Ila kutapeliwa kunauma wakuu

Mimi mkesha wa Christmas nilienda kupokea mrembo mkali kutoka mkoa pale magufuli stand ndan 🤣🤣🤣🤣

Nimeingia kuna bench zipo saa nane usiku hiyo kidogo tu kausingizi huwez amin waliondoka na simu na wallet 🤣🤣🤣

Walivyochana surual na viwembe afande alinicheka Sana 🤣🤣🤣🤣

Ukiona kibaka usiache kumpiga mawe
 
U
Uchawi upo Ila hapa ametengenezwa akili yake kutokana na namna matapeli walivyojiweka kimwonekano wao, na yale mazingira waliyoyatengeneza ya kuaminika Kwa kuwa na gari. Pia ni lazima Kuna mtu ndani ya bank kauza majina kamili ya mtapeliwa. Halafu kuna kitu bidada ametuficha, huenda aliahidiwa Asante hii ndiyo ikawa chambo ya kumshawishi apoteze muda wake kufanya hilo zoezi lililomgharimu.
 
Ndio maana Mimi Nina njia zangu za kufanya pindi tu nikikutana na watu nisiowaelewa basi kama wana Nia mbaya hawawezi kufanya kitu, sisi tuna nguvu ndani yetu.
 
Kuna kadawa kakuitwa ushuz wa shetani wakikupuliza sehemu ya ubongo wako inayodili na maamuzi inakua haifanyi kaz so wataamua wao kwa niaba yako apo akuna uchawi na hata hilo jina wewe ndio uliwatajia sema hukumbuki
 
Pole sana mkuu
 
Kitendo cha kuwapa AIRTIME, umekwishaaaa!!
 
Umeniudhi, kama vile nimeibiwa mimi!

Unafanya withdrawl ya kujifirisi kisha unaenda kukabidhi mpunga bila ya kuwa na doc yoyote inayohusu kutress hela waliyokuahidi!

Dah!

Habari zingine zinaumiza sana, bora mgelikuwa mnakaa nazo kimya mkishatendwa bhana.
 
Pol
Pole sana dada Lee tuwe makini sana na matapeli maana yanaumiza sana mambo kama haya nilishawahi kutapeliwa ada aisee siwez sahau hiki kipindi nilipata shida sana
 
Pole Sana

Kama hii story ni ya kweli .

Basi wajinga wanakufa na kuzaliwa na hawatoweza kuisha hapa duniani.

Unatepeliwa kijinga namna hiyo Mkuu.
Hawako bure wale umbwa watakuwa wanatumia madawa! Siku nikikuta raia wanamshughulikia tapeli lazima nimkate koromeo!
 
🤣🤣🤣🤣🤣

karibu mjini umeuanza mwaka vizuri sana inaonekana wewe bado untongotongo, na wajanja wamekusoma kitambo na hilo GAME limechezwa tangu upo humo benki na ukanasa mtegoni.Jina lako limetokea ndani ya benki😎

Next time ukiwa town kaza sura,tembea chapchap badili njia bila taarifa yaani shwaa pinda kulia rudi nyuma piga reverse dadeki yaani kwa kifupi TEMBEA ZIGZAG🤗

Ukiwa town ni mwiko kusimama hata ukiitwa majina yako ya UBATIZO huyo mtu kama anashida na wewe atakupigia simu. Ukiitwa ukaitika inakuwa ushameza ndoano wewe SAIKOLOJIA yako itaanza kukuzuzua mpaka wakulambe hela ndo utarudi kawaida.

Kilichokuzuzua wewe ni vipi hao wahuni wamelijua JINA LAKO NA CONFIDENCE WALIYONAYO ndo vituvilivyokuchanganya mda unajiuliza maswali akili yako inakosa utulivu wa kutafakari vyema kwa mda huo hapo ndo WAHUNI wanajichukulia point🤗🤗🤗 hizi ni mind GAMES ambazo zipo well calculated hakuna DAWA wale majini,ni akili tu!!!

Ukiwa town kaza sura, ukimwangalia mtu mkodolee macho straight,mwangalie machoni kwa macho ya ukali,hamna kucheka na kima yoyote yaani ubaya ubwela tu.

Ishi na hizo CODE hao wajinga wa mjini hawawezi kukuzoea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…