Ijumaa Kuu na katazo la kula nyama

Asante sana kwa mfano mwepesi mkuu.Shukria!
 
Kila nyumba ina sheria na hizo ni sheria za kanisa katoliki, kwan waislam mje mtuambie kwenye Quran ni aya ipi imekataza kuingia na viatu msikitini
Hata Yesu alivua viatu alipotaka kuswali.

Jianzie kufikiria hapo kwnz
 
Sasa unafuata maneno ya Mungu au utashi wa watu fulani?

Basi kwa maana hyo hata mfalme zumaradi ana hoja nzuri ya kuhubiri dini yake.
Unapingana na maandiko.Kuna sehemu kwenye injili,niliiona mwaka 1960 kabla ya Uhuru wa Tanganyika,kwamba kama yote aliyoyatenda na kuhubiri bwana Yesu yangeandikwa,vitabu vya dunia hii visingetosha.
 
Unapingana na maandiko.Kuna sehemu kwenye injili,niliiona mwaka 1960 kabla ya Uhuru wa Tanganyika,kwamba kama yote aliyoyatenda na kuhubiri bwana Yesu yangeandikwa,vitabu vya dunia hii visingetosha.
Kwahyo hata katazo halikuandikwa lakini alilitenda?


Hilo katazo la mwaka 1960 Leo halipo?
 
Ukisoma Bible kama kitini Cha Uraia lazima ule winga
 
Hii naona imekaa kihisia zaidi kuliko kiimani.Hisia ni suala la mtu binafsi,lakini Imani ni hakika ya mambo yaliyofanyika na Yale yatarajiwayo.
 
Tafsiri ya kitutusa hiyo!
Sio mimi niliyetunga hiyo tafsiri, imeandikwa kwenye biblia. Msalabani kwa Yesu ndio ushindi na ukombozi kamili wa mkristo yoyote. Wakristo wanapaswa kukumbuka kifo cha Yesu kristo pale msalabani kwa furaha, shangwe na ujasiri mkubwa.

Waefeso 1: 7 (Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi......)

Wagalatia 6:14 (Lakini mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu chochote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ...)
 
Kula nyama siyo alama ya furaha..inategemea a na mazingira...Kuna watu kunywa maziwa ni tendon la furaha...so sikubaliani na wewe
 
Hakuna andiko lo lote linalokataza kula nyama siku ya Ijumaa kuu! Huenda hayo ni mafundisho ya kirumi yaliyochomekwa kwenye mafundisho ya Kanisa.
Wakati wengine wanahuzunika kwa kifo cha Yesu msalabani,wengine ni furaha kwa sababu ni siku ambayo Mungu alimtoa Mwanae ili tusamehewe dhambi zetu hivyo kuokolewa na hukumu inayokuja juu ya kila mwanadamu ambaye hataki kutubu dhambi na kusamehewa.
 
Hatuna tena sababu ya kutafakari maovu yetu kwa kulinganisha na mateso aliyoyapata Yesu pale msalabani, tunapaswa moja kwa moja kumfuata Yesy kristo kwa furaha, shangwe na ujasiri mkubwa. Yesu alishashindana na kushinda kwa niaba yetu, sisi kusheherekee ushindi huo katika yeye tu.
 
Kuna jamii nyama ndio chakula chao cha siku zote cha kawaida kabisa na sio kitu cha kifahari, kwanini wajinyime chakula kisa ijumaa kuu?
 
Kufa kwa Yesu kristo msalabani ni jambo la furaha, shangwe na ushindi katika imani ya Kikristo maana ndio lilizaaa ukombozi, sasa kwanini watu wakae na huzuni, unyonge na kujinyima?

Wakristo kuleni vinono leo.
Kufa Leo Ijumaa Kuu ni Huzuni.... Kufufuka Jumapili ndio Furaha na Shangwe Mkuu!
 
Hii naona imekaa kihisia zaidi kuliko kiimani.Hisia ni suala la mtu binafsi,lakini Imani ni hakika ya mambo yaliyofanyika na Yale yatarajiwayo.
Aisee duh.
Hisia ni nini?
Imani ni nini?

Anyway pengine kuna jambo lako unalolitafuta hadi umeanzisha huu uzi.
 
Duh yani hapa nakula supu ya pumbu za kondoo na ndio naona huu uzi. Dadek
 
NANI AMEKUAMBIA USISHIKE, USIONJE WALA USIGUSE NYAMA LEO?

Waumini wa huko Kolosai nao walidanganywa kama wewe, wakafundishwa kwamba eti wasiguse, wasionje wala wasishike vyakula vya aina fulani, wakapewa mafundisho ya kusisitiza umuhimu pia wa kushika siku fulani na sikukuu fulani fulani zikakatazwa eti kwa sababu tarehe za sikukuu hizo hazikujulikana dhahiri. Mambo haya yalimchanganya sana Epafra, mwanzilishi na mchungaji wa kanisa la Kolosai. Alipotuma ujumbe kwa Paulo, Paulo baba yake wa kiroho akaliandikia kanisa ujumbe huu;

Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani, Msishike, msionje, msiguse; (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu? Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.
Kol 2:20‭-‬23 SUV

Sisi tuliokufa pamoja na Kristo, hatutaki tena mafundisho ya awali ya ulimwengu, yanayotuweka chini ya amri isiyohusiana na mpango wa Mungu wa wokovu. Kuna watu wanapenda sana dini za kukatazwa katazwa kila kitu, wanafikiri ndio utakatifu. Utakatifu sio kukatazwa kila kitu, bali ni kukatazwa yale tu yanayoharibu hekalu la Mungu, yaani mwili. Eti, usishike, usionje, usiguse! Ndio inasaidia msalaba kutenda kazi vizuri?

Ujumbe kwa Wakolosai unatufundisha kwamba hakuna kitu unachoweza kuongeza kwenye kifo cha Yesu Kristo ili kifanye kazi vizuri, yaani HUWEZI KUIBORESHA KAZI YA MSALABANI ETI ILI IWE BORA ZAIDI, NI BORA, INAJITOSHEKEZA. Yoh. 19:30

MAKANISA YANAYOFUNDISHA KWAMBA LEO WATU WASILE NYAMA YAMEJITUNGIA TU, HAKUNA MAAGIZO HAYO KWENYE BIBLIA. Makanisa yanayofundisha kuabudu malaika, kushika siku, na kutokusheherekea pasaka, YAMEJITUNGIA TU MAAGIZO HAYO. HAYO NI MAAGIZO YA WANADAMU, SIO MUNGU.

Mafundisho yasiyoweza kuzizuia tamaa za mwili hayafai katika kutunza wokovu na kumtukuza Kristo aliyeinuliwa juu sana aliye kichwa cha Kanisa. Sisi sio watu wa kawaida, maana tulihamishwa tayari, hatuwezi kujifunza mambo ya kule tulikohama, TULIHAMISHWA.

Naye alituokoa katika nguvu za giza, AKATUHAMISHA na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;
Kol 1:13‭-‬14 SUV

Oscar Wissa
Phm Mtoni Sabasaba
Dar Es Salaam, Tanzania
Facebook, Instagram & Twitter: evoscarmaulid
 
Kuna jamii nyama ndio chakula chao cha siku zote cha kawaida kabisa na sio kitu cha kifahari, kwanini wajinyime chakula kisa ijumaa kuu?
Hawajakatazwa hiyo 'jamii nyingine' wale tu as long as hawana imani na Kanisa Katoliki na mafundisho yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…