Ilala: DC Sophia Mjema athibitisha wagonjwa wa COVID-19 hospitali ya Amana kuleta fujo na kutaka kuondoka wakajitibie nyumbani

Mgonjwa kuondoka haulizwi daktari au daktari muangalizi au nesi kwenye ward husika bali mlinzi wa geti la kuingilia au kutoka![emoji15][emoji15]

Tumefika hatua mbaya sasa!!
Ukisikiliza mpaka mwisho DC kaongelea moja ya tatizo ni kwamba wanajiona wamepona ivyo awaoni sababu ya kubaki hospitali.

Yaleyale ya health promotion watu awaelewi ya kuwa Corona wakimaliza main attack (ambayo ni kama week mbili) utajiona umepona lakini bado wapo mwilini na hali ya kuumwa umwa inajirudia (it takes time to recover fully); isitoshe muda huo unaweza ambukuza watu wengine kama kawa.

Moja ya tatizo kubwa ni poor public health promotion approach somo hafifu sana linatolewa kwa umma kuhusu huu ugonjwa kitu ambacho kitapelekea kuongeza ukubwa wa tatizo lenyewe.

Lord have mercy
 
Ni hotuba ambayo ilivuruga na kufifisha kwa kiasi kikubwa nguvu ya kupambana na COVID ambayo ilikuwa imeanza kuzaa matunda.

Ni hotuba iliyoonyesha kuwashutumu wataalamu wa afya na huku ikija na njia mbadala za kulikabili janga hili zilizojaa hisia zisizo na uhalisia wala uhalali kiafya.

Ni hotuba ambayo Rais alionyesha waziwazi kuwa hayupo tayari kukubaliana na hali halisi bali anaongozwa zaidi na kile anachoamini. Tatizo hili linafanya mambo mengi ya msingi kukwama, siyo haya ya mapambano ya COVID 19 pekee.

Ni hotuba ambayo kimsingi aliiandaa bila kupata taarifa sahihi kutoka kwa wataalamu wa wizara husika. Inaonyesha alituma vijana wake kufanya uchunguzi ambao hata hivyo inaonyesha waliufanya kwa hisia za kumpendeza Rais zaidi.

Alishindwa kuongea mambo mengine ya muhimu kitaifa kama suala la mafuriko kwakuwa alijiandaa zaidi kutoa hisia zake juu ya jambo moja.

Ni kwa maana hiyo basi, hotuba yake iliwapa baadhi ya wagonjwa wa COVID 19 huko hospitali ya Amana kujiamini na kuvunja waziwazi utaratibu na muongozo wa kiafya kuhusu COVID 19 kutoka WHO.
 
Kila kitu kilikuwa zigzaga kwenye press ya Bwana Mkubwa, sijui tatizo lipo wapi mpaka unajiuliza hakuna mtu wa kumwambia Mzee hapa hapana.

Unajiuliza nani alimdangamya kuwa Kuna mtu anaweza kuweka virus kwenye Barakoa na yeye akaamini, vurugu zote hizi dunia nzima inahangaika halafu mtu akae kiwandani afanye kazi ya kujaza makorona kwenye Mask, hili hata ningeambiwa mimi ningetumia akili ya mbayuwayu
 
Haka ni kaugonjwa kadogo tu tuchape kazi.....

Vipi yule aliesema ni vimafua tu alishapona?
 
Lakini eti tunasali makanisani na misikitini kumueleza Mungu aiangalie TZ kwa huruma. Vyuo vikuu vyote tulivyonavyo navyo wamefunga badala ya kufanya tafiti za kuokoa watu. Bado watu wanadhani Korani na Biblia ni vitabu vya medicine. Inatia shaka sana!

Kila ukiangalia ulaya na America zinavyovurugwa, na jinsi watumishi wa afya wanavyohangaikia wagonjwa na bado wengine wanapoteza maisha, basi naamini hapa kwetu, COVID-19 inapiga inavyotaka.

Sekta yetu ya afya haina kujituma bali ni kutafuta kuhusudiwa tu! Kuna wanaojiita maprofesa pale Muhimbili najua sasa wako bize kuandika wapate pesa za miradi kama walivyopiga za UKIMWI bila lolote la maana, Hawawezi hata kubuni mbimu za kitabibu kuwasaidia wagonjwa! Kila mtu anapenda kupumzika na kula migahawani huku wagonjwa wakiteseka. Mtu si anaamua kusepa tu!
 
tumeambiwa waliotupa habari kuhusu au kuijua corona ni wanasayansi na si manabii, sasa hizi akili za kuaminisha watu waombe ili corona iishe sijui zinatoka wapi? au kuaminishwa kuwa waganga wa kienyeji wanaochanja watu chale za matako nao wataweza kuiondoa corona? tz tumelogwa sio siri!
 
😳 πŸ˜­πŸ™†β€β™‚οΈπŸ™†β€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…