IJUE SHERIA: Namna ya kumsaidia ndugu yako kupata dhamana Polisi

tatizo la askari wetu ni kujifanya wanajua sana, ukienda pale ukajifanya unaelewa mambo kama hivi mwisho wa siku yule aliyepo ndani ndio ataumia. watakufanyia sifa kwa kukulaza ndani zaidi ya hata ungejifanya mpole na kama huyajui hayo mambo. asante sana mkuu kwa elimu uliyoitoa ila nikukumbushe tuu police hawatoi elimu hiyo maana ndipo wanapopatia zao za kusuuza makoo.
 
mkuu somo zur,kwa maana hiyo kama nilivyosikia leo kua Tundu Lissu katoka kwa dhamana ya milioni 10 ,inamaana hayo ni maandishi tu ?na hakuna pesa iliyotolewa?

Sio Maandishi tu, inabidi uonyeshe unauwezo wa kulipa hizo pesa, wanaweza kuangalia assets, bank accounts, salary, your job, your business.
 
Dhamana ni haki ya msingi ya mtuhumiwa na siyo hatua Mkuu.

Mbona amesema kuwa ni haki ya mtuhumiwa na makosa yasiyodhaminika? Na ameenda mbele zaidi kuonesha hatua za kufikia hiyo haki.
 
Hakumlazimisha mbali mambo yote anavyodai mzazi wa mtoto wa kike walikua wanakutana gesti kwa makubaliano.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sasa kama walikuwa wamekubaliana hiyo ni sheria nyingine inayowahusu minors ( watoto wakifanya mapenzi), Kumbaka ni sheria nyingine kabisa. shitaka lilikuwa lipi?

Kwa sababu kumpa mimba mtu siyo illegal. Kumpa mtoto mimba (miaka midogo zaidi ya 18 ni illegal) Kama wote wawili ni watoto na wamekubaliana kufanya mapenzi ni sheria nyingine kabisa? adhabu siyo kubwa sana.

Kwa hiyo tunatakiwa tujue exactly what was he charged for (what was on the charge sheet)?
 
Wamemfungulia shitaka la kubaka na kusabisha mimba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu binafsi nimelipenda darasa ila kitu kimoja sijajua bado kwahiyo ukisikia Fulani kapewa dhamana kwa sh kadhaa mahakamani maaana yake nini hiyo hela analipa ndo anapewa dhamna au ikitokea katoweka mdhamini hulipa hyo hela
 
Mkuu binafsi nimelipenda darasa ila kitu kimoja sijajua bado kwahiyo ukisikia Fulani kapewa dhamana kwa sh kadhaa mahakamani maaana yake nini hiyo hela analipa ndo anapewa dhamna au ikitokea katoweka mdhamini hulipa hyo hela

Ikitokea katoweka ndiyo unalipa. Lakini unabidi uwaonyeshe ushaidi kabisa unaweza kulipa hizo pesa kabla kumpa dhamana.
 
Wamemfungulia shitaka la kubaka na kusabisha mimba.

Sent using Jamii Forums mobile app

sasa kubaka ni shikata kubwa, adhabu ni kubwa zaidi ya kama wote ni watoto walikubariana adhabu yake ni kama warning. Sasa kama wewe unaweza kuchukua mawasiliano yao yote, kwenye phone calls, emails, whatapps, skype's, facebook, instagrams, twitter, text messages, letters, picha, mashahidi (majirani, wanafunzi, marafiki, ndugu) kusema kama walikubariana, waliwaona wanapendana, unaweza kushinda hii case .

Lakini unatakiwa kuwa na evidence (ushahidi) to prove your case. Pia kama unaweza kuongea na huyu Msichana kama akasema anampenda huyu kijana na akulazimishwa bali walikuwa wanapendana na walikubariana utashinda hiyo case.

Mkuu kama unaweza tafuta wakili mzuri akusaidie.
 
kama unawafahamu polisi utaelewa kwamba namna ya kumsaidia ndugu yako kupata dhamana ya polisi ni kwenda na hela mfukoni, kwa mahakamani hakuna hakimu asiyekula rushwa, hata akikuambia hali ni mwongo. hiyo ndiyo dunia ambayo mwenyezi Mungu alipoiumba alitarajia itakuwa na watoa haki, watu wakaamua kuwa hivyo. nimefanya mahakamani muda mrefu hadi leo nafanya mahakamani, hakuna sehemu wanakula rushwa kama polisi na mahakama. anayebisha anyooshe mkono.
 



naomba nikujibu kama ifuatavyoo kwa kufuata mtiririko wa maswali yako
1. kama mtu hana kazi na hana mdhamini anaweza kujidhamini kwa kuapewa fomu maalumu atakayosaini na kuijaza ,
2. kwanza napenda nikueleze kuwa kutukana mtu siyo kosa ndogo ni kosa kama makosa mengine tu ya jinai , kwa kuwa amemvunjia mtu utu wake kwa kumdhalilisha kwa kumtusi hivyo lazma sheria ifuate mkondo wake ,. endapo atapatiwa dhamana na kutoroka akitiwa nguvuni inawezekana kutpatiwa dhamana tena kwakuwa atakuwa ameonyesha utovu wa nidhamu kwa kutokamilisha mashart aliyopewa baada ya dhamana
3. makosa ambayo mtu hawezipewa dhamana ni kama Uhujumu uchumi , makosa ya ugaidi, mauaji n.k
4. pitia hapo utapata majibu ya swali la 4 https://tls.or.tz/publication/view/zijue-haki-za-raia-katika-mfumo-jinai2/
 
Dhamana ni Haki na Siyo Upendeleo

Kwa kuwa dhamana ni haki ya mtu, hivyo anapoomba hapaswi kukataliwa bila sababu za msingi. Mahakamani na wanaharakati wa haki za binadamu wamesisitiza mara nyingi kuwa dhamana ni haki ya mshitakiwa pale anapotimiza masharti yake; kumnyima dhamana bila sababu ya msing ni kumkosesha haki ya msingi ya kuwa huru kwa mujibu wa sheria ( Ibara ya 13 kifungu kile cha 1 cha katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kinasema kwamba “ watu wote ni sawa mbele ya sheria , na wanayo haki, bila ubaguzi wowote, kulindwana kupata haki sawa mbele ya sheria”. Vile vile polisi au mahakama inapokataa kutoa dhamana ni lazima kuwe na sababu nzito zenye kuridhisha kabla ya kufikia uamuzi huo.

Hapa Tanzania uzoefu umeonyesha kuwa ni kesi za mauaji, wizi wa kutumia silaha na uhaini tu ambazo kutokana na uzito wake mtuhumiwa hawezi kuwekewa dhamana ila kesi nyingine zote zilizobaki, mshitakiwa anayohaki ya kuwekewa dhamana, pindi akitimiza masharti ya dhamana na mahakama ikaridhika. Kwa msingi huu dhamana ni haki ya mshitakiwa na kupewa dhamana ni katika kutimiza haki hiyo ya msingi.

Mahakama inaweza kukataa kutoa dhamana iwapo itakuwa imeridhika kuwa kutolewa kwa dhamana kutaharibu maana nzima ya kesi hiyo kuwepo mahakamani, kutavuruga kesi hiyo, au mshitakiwa anaweza kupata madhara ikiwa ataruhusiwa kurudi kwa jamii. Hali hii ndiyo inayosababisha kesi za mauaji na uhaini kukataliwa dhamana kwani adhabu yake ni nzito (kifo) ambapo ni rahisi mshitakiwa kushawishika kutoroka
 
ASANTE MKUU KWA ELIMU HII,SWALI LANGU KAMA POLISI AKININYIMA AU AKINISUMBUA AU AKIWEKA MAZINGINGIRA YA RUSHWA ILI NIMDHAMINI AU NIJIDHAMINI MWENYEWE.NI HATUA GANI NIFANYE AU NI ILI HAKI YANGU HII ISIPOTEE BURE?
 
ASANTE MKUU KWA ELIMU HII,SWALI LANGU KAMA POLISI AKININYIMA AU AKINISUMBUA AU AKIWEKA MAZINGINGIRA YA RUSHWA ILI NIMDHAMINI AU NIJIDHAMINI MWENYEWE.NI HATUA GANI NIFANYE AU NI ILI HAKI YANGU HII ISIPOTEE BURE?
unaaswa kumripoti kwa mkuu wake wa kitu na kama mkuu wake wa kituo ukahisi au asipochukua hatua yoyote unaweza fikisha taarifa zako kwa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…