Ikulu ya Dar, litokee hili, fikiria itakuwaje ?

Kijakazi

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
7,093
Reaction score
10,469
Wananchi wa Sri Lanka wavamia Ikulu ya nchi yao, tazama picha chini, ikumbukwe Jeshi la nchi haliruhusiwi kushambulia Wananchi Kikatiba, kweli kuna nchi zimepinda, lkn haya yote ni matokeo ya dharau na majibu ya hovyo kwa watu ambao tayari wanataabika, …




 

Attachments

  • 1657377927840.jpeg
    48.1 KB · Views: 20
  • 1657378145798.jpeg
    64.3 KB · Views: 9
Kakopa mpaka akawa akopeshiki mbaya zaidi zile fedha ikawa zinamnufaisha yeye na marafiki zake akulizika akawauzia bandari wachina ayaa akaingia choo cha kike kwenda urusi apewe mafuta ya mkopo wanaojierewa wakaona mbali huyu jamaa anauza nchi kwa ufupi jamaa alikuwa fisadi sana
 
Lets look on other Parameters... Tabora ina km za mraba 72,000 na ina watu milioni mbili na ushehe.

Kisiwa kikuu cha Sri lanka kina km za mraba 65,000 na kuna watu milioni ishirini na moja!

Unategemea hali ya maisha itakuwaje kisiwani humo?

Yani idadi ya wa Sri lanka ni sawa na idadi ya wacanada wanaoishi kwenye takriban 10,000,000 km sq.
 
inawezekana tu ni kuwa wamoja ila kwa Tz ni ngumu...
Huwa nasema kila siku tuombe Mungu nchi iliyotulia kama yetu isitokee hivi kwani ikishatokea mara moja itakuja kuwa ndiyo kawaida, na kuimaliza tena ni shida kubwa. Ndiyo maana wenye akili wanataka viongozi wabadilke kabla wananchi hawajajanjaruka.
 
Watanzania hawataiga huu ujinga wataiga mambo mengine mazuri
 

Lakini bado Sri lanka imetuzidi Tanzania tena kwa mbali tu, kwa maana nyingine bado maisha ya mtu wa Sri Lanka ni bora kuliko Tanzania!
 
Lakini bado Sri lanka imetuzidi Tanzania tena kwa mbali tu, kwa maana nyingine bado maisha ya mtu wa Sri Lanka ni bora kuliko Tanzania!
wasingepanick namna hii kwenye mafuta.

umaskini unatafsiriwa wakati wa dharura kama huu.
nchi ambayo ina utawala mbovu namna hiyo unahesabuje imekuzidi!!

imekuzidi nini?4
 
Kmmke hapa kwetu kuna mang'ombe hayawezi kutokea hayo
 
wasingepanick namna hii kwenye mafuta.

umaskini unatafsiriwa wakati wa dharura kama huu.
nchi ambayo ina utawala mbovu namna hiyo unahesabuje imekuzidi!!

imekuzidi nini?4

Labda wameamka tu, wakati mwingine wananchi kujitoa kwa wingi wao kuipinga Serikali inayowakandamiza ni kielelezo cha kujitambua na siyo umasikini tu, North Afrika (Tunisia, Algeria na hata Egypt) wananchi waliingia barabarani pia kuondoa Serikali sasa unaweza kulinganisha uchumi wa Tunisia au Algeria na Tanzania ?

Hao watu bado wana matumaini na ndiyo maana wameamua kufanya hivyo, ukiona nchi kuna umasikini uliopitiliza na Viongozi wana kibuli na hawajali chochote halafu wananchi wake hawafanyi chochote kuna 2, aidha low IQ ya wananchi husika au kukata tamaa kabisa!
 
Vipi kuhusu Singapore
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…