Ikiwa Mazishi ni Ibada, basi usiingilie ibada za wafu. Waache wafu wawazike wafu wenzao

Ikiwa Mazishi ni Ibada, basi usiingilie ibada za wafu. Waache wafu wawazike wafu wenzao

Mwl Makungu bado uko baridi ndugu yangu. Umeongea point sana. Ila sijui kwa nini nimekumbuka ndungu Mwl Deo yule Mwl wa Nyamagana aliyefunga. Alikuaga na maandiko fulani.

Sasa kijana naona baada ya siasa kukuvuruga umepata mvurugano wa idol.

Sent from my Pixel 3a XL using JamiiForums mobile app
 
Mfano wako wa Musa na Elia si sahihi na pia mfano wako wa Razaro na tajiri pia si sahihi.
 
Ukiangalia kwa umakini utaona Nimezungumzia wafu wa aina . Wafu ambao miili yao iliishazikwa na wafu ambao wako hai kimwili lkn wamekufa ktk utu wao rohoni /nafsini .
Ni Sawa na kusema Wana macho lakini hawaoni; Waacheni vipofu wapotezane njia wenyewe.

Wana masikio lakini hawasikii, waachane viziwi wapigiane kelele wao kwa wao.

Kwa maana hiyo watahubiriwa na kusikia lakini hawataamini, watonyeshwa hadi miujiza lakini hawatasadiki, hivyo basi waacheni wachague njia waliyoichagua kuuiendea. (Hawa wote wameamua kupotezana).

Ni sawa na kuzikana kwa wafu.
 
Ikiwa Mazishi ni Ibada , Basi Usiingilie Ibada za Wafu . Waache Wafu Wawazike Wafu Wenzao..
💫💫💫💫💫

©️Mwl. Makungu m.s
0743781910

Wana Heri wafu wafao katika Bwana. Naam asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa Matendo yao yafuatana nao ( ufunuo 14:13).

Maana wafu wote wanalo tumaini ya kuwa Siku moja watatafufuliwa . Lakini ni wafu wachache walio na uhakika wa wapi wataelekea baada ya kufufuliwa.

Ni utamaduni wetu wa kuziosha maiti na kuzisafisha na kuzivalisha suti au sanda . Lkn yote hayo ni maandalizi ya kuzifukia chini ya udongo.

Nenda kaizike maiti , lkn usiingilie ibada za wafu.
Huwa tunazika maiti, lkn hatuziki wafu. Wafu hawafi. Wafu wanaishi . Pengine hujanielewa Bado . Ni hivi , huwa tunazika miili ya wafu lkn hatuwaziki wafu. tunazika mwili lkn hatuziki nafsi . Nafsi haifi.

Umepata kusoma kisa cha Lazaro na tajiri ktk Biblia? Wote wawili walikuwa wafu . Miili yao iliishazikwa zamani duniani . Lakini wanaonekana wako mahali fulani tofauti wakiwa hai wanajadiliana . Mmoja anastarehe mwingine anataabika. Miili inakufa ,maiti zinazikwa , lakini Wafu wanaishi.

Ufunuo wa Yohana 6:9 " Na alipoifungua muhuri ya tano , nikaona chini ya madhabau roho zao waliochinjwa kwaajili ya neno la Mungu , na kwaajili ya ushuhuda waliokuwa nao. Wakalia kwa sauti kuu, wakisema , Ee Mola , Mtakatifu , Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu , Wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi ? Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu , nyeupe , wakaambiwa wastarehe Bado muda mchache , hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na Ndugu zao , watakaouawa vile vile Kama wao."

Ukisoma hapo juu unapata picha gani juu ya wafu ? Kuna Wafu wapo hai wanastarehe.

Unakumbuka Yesu alitokewa na Nani pale mlimani wakati akiomba? Alitokewa na wafu, nabii Musa na nabii Elia wakazungumza nae. Kwa lugha ya kiswahili sanifu Tunasema alitokewa na mizimu( yaani watu waliowahi kuishi katika hii dunia na baadae wakafa au wakaondoka ktk hii dunia) . Mzimu wa Musa na mzimu wa Elia . Wafu hawafi , wafu wanaishi. Inayokufa ni miili..

Yule Mwanamke mwenye pepo wa utambuzi ( mchawi/ mganga) anamwambia mfalme Sauli je! Ni Nani nitakayekupandishia? Naye akasema , Nipandishie Samweli ( nabii ambaye amekwishakufa na kuzikwa) . Yule mwanamke akampandisha Samwel kutoka ktk nchi ( ardhi/ kuzimu) . Nao nabii Samwel ( mzimu) na mfalme Sauli wakazungumza ..

Japo wanatheolojia wengine huwa wanasema kuwa Samwel aliyepandishwa toka kuzimu siyo Samwel . Ni pepo , jini au shetani lililojivika mwili wa Samweli. Lakini ukilisoma andiko hili ktk Biblia Hakuna mahali wala mstari wowote pameandikwa kukanusha kuwa yule alikuwa ni Samwel wa uongo, pepo , jini au shetani aliyezuka. Hili la Samwel wa uongo au wa ukweli siyo somo langu kwa leo . Leo nataka tu kukwambia kuwa * wafu wanaishi* .. Wanaishi katika dunia yao . Wanaishi katika ulimwengu wa roho. Wapo walio kuzimu na wapo waliokwisha tangulia peponi. Wanaishi maisha yao .

Kama wewe Bado mwili wako una uhai na uzima Basi usiingilie maisha ya wafu.

Lakini ktk Injili Yesu anakuja kutuonesha kitu cha tofauti kbs . Siyo tu kwamba Wafu wapo kuzimu na peponi tu , bali kuna wafu wapo duniani. Tupo nao tunaishi nao .

Yesu anamwambia mtu aliyemuomba akamzike baba yake, "waache wafu wawazike wafu wenzao" .

Huyu mtu anamuomba Yesu aende akauzike mwili wa baba yake , lkn Yesu anamwambia waache wafu wawazike wafu wenzao.
Hapa tunaona ya kuwa Kumbe Kuna Wafu wapo duniani ,wanatembea, wanaongea , wanakula , na pengine wanaongoza watu. Maana wafu waliokufa mwili wasingeweza kwenda kuuzika mwili wa mfu mwenzao .
Hii tafsiri yake ni kwamba , mwili huu wa mfu aliyetakiwa kwenda kuzikwa ulienda kuzikwa na watu wafu ambao hawajakufa mwili. Wamekufa rohoni na akilini. Nielewe vizuri hapa , hawajakufa roho Wala hawajakufa akili ,Bali wamekufa rohoni na akilini.
Miili yao ipo hai. Roho zao zipo hai . Akili zao zipo hai . Lkn Matendo yao ya mwili yanayoongozwa na roho na akili siyo Matendo yanayostahili kuwa ya mtu aliye hai rohoni ..
Wanahesabika kuwa wamekufa ktk ulimwengu wa roho..

Ikiwa mazishi ni ibada . Basi usiingilie ibada za wafu waache wafu wawazike wafu wenzao.

Kuna watu tupo nao tunaishi nso lkn waliishakufa tyr . Ni wafu . Matendo yao machafu , ya kinyama hayastahili kuwa ya Binadamu aliye hai.
Mtu akiishakufa amekufa . Ameondoka ktk ulimwengu huu .
Japo ni utamaduni, lkn Hata tukijitahidi kuuosha, kuusafisha, kuutakasa na kuuvalisha vizuri mwili wake, Haiondoi ukweli ya kuwa anakwenda kufukiwa na udongo chini ya ardhi.

Kwanini unahangaika kuwasafisha wafu ( sijasema maiti) . Unatumia gharama kubwa , muda wako na nguvu zako bure kuwasafisha wafu na unajua ya kuwa huwezi kubadilisha ukweli kuwa wanaenda kufukiwa na udongo chini ya ardhi!!??

Usiingilie ibada za wafu waache wafu wawazike wafu wenzao.

Wafu wanaelewana vizuri . Wanapata na muda Wanapiga story zao km Lazaro na tajiri. Wewe unaingilia story zao ambazo hazikuhusu. Unataka kumsafisha tajiri mfu . Mfu ni mfu tu . Haibadilishi ukweli hata Kama akitokea km mzimu wa Musa na Elia. Aliishakufa. Hayupo ktk dunia hii.

Ukihangaika kumsafisha mfu iwe ni bure au kwa gharama nawe unageuka kuwa mfu unayetembea . Wote mnakuwa wafu. Mmekufa kiroho na kiakili..

Je! Unaishi na mfu? Unafanya kazi na mfu? Unasoma na mfu ? Unaongozwa na mfu ? Unaongoza wafu?

Kuwa makini . Wafu wanaotembea wamekufa kiroho na kiakili . Ni wabaya wachafu kuliko wafu waliokufa kimwili .

Mungu JEHOVA wasamehe wafu wanaotembea maana hawajui walitendalo . Lkn wasaidie Sana wahangaikao kuwasafisha wafu maana hawajui kuwa wanageuka kuwa wafu wa kiakili . .

Ikiwa mazishi ni ibada Basi usiingilie ibada za wafu. Waache wafu wawazike wafu wenzao.

Makungu m.s
0743781910
23 April 2023
kwaiyo aliposema mshahara wa dhambi ni mauti ww unasema hapana alikosea kinachokufa n mwil.🤣😇🤣😇
 
Mnaowasha mishumaa makaburini,

Mnaofanya kumbukumbu ya mfu siku ya arobaini,

Mnaokula nyama msibani acheni,

Jueni kuwa mnafanya IBADA ya wafu.
Wanakula vyakula vya ki-agano,Ibada🙌🙌
 
Nyama msibani inafanyaje?kwani imefanyiwa tambiko lolote?
Vyakula vingi vya misibani,40,3...and the like vinakuwaga vimefanyiwa Ibada!
Sio wote ila %kubwa ...hasa upande wa pili!
Jitahidi sn usiwe mlaji wa hivyo vyakula
 
Baadhi/Wengi wasiookoka, ingawa Si wote,,wenye kushika Mila mbovu,katika misiba Hasa ktk arobaini, huchanganya na kipande Cha nyama ya mfu au maji au uchafu wa marehemu kimazingara sufuriani Ili mshiriki chakula kama IBADA na mfu.

Ni vizuri kutakasa chakula kabla ya kula, bt kuondoa sintofahamu Kwa tahadhari epuka kula nyama misibani.

Magonjwa mengi ya kuoza mwilini au kansa ni matokeo ya kula nyama au uchafu wa wafu.

Misibani Huwa ni Mahali spesho wachawi huwatafuta watu kupitia vyakula. Sababu katika msiba wenye watu 100 Kwa Mfano, uwe na HAKIKA hutakosa wachawi 20 au zaidi.

Sorry kukwambia mambo ambayo yaeza kuwa beyond your expectation.
Hizo paragraph 2 za mwisho ndo ilivyo!
Na sijui kwann wachawi wanapenda sn kufanya vituko msibani!

Kumuongezea ,ma inategemea marehemu amekufaje, mfano km kafa Kwa mpango wa Mungu hakuna shida ila km ndo nguvu za Giza zimemuondoa uwe na uhakika roho za kichawi zitatawala msiba
 
Ni Sawa na kusema Wana macho lakini hawaoni; Waacheni vipofu wapotezane njia wenyewe.

Wana masikio lakini hawasikii, waachane viziwi wapigiane kelele wao kwa wao.

Kwa maana hiyo watahubiriwa na kusikia lakini hawataamini, watonyeshwa hadi miujiza lakini hawatasadiki, hivyo basi waacheni wachague njia waliyoichagua kuuiendea. (Hawa wote wameamua kupotezana).

Ni sawa na kuzikana kwa wafu.
Naaam
 
Ikiwa Mazishi ni Ibada , Basi Usiingilie Ibada za Wafu . Waache Wafu Wawazike Wafu Wenzao..
💫💫💫💫💫

©️Mwl. Makungu m.s
0743781910

Wana Heri wafu wafao katika Bwana. Naam asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa Matendo yao yafuatana nao ( ufunuo 14:13).

Maana wafu wote wanalo tumaini ya kuwa Siku moja watatafufuliwa . Lakini ni wafu wachache walio na uhakika wa wapi wataelekea baada ya kufufuliwa.

Ni utamaduni wetu wa kuziosha maiti na kuzisafisha na kuzivalisha suti au sanda . Lkn yote hayo ni maandalizi ya kuzifukia chini ya udongo.

Nenda kaizike maiti , lkn usiingilie ibada za wafu.
Huwa tunazika maiti, lkn hatuziki wafu. Wafu hawafi. Wafu wanaishi . Pengine hujanielewa Bado . Ni hivi , huwa tunazika miili ya wafu lkn hatuwaziki wafu. tunazika mwili lkn hatuziki nafsi . Nafsi haifi.

Umepata kusoma kisa cha Lazaro na tajiri ktk Biblia? Wote wawili walikuwa wafu . Miili yao iliishazikwa zamani duniani . Lakini wanaonekana wako mahali fulani tofauti wakiwa hai wanajadiliana . Mmoja anastarehe mwingine anataabika. Miili inakufa ,maiti zinazikwa , lakini Wafu wanaishi.

Ufunuo wa Yohana 6:9 " Na alipoifungua muhuri ya tano , nikaona chini ya madhabau roho zao waliochinjwa kwaajili ya neno la Mungu , na kwaajili ya ushuhuda waliokuwa nao. Wakalia kwa sauti kuu, wakisema , Ee Mola , Mtakatifu , Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu , Wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi ? Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu , nyeupe , wakaambiwa wastarehe Bado muda mchache , hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na Ndugu zao , watakaouawa vile vile Kama wao."

Ukisoma hapo juu unapata picha gani juu ya wafu ? Kuna Wafu wapo hai wanastarehe.

Unakumbuka Yesu alitokewa na Nani pale mlimani wakati akiomba? Alitokewa na wafu, nabii Musa na nabii Elia wakazungumza nae. Kwa lugha ya kiswahili sanifu Tunasema alitokewa na mizimu( yaani watu waliowahi kuishi katika hii dunia na baadae wakafa au wakaondoka ktk hii dunia) . Mzimu wa Musa na mzimu wa Elia . Wafu hawafi , wafu wanaishi. Inayokufa ni miili..

Yule Mwanamke mwenye pepo wa utambuzi ( mchawi/ mganga) anamwambia mfalme Sauli je! Ni Nani nitakayekupandishia? Naye akasema , Nipandishie Samweli ( nabii ambaye amekwishakufa na kuzikwa) . Yule mwanamke akampandisha Samwel kutoka ktk nchi ( ardhi/ kuzimu) . Nao nabii Samwel ( mzimu) na mfalme Sauli wakazungumza ..

Japo wanatheolojia wengine huwa wanasema kuwa Samwel aliyepandishwa toka kuzimu siyo Samwel . Ni pepo , jini au shetani lililojivika mwili wa Samweli. Lakini ukilisoma andiko hili ktk Biblia Hakuna mahali wala mstari wowote pameandikwa kukanusha kuwa yule alikuwa ni Samwel wa uongo, pepo , jini au shetani aliyezuka. Hili la Samwel wa uongo au wa ukweli siyo somo langu kwa leo . Leo nataka tu kukwambia kuwa * wafu wanaishi* .. Wanaishi katika dunia yao . Wanaishi katika ulimwengu wa roho. Wapo walio kuzimu na wapo waliokwisha tangulia peponi. Wanaishi maisha yao .

Kama wewe Bado mwili wako una uhai na uzima Basi usiingilie maisha ya wafu.

Lakini ktk Injili Yesu anakuja kutuonesha kitu cha tofauti kbs . Siyo tu kwamba Wafu wapo kuzimu na peponi tu , bali kuna wafu wapo duniani. Tupo nao tunaishi nao .

Yesu anamwambia mtu aliyemuomba akamzike baba yake, "waache wafu wawazike wafu wenzao" .

Huyu mtu anamuomba Yesu aende akauzike mwili wa baba yake , lkn Yesu anamwambia waache wafu wawazike wafu wenzao.
Hapa tunaona ya kuwa Kumbe Kuna Wafu wapo duniani ,wanatembea, wanaongea , wanakula , na pengine wanaongoza watu. Maana wafu waliokufa mwili wasingeweza kwenda kuuzika mwili wa mfu mwenzao .
Hii tafsiri yake ni kwamba , mwili huu wa mfu aliyetakiwa kwenda kuzikwa ulienda kuzikwa na watu wafu ambao hawajakufa mwili. Wamekufa rohoni na akilini. Nielewe vizuri hapa , hawajakufa roho Wala hawajakufa akili ,Bali wamekufa rohoni na akilini.
Miili yao ipo hai. Roho zao zipo hai . Akili zao zipo hai . Lkn Matendo yao ya mwili yanayoongozwa na roho na akili siyo Matendo yanayostahili kuwa ya mtu aliye hai rohoni ..
Wanahesabika kuwa wamekufa ktk ulimwengu wa roho..

Ikiwa mazishi ni ibada . Basi usiingilie ibada za wafu waache wafu wawazike wafu wenzao.

Kuna watu tupo nao tunaishi nso lkn waliishakufa tyr . Ni wafu . Matendo yao machafu , ya kinyama hayastahili kuwa ya Binadamu aliye hai.
Mtu akiishakufa amekufa . Ameondoka ktk ulimwengu huu .
Japo ni utamaduni, lkn Hata tukijitahidi kuuosha, kuusafisha, kuutakasa na kuuvalisha vizuri mwili wake, Haiondoi ukweli ya kuwa anakwenda kufukiwa na udongo chini ya ardhi.

Kwanini unahangaika kuwasafisha wafu ( sijasema maiti) . Unatumia gharama kubwa , muda wako na nguvu zako bure kuwasafisha wafu na unajua ya kuwa huwezi kubadilisha ukweli kuwa wanaenda kufukiwa na udongo chini ya ardhi!!??

Usiingilie ibada za wafu waache wafu wawazike wafu wenzao.

Wafu wanaelewana vizuri . Wanapata na muda Wanapiga story zao km Lazaro na tajiri. Wewe unaingilia story zao ambazo hazikuhusu. Unataka kumsafisha tajiri mfu . Mfu ni mfu tu . Haibadilishi ukweli hata Kama akitokea km mzimu wa Musa na Elia. Aliishakufa. Hayupo ktk dunia hii.

Ukihangaika kumsafisha mfu iwe ni bure au kwa gharama nawe unageuka kuwa mfu unayetembea . Wote mnakuwa wafu. Mmekufa kiroho na kiakili..

Je! Unaishi na mfu? Unafanya kazi na mfu? Unasoma na mfu ? Unaongozwa na mfu ? Unaongoza wafu?

Kuwa makini . Wafu wanaotembea wamekufa kiroho na kiakili . Ni wabaya wachafu kuliko wafu waliokufa kimwili .

Mungu JEHOVA wasamehe wafu wanaotembea maana hawajui walitendalo . Lkn wasaidie Sana wahangaikao kuwasafisha wafu maana hawajui kuwa wanageuka kuwa wafu wa kiakili . .

Ikiwa mazishi ni ibada Basi usiingilie ibada za wafu. Waache wafu wawazike wafu wenzao.

Makungu m.s
0743781910
23 April 2023
kwa ujinga huu, lazima Kiranga apate nguvu.
Nafsi hai=udongo+pumzi ya Mungu. hivi vitu vikitengana hakuna uhai wala kujua chochote

Mwa 2:7 SUV​

BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
SOMA VIZURI biblia yako ili usituabishe tunaoiamini

Mhubiri 9:5​

Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui chochote, hawana tuzo zaidi, hata kumbukumbu yao imesahaulika.

Mhubiri 9:10​

Kila unachotaka kufanya kifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima huko kuzimu unakokwenda.
Yale ya tajiri aliyekufa akakutana na tajiri ni mifano tu
Mfano kuna sehemu kwenye hicho kisa inasema yule masikini alikaa kwenye kifua cha Ibrahim, sasa kama masikini wakifa wanakaa kwenye kifua cha Ibrahim ,hicho kifua ni kipana kiasi gani
 
Ikiwa Mazishi ni Ibada , Basi Usiingilie Ibada za Wafu . Waache Wafu Wawazike Wafu Wenzao..
💫💫💫💫💫

©️Mwl. Makungu m.s
0743781910

Wana Heri wafu wafao katika Bwana. Naam asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa Matendo yao yafuatana nao (ufunuo 14:13).

Maana wafu wote wanalo tumaini ya kuwa Siku moja watatafufuliwa. Lakini ni wafu wachache walio na uhakika wa wapi wataelekea baada ya kufufuliwa.

Ni utamaduni wetu wa kuziosha maiti na kuzisafisha na kuzivalisha suti au sanda . Lkn yote hayo ni maandalizi ya kuzifukia chini ya udongo.

Nenda kaizike maiti , lkn usiingilie ibada za wafu. Huwa tunazika maiti, lkn hatuziki wafu. Wafu hawafi. Wafu wanaishi . Pengine hujanielewa Bado. Ni hivi, huwa tunazika miili ya wafu lkn hatuwaziki wafu. tunazika mwili lkn hatuziki nafsi . Nafsi haifi.

Umepata kusoma kisa cha Lazaro na tajiri ktk Biblia? Wote wawili walikuwa wafu . Miili yao iliishazikwa zamani duniani. Lakini wanaonekana wako mahali fulani tofauti wakiwa hai wanajadiliana . Mmoja anastarehe mwingine anataabika. Miili inakufa ,maiti zinazikwa, lakini Wafu wanaishi.

Ufunuo wa Yohana 6:9 " Na alipoifungua muhuri ya tano , nikaona chini ya madhabau roho zao waliochinjwa kwaajili ya neno la Mungu , na kwaajili ya ushuhuda waliokuwa nao. Wakalia kwa sauti kuu, wakisema , Ee Mola , Mtakatifu , Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu , Wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi ? Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu , nyeupe , wakaambiwa wastarehe Bado muda mchache , hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na Ndugu zao , watakaouawa vile vile Kama wao."

Ukisoma hapo juu unapata picha gani juu ya wafu ? Kuna Wafu wapo hai wanastarehe.

Unakumbuka Yesu alitokewa na Nani pale mlimani wakati akiomba? Alitokewa na wafu, nabii Musa na nabii Elia wakazungumza nae. Kwa lugha ya kiswahili sanifu Tunasema alitokewa na mizimu (yaani watu waliowahi kuishi katika hii dunia na baadae wakafa au wakaondoka ktk hii dunia) . Mzimu wa Musa na mzimu wa Elia. Wafu hawafi, wafu wanaishi. Inayokufa ni miili.

Yule Mwanamke mwenye pepo wa utambuzi (mchawi/ mganga) anamwambia mfalme Sauli je! Ni Nani nitakayekupandishia? Naye akasema , Nipandishie Samweli (nabii ambaye amekwishakufa na kuzikwa) . Yule mwanamke akampandisha Samwel kutoka ktk nchi (ardhi/ kuzimu). Nao nabii Samwel (mzimu) na mfalme Sauli wakazungumza.

Japo wanatheolojia wengine huwa wanasema kuwa Samwel aliyepandishwa toka kuzimu siyo Samwel . Ni pepo , jini au shetani lililojivika mwili wa Samweli. Lakini ukilisoma andiko hili ktk Biblia Hakuna mahali wala mstari wowote pameandikwa kukanusha kuwa yule alikuwa ni Samwel wa uongo, pepo , jini au shetani aliyezuka. Hili la Samwel wa uongo au wa ukweli siyo somo langu kwa leo . Leo nataka tu kukwambia kuwa * wafu wanaishi* .. Wanaishi katika dunia yao . Wanaishi katika ulimwengu wa roho. Wapo walio kuzimu na wapo waliokwisha tangulia peponi. Wanaishi maisha yao .

Kama wewe Bado mwili wako una uhai na uzima Basi usiingilie maisha ya wafu.

Lakini ktk Injili Yesu anakuja kutuonesha kitu cha tofauti kbs . Siyo tu kwamba Wafu wapo kuzimu na peponi tu , bali kuna wafu wapo duniani. Tupo nao tunaishi nao.

Yesu anamwambia mtu aliyemuomba akamzike baba yake, "waache wafu wawazike wafu wenzao" .

Huyu mtu anamuomba Yesu aende akauzike mwili wa baba yake , lkn Yesu anamwambia waache wafu wawazike wafu wenzao. Hapa tunaona ya kuwa Kumbe Kuna Wafu wapo duniani ,wanatembea, wanaongea , wanakula, na pengine wanaongoza watu. Maana wafu waliokufa mwili wasingeweza kwenda kuuzika mwili wa mfu mwenzao.

Hii tafsiri yake ni kwamba, mwili huu wa mfu aliyetakiwa kwenda kuzikwa ulienda kuzikwa na watu wafu ambao hawajakufa mwili. Wamekufa rohoni na akilini. Nielewe vizuri hapa, hawajakufa roho Wala hawajakufa akili ,Bali wamekufa rohoni na akilini.

Miili yao ipo hai. Roho zao zipo hai. Akili zao zipo hai. Lkn Matendo yao ya mwili yanayoongozwa na roho na akili siyo Matendo yanayostahili kuwa ya mtu aliye hai rohoni. Wanahesabika kuwa wamekufa ktk ulimwengu wa roho.

Ikiwa mazishi ni ibada . Basi usiingilie ibada za wafu waache wafu wawazike wafu wenzao.

Kuna watu tupo nao tunaishi nso lkn waliishakufa tyr. Ni wafu. Matendo yao machafu, ya kinyama hayastahili kuwa ya Binadamu aliye hai. Mtu akiishakufa amekufa . Ameondoka ktk ulimwengu huu. Japo ni utamaduni, lkn Hata tukijitahidi kuuosha, kuusafisha, kuutakasa na kuuvalisha vizuri mwili wake, Haiondoi ukweli ya kuwa anakwenda kufukiwa na udongo chini ya ardhi.

Kwanini unahangaika kuwasafisha wafu (sijasema maiti). Unatumia gharama kubwa , muda wako na nguvu zako bure kuwasafisha wafu na unajua ya kuwa huwezi kubadilisha ukweli kuwa wanaenda kufukiwa na udongo chini ya ardhi?

Usiingilie ibada za wafu waache wafu wawazike wafu wenzao.

Wafu wanaelewana vizuri . Wanapata na muda Wanapiga story zao km Lazaro na tajiri. Wewe unaingilia story zao ambazo hazikuhusu. Unataka kumsafisha tajiri mfu. Mfu ni mfu tu. Haibadilishi ukweli hata Kama akitokea km mzimu wa Musa na Elia. Aliishakufa. Hayupo ktk dunia hii.

Ukihangaika kumsafisha mfu iwe ni bure au kwa gharama nawe unageuka kuwa mfu unayetembea. Wote mnakuwa wafu. Mmekufa kiroho na kiakili.

Je, Unaishi na mfu? Unafanya kazi na mfu? Unasoma na mfu? Unaongozwa na mfu? Unaongoza wafu?

Kuwa makini. Wafu wanaotembea wamekufa kiroho na kiakili. Ni wabaya wachafu kuliko wafu waliokufa kimwili.

Mungu JEHOVA wasamehe wafu wanaotembea maana hawajui walitendalo. Lkn wasaidie Sana wahangaikao kuwasafisha wafu maana hawajui kuwa wanageuka kuwa wafu wa kiakili.

Ikiwa mazishi ni ibada Basi usiingilie ibada za wafu. Waache wafu wawazike wafu wenzao.

Makungu m.s
0743781910
23 April 2023
Udongo+pumzi ya Mungu=nafsi hai
vikitengana hivi vitu hakuna kimojawapo kinaweza kusimama peke yake kikiwa hai
Lazaro na Ibrahim was just teaching example , nothing was real
mfano inasema masikini alikuwa kifuani kwa Ibrahim, so wafu wote wanalala vifuani mwa Ibrahim au, ni kipana kiasi gani
Yesu alisema Lazaro amelala, alivoona wanashangaa ,ndo akawaambia amekufa
Kifo ni kama usingizi, ukisinzia hujui chochote
Ukiamini wafu wana nafsi isiyokufa, unajiletea imani ya mizimu. yaani unakaribisha majini yajigeuze wafu yaje yakutishe kuwa ni mfu kakutokea

Chukua hii Wafu hawajui lolote

Mhubiri 9:5​

kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lolote, wala hawana tuzo tena; maana hata kumbukumbu lao limesahauliwa.
 
Kisayansi.
Sayansi ya Lugha(Isimu); mtu akiyekufa huitwa Mfu au marehemu. Wingi wa Mfu ni wafu. Mwili wa marehemu au Mfu ndio huitwa Maiti. Hiyo ni lugha, tukio la mtu Kufa huitwa kifo au mauti.

Sayansi ya mwili, anatomy, physiology na mambo ya utabibu;
Ukisema MTU amekufa, tafsiri yake Hana ajualo, hajui chochote, Hana uwezo wowote ule. Kwani Viungo vyote (organs) na mifumo ya Viungo (organ systems) zote zimekufa, yaani hazifanyi kazi na hazina uwezo tena WA kufanya kazi. Hiyo ndio tafsiri ya Kifo,

Wafu hawawezi kuzikana Kwa sababu Mfu Hana uwezo wa kufanya Jambo lolote.

Kisa cha Lazaro na tajiri sio kisa halisi, Kwa Sisi wataalamu WA Lugha tunaita Metaphor, huwezi tolea reference ya hoja yako Kwa metaphor (tukio ambalo sio halisi). Ni Sawa na Metaphor (kisa au mfano) wa Mpanzi au Msamaria Mwema.

Metaphor ni moja ya vipengele vya Fasihi simulizi. Hivyo Yesu alitumia tuu Fasihi kubuni kisa hicho ambacho sio halisi.

Kisa cha Sauli, ukikisoma Kwa kina na utambuzi, unakuja kugundua kuwa SAULI HAKUMUONA SAMWELI, Ila Yule Mwanamke mchawi ndiye alimuona(alidanganya Kwa sababu wachawi ni waongo) ni kama wanavyofanya wanamazingaombwe au hawa waganga WA kienyeji WA siku hizi au hawa wafufua Misukule. Uongo mtupu.

Sauli alikuwa akiongea na mtu aliyedhani ni Samweli. Lakini hakuongea na Samweli Kwa sababu hakumwona.

Embu soma hizi Aya;
1 Samweli 28
11Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani?”
Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.”
12 Yule mwanamke alipomwona Samweli, alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamuuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.”
13 Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini?”
Yule mwanamke akasema, “Naona mungu unapanda kutoka ardhini.”
14 Sauli akamuuliza, “Ni mfano wa nini?”
Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.”
Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi, uso wake hadi ardhini.
.”

Yaani Sauli hakumuona MTU yeyote, yeye alidanganywa na Yule Mwanamke mchawi na sio vinginevyo.
Kusema Samweli alifufuliwa ni Uongo mkubwa. Kwa sababu hakuna ushahidi WA Jambo Hilo. Huyo Sauli mwenyewe aliyetaka Kufufuliwa Kwa Samweli hakumuona. Iweje wewe na Mimi tunayesoma tuseme aliyefufuliwa ni Samweli?

Kisa cha Yesu kutokewa na Musa na Eliya bado hakithibitishi kuwa wafu wanaongea au wanaweza kutenda kama Waliohai.
Hapa hoja kuu ni kuwa Eliya inaripotiwa Hakufa alipalizwa Kwa magari ya farasi yenye Moto. Hivyo Eliya sio Mfu yaani Hakufa.

Musa mambo ni 50"50 Ukisema Hakufa ni Sawa Kwa sababu hakuna ushahidi wa kuwa alikufa. Kwani maandiko ya kisa chake yanaonyesha mwili wake haukupatikana Huko Mlimani. Hivyo akitokea MTU akisema Musa Hakufa atakuwa na hoja Kwa sababu hakuna ushahidi WA kifo chake.

Lakini pia akitokea mtu akisema alikufa, sasa huyu hoja zake lazima zisithibitishwe,

Yud 1:9​

Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee"

Aya hii inaweza kutumiwa kama uthibitisho kuwa Musa alikufa lakini haijitoshelezi na inautata mkubwa. Na inajitatiza kulinganisha na miiko ya maandiko.
Kinachogombewa ni mwili wa Musa Wakati huohuo mwili unatakiwa kurudi mavumbini kama kauli ya Mungu ulivyosema.

KITEOLOJIA;
Mtu aliyehai ambaye amemuasi Mungu huyo huitwa MFU, LAKINI sharti awe Hai katika mwili.
Yaani Nafsi yake imekufa lakini yu hai katika mwili. Nafsi unazungumzia ishu ya Attitude, Akili, fikra, upendo, hasira, chuki, n.k. ni vitu visivyoshikika.

Ni Sawa na mwanandoa aliyeoa au kuolewa. Yupo ndani ya Ndoa lakini aseme Moyo wake umekufa, haumpendi tena mumewe au Mkewe. Lakini haimaanishi MTU huyo kafa.

Wafu Hawana ibada Kwa sababu wamekufa.
Hoja siyo kufufuka Kwa Samweli Bali mtoa hoja anatukumbusha kuwa roho Huwa hazifi bali miili ndiyo hufa
 
Udongo+pumzi ya Mungu=nafsi hai
vikitengana hivi vitu hakuna kimojawapo kinaweza kusimama peke yake kikiwa hai
Lazaro na Ibrahim was just teaching example , nothing was real
mfano inasema masikini alikuwa kifuani kwa Ibrahim, so wafu wote wanalala vifuani mwa Ibrahim au, ni kipana kiasi gani
Yesu alisema Lazaro amelala, alivoona wanashangaa ,ndo akawaambia amekufa
Kifo ni kama usingizi, ukisinzia hujui chochote
Ukiamini wafu wana nafsi isiyokufa, unajiletea imani ya mizimu. yaani unakaribisha majini yajigeuze wafu yaje yakutishe kuwa ni mfu kakutokea

Chukua hii Wafu hawajui lolote

Mhubiri 9:5​

kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lolote, wala hawana tuzo tena; maana hata kumbukumbu lao limesahauliwa.
Hoja ni kuwa roho haifi bali humrudia Mungu baada ya kutengana na mwili
 
Back
Top Bottom