Monduli na kuwatumia vita vya Kagera. Kumbuka Vita vya kagera vilitokana nqa Nyerere kufuga vikundi vya waasi wa Kitusi huko Kagera na Amin kuamua kuja vichakaza, Kifupi sisi ndio tuliwachokoza na tulitumika kama Proxy tu, ila nia ilikuwa ni Kagame na Museven watawale Uganda na Rwanda.

Kibanga nadhani umetoka kwenye mstari kishabiki!

mtoa thread amejitahidi kugusa maeneo mengi iwapo unataarifa pia tuwekee tusome. Napingana na wewe kuwa Amini alivamia Tanzania kupiga watusi, huo ni uwongo nadhani unataka kuchafua mada sijui Kwa lengo gani. Ikumbukwe kua hata Obote alikuwa hapa Tanzania baada ya kupinduliwa na TAnzania iliendelea kumheshimu Kama head of state wa Uganda. Nadhani hilo ndilo lilimchukiza sana Idd Amin. Pia habari ya kagame na Museveni kuandaliwa na Nyerere Kwa makusudi ya kutawala Rwanda na Uganda ni uzushi wa wahutu hasa walioshiriki mauaji ya kimbali.
 
Yericko Nyerere

Sasa nimeamini kuwa UKOO wa NYERERE ni WATUSI.

Umepotosha sana historia Ndugu yangu sijuhi kwanini.Ila Historia haiwezi kukamilika bila kuzungumzia yafuatayo:-

1. Uhusiano wa Kanisa Katoliki katika kuchochea chuki za Watusi na wahutu.

2. Mauji ya Wahutu zaidi ya 200,000. Miaaka ya 60. Maana wewe makala yako yote unaonyesha ni watusi tu ndio waliouwawa lakini wahutu hapana, Hii ni chuki ya moja kwa moja kwa wahutu.

3. Utunguaji wa ndege uwezi kuuzungumzia bila kutuambia kuwa na Raisi wa Burundi aliuwawa pia.

4. Huwezi kuzungumzia the Rise of Museven na Kagame bila kuzungumzia Vita vya Kagera zidi ya Idd amini, Pia kutukumbusha kuwa hawa Museven na Kagame Nyerere aliwafundisha mwenyewe Monduli na kuwatumia vita vya Kagera. Kumbuka Vita vya kagera vilitokana nqa Nyerere kufuga vikundi vya waasi wa Kitusi huko Kagera na Amin kuamua kuja vichakaza, Kifupi sisi ndio tuliwachokoza na tulitumika kama Proxy tu, ila nia ilikuwa ni Kagame na Museven watawale Uganda na Rwanda.

Kibanga nadhani umetoka kwenye mstari kishabiki!

mtoa thread amejitahidi kugusa maeneo mengi iwapo unataarifa pia tuwekee tusome. Napingana na wewe kuwa Amini alivamia Tanzania kupiga watusi, huo ni uwongo nadhani unataka kuchafua mada sijui Kwa lengo gani. Ikumbukwe kua hata Obote alikuwa hapa Tanzania baada ya kupinduliwa na TAnzania iliendelea kumheshimu Kama head of state wa Uganda. Nadhani hilo ndilo lilimchukiza sana Idd Amin. Pia habari ya kagame na Museveni kuandaliwa na Nyerere Kwa makusudi ya kutawala Rwanda na Uganda ni uzushi wa wahutu hasa walioshiriki mauaji ya kimbali.
 
Read between the lines! "inasemekana.....halafu kuhusika sio lazima uwepo physically"
Mkuu unajuwa watu wengine ufikilia wahusika lazima wawe kwenye tukio ndio wahusike na uharifu!! Ukweli wa mambo ni kwamba kulikuwa na tofauti kubwa ya approach au tuseme stratergy ya vita vya msituni kati ya Fred na Kagame, Fred ali-prefer softly softly approach i.e kuelimisha raia kwenye area iliyokombolewa na wapiganaji wa msituni kabla hawajasongo mbele kwenye area nyingine, the idea behind all this ni kwamba kwa kufanya hivyo watahungwa mkono na raia wa Rwanda bila ya kujali ukabila, Kagame na radical wenzake waliona approach ya Fred itawachelewesha sana! Wenyewe walikuwa wanataka approach ya voda fasta. Kati ya Fred na Kagame, Fred alikuwa na experience kwenye nyanja ya vita kuliko Kagame, Fred vile vile aliwahi kushiriki katika vita vya ukombozi wa Msumbiji kama mafunzo, Kagame taaluma yake ilikuwa ni upande wa Intelligency aliyo somea hapa Tanzania. Sasa nini kilitokea - Fred aliongozana na wanajeshi wenzake wa Kitutsi kutoka Uganda na kwenda mpakani mwa Rwanda na Uganda kuanzisha vita vya kumung'oa Rais Habyalimana madarakani yeye akiwa kama kamanda wao, inaelezwa kwamba siku ya kwanza au ya pili Fred alipigwa risasi ya kichwani na kufariki hapo hapo! Wanadai aliuwawa na risasi za adui lakini hiyo si kweli aliye muua na afisa mwenzake ambaye akupendelea approach ya Fred ya softly softly wanasema siyo kwamba Mh.Kagame hakujua kitakacho mtokea Fred eventually kwa kuwa muuaji alikuwa na kawaida ya kuwasiliana na Mh.Kagame akiwa masomoni Merikani sasa nani alitoa amri ya kumumaliza Fred haijulikani. One more thing Fred alikuwa very close na familia ya M7 kuanzia M7 mwenyewe na mkewe na mdogo wake M7 Mh. Col. Salim Saleh, kwa hiyo kifo cha Fred kiliwauzunisha sana. Mkewe M7 aliwahi kunusurika kifo wakati wa vita vya msituni kati ya jeshi la OBOTE na M7, mama huyo alikuwa intercepted kwenye kizuizi cha barabarani na majeshi ya OBOTE, ni Fred na makomando wenzake ndio walimuokoa mama huyo(Jannet). Inasemekana vile vile kwamba M7 alitumia ujanja wa kumpeleka PK kwenye mafunzo ya kijeshi huko Merikani ni (kama alilazimishwa vile) ili hasiwepo wakati vita ya kukomboa Rwanda i.e alipendelea Fred ndiye aongoze vita hiyo - kwa nini? That's a million dollar question, inaelekea M7 na PK don't trust each other by 100% personally namuonaga PK yuko straight forward he speaks his mind without mincing words 'am not sure about M7, miaka ya nyuma walihai kukorofishana walikaa muda mrefu bila ya kujuliana hali!! Kagame hana mchezo bwana.
 
Kibanga nadhani umetoka kwenye mstari kishabiki!

mtoa thread amejitahidi kugusa maeneo mengi iwapo unataarifa pia tuwekee tusome. Napingana na wewe kuwa Amini alivamia Tanzania kupiga watusi, huo ni uwongo nadhani unataka kuchafua mada sijui Kwa lengo gani. Ikumbukwe kua hata Obote alikuwa hapa Tanzania baada ya kupinduliwa na TAnzania iliendelea kumheshimu Kama head of state wa Uganda. Nadhani hilo ndilo lilimchukiza sana Idd Amin. Pia habari ya kagame na Museveni kuandaliwa na Nyerere Kwa makusudi ya kutawala Rwanda na Uganda ni uzushi wa wahutu hasa walioshiriki mauaji ya kimbali.

Mkuu umeongea ukweli tupu,

Tatizo ndugu wengi hapa wanazungumza kwa hisia zaidi badala yakuusaka ukweli
 
Ni kichekesho wanyarwanda wana mipango kabambe ya kuiba ardhi ya congo wakati bomu la vita ya ukabila linanunikia nchi kwao. Wa sikilize ushauri wa Rais. kikwete na waishi kwa amani. Maisha ya kunyanyasana kikabila,dini na vinginevyo yamepitwa na wakati.
 
MALCom umenena kweli hilo linawezekana. Ila history hutufundisha tutokako, bado tunahitaji elimu ya kutosha. Kweli mgogoro wa Congo umenifundisha sana historia ya nchi za maziwa makuu. Kumbe wahutu, watusi pia wako Tanzania, Uganda Burundi na Rwanda? Kweli?
 
Mkuu unajuwa watu wengine ufikilia wahusika lazima wawe kwenye tukio ndio wahusike na uharifu!! Ukweli wa mambo ni kwamba kulikuwa na tofauti kubwa ya approach au tuseme stratergy ya vita vya msituni kati ya Fred na Kagame, Fred ali-prefer softly softly approach i.e kuelimisha raia kwenye area iliyokombolewa na wapiganaji wa msituni kabla hawajasongo mbele kwenye area nyingine, the idea behind all this ni kwamba kwa kufanya hivyo watahungwa mkono na raia wa Rwanda bila ya kujali ukabila, Kagame na radical wenzake waliona approach ya Fred itawachelewesha sana! Wenyewe walikuwa wanataka approach ya voda fasta. Kati ya Fred na Kagame, Fred alikuwa na experience kwenye nyanja ya vita kuliko Kagame, Fred vile vile aliwahi kushiriki katika vita vya ukombozi wa Msumbiji kama mafunzo, Kagame taaluma yake ilikuwa ni upande wa Intelligency aliyo somea hapa Tanzania. Sasa nini kilitokea - Fred aliongozana na wanajeshi wenzake wa Kitutsi kutoka Uganda na kwenda mpakani mwa Rwanda na Uganda kuanzisha vita vya kumung'oa Rais Habyalimana madarakani yeye akiwa kama kamanda wao, inaelezwa kwamba siku ya kwanza au ya pili Fred alipigwa risasi ya kichwani na kufariki hapo hapo! Wanadai aliuwawa na risasi za adui lakini hiyo si kweli aliye muua na afisa mwenzake ambaye akupendelea approach ya Fred ya softly softly wanasema siyo kwamba Mh.Kagame hakujua kitakacho mtokea Fred eventually kwa kuwa muuaji alikuwa na kawaida ya kuwasiliana na Mh.Kagame akiwa masomoni Merikani sasa nani alitoa amri ya kumumaliza Fred haijulikani. One more thing Fred alikuwa very close na familia ya M7 kuanzia M7 mwenyewe na mkewe na mdogo wake M7 Mh. Col. Salim Saleh, kwa hiyo kifo cha Fred kiliwauzunisha sana. Mkewe M7 aliwahi kunusurika kifo wakati wa vita vya msituni kati ya jeshi la OBOTE na M7, mama huyo alikuwa intercepted kwenye kizuizi cha barabarani na majeshi ya OBOTE, ni Fred na makomando wenzake ndio walimuokoa mama huyo(Jannet). Inasemekana vile vile kwamba M7 alitumia ujanja wa kumpeleka PK kwenye mafunzo ya kijeshi huko Merikani ni (kama alilazimishwa vile) ili hasiwepo wakati vita ya kukomboa Rwanda i.e alipendelea Fred ndiye aongoze vita hiyo - kwa nini? That's a million dollar question, inaelekea M7 na PK don't trust each other by 100% personally namuonaga PK yuko straight forward he speaks his mind without mincing words 'am not sure about M7, miaka ya nyuma walihai kukorofishana walikaa muda mrefu bila ya kujuliana hali!! Kagame hana mchezo bwana.

Kuna mmoja wawadau amelieleza hapo kurasa za nyuma akisema Mwalimu Nyerere alimsaidia PK kuingia madarakani jambo ambalo sio kweli
 
king king Yericko Nyerere

acheni kulalamika huu ndio muda muafaka wa kujipanga na kuikomboa nchi yenu kutoka kwenye mikono ya dikteta huyu anayenuka damu.
 
Last edited by a moderator:
Ndo tatizo lenu wabongo,hapo ulipoishia ndipo ulipofeli kukomesha uovu,Yericko Nyerere nimwovu kwenye hili na amenishangaza sana hata mimi,ni wiki iliyopita sijui nilikuwa nasoma gazeti gani la kibongo linaelezea jinsi makamanda wa Paul Kagame walivyokimbia nchi na huyo mmoja ni mtusi anakiri wazi kwamba serikali ya Kagame ni ya kiuaji anaendelea kusema kuwa ameua wahutu wengi sana na kuwamaga mizoga yao kwa maelfu mtoni iliwe namba na akatoa pendekezo kuwa hata mifupa mingi iliyohifadhiwa kwenye jumba la makumbusho ya mauaji ya kimbari ni mabaki ya jamii zote mbili za kihutu na kitutsi na akapendekeza ufanywe hata uchunguzi wa vinasaba(DNA) kuthibitisha hayo madai yake.Sasa mtu kama Yericko anapofunguka kimbwigambwiga hapa na akiachiwa tu nyie mnaofahamu kwa kutomalizia mnachoahamu kinachoweza kuwa msaada wa kutufanya tusiendelee kupoteza muda hapa,kukaa kwenu kimya ni uangamivu wa muda wetu wa maana,wewe funguka tu kisha utuachie wadau tumuweke mahali pake panapomfaa.

jilaumuni nyie mnaotangatanga, wabongo ni imara! jipangeni huu ndiyo muda wa kuikomboa nchi yenu!
 
jilaumuni nyie mnaotangatanga, wabongo ni imara! jipangeni huu ndiyo muda wa kuikomboa nchi yenu!

Humu ndani kuna watu wanashabikia vita,tena wao risasi ikipigwa ndio watakua wa kwanza kutimua,majambazi yamawashinda eti mnataka vita ya kukomboa tanzania,tanzania imevamiwa nanani? nyie ndio mnaitwa wachochezi shauri yako,kesho usije sema nilikua natania tu,acha watanzania na wanyarwanda waishi kwa amani wapambane na adui umasikini na ujinga.
 
Humu ndani kuna watu wanashabikia vita,tena wao risasi ikipigwa ndio watakua wa kwanza kutimua,majambazi yamawashinda eti mnataka vita ya kukomboa tanzania,tanzania imevamiwa nanani? nyie ndio mnaitwa wachochezi shauri yako,kesho usije sema nilikua natania tu,acha watanzania na wanyarwanda waishi kwa amani wapambane na adui umasikini na ujinga.

mbona unaishi maisha ya kujishuku? Tanzania haijavamiwa bado tuna uwezo mkubwa sana wa kuwadhibiti hata mpaka wa kagera vita ikianza hamsogei, nilikuwanawahamasiha wahutu waache kulalamika wadai kwa nguvu haki yao ya kuishi kwa amani bila ubaguzi ndani ya rwanda .
 
acheni kulalamika huu ndio muda muafaka wa kujipanga na kuikomboa nchi yenu kutoka kwenye mikono ya dikteta huyu anayenuka damu.

[h=2]Xenophobia is what Rwandans in Tanzania are facing[/h]



Editor,

Following the second massive expulsion of Rwandans from Tanzania by the same government of Jakaya Mrisho Kikwete shows extreme “xenophobia” within the ‘Socialist State of Tanzinia’.

The late President Milton Obote in 1980-1982 expelled Rwandans who had lived in Uganda since 1940s, 50s, 60s and 70s but he died still regretting this inhumane act he did against Rwandans at that time.

This is the same tragedy Jakaya Kikwete is inflicting against Rwandans who even have their sons and daughters that have contributed to the economy of Tanzania. Kikwete’s acts are against African values of brotherhood, unity and cultural, family ties and lineage.

I pray that may God/Allah unfold xenophobia that has characterised Tanzania leaders to the extent that it has affected regional integration initiatives. We appreciate what the Rwandan Government is doing to receive and resettle those expelled by fellow Africans.

Bruce Ruhetamyambi, Kigali, Rwanda

Reaction to the story, “Govt reassures Tanzanians as Kikwete kicks out Rwandans”, (The New Times, August 9)





[h=2]Comments[/h]
Throughout his two decades exile, Obote was residing like a pauper in a squalid garage rented for him by the Zambian government while Mobutu who too expelled Rwandans was too expelled from Togo and later accommodated in Morocco where he died a miserable man after a long illness of prostate cancer.

comment-37f.png
01:22:40 Wednesday 14th, August 2013 London - Moses Wamba
Reply | Close​


I think most of the media in Rwanda are reporting FALSE INFORMATIONS about Tanzania. The government of Tanzania is expelling all illegal immigrants even Europeans

comment-37f.png
01:55:51 Wednesday 14th, August 2013 Arusha - Kelvin
Reply | Close​
Idiamini Dada expelled Indians he also faced the similar as he took refuge in SAUDI. Tanzanians remembers this. But, why Mwalimu Nyerere did not do this in the war against capitalism the Indians were safe by then.

comment-37f.png
08:54:52 Wednesday 14th, August 2013 Nairobi - Leonard Kiraga to Kelvin
Reply | Close​




Sigh! You guys are still on it. Our president will be very fine after retirement and both governments (TZ and Rwanda) have acknowledged this transaction is done. Let it go and leave with it.

comment-37f.png
09:24:20 Wednesday 14th, August 2013 dar - tz1
Reply | Close​


the expulsoins, support 4,fdlr and his military involvement in drc is part of kikwete,s and cohorts conspiracy against rwanda.

comment-37f.png
10:03:22 Wednesday 14th, August 2013 kampala - john nyabutsitsi
Reply | Close​


The media should serve as a voice of reason, not as a tool to flare up conflict between two neighbour countries. Rwanda and Tanzania will remain neighbors after all this hostility. And please note, personal attacks against any of our two presidents do not show any trace of civility to whoever is making them.

comment-37f.png
12:27:21 Wednesday 14th, August 2013 Belgium - Xaveri Rushema
Reply | Close​


I must stress this to you. Goma, Rutshuru and Masisi belongs to Congolese. You tutsis can only dream about your Volcan Republic.

comment-37f.png
12:53:47 Wednesday 14th, August 2013 London UK - Bohulu nkumu
Reply | Close​
With these kinds of statements against a section of his country's population, people like Bohulu nkumu (and the useful foreign ------ who support them) wonder why Kinyarwanda-speaking Congolese are up in arms.
When - it seems it is no longer if - the DRC eventually fragments into tribal-based entities, let's not wonder what brought it about. The cause is staring us right in the face in these kinds of black-and-white declarations. And anyone who claims that these kinds of sentiments - which invariably also reflect what is being done on the ground - still does not justify insurrections, I will say, rebellions have arisen in different places and at different times in history on much less provocation than this.
So if the likes of Bohulu nkumu is setting on bringing the DRC house down on the head of its diverse peoples, he is going about it in the best way possible. Go on friend, you will definitely reap what you are busy sowing.
 
Jeshi la Polisi Tanzania, Usalama wa
Taifa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi
Tanzania JWTZ pamoja na Viongozi
wote wa Mikoa husika hakikisheni
mnaendelea na msako wa
kuwaondoa Wahamiaji haramu wote
yaani wale wanaoishi bila Vibali. Pia
zichukuliwe hatua kali za kisheria
kwa wale wahamiaji haramu ambao
hawakutii ule muda muafaka
tuliowapa warudi kwao. Napenda
kuwahakikishia ya kuwa zoezi hili
halitaishia mkoani Kagera tu, bali
Tanzania nzima. Serikali yenu
inafahamu vema walipo hawa
wahamiaji haramu hususani kutoka
Rwanda. Ndugu Wananchi wa
Tanzania, Serikali yetu imepeleka
Batalioni nchini Congo ili kulinda
amani kukabiliana na kukabiliana na
waasi wanaojulikana kwa jina la m23
nchini humo.
Waasi hawa m23 wataondoka nchini
DRC muda si mrefu kwa kipigo kizito
watakachokipata kutoka kwa
majeshi ya UN yaliyopo DRC
yakiongozwa na Brigedia Jenerali
James Mwakibolwa. Wakishaondoka
Congo UTAPITA MSAKO WA HALI YA JUU
SANA ILI KUWAONDOA WARWANDA
NCHINI HUMO. Napenda
kuwahakikishia ya kwamba HAKUNA
NCHI YOYOTE INAYOWEZA IKATUTISHIA
AMANI WATANZANIA. Tunaliamini JWTZ
kwa kuwa lipo Imara sana, ndani na
nje ya Tanzania.
Ni mimi Mheshimiwa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kupitia JamiiForums. Mungu Ibariki
Afrika, Mungu Ibariki Tanzania.
Asanteni kwa Kunisikiliza.
 
Back
Top Bottom