Ikifika Derby ya October, wazee wa Yanga watakuwa wamesogeza umri kwa miezi miwili

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Jana vijana wa Ultrasound waliwatoa ulimi kweli kweli vyura wakongwe bado kidogo watapike nyonga. Baada ya mechi tuliwaona kina Mzee Aucho viungo vyote havifanyi kazi hata kutembea kwenda vyumbani ilikuwa shida.

Tunaenda kuongeza chuma moja matata sana kusimama pale namba 9 akishare namba na Mukwala.

Derby ijayo mwezi wa 10 hawa chura wazee watakuwa tayari wamesogeza umri kwa miezi 2 na hapo kati watakuwa wameshagongwagongwa visigino na wahuni wa mikoani (ukiacha zile timu 7 zilizo chini ya GSM). Hapohapo vijana wa Ultrasound watakuwa wameshaanza kupata physics. Miezi miwili katika uzee ni kama miaka 2, kama hauniamini mimi muulize babako.

Ubaya Ubwela!
 
Mnasajili za paniki, hiyo itaendelea kupokea vipigo vya Yanga hadi maji iite mma.
 
Watu mna maneno sana. Umefanya nicheke sana ndugu yangu. Ngoja Oktoba ifike tuone.

Ova
 
Watu mna maneno sana. Umefanya nicheke sana ndugu yangu. Ngoja Oktoba ifike tuone.

Ova
Chekeni sana hadi mtakapopigwa mara ya nne mfululizo ndipo akili zitakapowakaa vizuri.

Mlisema 8/8 mmekula kimoja, sasa mmehamisha magoli mnangojea Oktoba.

Hiyo Oktoba mjue Pacome na Nzengeli bado wapo, tena mna bahati Ki jana hakuwa na mchezo mzuri.
 
Hata kama hao wakiwepo SAYVILLE amefafanua vizuri vile watakuwa baada ya miezi miwili. Ameelezea kwa sayansi ya ukuaji.

Ova
 
Mashabiki wa Aina hii ni hasara kubwa Kwa Simba.
 
Nguvu ya yanga haipo kwa wachezaji, nguvu ipo kwa viongozi na wanachama. Yanga kamati haina mtu maskini
Unamaanisha lile goli la max limefungwa na viongozi? Sheria iwekwe ili anaekuwepo kwenye jukwaa la michezo awe alishaucheza mpira na sio vijana upinde wanakuja kulinajisi hili jukwaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…