IJUE SHERIA: Namna ya kumsaidia ndugu yako kupata dhamana Polisi

IJUE SHERIA: Namna ya kumsaidia ndugu yako kupata dhamana Polisi

Asante, umesema dhamana hutolewa bure

maswali:-

1) Kama mtu hana kazi na hana watu wakumdhamini, umesema anaweza kujidhamini mwenyewe, vitu gani itabidi avitoe ili aruhusiwe kujidhamini?
2) Kama mtu alipewa dhamana akakimbia, (kosa lilikuwa dogo kama labda kutukunana), akikamatwa bado anaweza kupewa dhamana ya pili?
3) Unayo List ya makosa watu wanaweza kupewa dhamana na makosa ambayo watu hawawezi kupewa dhamana? iyo itawasaidia watu,
4. Unaweza kuonyesha kuweka website ya government na vifungu vinavyo onyesha rights za mtu aliyekamatwa?

Jiongeze mtoto wa kiume usipende kutafuniwa kila kitu.....na hili ndio tatizo letu vijana sisi siku hizi hatutaki kusumbua akili zetu kabisa jamaa amekupa elimu kiasi basi nawe sumbua akili basi hata kidogo. TAFUTA KATIBA YA TANZANIA SOMA
 
Jiongeze mtoto wa kiume usipende kutafuniwa kila kitu.....na hili ndio tatizo letu vijana sisi siku hizi hatutaki kusumbua akili zetu kabisa jamaa amekupa elimu kiasi basi nawe sumbua akili basi hata kidogo. TAFUTA KATIBA YA TANZANIA SOMA

Siyo kwa ajiri yangu, ni kwa ajiri ya kuwasaidia wengine hambao hawajui watapata hayo maelezo wapi. Yani itakuwa vizuri kama hapa kutakuwa na maelezo yote (one stop shop) kuwa mambo ya dhamana (different scenarios).

Mtu anaweza kukamatwa halafu hana muda mwingi wa kutafuta information about his right, labda yuko ndani (Jela). Na labda anapewa dakika kumi tu kutumia simu yake. Sasa kama anaweza kuja hapa na akapata kitu kitakachomsaidia ni vizuri, au wewe unaonaje? Hii ndiyo maana ya majadiliano kusaidiana.

Unajua ukiwa unataka dhamana hauwezi tu kumwambia polisi sheria ina sema ni haki yangu na kupata dhamana.

Inabidi ujue kipengele kinachokupa dhamana, hata akiende kukisoma anaona uko kweli. Inabidi useme kutokana na katiba, section.., paragraph ..., kifungu namba..., sheria ya mwaka... inanipa haki ya kupata dhamana. Kwahiyo naomba dhamana kutokana na hiyo kipengele cha katiba ya Tanzania. Watajua unajua kitu gani unachosema na unajua sheria na umesoma katiba.

Mkuu, Mwache Mkuu aliyeanzisha uzi ajibu au mtu mwingine. Calm down a little bit life is too short.
 
DHAMANA NI NINI?

Dhamana ni hatua ambayo mtuhumiwa wa kosa fulani huachiwa huru kwa muda, ili kusubiri hatua za kufikishwa mahakamani, au kama tayari amefikishwa mahakamani husubiri kuendelea na kesi kwa siku zijazo.

Kwa hiyo, ili lije suala la dhamana ni lazima uwe umetuhumiwa polisi au tayari umefikishwa mahakamani. Ieleweke kuwa kuna aina kuu mbili za dhamana. Kwanza dhamana ya polisi na pili dhamana ya mahakamani. Hapa tunazungumzia dhamana ya polisi.

UKIOMBWA FEDHA KWA AJILI YA DHAMANA KATAA

Dhamana hutolewa bure. Ieleweke wazi kuwa hakuna malipo yoyote yanayotakiwa kutolewa ili mtuhumiwa au mshtakiwa akubaliwe dhamana. Mchezo huu wa kuomba fedha ili mtu apate dhamana umetamalaki zaidi vituo vya polisi.

Wewe kama raia, unalotakiwa kujua ni moja tu kuwa hakuna sheria inayomtaka raia kutoa fedha ili apate dhamana. Serikalini hakuna risiti ya malipo ya dhamana. Kama wewe utaamua kutoa fedha hiyo ujue umetoa kwa sababu zako lakini sheria iko hivyo. Ifikie hatua raia wajisimamie kwa kukataa kutoa fedha kununua dhamana.

Hakuna kitu ambacho askari anaweza kukufanya ikiwa utakataa kutoa fedha kwa ajili ya dhamana. Hakipo kabisa kinachohitajika ni ujasiri wako tu kwa kumwambia askari kwamba ‘sikupi fedha kwa kuwa dhamana hainunuliwi.

Usikubali kutoa fedha kwa ajili ya dhamana, ni kosa na fedha hizo ni rushwa. Na hiyo ni kwa dhamana zote — ya polisi pia ya mahakamani. Katika taratibu za kupata dhamana hamna kulipa fedha.

POLISI WANALAZIMIKA KUKUPA DHAMANA

Hapo juu nimesema kuwa ili upate dhamana hutakiwi kutoa chochote kitu isipokuwa kuna mambo yanazingatiwa ili upate dhamana.

Baadhi ya mambo hayo ni haya;

(a) Kisheria ikiwa makazi yako au anuani yako ya makazi inajulikana vyema au haijulikani, lakini umewafanya polisi kuijua na wakajiridhisha kwamba kweli fulani haya ndiyo makazi yake, basi ni sababu ya kupatiwa dhamana. Hii ni kwa sababu lengo kuu la dhamana ni ili utakapohitajika upatikane kwa urahisi.

(b) Ikiwa kosa alilotenda mtu ni la kudhaminika, hakuna haja ya kuendelea kumshikilia. Sheria imeshaweka wazi makosa yapi dhamana ya mtu itolewe na makosa yapi isitolewe. Baadhi ya makosa ambayo mtu hatakiwi kupata dhamana ni kama kuua kwa kukusudia (murder), uhaini (treason), wizi wa kutumia silaha na kadhalika.

Ajabu ni kuwa kwenye vituo vyetu vya polisi unakuta hata mwenye kosa la kutukana naye ananyimwa dhamana. Hii ni kinyume cha sheria na muda umefika wa raia wenyewe kuyakataa haya.

(c) Pia kama mtuhumiwa hana kumbukumbu (criminal records) zozote za uhalifu, nayo ni sababu au kigezo cha kumfanya apewe dhamana haraka. Hakuna sababu ya kuendelea kumshikilia mtu ambaye kwa kumbukumbu hakuwahi kutenda kosa lolote la jinai hapo kabla. Kisheria kutokuwa na kumbukumbu za uhalifu hapo awali ni dalili za uaminifu na ukweli. Hii nayo ni sababu ya kisheria na yafaa izingatiwe sana huko vituo vya polisi.

(d) Pia ikiwa polisi itajiridhisha kwamba mtuhumiwa atatimiza masharti ya dhamana atakayopewa kama kufika siku na saa atakayoamriwa, basi hakuna haja ya kumng’ang’ania. Hii nayo ni kati ya sababu za kisheria ambazo huwa hazipewi nafasi kwenye vituo vya polisi na hivyo kuendelea kulifanya suala la dhamana kuwa gumu.

NAMNA YA KUJIANDAA NA DHAMANA

Ni vema sana unapopata taarifa za ndugu yako kushikiliwa kituo cha polisi kujiandaa na dhamana. Usitoke nyumbani kwenda kituoni bila kujiandaa na dhamana. Na hii ni iwe una uhakika amefanya kosa fulani au huna uhakika. Zaidi kama unajua kosa lake ni la kudhaminika basi umuhimu wa kujiandaa na dhamana huongezeka.

La kuzingatia sana; hakikisha unapotoka nyumbani una barua inayokutambulisha kwa suala la dhamana kutoka Serikali za Mitaa. Ukienda Serikali za Mitaa wanazijua hizi barua. Pia kama ni mwajiriwa usisahau kwenda na kitambulisho chako cha kazi.

Hii husaidia kutopoteza muda kwa kurudishwarudishwa huku ndugu yako akiendelea kusota polisi. Kwa kujiandaa utamwokoa ndugu yako na zahma ya kulala au kukaa selo. Usiende polisi ukiwa hujajiandaa kwa kuwa kufanya hivyo ni kupoteza muda tu.

OMBA KUJIDHAMINI MWENYEWE, INARUHUSIWA

Kuna watu wamekuwa wakikosa dhamana kwa kukosa wadhamini. Lakini polisi wamekuwa hawawaelezi watu hawa haki hii ya kujidhamini wenyewe. Mtu akikosa mdhamini na polisi nao wanakaa kimya mtu anaendelea kusota. Hili si sawa kwa kuwa moja ya majukumu waliyonayo polisi ni kuwaelimisha watuhumiwa haki zao za msingi.

Aidha, kama ulikuwa hujui ndiyo ujue kuanzia leo kuwa inaruhusiwa kujidhamini mwenyewe na ukaondoka kituo cha polisi bila kuhitaji ndugu yeyote kukudhamini.

Unachotakiwa kufanya kama uko mikononi mwa polisi ni kusema tu kwamba ‘nahitaji kujidhamini’ ili upewe fomu maalum uijaze na uondoke. Usisahau kuliomba hili ni haki yako.
Samahani mkuu mie imenikuta tatizo la kukosa dhamana kwa mdogo wangu anayeshitakiwa kwa kumpa ujauzito.mwanagunzi japo sina uhakika kama kweli aliempa ni huyu mdogo wangu,,,, ajabu nilifuata taratibu zote za kupata dhamana kutoka serikali ya kijiji kuanzia kwa mwenyekiti wangu wa kitongoji.mpaka ofisi ya mtendaji kijiji na kata na nikapewa nakala za utambulisho,

Ajabu kufika mahakamani hakimu baada ya kumsomea mashitaka yake mdogo wangu na kusema dhamana iko wazi akaomba watu wawili wa kumdhamini nikatoka mie na ndugu yangu kila mmoja na vielelezo husika tatzo likaja hakimu kutotambua udhibitisho wetu akidai tuwasilishe hati za mali isiyohamishika kama nyumba au kiwanja wakati vielelexo vyote kutoka kwa afsa mtendaji vikieleza bayana maana kama hati sehemu ninapoishi hakuna hati wala ofa. Ningependa kujua hii ni sawa kweli mkuu maana baada ya kutoa pesa kiasi cha laki tano dhamana ilikubaliwa hapo ndipo nilibaki na mshangao..

Na ningependa kujua kosa.la watoto kupeana ujauxito.linadhaminika au la maana mdogo wangu ana miaka kumi na sita lakini kahitimu kidato cha nne.mwaka jana na kubahatika kuendelea na masomo lakini aliyepewa mimba.ana umri wa.miaka kumi na nane hivyo ningependa kujua aliyebakwa ni yupi kati ya hawa watoto'

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samahani mkuu mie imenikuta tatizo la kukosa dhamana kwa mdogo wangu anayeshitakiwa kwa kumpa ujauzito.mwanagunzi japo sina uhakika kama kweli aliempa ni huyu mdogo wangu,,,, ajabu nilifuata taratibu zote za kupata dhamana kutoka serikali ya kijiji kuanzia kwa mwenyekiti wangu wa kitongoji.mpaka ofisi ya mtendaji kijiji na kata na nikapewa nakala za utambulisho,

Ajabu kufika mahakamani hakimu baada ya kumsomea mashitaka yake mdogo wangu na kusema dhamana iko wazi akaomba watu wawili wa kumdhamini nikatoka mie na ndugu yangu kila mmoja na vielelezo husika tatzo likaja hakimu kutotambua udhibitisho wetu akidai tuwasilishe hati za mali isiyohamishika kama nyumba au kiwanja wakati vielelexo vyote kutoka kwa afsa mtendaji vikieleza bayana maana kama hati sehemu ninapoishi hakuna hati wala ofa. Ningependa kujua hii ni sawa kweli mkuu maana baada ya kutoa pesa kiasi cha laki tano dhamana ilikubaliwa hapo ndipo nilibaki na mshangao..

Na ningependa kujua kosa.la watoto kupeana ujauxito.linadhaminika au la maana mdogo wangu ana miaka kumi na sita lakini kahitimu kidato cha nne.mwaka jana na kubahatika kuendelea na masomo lakini aliyepewa mimba.ana umri wa.miaka kumi na nane hivyo ningependa kujua aliyebakwa ni yupi kati ya hawa watoto'

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu pole na maswahibj ya dogo ila dogo mbaya kamtia mimba mtu anayemzidi umri.
 
Hivi polisi akikunyima dhamana kwa makusudi unaweza kuwafungulia kesi na wao kwa kosa hilo la kukunyima dahamana?? Maana mtu anaweza kuonga polisi ilimladi ulale ndani tuuuu..
 
DHAMANA NI NINI?

Dhamana ni hatua ambayo mtuhumiwa wa kosa fulani huachiwa huru kwa muda, ili kusubiri hatua za kufikishwa mahakamani, au kama tayari amefikishwa mahakamani husubiri kuendelea na kesi kwa siku zijazo.

Kwa hiyo, ili lije suala la dhamana ni lazima uwe umetuhumiwa polisi au tayari umefikishwa mahakamani. Ieleweke kuwa kuna aina kuu mbili za dhamana. Kwanza dhamana ya polisi na pili dhamana ya mahakamani. Hapa tunazungumzia dhamana ya polisi.

UKIOMBWA FEDHA KWA AJILI YA DHAMANA KATAA

Dhamana hutolewa bure. Ieleweke wazi kuwa hakuna malipo yoyote yanayotakiwa kutolewa ili mtuhumiwa au mshtakiwa akubaliwe dhamana. Mchezo huu wa kuomba fedha ili mtu apate dhamana umetamalaki zaidi vituo vya polisi.

Wewe kama raia, unalotakiwa kujua ni moja tu kuwa hakuna sheria inayomtaka raia kutoa fedha ili apate dhamana. Serikalini hakuna risiti ya malipo ya dhamana. Kama wewe utaamua kutoa fedha hiyo ujue umetoa kwa sababu zako lakini sheria iko hivyo. Ifikie hatua raia wajisimamie kwa kukataa kutoa fedha kununua dhamana.

Hakuna kitu ambacho askari anaweza kukufanya ikiwa utakataa kutoa fedha kwa ajili ya dhamana. Hakipo kabisa kinachohitajika ni ujasiri wako tu kwa kumwambia askari kwamba ‘sikupi fedha kwa kuwa dhamana hainunuliwi.

Usikubali kutoa fedha kwa ajili ya dhamana, ni kosa na fedha hizo ni rushwa. Na hiyo ni kwa dhamana zote — ya polisi pia ya mahakamani. Katika taratibu za kupata dhamana hamna kulipa fedha.

POLISI WANALAZIMIKA KUKUPA DHAMANA

Hapo juu nimesema kuwa ili upate dhamana hutakiwi kutoa chochote kitu isipokuwa kuna mambo yanazingatiwa ili upate dhamana.

Baadhi ya mambo hayo ni haya;

(a) Kisheria ikiwa makazi yako au anuani yako ya makazi inajulikana vyema au haijulikani, lakini umewafanya polisi kuijua na wakajiridhisha kwamba kweli fulani haya ndiyo makazi yake, basi ni sababu ya kupatiwa dhamana. Hii ni kwa sababu lengo kuu la dhamana ni ili utakapohitajika upatikane kwa urahisi.

(b) Ikiwa kosa alilotenda mtu ni la kudhaminika, hakuna haja ya kuendelea kumshikilia. Sheria imeshaweka wazi makosa yapi dhamana ya mtu itolewe na makosa yapi isitolewe. Baadhi ya makosa ambayo mtu hatakiwi kupata dhamana ni kama kuua kwa kukusudia (murder), uhaini (treason), wizi wa kutumia silaha na kadhalika.

Ajabu ni kuwa kwenye vituo vyetu vya polisi unakuta hata mwenye kosa la kutukana naye ananyimwa dhamana. Hii ni kinyume cha sheria na muda umefika wa raia wenyewe kuyakataa haya.

(c) Pia kama mtuhumiwa hana kumbukumbu (criminal records) zozote za uhalifu, nayo ni sababu au kigezo cha kumfanya apewe dhamana haraka. Hakuna sababu ya kuendelea kumshikilia mtu ambaye kwa kumbukumbu hakuwahi kutenda kosa lolote la jinai hapo kabla. Kisheria kutokuwa na kumbukumbu za uhalifu hapo awali ni dalili za uaminifu na ukweli. Hii nayo ni sababu ya kisheria na yafaa izingatiwe sana huko vituo vya polisi.

(d) Pia ikiwa polisi itajiridhisha kwamba mtuhumiwa atatimiza masharti ya dhamana atakayopewa kama kufika siku na saa atakayoamriwa, basi hakuna haja ya kumng’ang’ania. Hii nayo ni kati ya sababu za kisheria ambazo huwa hazipewi nafasi kwenye vituo vya polisi na hivyo kuendelea kulifanya suala la dhamana kuwa gumu.

NAMNA YA KUJIANDAA NA DHAMANA

Ni vema sana unapopata taarifa za ndugu yako kushikiliwa kituo cha polisi kujiandaa na dhamana. Usitoke nyumbani kwenda kituoni bila kujiandaa na dhamana. Na hii ni iwe una uhakika amefanya kosa fulani au huna uhakika. Zaidi kama unajua kosa lake ni la kudhaminika basi umuhimu wa kujiandaa na dhamana huongezeka.

La kuzingatia sana; hakikisha unapotoka nyumbani una barua inayokutambulisha kwa suala la dhamana kutoka Serikali za Mitaa. Ukienda Serikali za Mitaa wanazijua hizi barua. Pia kama ni mwajiriwa usisahau kwenda na kitambulisho chako cha kazi.

Hii husaidia kutopoteza muda kwa kurudishwarudishwa huku ndugu yako akiendelea kusota polisi. Kwa kujiandaa utamwokoa ndugu yako na zahma ya kulala au kukaa selo. Usiende polisi ukiwa hujajiandaa kwa kuwa kufanya hivyo ni kupoteza muda tu.

OMBA KUJIDHAMINI MWENYEWE, INARUHUSIWA

Kuna watu wamekuwa wakikosa dhamana kwa kukosa wadhamini. Lakini polisi wamekuwa hawawaelezi watu hawa haki hii ya kujidhamini wenyewe. Mtu akikosa mdhamini na polisi nao wanakaa kimya mtu anaendelea kusota. Hili si sawa kwa kuwa moja ya majukumu waliyonayo polisi ni kuwaelimisha watuhumiwa haki zao za msingi.

Aidha, kama ulikuwa hujui ndiyo ujue kuanzia leo kuwa inaruhusiwa kujidhamini mwenyewe na ukaondoka kituo cha polisi bila kuhitaji ndugu yeyote kukudhamini.

Unachotakiwa kufanya kama uko mikononi mwa polisi ni kusema tu kwamba ‘nahitaji kujidhamini’ ili upewe fomu maalum uijaze na uondoke. Usisahau kuliomba hili ni haki yako.
Shukrani kwa elimu mkuu,,umefanya vema sana....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dhamana ni haki ya msingi ya mtuhumiwa na siyo hatua Mkuu.
Nafahamu hilo mdau ila katika kuhakikisha unapata haki yako ya misingi lazma kuna hatua unazofuata . hivyo kama ilivyo katika damana , ili uweze kumwekea mtu dhamana kuna masharti na hatua lazma uzikamilishe ndipo upate haki yako
Mkuu namwomba Mwenyezi Mungu akubariki sana Wewe pamoja na Familia yako nzima bila kusahau hadi Wazazi wako wote kwani Wamezaa Mtoto mwenye roho nzuri, mwenye upendo kwa kila Mtu na huruma pia. Binafsi naomba nikuambie tu kuwa umenipa Elimu kubwa na yenye thamani sana Kwangu ambayo naamini sitoitumia Mimi tu peke yangu bali Vizazi na Vizazi.

Naomba mafuriko ya baraka na neema kutoka Mbinguni kwa Mwenyezi Mungu yote yakufikie Wewe. Nina uhakika kabisa kwamba hii Elimu uliyotupa hapa kuna Watu wengine ama wangetulipisha au wangetulazimisha twende katika Mitandao yao ili tukipate hiki ambacho Mpendwa wetu Wewe Member wa JF umetuwekea hapa bure kabisa.

Akhsante sana Mkuu.
nashukuru sana mkuu
Asante, umesema dhamana hutolewa bure

maswali:-

1) Kama mtu hana kazi na hana watu wakumdhamini, umesema anaweza kujidhamini mwenyewe, vitu gani itabidi avitoe ili aruhusiwe kujidhamini?
2) Kama mtu alipewa dhamana akakimbia, (kosa lilikuwa dogo kama labda kutukunana), akikamatwa bado anaweza kupewa dhamana ya pili?
3) Unayo List ya makosa watu wanaweza kupewa dhamana na makosa ambayo watu hawawezi kupewa dhamana? iyo itawasaidia watu,
4. Unaweza kuonyesha kuweka website ya government na vifungu vinavyo onyesha rights za mtu aliyekamatwa?
soma hyo attachment niliyokutumia hapo utaweza kupata A B C ya vifungu vinavyoonyesha haki za mtu aliyetiwa nguvuni , pia kitakuonyesha makosa gani mtu atapatiwa dhamana na yapi hawezi patiwa dhamana na ni kwa nini . mfano makosa ya uhujumu uchumi na mauaji kwa kukusudia huwezi patiwa dhamana
 

Attachments

Yani ukijua sheria ni raha sana..
Ngoja nianze kusoma OUT...
Maana sasa ukisema utafute mwanasheria ujue lazima uwe na ela ndeefu...

Kujua sheria ni kama kujua lugha...huwezi pata shida mjini...
Asante kwa darasa la bure kaka!
 
soma hyo attachment niliyokutumia hapo utaweza kupata A B C ya vifungu vinavyoonyesha haki za mtu aliyetiwa nguvuni , pia kitakuonyesha makosa gani mtu atapatiwa dhamana na yapi hawezi patiwa dhamana na ni kwa nini . mfano makosa ya uhujumu uchumi na mauaji kwa kukusudia huwezi patiwa dhamana

nzuri, thanks.
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia kwa dhamana mbunge wa Singida Mashariki Mhe.Tundu Lissu, kinyume na maombi yaliyowekwa na mawakili wa Jamhuri ya kuzuia asipewe dhamana.

Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Wilbard Mashauri amesema, baada ya kupitia hoja za serikali na majibu ya mawakili wa utetezi, haoni mantiki ya kuzuia dhamana kwa Lissu. Hivyo mahakama hiyo imemuachia Lissu kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya Sh.10 milioni, kila mmoja.!
 
DHAMANA NI NINI?

Dhamana ni hatua ambayo mtuhumiwa wa kosa fulani huachiwa huru kwa muda, ili kusubiri hatua za kufikishwa mahakamani, au kama tayari amefikishwa mahakamani husubiri kuendelea na kesi kwa siku zijazo.

Kwa hiyo, ili lije suala la dhamana ni lazima uwe umetuhumiwa polisi au tayari umefikishwa mahakamani. Ieleweke kuwa kuna aina kuu mbili za dhamana. Kwanza dhamana ya polisi na pili dhamana ya mahakamani. Hapa tunazungumzia dhamana ya polisi.

UKIOMBWA FEDHA KWA AJILI YA DHAMANA KATAA

Dhamana hutolewa bure. Ieleweke wazi kuwa hakuna malipo yoyote yanayotakiwa kutolewa ili mtuhumiwa au mshtakiwa akubaliwe dhamana. Mchezo huu wa kuomba fedha ili mtu apate dhamana umetamalaki zaidi vituo vya polisi.

Wewe kama raia, unalotakiwa kujua ni moja tu kuwa hakuna sheria inayomtaka raia kutoa fedha ili apate dhamana. Serikalini hakuna risiti ya malipo ya dhamana. Kama wewe utaamua kutoa fedha hiyo ujue umetoa kwa sababu zako lakini sheria iko hivyo. Ifikie hatua raia wajisimamie kwa kukataa kutoa fedha kununua dhamana.

Hakuna kitu ambacho askari anaweza kukufanya ikiwa utakataa kutoa fedha kwa ajili ya dhamana. Hakipo kabisa kinachohitajika ni ujasiri wako tu kwa kumwambia askari kwamba ‘sikupi fedha kwa kuwa dhamana hainunuliwi.

Usikubali kutoa fedha kwa ajili ya dhamana, ni kosa na fedha hizo ni rushwa. Na hiyo ni kwa dhamana zote — ya polisi pia ya mahakamani. Katika taratibu za kupata dhamana hamna kulipa fedha.

POLISI WANALAZIMIKA KUKUPA DHAMANA

Hapo juu nimesema kuwa ili upate dhamana hutakiwi kutoa chochote kitu isipokuwa kuna mambo yanazingatiwa ili upate dhamana.

Baadhi ya mambo hayo ni haya;

(a) Kisheria ikiwa makazi yako au anuani yako ya makazi inajulikana vyema au haijulikani, lakini umewafanya polisi kuijua na wakajiridhisha kwamba kweli fulani haya ndiyo makazi yake, basi ni sababu ya kupatiwa dhamana. Hii ni kwa sababu lengo kuu la dhamana ni ili utakapohitajika upatikane kwa urahisi.

(b) Ikiwa kosa alilotenda mtu ni la kudhaminika, hakuna haja ya kuendelea kumshikilia. Sheria imeshaweka wazi makosa yapi dhamana ya mtu itolewe na makosa yapi isitolewe. Baadhi ya makosa ambayo mtu hatakiwi kupata dhamana ni kama kuua kwa kukusudia (murder), uhaini (treason), wizi wa kutumia silaha na kadhalika.

Ajabu ni kuwa kwenye vituo vyetu vya polisi unakuta hata mwenye kosa la kutukana naye ananyimwa dhamana. Hii ni kinyume cha sheria na muda umefika wa raia wenyewe kuyakataa haya.

(c) Pia kama mtuhumiwa hana kumbukumbu (criminal records) zozote za uhalifu, nayo ni sababu au kigezo cha kumfanya apewe dhamana haraka. Hakuna sababu ya kuendelea kumshikilia mtu ambaye kwa kumbukumbu hakuwahi kutenda kosa lolote la jinai hapo kabla. Kisheria kutokuwa na kumbukumbu za uhalifu hapo awali ni dalili za uaminifu na ukweli. Hii nayo ni sababu ya kisheria na yafaa izingatiwe sana huko vituo vya polisi.

(d) Pia ikiwa polisi itajiridhisha kwamba mtuhumiwa atatimiza masharti ya dhamana atakayopewa kama kufika siku na saa atakayoamriwa, basi hakuna haja ya kumng’ang’ania. Hii nayo ni kati ya sababu za kisheria ambazo huwa hazipewi nafasi kwenye vituo vya polisi na hivyo kuendelea kulifanya suala la dhamana kuwa gumu.

NAMNA YA KUJIANDAA NA DHAMANA

Ni vema sana unapopata taarifa za ndugu yako kushikiliwa kituo cha polisi kujiandaa na dhamana. Usitoke nyumbani kwenda kituoni bila kujiandaa na dhamana. Na hii ni iwe una uhakika amefanya kosa fulani au huna uhakika. Zaidi kama unajua kosa lake ni la kudhaminika basi umuhimu wa kujiandaa na dhamana huongezeka.

La kuzingatia sana; hakikisha unapotoka nyumbani una barua inayokutambulisha kwa suala la dhamana kutoka Serikali za Mitaa. Ukienda Serikali za Mitaa wanazijua hizi barua. Pia kama ni mwajiriwa usisahau kwenda na kitambulisho chako cha kazi.

Hii husaidia kutopoteza muda kwa kurudishwarudishwa huku ndugu yako akiendelea kusota polisi. Kwa kujiandaa utamwokoa ndugu yako na zahma ya kulala au kukaa selo. Usiende polisi ukiwa hujajiandaa kwa kuwa kufanya hivyo ni kupoteza muda tu.

OMBA KUJIDHAMINI MWENYEWE, INARUHUSIWA

Kuna watu wamekuwa wakikosa dhamana kwa kukosa wadhamini. Lakini polisi wamekuwa hawawaelezi watu hawa haki hii ya kujidhamini wenyewe. Mtu akikosa mdhamini na polisi nao wanakaa kimya mtu anaendelea kusota. Hili si sawa kwa kuwa moja ya majukumu waliyonayo polisi ni kuwaelimisha watuhumiwa haki zao za msingi.

Aidha, kama ulikuwa hujui ndiyo ujue kuanzia leo kuwa inaruhusiwa kujidhamini mwenyewe na ukaondoka kituo cha polisi bila kuhitaji ndugu yeyote kukudhamini.

Unachotakiwa kufanya kama uko mikononi mwa polisi ni kusema tu kwamba ‘nahitaji kujidhamini’ ili upewe fomu maalum uijaze na uondoke. Usisahau kuliomba hili ni haki yako.
mkuu somo zur,kwa maana hiyo kama nilivyosikia leo kua Tundu Lissu katoka kwa dhamana ya milioni 10 ,inamaana hayo ni maandishi tu ?na hakuna pesa iliyotolewa?
 
Back
Top Bottom