Ilala: DC Sophia Mjema athibitisha wagonjwa wa COVID-19 hospitali ya Amana kuleta fujo na kutaka kuondoka wakajitibie nyumbani

Ilala: DC Sophia Mjema athibitisha wagonjwa wa COVID-19 hospitali ya Amana kuleta fujo na kutaka kuondoka wakajitibie nyumbani

Assume baadhi ya hao wagonjwa wapande mabasi kwenda kwa waganga huko mikoani au kutambika mizimu, rate ya spread itakuwaje?

Tuna tatizo la uongozi katika nchi hii
Ni Mungu anajua ndugu. Na wale ambao wanajihi na wako majumbani wataogopa kwenda kujikabidhi hospitali kwa sababu hawatakuwa na huduma, watakua tayari kufia kwa waganga wa kienyeji ama majumbani kwao.
 
inasemekena hapo Amana madaktari wamelewewa na kazi wagonjwa wanachoka kusubiri
 
Lakini Magu alisema hakuna haja ya kumuweka mtu ndani kwa siku 14 nadhani wameitendea haki kauli yake

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini hio lock down ya siku 14 si iko kitaalamu zaidi? Maana yake ni kwamba kirusi kinaonekana zaidi baada ya muda huo, kwa sababu ndio muda wake wa kujionesha. Tusipuuze maoni ya watalaamu wa afya
 
Mgonjwa wa Covid-19 ambae anashindwa hata kupumua ataweza kubeba maiti? Maana huu ugonjwa unaathiri sana mfumo wa hewa kwa muda mfupi sana.
Ulete ubishi wa kijinga watu walio amana sio wagonjwa mahututi
Mahututi wapo mloganzira.

Amana watu wapo fiti hata Paring ya mtu mbili wanaweka
Corona hata ww hapo unaweza kuwa nayo endapo kama utapata bahati ya kupimwa..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wito wangu kwa WATANZANIA:
  • Fuateni mapendekezo ya wataalam- Wizara ya afya na madaktari sio wanasiasa
  • Epukeni mikusanyiko- Makanisani, misikitini, kwenye ndoa, mazishi n.k
  • Usisubiri serikali ikuwekee sheria, jiwekee mwenyewe.
 
Back
Top Bottom