Iko siku machinga watawashika viongozi pabaya

Iko siku machinga watawashika viongozi pabaya

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Siku 4 baada ya kijana Hamza kusababisha mauaji ya wapendwa wetu pale Selander Bridge nilikwenda Airport kuwapokea jamaa zangu kutoka Ulaya. Tukiwa kwenye gari langu kuelekea Mikocheni, njiani kwenye barabara ya Nyerere tukaona vibanda vingi vichafuvichafu njia nzima kutoka Airport hadi Vingunguti vya watu wanaouza chai na supu.

Wageni wangu wakaniukiza vile vibanda kandokando ya barabara ya kutoka airport ni vya akina Nani? Wanajulikana wote wanaofanya kazi kwenye vibanda vile?

Je, viongozi wenu na wageni muhimu wanaofika nchini kupitia airport hii wanatumia barabara hii pia au Kuna barabara nyingine? Kama ni hii mnawalinda vipi na snipers wanaoweza kutumia vibanda hivi kuwalenga? Mimi sikuwa na majibu sahihi kwa maswali Yao.

Siasa uchwara zinatufanya tuone ni sawa machinga kufanya kazi popote kwa aina yoyote. Siasa uchwara haziwaoni machinga wanaochafua mazingira, wanaojenga vibanda hata barabara ya airport lango kuu la nchi, njia za waenda kwa miguu, njia za maji na mitaro ya majitaka, mbele ya maduka ya wanaolipa Kodi na chini ya nyaya za umeme wa msongo mkubwa.

Iko siku vibanda hivi vichafu vitageuka maficho ya magaidi. Tuvute muda TU.
 
Ni aibu sana posta wamejaaa kibao wanapika mihogo moshi kama wote afu kuna maofisi makubwa, serikal iangalie namna ya kudeal na hawa watu, wanaharibu hata mandhari ya jiji, wanaweka vibanda kwenye njia za watembea kwa miguu, kodi hawalipi
 
Ni aibu sana posta wamejaaa kibao wanapika mihogo moshi kama wote afu kuna maofisi makubwa, serikal iangalie namna ya kudeal na hawa watu, wanaharibu hata mandhari ya jiji, wanaweka vibanda kwenye njia za watembea kwa miguu, kodi hawalipi
Tuna viongozi wanaobembeleza kuendelea kubaki kwa njia ya machinga, lakini hii inawasaidia kwa muda tu, muda ukifika shida itaibuka tu watashindwa pa kuwaweka na kugeuka tatizo la serikali.
 
Mpaka sasa hali ishakuwa mbaya hao watu hawawawezi tena ,sasa hivi machinga na bodaboda ni kama wana sheria na taratibu zao tofauti kabisa na za nchi yetu na wakiguswa tu wanadai wananyanyaswa eti kwa vile Magufuli kafa huku wao wakijiamulia chochote wanachojisikia serikali ikitaka kurekebisha hii hali itabidi ifumbe macho vinginevyo.............
 
Kiini cha tatizo ni kukosekana kwa ajira, hii ni njia ya wananchi kujipatia rizki.
No ni kutokutnamini secta ya mipango miji, urban social and infrastructural design hii unaweza andika na kupata phd
 
Siku hizi kila nyumba ina duka au kila mwenye kiwanja barabarani anajenga frame, ni uchafu tu. Na ni kinyume na sheria ya mipango miji, tumeharibu Sana miji yetu
 
Jibu ni moja tu, watu hawana ajiri na ile ni njia sahihi ya wao kujipatia vipato halali..hili bom la ukosefu wa ajira ipo siku litalipuka tu.
 
No ni kutokutnamini secta ya mipango miji, urban social and infrastructural design hii unaweza andika na kupata phd
Wakati wa uchaguzi manifesto ya Chadema ilielezea kuwajengea machinga vibanda vyenye hadhi ili waweze kufanya biashara katika hali zote za hewa. Pia walisema iko haja ya kuweka sehemu zitakozoendesha biashara kwa masaa 24 ya siku.
 
Back
Top Bottom