Ni bahati nzuri kwamba safari hii aliyeupitia uchochoro huo kapita bila kukusudia, hakupanga iwe hivyo. Lakini natabiri kuwa baada ya watu kuuona uwezekano huo kuna watu wataanza kuufanya uwe mojawapo ya mikakati yao. Hii ni hatari kwa rais aliyeko madarakani. Nashauri utaratibu huu ufutwe haraka kwa maslahi ya taifa.
Makamu wa Rais abaki na nafasi yake hiyohiyo, akitaka urais asubiri muda ufike agombee.
Ikitokea bahati mbaya kama iliyotokea kwa hayati JPM, basi makamu awe kaimu rais kwa muda maalum (kama mwezi tu), chama chake kiteue mtu mwingine kwa utaratibu rasmi, jina lipelekwe bungeni kuthibitishwa awe rais hadi muda wa uchaguzi mkuu kwa mujibu wa kalenda utakapowadia.